30/08/2026
LEADING FROM BEHIND PART 2"KUONGOZA KUTOKEA NYUMA SEHEMU YA PILI" (BY PROPHET DOMINIC MWINYUKA)
Chochote unachokipata kabla hujamtukuza mwanadamu mtukuze kwanza Mungu, unapoona mwingine amekutangulia kubarikiwa wewe pia unaweza ukafanikiwa. Wakati wote kuna nafasi juu ya kufanikiwa.(Mwanzo 4:1-5)
Biblia inasema Kaini alipoona sadaka ya ndugu yake imekubaliwa aliwaza je yake itakubaliwa? Kaini kabla ya kumuua ndugu yake alijiua yeye kwanza ndani.
Hata k**a upo chini ya jua ipo nafasi yako tena usijiue, je ulishawahi kujiua kwa kuona mafanikio ya mtu mwingine? Mungu anaweza kukupa maisha mazuri ya mbele wakati wanadamu wamekukatia tamaa, ukiona Mungu anakutoa kwenye uzuri wa macho upo uzuri anakupa uliojificha.
Kuna yule akuonaye zaidi ya wanadamu, hatazami k**a mwanadamu atazamavyo, Eli-Elion akuone tena. Kuongoza kutoka nyuma lazima uwe na moyo wa unyenyekevu ndani ya moyo wa unyenyekevu kuna kujazilizwa na kupewa package yako. Popote Mungu anapomuweka mtu wake hajakosea. Huwezi kutawala k**a bado mtawala yupo kwenye kiti chake, lazima ujifunze kutawala akiwa bado anatawala.(Mwanzo 16:5-11)
Pale mahali unapotaka kupaingia unahitaji UVUMILIVU TU na kujifunza sauti ya Mungu, yule ambaye alinyanyasika Mungu alienda kuuzidisha uzao wake. Vita unavyovipitia leo ni ukubwa wa utukufu wa kesho yako, kuna vitu vingine vigumu usiwaambie watu baki navyo k**a kiongozi na Mungu atakupa mwongozo wa kesho.
NAMNA YA KUONGOZA KUTOKEA NYUMA
1.Jiondoe kutoka kwenye historia ya nyuma/usijilinganishe maisha yako na ya sasa, futa historia ya nyuma. Uumbaji wetu si tumboni tu hata k**a umekua bado uumbaji wako unaendelea.
(2 Wakorinto 5:16-17, Zab 139:14-15)
2.Mwamini Mungu kwa yale usiyoyaona hata kwa macho ya nyama, Abraham alibarikiwa kwa kuona na yeye akaamini ndani ya moyo wake, wewe anza kuamini kwa kuona na Mungu atakuletea.
Hata k**a unachokigusa kinakufa unaweza kuongoza tena, ila unatakiwa uwe mwaminifu kwenye kila kitu unachofanya.