18/02/2024
MAAMUZI YA MTU KUMILIKI
Na MCH: PAULO DOTTO
Ili mtu aweze kumiliki ni lazima azikane njia zake zote potofu na kufata maagizo ya Mungu maana yeye ndiye mpaji
Danieli 3:28
Nebukadreza akanena, akasema, Na ahimidiwe Mungu wa Shadraka, na Meshaki, na Abednego; aliyemtuma malaika wake, akawaokoa watumishi wake waliomtumaini, wakaligeuza neno la mfalme, na kujitoa miili yao ili wasimtumikie mungu mwingine, wala kumwabudu, ila Mungu wao wenyewe.
👉Ili kuweza kumiliki, mtu anahitaji kuingia ghalama kubwa ya vile alivyonavyo
🤲Mathayo 19:15-22
[15]Mtu Aliyekuwa Tajiri
[16]Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele?
[17]Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri.
[18]Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo,
[19]Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako k**a nafsi yako.
[20]Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena?
[21]Yesu akamwambia, Ukitaka kuwa mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.
[22]Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.