Efatha Church Kihonda

Efatha Church Kihonda We bring the world to Jesus by the blood of Jesus

ALHAMISI YAKO IMEBARIKIWA.Mwanangu, MUNGU anamtafuta Mtu mmoja ambaye atakubali kufanya Mapenzi yake ili apate Kumbariki...
08/04/2021

ALHAMISI YAKO IMEBARIKIWA.

Mwanangu, MUNGU anamtafuta Mtu mmoja ambaye atakubali kufanya Mapenzi yake ili apate Kumbariki. Je Mtu huyo ni Wewe?

Mpende YESU, Mfurahishe YESU, Ishi Maisha MATAKATIFU.

Alhamisi yako IMEBARIKIWA.

2 Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya...
28/02/2021

2 Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.”

•Ya kale yamepita: Unapaswa kuwa Mpya katika kila kona ya Maisha yako; unakuta mtu namna ambavyo baba na mama yake walivyokuwa wanaishi mtindo ule ule wa maisha ndivyo na yeye anaishi, haya ni mambo ya kale, usifikiri kuwa namna ambavyo baba na mama yako waliishi ni nzuri kwako, la! bali ilikuwa kwao, haijalishi walikuwa wanaishi maisha mazuri kiasi gani ni kwa ajili yao na sio kwa ajili yako wewe unapaswa kuishi Maisha yako Mapya na Bora zaidi yao.

Chochote kinachokuvuta nyuma na kukushikilia na kukufanya k**a ni mtindo wa maisha lazima kiondoke kwako maana sio cha kwako bali unahitaji kuwa Mpya.

Mungu anaweza kufanya chochote utakacho au unachohitaji hivyo hakikisha ya kale yameenda, kwa sababu hauwezi kupata vitu kutoka kwa Mungu k**a ya kale yakiwa bado yamekushikilia.

Ukitaka kupata vitu kutoka kwa Mungu na ukitaka kuchanua, kustawi, kung’aa vinakuja tu kwa Neema ila hakikisha wewe ni kiumbe kipya na ya kale hakikisha hayakusumbui.
Tatizo ni kuwa watu hawajui ya kale, k**a hauyajui utaishi pamoja na hayo ya kale, je unajua mapya? K**a hauyajui hautakaa uyapate.

Katika dunia hii watu hawataki mambo mapya kwa sababu wanaogopa mabadiliko, k**a haupendi mabadiliko basi hautakaa uyapate mambo mapya na kamwe hauwezi kuwa mtu mpya.
Ukizaliwa upya unakuwa katika Neema ya Mungu na ukiwa katika hiyo Neema unaishia katika Utukufu.
Ya kale lazima yaende ili kuruhusu mapya yakujilie katika maisha yako, ndipo uweze kuona Utukufu wa Mungu katika maisha yako.

MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA – KANISA LA EFATHA MWENGE.

IBADA YA JUMAPILI  TAREHE 28/2/2021 – KANISA LA EFATHA MWENGE.MCHUNGAJI AIMANA DOMINICK.Zaburi 119:121-126 “Nimefanya hu...
28/02/2021

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 28/2/2021 – KANISA LA EFATHA MWENGE.
MCHUNGAJI AIMANA DOMINICK.

Zaburi 119:121-126 “Nimefanya hukumu na haki, Usiniache mikononi mwao wanaonionea. Uwe mdhamini wa mtumishi wako, apate mema, Wenye kiburi wasinionee. Macho yangu yamefifia kwa kuutamani wokovu wako, Na ahadi ya haki yako. K**a zilivyo rehema zako umtendee mtumishi wako, Na amri zako unifundishe. Mimi ni mtumishi wako, unifahamishe, Nipate kuzijua shuhuda zako. Wakati umewadia Bwana atende kazi; Kwa kuwa wameitangua sheria yako.”

Ukiamua kuzifuata sheria za Bwana YEYE ataanza kazi ndani yako na yule anayekuonea katika maisha yako kwa sababu ya kuzaliwa kwako atapewa tangazo la kutokukufuatilia tena, nawe ndipo utaona FURAHA na USTAWI katika maisha yako.

UKIRI:
Bwana wa Utukufu kwa gharama yoyote nimeamua kuzitii sheria zako, kwa ajili ya hilo usiniache mikononi mwa wanaonionea; leo naomba uwe mdhamini wangu ili nikale mema uliyoniandalia ili wenye kiburi wasiendelee kunionea.
Bwana ukanitendee leo ili niendelee kutunza maagizo yako, kwa maana wewe umesema katika Zaburi 119: 126 “Wakati umewadia Bwana atenda kazi;………” Eeh Bwana niko tayari kuona kazi unayokwenda kutenda kwangu ili wale waliokuwa wananionea kutokana na kuzaliwa kwangu wasinionee tena, kwa maana nimeamua kuzishika sheria zako.

Katika mwaka huu wa KUSONGA MBELE nifanye NISONGE MBELE katika kila eneo la maisha yangu na sio kuwa wa kushindwa, mgonjwa, wa kurudi nyuma, n.k, na nikapate yale yote ambayo Bwana umeniandalia. Huu ndio ukiri wangu kwako Bwana.

ALHAMISI YAKO IMEBARIKIWA.Mwanangu, zingatia yafuatayo na uyaweke katika Akili yako; Uwe MWAMINIFU kwa Madogo na Makubwa...
27/08/2020

ALHAMISI YAKO IMEBARIKIWA.

Mwanangu, zingatia yafuatayo na uyaweke katika Akili yako; Uwe MWAMINIFU kwa Madogo na Makubwa, Uwe MTII na Mwenye KUJITOA. Unapozingatia hayo, MUNGU anakutazama.

YESU Anakupenda.

IJUMAA YAKO IMEBARIKIWA.Mwanangu; Amua kushinda nawe UTASHINDA. Ishi Maisha ya Kumfurahisha MUNGU naye kamwe hatakuacha....
21/08/2020

IJUMAA YAKO IMEBARIKIWA.

Mwanangu; Amua kushinda nawe UTASHINDA. Ishi Maisha ya Kumfurahisha MUNGU naye kamwe hatakuacha. Hivyo mfanye MUNGU akufurahie kwa kuamua kuishi Maisha Matakatifu.

YESU Anakupenda, YESU Anakujali.

JUMATANO YAKO IMEBARIKIWA.Mwanangu, kwa jinsi unavyozingatia Mambo ya Mungu, ndivyo atakavyokujali. Usiwapendeze Wanadam...
19/08/2020

JUMATANO YAKO IMEBARIKIWA.

Mwanangu, kwa jinsi unavyozingatia Mambo ya Mungu, ndivyo atakavyokujali. Usiwapendeze Wanadamu bali Mpendeze Mungu.

Ishi Maisha MATAKATIFU Mwanangu, BABA Anakupenda, BABA Anakuwazia Mema, fuata ninachokuelekeza.

Yesu anakupenda, Yesu anakujali ishi maisha matakatifu.
18/08/2020

Yesu anakupenda, Yesu anakujali ishi maisha matakatifu.

IBADA YAJUMAPILI 16/08/2020SOMO: RUHUSU CHANGAMOTO ZIKUZALIE FAIDAMCHUNGAJI  RACHEL SUSULEChangamoto yoyote yaweza kukuz...
18/08/2020

IBADA YAJUMAPILI 16/08/2020
SOMO: RUHUSU CHANGAMOTO ZIKUZALIE FAIDA
MCHUNGAJI RACHEL SUSULE

Changamoto yoyote yaweza kukuzalia faida K**a utazingatia. Changamoto ni mlango wa wewe kutoka. changamoto inakufanya Uwe imara. Yaweza kuwa una changamoto nyingi lakini usiogope, muamini Mungu kuwa unaweza kukabiliana nazo na hakikisha kila changamoto unaipangua kwa kuipa majibu.
Mbinguni hawaingii walioshindwa, mbinguni wanaingia washindi tu.
Kuna watu waliopitia changamoto fulani wakashinda na ikawazalia faida, muhimu ni kukubali kuwa juu ya hao unaowaona ni maadui leo maana hao ndio watakaokuzalia faida na kukupeleka kwenye ustawi wako.

TUONE WALIOPOKEA CHANGAMOTO KWA SHUKRANI
1. Tunasoma habari za Yusufu alipitia changamoto akashinda akastawi Sana. Kwa nini Yusufu alistawi Sana kwa sababu alikubali kupokea changamoto, alijua Mungu atakuwa pamoja nae.

Mwanzo 39:2-4
Matendo 7:9-10

Changamoto ya Yusufu ni ushuhuda Hadi leo ilimpelekea kuwa mtu mkuu.
Wakati mwingine changamoto inakuingiza darasani ujifunze jambo kupitia hicho unachopitia. Mungu akiona umepokea kwa Moyo wa SHUKRANI anakuwa pamoja nawe. Wakati mwingine Mungu anataka kukuletea ustawi, utajiri, Mali na mambo mazuri.
Swali je upo tayari kupokea changamoto kwa Moyo wa shukrani?

Zaburi 117:1-3Haleluya.Enyi mataifa yote, msifuni Bwana, Enyi watu wote mhimidini.Maana fadhili zake kwetu sisi ni kuu,N...
17/08/2020

Zaburi 117:1-3
Haleluya.
Enyi mataifa yote, msifuni Bwana,
Enyi watu wote mhimidini.
Maana fadhili zake kwetu sisi ni kuu,
Na uaminifu wa Bwana ni wa milele.

IBADA YA JUMAPILI 16/08/2020Mtumishi Benny Nzulunge akiongoza maombi katika Ibada
17/08/2020

IBADA YA JUMAPILI 16/08/2020

Mtumishi Benny Nzulunge akiongoza maombi katika Ibada

Address

Kihonda
Morogoro

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Kihonda posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share