Pastor Katana Mwangome M'baya

Pastor Katana Mwangome M'baya Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Pastor Katana Mwangome M'baya, Religious organisation, Morogoro.

ALHAMISI: 09-02-2023SOMO:MAMBO 10 YA KUFANYA KILA SIKU NA KILA WAKATI, ILI KUFANYA SIKU YAKO IWE YA BARAKAMHUBIRI: MCHUN...
10/02/2023

ALHAMISI: 09-02-2023
SOMO:MAMBO 10 YA KUFANYA KILA SIKU NA KILA WAKATI, ILI KUFANYA SIKU YAKO IWE YA BARAKA
MHUBIRI: MCHUNGAJI KATANA MWANGOME M'BAYA.
KANISA: HEKALU LA NEEMA- BIGWA- MOROGORO

Katika maisha kuna vitu unatakiwa uvifanye kila siku, mara kwa mara, ni mambo ya ki-Mungu, Usipoyafanya utakosa amani kwenye maisha yako.

1) Kusifu na kuabudu.
Sio kuimba tu bali unamueleza Mungu sifa zake, uweza wake, nguvu zake,unampa Mungu dhabihu ya sifa kwa maneno ya kinywa chako.

Waebrania 13:15
Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake.

Unapoamka asubuhi unamsifu Mungu, itakufanya uwe na amani. Mungu anakaa katika sifa zake.

2) Kuhubiri na kutangaza habari njema.

1 Mambo ya Nyakati 16:23-27
Mwimbieni BWANA, nchi yote;
Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.
Wahubirini mataifa habari za utukufu wake,
Na watu wote habari za maajabu yake.
Kwa kuwa BWANA ni mkuu mwenye kusifiwa sana;
Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.

Maana miungu yote ya watu si kitu;
Lakini BWANA ndiye aliyezifanya mbingu.
Heshima na adhama ziko mbele zake;
Nguvu na furaha zipo mahali pake.

Waambie watu habari za utukufu wake, watu unaokaa nao, unaoishi nao, kazini kwako. Waambie wajue ukuu wake Mungu wako unaemwamini, alipokutoa na jinsi alivyokupigania.

3) Kukusanyika katika ibada ( Fellowship).

Matendo ya Mitume 2:46
Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,

Usiache kuwa na ushirika na Mungu nenda ibada kwa moyo mmoja kwa kupenda bila kusukumwa na mtu.

4) Kusoma na kutafakari neno la Mungu.

Zaburi 1:2
Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo,
Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.

Usiache siku ikapita bila hujasoma neno la Mungu ,unaposoma neno kuna vitu utagundua kwenye maisha yako hukutakiwa kuwa navyo.

Kwa kusoma neno utakumbuka ahadi za Mungu Katika neno la Mungu kuna ahadi ulitakiwa uwe nazo unaposoma utakumbushwa ni kipi ulitakiwa uwe nacho.

1 Mambo ya Nyakati 16:17-18
Alilomthibitishia Yakobo kuwa amri,
Na Israeli liwe agano la milele.
Akisema, Nitakupa wewe nchi ya Kanaani,
Iwe urithi wenu mliopimiwa;

5) Tunza furaha.
1 Wathesalonike 5:16
Furahini siku zote;

Kila siku unatakiwa uitunze furaha yako. Furaha haihamishiki huwezi kuhamisha furaha ya Jana ukaileta leo, ukiwa mtu wa kununa utapata magonjwa ,muepuke mtu anayekuondolea furaha yako.

Wafilipi 4:4
Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini

Furahi hata k**a huna kazi ,huna pesa unatakiwa furahia upendo wa kristo.

6) Shukurani
1 Wathesalonike 5:18
shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.

Usiwe mtu wa lawama ,usiwe mtu wa manung'uniko pamoja na changamoto unazopitia, ni mangapi Mungu aliyokutendea unakosa kumshukuru? Kuna watu maisha yao ni lawama tu, jifunze kumshukuru Mungu.

7) Kufanya huduma au kazi ya Mungu.l

1 Wakorintho 15:58
Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.

Kuna watu wenye huduma ya kuombea, kutia moyo, kushuhudia, kuegemeza, jiimarishe katika Bwana fanya kwa bidii, usiangalie au kuvunjwa moyo na mtu.

8) Maombi(kuomba).

Luka 18:1
Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.

Luka 21:36
Basi, kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.

Usipoomba kuna vitu hutaepushwa, kuna majaribu utaingia, tunapaswa kuomba, kukesha bila kukata tamaa, ukiomba Mungu atakunusuru na mabaya yaliyopangwa juu yako.

Waefeso 6:18-19
kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;
Pia na kwa ajili yangu mimi, nipewe usemi kwa kufumbua kinywa changu, ili niihubiri kwa ujasiri ile siri ya Injili;

Kwa sala, na maombi kudumu kwa kuwaombea watakatifu.

Ukiomba na kuona maombi yako yanaisha mapema, badilisha mazingira ya maombi na mtindo wa kuomba. K**a umepiga magoti, simama au tembea, n.k

Omba unapohisi hatari, unapokuwa njia panda omba, unapokosea au umetenda dhambi usimkimbie Mungu,bali mkimbilie kwa toba.

Kuna aina nyingi za maombi lazima ujue unaomba maombi gani kuna maombi ya Shukurani, vita, kukata rufaa, n.k.

9) Zuia ulimi wako usinene mabaya au hila.

1 Petro 3:10
Kwa maana,
Atakaye kupenda maisha,
Na kuona siku njema,
Auzuie ulimi wake usinene mabaya,
Na midomo yake isiseme hila.

Utakosa raha, utakosa amani, utakosa baraka maishani, k**a kinywa chako kitanena hila au mabaya. Mabaya na hila vinakuondolea furaha yako. Mengine yatakayokuondolea furaha ni;

a) Umbeya/ usengenyaji
Umbeya ni kuongea habari ambazo hujaulizwa. Kusengenya ni kuongea habari za mtu ambaye hayupo ambapo akiwepo huwezi kuziongea
b) Uchonganishi au udhalilishaji
Uchonganishi ni kuwakosanisha watu bila wao kujua.

c) Matusi yasitoke kinywani mwenu.

d) Uongo na uzushi
Maneno ya udhaifu k**a vile, Nitapata kazi kweli?, nitafanikiwa kweli?, nitapona kweli?

10) Utoaji wa sadaka.
Matendo mema, utu, ukarimu, n.k.

2 Wakorintho 9:8-9
Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;
k**a ilivyoandikwa,
Ametapanya, amewapa maskini,
Haki yake yakaa milele.

Ndugu msomaji na mfuatiliaji wa somo hili, Mungu anatupa maelekezo jinsi ya kutengeneza maisha ya ushindi siku zote. Kubali kufuata na kuyaishi haya, utamwona Mungu maishani.

K**a umeguswa na somo hili na unataka kumpa Yesu maisha yako, yaani kuokoka, au kuzaliwa mara ya pili, karibu kanisani kwetu, au nenda kanisa la kiroho karibu na wewe, mwone mchungaji atakusaidia. Ubarikiwe. Amen.

Kwa msaada zaidi na maombezi, fika kanisani, Hekalu la Neema, Bigwa Morogoro. Au wasiliana nasi kwa simu 0689213966, au kupitia FACEBOOK:Pastor Katana Mwangome M'baya, na kwa YOUTUBE: Pst Katana. Pia unaweza kutoa sadaka yako kwa Mungu kupitia M- pesa 0752119763 au Tigo-pesa 0654894607, Mungu akubariki. Amen

` JUMANNE:07-02-2023SOMO:DHAMBI AU ROHO YA MAZOEAMHUBIRI:MCHUNGAJI KATANA MWANGOME M’BAYAKANISA: HEKALU LA NEEMA- BIGWA-...
10/02/2023

` JUMANNE:07-02-2023
SOMO:DHAMBI AU ROHO YA MAZOEA
MHUBIRI:MCHUNGAJI KATANA MWANGOME M’BAYA
KANISA: HEKALU LA NEEMA- BIGWA-MOROGORO.

Kuna wakati mtu unatendewa jambo hata husemi asante, kutendewa jambo kwako unaona ni kawaida, ni mazoea. Mazoea ni tabia ya kuchukulia mambo muhimu, na ya msingi kwa uzito usiostahili, na hii imewazuilia watu wengi wasipige hatua katika maisha.

Mungu hazoeleki ni mpya kila siku, ana mambo mapya kila siku ambayo wewe hukuyawaza wala kuyafikiria. Mtu mwingine akikosa ibada, anaona ni jambo la kawaida, na kuna vitu vingi unavifanya unaona ni vya kawaida. Mungu anafanya miujiza mingi, anafanya mambo mengi kwako, lakini umeyakosa sababu ya mazoea yako ya kuona kila kitu na cha kawaida.

Kuna ndoa nyingi pia zinaharibika kwa sababu mke na mume wamezoeana. Mapokeo yanaweza kukufanya kuukosa kabisa muujiza wako. Mazoea ni tamaduni, tena ni dhambi. Mazoea yanakufanya usipokee vitu vingi toka kwa Mungu.

Tabia hii ya mazoea ikijengeka ndani yako, kunazaliwa kitu kinaitwa dharau.
Mithali 8:17-18
Nawapenda wale wanipendao,
Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
Utajiri na heshima ziko kwangu,
Naam, utajiri udumuo, na haki pia.

Unapoona mambo ya msingi ni kawaida, ujue kuna vitu utavikosa. Mambo ya Mungu yanachukuliwa kwamba ni ya msingi na tena kwa bidii, sio kwa ulegevu wala kwa mazoea. Unaweza ukajikuta ufarisayo unazaliwa ndani yako, ukajiona una roho wa Mungu kumbe huna, kuna vitu unagharamika maishani mwako, na shetani amekufanya uone ni vya kawaida.

Farisayo ni mtu wa tabia gani? Farisayo no mtu anafanya vitu ili aonekane machoni pa watu. Ukianza kuyaona moyo wako unafanya mambo au jambo ili uonekane machoni pa watu, ujue roho ya farisayo imeshazaliwa ndani yako.

Mazoea yanapokuwepo katika maisha ya mtu, yanafanya roho ya shetani kushambulia familia na kanisa pia.

Mazoea yatakufanya uwe kipofu, hata Mungu aseme jambo huoni, unakuwa hujui unapoelekea wala kinachoendelea. Mazoea yanashusha kiroho cha mtu, utaenda ibada lakini hutaongezeka maarifa, hutaona badiliko lolote, moyoni mwako.

Mazoea yanakuletea uone wizi, au uzinzi ni kawaida, kutokuomba ni kawaida, mwingine yuko ibada ni wakati wa kuomba, kwa sababu ya mazoea utaona haombi, hajishuhulishi na lolote, mazoea ni mabaya, ni njia ya kishetani ya kukudumaza. Kataa roho ya mazoea maishani mwako katika jina la Yesu.

Yohana 14:8-9
Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha.
Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?

Unaanza kuona mchungaji wako ni wa kawaida, unaona filipo alimzoea Yesu akamwona wa kawaida. Wako wakristo wengi shetani amewafikisha mahali pa mazoea.

Mazoea yanakufanya usione umuhimu wa mtu, huoni faida yake, unamwona wa kawaida, kumbe baraka yako iko kwake, wewe unamwona wa kawaida tu, utakosa mengi. Nakushauri umwombe Mungu uondokane na roho ya mazoea, uone kuwa wako watu Mungu anawaleta kwako ili wakusaidie wakufikishe mahali upokee baraka yako.

Hasa unakuta mtu umezaliwa nae, umesoma nae, mmekua pamoja, unaangalia kimwili tu.
Kabla Samsoni hajatobolewa macho alianza kuona nguvu za Mungu ni za kawaida, aliposhinda vitani akaona ni kawaida.

Mazoea yatakuondoa kwanye kusudi alilokuitia Mungu.
Waefeso 2:1-2
Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu; ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi.

Mungu anaweza kumleta mtu kwako, ukamwona wa kawaida, sababu macho hayaoni tena.

Marko 6:3-5
Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda, na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake.
Yesu akawaambia, Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake mwenyewe, na kwa jamaa zake, na nyumbani mwake
Wala hakuweza kufanya mwujiza wo wote huko, isipokuwa aliweka mikono yake juu ya wagonjwa wachache, akawaponya.

Mapokeo na tamaduni zimetufanya tunamkosa Mungu, kujua madhaifu ya mtu haimaanishi kuwa yeye sio mtumishi wa Mungu. Shetani anakuonyesha madaifu ya mtu, ili usipokee muujiza wako.

Marko 7:7-9
Nao waniabudu bure,
Wakifundisha mafundisho
Yaliyo maagizo ya wanadamu,
Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu.
Akawaambia, Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu.

Mazoea, liturujia yatakufanya usipokee lolote toka kwa Mungu, kinachofanya usipokee ni kufuatilia mapungufu, dosari za mtu. Jiulize wewe ni safi? Huna mapungu wewe? Kwa nini unapoteza muda kufiatilia yasiyokuongezea chochote? Mtafute Yesu kwa bidii, utaona baraka.

Mathayo 12:46-50
Alipokuwa katika kusema na makutano, tazama, mama yake na ndugu zake walikuwa wakisimama nje, wataka kusema naye
Mtu mmoja akamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kusema nawe.
Akajibu, akamwambia yule aliyempasha habari, Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni akina nani
Akawanyoshea mkono wanafunzi wake, akasema, Tazama, Mama yangu na ndugu zangu!
Kwa maana ye yote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyu ndiye ndugu yangu, na umbu langu.

Usidharau watumishi wa Mungu, mwone Mungu ndani yao, utazipata baraka zako alizoweka ndani yao kwa ajili yako.

Watu wa Yesu, msikubali roho ya mazoea ikae ndani yenu, itakukosesha mengi toka kwa Yesu. Yesu ana mengi ya kutusaidia, tumekosa msaada wake kwa kuruhusu mazoea ndani yetu. Kataa roho ya mazoea na Mungu atakusaidia. Amen.

Kwa msaada zaidi na maombezi fika kanisani, Hekalu la Neema, Bigwa-Morogoro. Au wasiliana nasi kwa simu 0689213966, au kipitia FACEBOOK: pastor Katana Mwangome M’baya, na kwa YOUTUBE:Pst Katana. Pia unaweza kutoa sadaka yako kwa Mungu kupitia M-pesa 0752119763 au Tigo-pesa 0654894607. Mungu akubariki. Amen.

JUMAPILI:05-02-2023SOMO:KWA NINI TUFUNGE NA KUOMBAMHUBIRI:MCHUNGAJI KATANA MWANGOME M’BAYAKANISA: HEKALU LA NEEMA- BIGWA...
10/02/2023

JUMAPILI:05-02-2023
SOMO:KWA NINI TUFUNGE NA KUOMBA
MHUBIRI:MCHUNGAJI KATANA MWANGOME M’BAYA
KANISA: HEKALU LA NEEMA- BIGWA-MOROGORO.

Sababu za kimwili kwanini tunafunga, Unapofunga mafuta ya mwilini yanayeyushwa ili mwili uweze kutenda kazi na afya yako iwe imara.

Sababu za kiroho kwa nini tunafunga;

1). Ni Ishara ya unyenyekevu kwa Mungu ,Ili tupate nguvu na neema.

Ili uzipate na kuziona nguvu za kiroho maishani unahitaji ufunge na kuomba. Usipofunga na kuomba utakaa eneo moja la maisha, unakuwa mtu wa kawaida.

Unahitaji ufunge na kuomba Ili tupate neema ya kuinuliwa. Kuinuliwa ni kushuka na kunyenyekea kwa Mungu. Kutokufunga inaonyesha una kiburi, umejitosheleza, huhitaji msaada wa Mungu, huhitaji maarifa na msaada wa Mungu.

Njia mojawapo inayoonyesha unahitaji msaada wa Mungu katika maisha yako ni kufunga na kuomba.

1 Petro 5:6
Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;

Unyenyekevu katika kufunga kunaanza mwanzo wa wiki au mwisho wa wiki, mwanzo unaomba k**a vile unavyoomba usiku unaitabiria siku yako ,unafanya vita na mamlaka za giza , na mwisho unamaliza kwa shukurani unamshukuru Mungu kwa wema na fadhili zake kwako.

2). Tunafunga ili kupenya au kushinda mambo fulani yanayoinuka kinyume chetu.

Kuna vitu havitaondoka kwako ni mpaka uamke usiku na kuomba mwenyewe .Kuna Baraka tunazipata kwa sababu ya neema, Mungu anaachilia neema kwa kila mtu. Baraka zingine ni za agano ,hizi zinahitaji nguvu yako ya kupambana kiroho zinahitaji neema yako binafsi. Mungu anahitaji kuona uwezo ulio ndani yako , kuna Baraka zinahitaji wewe mwenyewe ujisimamie na kupambana.

3). Tupate msaada wa Mungu ili tupate kutimiza lile kusudi la Mungu aliloweka ndani yetu.

Matendo ya Mitume 26:22
Basi kwa kuwa nimeupata msaada utokao kwa Mungu nimesimama hata leo hivi nikiwashuhudia wadogo kwa wakubwa, wala sisemi neno ila yale ambayo manabii na Musa waliyasema, kwamba yatakuwa;

Unahitaji msaada kwenye ndoa ,mahali pa kazi ,biashara ni lazima ufunge na kuomba

2 Wafalme 6:27
Akasema, BWANA asipokusaidia, nikusaidieje mimi? Ya sakafuni, au ya shinikizoni?

2 wakorintho 11:27

2 Wakorintho 11:27
[27]katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi.

Paulo anaonyesha jinsi alivyopata msaada wa ki-Mungu ,tunafunga ili tupate msaada wa kimungu.

4). Tunafunga ili kushinda majaribu ambayo yamekuzuia kusonga mbele ,kuna majaribu tunaingia ni kwa sababu hatukeshi na kuomba na pia hatufungi na kuomba.

Luka 4:1
Na Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani.

Yesu alifunga ili apate nguvu ,na ushindi wa majaribu ni kwa sababu alipata neema. Kwa kadiri unavyonyenyekea, na kujidhabihu ndio unapata neema zaidi. Funga na kuomba juu ya changamoto ulizo nazo, mwambie Mungu aingilie kati na atakusaidi
Kufunga ni makubaliano kati yako wewe na Mungu.

Kwa msaada zaidi na maombezi fika kanisani, Hekalu la Neema, Bigwa-Morogoro. Au wasiliana nasi kwa simu 0689213966, au kipitia FACEBOOK: pastor Katana Mwangome M’baya, na kwa YOUTUBE:Pst Katana. Pia unaweza kutoa sadaka yako kwa Mungu kupitia M-pesa 0752119763 au Tigo-pesa 0654894607. Mungu akubariki. Amen.

ALHAMISI:02-02-2023SOMO:HATUA TANO ILI KUWA NA MFUNGO WENYE MATOKEOMHUBIRI:MCHUNGAJI KATANA MWANGOME M’BAYAKANISA: HEKAL...
10/02/2023

ALHAMISI:02-02-2023
SOMO:HATUA TANO ILI KUWA NA MFUNGO WENYE MATOKEO
MHUBIRI:MCHUNGAJI KATANA MWANGOME M’BAYAKANISA: HEKALU LA NEEMA- BIGWA-MOROGORO

Si kila aliyefunga alipata matokeo aliyotarajia. Kuna watu wanaingia kwenye mfungo ni kwa sababu hawana chakula. Namna hii ni vigumu sana kupata matokeo uliyotarajia ya kufunga kwako kwa sababu umefunga bila utaratibu, umefunga kwa kufuata dini na dhehebu, hii ni kwa sababu ya kutokuijua kweli au neno la Mungu.

Yohana 8:31-32
Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.

Unapofunga inahitajika ujiandae kiakili. Kufunga maana yake ni kwenda kukutana na Mungu, inahitajika ujiandae kwenda kukutana na Mungu na kupokea kutoka kwake.

Mithali 11:29
Ataabishaye nyumba yake mwenyewe ataurithi upepo; Mpumbavu atakuwa mtumwa wa mtu mwenye moyo wa akili.

Kuna watu wanaenda kufunga huku hawajui familia zao watakula nini, watu wa nyumba kwake wataishije. Mungu anatuonya leo, kwamba tusitaabishe familia zetu, maana asiyewatunza wa nymbani mwake ni mbaya kuliko asiyeamini.

Kuna Baraka zinapatikana kwa kuamka usiku wa manane na kuomba, pia kuna Baraka ambazo huwezi kuzipata ni mpaka ufunge na kuomba, hatua za kufuata unapopanga kuingia kwenye mfungo;

Hatua ya kwanza; NI LAZIMA UWE NA MALENGO AU MAONO YA KUFUNGA KWAKO.
UNATAKA KUFUNGA ILI IWEJE?ILI UFANYIWE NINI?

Luka 18:40-41
Yesu akasimama, akaamuru aletwe kwake; na alipomkaribia, alimwuliza,
Wataka nikufanyie nini? Akasema, Bwana, nipate kuona.

Bartimayo alikuwa alishapanga nikikutana na Yesu nitamwambia neno moja tu 'NIPATE KUONA' Yesu alipomuuliza wataka nikufanyie nini, alikuwa na jibu, ‘nataka nipate kuona’. Wewe unapokuwa umefunga unalenga nini ?unahitaji nini?

Usifunge kwa kufuata mkumbo, usikurupuke wala usiende kwa mazoea. Simama na ulilokusudia Mungu akufanyie.

Hatua ya pili; KUJITOA (COMMITMENT), NI GHARAMA GANI UTALIPA KWENYE MFUNGO WAKO.

Kufunga sio kitu rahisi. Gharama ya kitu inaonyesha uthamani ya kitu. Kila kazi ina faida yake, kuamka usiku wa manane na kuomba, si kitu rahisi lakini kuna faida yake na kufunga pia inahitaji kujitoa, nafsi, mwili, na roho yako. Kuna faida yake.

Mfano; ni lazima ujiulize, mfungo wangu ni wa siku ngapi, ni aina gani ya mfungo niutumie, nitakunywa maji au kavu, au nitakula matunda tu.

Mithali 14:23
Katika kila kazi mna faida;
Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

Unatakiwa utende kila kitu kwa unyoofu, ujiulize kwa mfungo huu ni vitu gani sitakiwi kuwa navyo, au nisifanye kitu gani? Ni vitu gani nitajitenge navyo, ni muda gani nitakuwa kwenye maombi, panga ratiba yako ya siku ya mfungo, je utaanza kusoma neno saa ngapi, utaomba saa ngapi, utamsifu Mungu muda gani, utafanya vita muda upi? Weka ratiba.

Mshahara unategemeana na kazi iliyofanyika, kiwango cha faida inategemeana na kiwango cha kazi, ni Gautama kiasi gani umeweka, itakupa matokeo makubwa zaidi.

Hatua ya tatu; JIANDAE KIROHO

Mithali 16:1
Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu;
Bali jawabu la ulimi hutoka kwa BWANA.

Juweke sawa na Mungu kabla hujaenda kufunga, unajiandaaje kiroho? Andaa moyo wako.

• Omba toba, yaani tengeneza na Mungu, wewe unajua udhaifu wako. Weka vizuri moyo, nafsi na mwili. Maandiko yanasema, Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe muwe kamili bila lawama.

• Samehe. Achilia watu ulioweka moyoni. Samehe watu unaokaa nao, unaoishi nao, ndugu zako, wakristo wenzako, watu wa kazini kwako. Usibebe watu moyoni, kumbuka unaenda kukutana na Mungu, aukute moyo wako uko safi na hali ya utulivu, yaani moyo una amani.

• Tafuta maandiko utakayosimama nayo kwenye mfungo wako. Kila hitaji lina maandiko yake. Mungu hajibu maombi tunayoomba, ila Mungu anajibu neno lake katika maombi.

Yeremia 1:12
Ndipo BWANA akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize.

Mungu angekuwa anajibu k**a tunavyoomba, basi tusingekuwepo, maana wapo watu wanaomba maombi mabaya, wanaomba ufe, ufukuzwe kazi, usifanikiwe, uharibikiwe, n.k.

Hatua ya nne; JIWEKEE RATIBA YAKO YA SIKU YAKO YA MFUNGO.

Asubuhi, mchana, jioni, usiku utafanya nini? Hakikisha unasimamia ratiba yako itimie, iende k**a ulivyopanga maana shetani ni mvurugaji, anaweza akaingiza ratiba zake ukajikuta hakuna ulichofanya kwa siku nzima.

Usiendeshwe na msisimko, mhemko, au kukurupuka. Wala usichokoze vita ambayo hujajiandaa nayo.

1 Wakorintho 14:40
Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.

Hatua ya tano; TARAJIA MATOKEO KWA KUONYESHA SHUKURANI.

Imba nyimbo za shukurani kwa kinywa chako.

Zaburi 149:6
Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao,
Na upanga mkali kuwili mikononi mwao.

ni muhimu na lazima uamini kwamba kuna kitu Mungu ametenda, kwa maombi uliyoomba kwake.

1 Wakorintho 15:58
Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.

Ndugu msomaji na mfuatiliaji wa somo hili mfungo wenye matokeo, kila unachofanya kwa uaminifu mbele za Mungu, sio bure, taabu ya kuamka usiku na kuomba sio bure, changamoto unazokutana nazo wakati wa kufunga na kuzishinda, sio bure kwa Mungu, utayaona matokeo, utaona hatua, utaona ushindi, na upenyo na baraka ya Mungu

Mungu akubariki, endelea kutafakari na kuishi katika maarifa haya. Amen.

Kwa msaada zaidi na maombezi fika kanisani, Hekalu la Neema, Bigwa-Morogoro. Au wasiliana nasi kwa simu 0689213966, au kipitia FACEBOOK: pastor Katana Mwangome M’baya, na kwa YOUTUBE:Pst Katana. Pia unaweza kutoa sadaka yako kwa Mungu kupitia M-pesa 0752119763 au Tigo-pesa 0654894607. Mungu akubariki. Amen.

JUMANNE:31-01-2023SOMO: NGUVU YA MAOMBI USIKU WA MANANEMHUBIRI:MCHUNGAJI KATANA MWANGOME M’BAYAKANISA: HEKALU LA NEEMA- ...
10/02/2023

JUMANNE:31-01-2023
SOMO: NGUVU YA MAOMBI USIKU WA MANANE
MHUBIRI:MCHUNGAJI KATANA MWANGOME M’BAYA
KANISA: HEKALU LA NEEMA- BIGWA-MOROGORO.

Siku inaanza saa sita usiku. Na usiku wa manane ni kuanzia saa sita hadi saa kumi alfajiri. Asubuhi na mapema inaanza saa sita Usiku hadi saa tisa. Usiku wa manane ni muda ambao ukiutumia kwa maombi unapata ushindi, lakini pia usiku wa manane ni mida ambayo ni migumu sana kuomba. Unahitaji kujikana ili uweze kushinda maombi ya usiku wa manane.

Wafilipi 4:13
Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu

Ukiwa na nidhamu katika maombi haya utaona vitu vikitokea maishani mwako, ukitaka upokee vitu vya tofauti na wengine anza kutenda au kuchukua hatua zaidi yaw engine. Usiku wa manane ni wito. Mungu anaalika watu , anasema inuka usiku ulalamike mbele za Mungu, kuna Baraka zinazimwa usiku wa manane.

Maombolezo 2:19
Inuka, ulalamike usiku,Mwanzo wa makesha yake;
Mimina moyo wako k**a maji usoni pa Bwana; Umwinulie mikono yako;
Kwa uhai wa watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa,
Mwanzo wa kila njia kuu.

Kuna vitu ambavyo huwezi kushinda mpaka uamke usiku wa manane uombe, Paulo na Sila walimsifu Mungu usiku wa manane milango ya gereza ikafunguka.

Kwanini usiku wa manane, watu ambao waliutumia usiku wa manane kwenye biblia;

Ibrahim
Mwanzo 19:27
Ibrahimu akatoka asubuhi kwenda mahali aliposimama mbele za BWANA,

Yakobo(Israel)
Mwanzo 28:18
Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha k**a nguzo, na kumimina mafuta juu yake.

Mungu mwenyewe alitenda kazi usiku.
Kutoka 12:29
Hata ikawa, usiku wa manane BWANA akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, tangu mzaliwa wa kwanza wa Farao aliyeketi katika kiti chake cha enzi, hata mzaliwa wa kwanza wa mtu aliyefungwa katika nyumba ya wafungwa; na wazaliwa wa kwanza wote wa wanyama.

Yesu kristo aliamka usiku wa manane
Marko 1:35
Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko.

Ukitaka kupokea vitu visivyo vya kawaida fanya vitu au amua kufanya vitu visivyo vya kawaida.

Maombi ya usiku wa manane ni ya muhimu sana kwa mtu aliyeokoka kwa sababu zifuatazo;

1). Madhabahu nyingi za shetani zinajengwa na kutiwa nguvu kwa kutoa sadaka zao (kafara). Hivyo maombi ya usiku wa manane kwa kutumia neno la Mungu na jina la Yesu unaweza kuzuia hizo madhabahu zisijengwe na kafara zao kuwa si kitu. Amka usiku wa manane kuomba ili upate ushindi wako na familia.

Kutoka 8:20
BWANA akamwambia Musa, Inuka asubuhi na mapema usimame mbele ya Farao; angalia! Atoka aende majini; kamwambie, BWANA asema, Wape watu wangu ruhusa waende zao, ili wanitumikie mimi.

2). Ndio wakati adui anaharibu hatima za watu. Huu ndio mda ambao hatima za watu zinaharibiwa ghafla. Shida za ghafla kwenye ndoa, kanisa, watoto, afya, kiuchumi, kikazi, n.k. Mambo yanayotokea ghafla maishani, yanatengenezwa na shetani, sio tu jambo la kawaida. Chukua hatua amka usiku wa manane omba Mungu utaona vitu hivyo vikitoweka.

Ayubu 34:24
Yeye huwavunja-vunja mashujaa pasina kuwachunguza,
Na kuwaweka wengine mahali pao

3). Ndio wakati adui anapanda magugu. Magugu ni mambo au tabia zinazoibuka ambazo hazikuwepo, sio za kawaida, hazipo ndani ya familia, mambo au tabia za kigeni zinaanza kuonekana ambazo hazikuzoeleka ndani ya familia au jamii. K**a vile kiburi, uongo,wizi, ghafla vinaonekana vikitenda kazi ndani ya mtu.

Mathayo 13:24-25
Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake; lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.

4). Ndio wakati adui hubadilisha hatima ya mtu. Unajikuta badala ya kwenda mbele unarudi nyuma, badala kuwa utajiri unarudi kuwa maskini, toka furaha kwenda huzuni, ujasiri kwenda mashaka, n.k. maandiko yanena wazi kuwa sisi ni uzao mteule.

1 Wafalme 3:19-21
Na mtoto wa mwanamke huyu akafa usiku, maana alimlalia. Akaondoka kati ya usiku, akamwondoa mtoto wangu ubavuni pangu, mimi mjakazi wako nilipokuwa usingizini, akamweka kifuani pake, na mtoto wake mwenyewe, aliyekuwa amekufa, akamweka kifuani pangu. Nilipoondoka asubuhi nimnyonyeshe mtoto wangu, kumbe? Amekufa. Hata asubuhi nilipomtazama sana, kumbe! Siye mtoto wangu niliyemzaa.

Walipokuwa wamelala usingizi ndipo akabadilishiwa mtoto. Amka usiku wa manane uombe tuondokane na kubadilishiwa hatima zetu katika jina la Yesu.

5). Ndio wakati adui hurusha mishale. Mshale ni kitu kinachokukea ghafla ambacho baadaye kikiondoka unabakia na kovu. Kupoteza ghafla, ulemavu wa ghafla, hasara ya ghafla, ajali ya ghafla, ugonjwa wa ghafla. Kuna uharibifu mkubwa unafanywa usiku, hutakiwi ulale tu, amka uombe. katika jina la Yesu.

Unapoamka usiku ufanyeje, au uombeje?

a). Amka mpe Mungu sifa na shukurani, licha ya taabu na changamoto zilizopo.
Zaburi 119:62
Katikati ya usiku nitaamka nikushukuru,
Kwa sababu ya hukumu zako za haki.

b). Amrisha siku yako, tabiria siku yako, ipe mwongozo, iandike kwa kinywa chako, itamkie na kuiamuru utakavyo, hatima yako iko kwa Mungu na wewe mwenyewe.

c). Pambana na kifungo cha msingi. Roho za familia, tabia, mizimu, zinazokufuatilia, pambana na malango ya familia, magonjwa, balaa, majanga ya kifamilia, pambana nazo, zikatae, zibomoe, zing’oe,ziharibu ziangamize kwa nguvu za Mungu zilizo ndani yako.

Familia yako ina misingi yake, na malango yake, lakini maombi ya usiku wa manane, yatatikisa misingi na kufungua malango yaliyofungwa katika jina la Yesu.
Matendo ya Mitume 16:25
Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.

d). Amka ung’oe, ubomoe, uharibu, malango ya kuzimu, malango ya mateso, kutokupiga hatua kwa jina la Yesu.
Waamuzi 16:3
Basi Samsoni akalala hata usiku wa manane, akaondoka katikati ya usiku, akaishika milango ya lango la mji, na miimo yake miwili, akaing’oa pamoja na komeo lake, akajitwika mabegani, akavichukua hata kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni.

e). Amka pambana na nguvu zinazoshikilia mji, mtaa, kijiji, n.k. watenge watendao uovu, wasijeamua mabaya juu yetu
Zaburi 101:8
Asubuhi hata asubuhi nitawaharibu
Wabaya wote wa nchi.
Niwatenge wote watendao uovu
Na mji wa BWANA.

f). Amka upate ufunuo wa kiungu. Ni wakati utasikia sauti ya Mungu ikisema nawe na kukupa maelekezo, ni wakati masikio yako yanaweza kusikia sauti ya Mungu.
Isaya 50:4
Bwana MUNGU amenipa ulimi wa hao wafundishwao, nipate kujua jinsi ya kumtegemeza kwa maneno yeye aliyechoka, huniamsha asubuhi baada ya asubuhi; huniamsha, sikio langu lipate kusikia k**a watu wafundishwao.

g). Ni wakatu wa kukutana na Mungu, maana Mungu anatafuta mtu.
Mathayo 25:6
Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.

h). Fanya maombi kwa watoto wako na familia; mtoto ana maeneo matatu ya kuombea;

• Hatima ya kiroho. Watoto wamjue Mungu wa kweli na kumcha katika maisha yao
• Hatima ya Elimu, watoto wapate elimu, wafaulu, wasonge mbele kielimu

• Hatima ya kiuchumi. Wajue njia za kutafuta pesa na sio kuomba tu na kusubiria, wajue pesa inatafutwa.

• Hatima ya ndoa. Wawe na ndoa njema ya kimungu baadaye maishani mwao.
Mathayo 11:5-6
vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.
Naye heri awaye yote asiyechukizwa nami.

Ndugu unaesoma somo hili, ni wakati wetu Mungu ametufunulia haya, tuamke usiku wa manane tuombe na kuutafuta uso wa Mungu wetu, nae atatusaidia. Amen. Ubarikiwe.

Kwa msaada zaidi na maombezi fika kanisani, Hekalu la Neema, Bigwa-Morogoro. Au wasiliana nasi kwa simu 0689213966, au kipitia FACEBOOK: pastor Katana Mwangome M’baya, na kwa YOUTUBE:Pst Katana. Pia unaweza kutoa sadaka yako kwa Mungu kupitia M-pesa 0752119763 au Tigo-pesa 0654894607. Mungu akubariki. Amen.

JUMAPILI: 29-1-2023Somo:JIFUNZE KUJIWEKEA HAZINA YAKO MBINGUNIMHUBIRI: MCHUNGAJI KATANA MWANGOME M'BAYA.KANISA: HEKALU L...
10/02/2023

JUMAPILI: 29-1-2023
Somo:JIFUNZE KUJIWEKEA HAZINA YAKO MBINGUNI
MHUBIRI: MCHUNGAJI KATANA MWANGOME M'BAYA.
KANISA: HEKALU LA NEEMA- BIGWA- MOROGORO

Mathayo 6:19-21
Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba; bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi; kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.

Ukifanya jambo lifanye kwa ajili ya utukufu wa Mungu, usifanye kitu ukitarajia kulipwa au kusifiwa na watu, ukifanya kwa Bwana, utapata baraka toka kwake. Usiweke tumaini lako kwa vitu ulivyonavyo, wala usifanye chochote kwa kutaka malipo. Kuweka hazina ni kudhamiria na kumtazama Yesu.

Imani ni njia ya Mungu ya kutenda kazi maishani mwetu, ni daraja la kupokea kutoka kwa Mungu.

Mashaka ni njia ya shetani ya kutenda kazi. Shetani anajua ukitoa kwa ajili ya Mungu utabarikiwa, hivyo anakuletea mashaka ili uone kumtolea Mungu ni kupoteza au hakuna faida. Kuwa na Mashaka ni kumdharau Mungu na neno lake.

Malaki 3:14
Mmesema, Kumtumikia Mungu hakuna faida; na, Tumepata faida gani kwa kuyashika maagizo yake, na kwa kwenda kwa huzuni mbele za BWANA wa majeshi?

Roho ya mashaka inaingizwa ndani yako ili uone hakuna faida kulishika neno la Mungu, na kuona wale watendao uovu ndio wenye heri.

Ili wewe upate baraka weka tumaini lako kwa Yesu, usiruhusu mashaka kuingia ndani yako. Mashaka yakiingia imani inaondoka.

Mungu ametupa mbegu ya imani, kazi ya kuikuza imani ni yako. Utaikuza imani yako kwa kulisoma neno LA Mungu na kuomba. Kitendo chochote cha imani kinaleta nguvu toka kwa Mungu.

Onyo kuhusu hazina.

Nafasi tuliyo nayo ni ya muda tu, kazi ni ya muda, mali tulizonazo ni za muda tu, kadhalika uzima,cheo,umri, ni wa muda tu. ... Muda huu mchache tuliyopewa weka hazina yako kwa Mungu kwa bidii. Kila mmoja wetu ni lazima atii maonyo ya Yesu na kujichunguza mioyoni mwetu k**a kuna ubinafsi na choyo.

Luka 12:15
Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.
Kuna watu wana choyo hadi kwa Yesu mwenyewe. Tumejisahau sana maana vitu vyote tulivyo navyo ni kwa ajili ya Mungu, vyote vyatoka kwake. Unafanya nini na mali aliyokupa Mungu?

Njia NNE za kuweka hazina mbinguni;

1). Kuwajali wajane, yatima na wasiojiweza. Watu wengi wameinua dini kuliko Mungu, majina ya watu yameinuliwa kuliko jina la Yesu.

Yakobo 1:27
Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.

Zaburi 68:5
Baba wa yatima na mwamuzi wa wajane,
Mungu katika kao lake takatifu.

2). Kusimama na watumishi wa Mungu hasa wazazi wa kiroho

2 Wafalme 4:8
Hata ikawa siku moja, Elisha alikwenda Shunemu; na huko kulikuwa na mwanamke mmoja mwenye cheo; naye akamshurutisha aje ale chakula. Ikawa kila alipopita njia ile, huingia kula chakula.

Wazazi wetu wa kiroho (wachungaji) wanamuwakilisha Mungu duniani, wazazi hawa sana agano na wewe,

Kuna baraka unapata kwa kuwategemeza watumishi wa Mungu.
Jifunze kuwapongeza watu wanapofanya vizuri. Peleka zaka kamili ili kiwepo chakula cha kutosha katika nyumba ya Mungu.

3). Jenga ufalme wa Mungu (Kusimama na huduma),
Huduma yeyote inayoendelea kuna watu wamesimama, kuna watu wana mzigo na huduma. Huduma sio mali ya mtu ni mali ya Mungu. Kuna watu wamewekeza kwa Mungu, wanategemeza huduma, wanajenga makanisa wengine hawajamjua Yesu, ila wamejifunza kuwekeza.
Hagai 1:4

4). Dhabihu/ Kujidhabihu

Warumi 12:1-2
Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.
Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

Mwili wako ni hekalu la Mungu. Mungu anakaa ndani ya mtu, hakai kwenye majengo yaliyojengwa kwa Mawe na matofali. Ibada yenye maana ni kwanza kudhabihu mwili wako, ya pili ni moyo wako, ya tatu ni zaka.

Malaki 3:10
Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema BWANA wa majeshi; mjue k**a sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.

Kwa msaada zaidi na maombezi, fika kanisani, Hekalu LA Neema, Bigwa Morogoro. Au wasiliana nasi kwa simu 0689213966, au kupitia FACEBOOK:Pastor Katana Mwangome M'baya, na kwa YOUTUBE: Pst Katana. Pia unaweza kutoa sadaka yako kwa Mungu kupitia M- pesa 0752119763 au Tigo-pesa 0654894607, Mungu akubariki. Amen

Address

Morogoro

Telephone

+255689213966

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Pastor Katana Mwangome M'baya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Pastor Katana Mwangome M'baya:

Share