28/05/2026
NewDay-NewPower
Prayer Devotion
Thu 28 May
ESTA MWANAMKE SHUJAA WA MAOMBI
Sijui unawaza nini unaposikia jina Esta; ila mimi huwa nawaza dada fulani mnyenyekevu ila shujaa wa imani ndani yake; dada aliyekuwa na shauku ya Mungu ya kila siku.
🫶 Esta alimpenda Mungu na alimwamini Mungu; na alikuwa na shuhuda za kutosha kuhusu Mungu; kufunga na kuomba ilikuwa ni sehemu ya maisha yake.
🏹 Alikuwa na ufahamu kuhusu vita vya kiroho; alijua chochote mbele yake ni Mungu anakiongoza; ila pia alijua ili kuishinda mizimu ya Umedi na Uajemi basi ilihitaji kufunga na kuomba.
💥 Alitoa uzoefu wa maombi kwa Mordekai ambaye aliposikia habari mbaya akavaa magunia ishara ya kunyenyekea mbele za Bwana; ila Esta alienda mbali zaidi; alijumrisha na kufunga; tena alifundisha wajakazi wake wote; nina hakika na watoto wake; kuhusisha maombi na kufunga.
🧨🔥 Haleluya, maombi yamebeba nguvu; maombi yamebeba kibali; kwa maombi esta akapa kibali toka kwa Bwana; kibali ambacho hakiwezi shindwa popote na hakiwezi zuiliwa na yoyote.
🧡♥️ Kwenye maombi tunakusanya harufi nzuri kutokea kwa Bwana (Ufunuo 8:1-5) na hapo tunapata neema toka kwa Bwana (Ebra 4:12) hiyo inazalisha kibali kwenye maisha yetu.
🎻🎉 kwa kibali hiko; Esta akapita mbele ya mfalme; kinyume cha sheria; akamsh*taki yule adui wa Wayahudi Hamani; akaangamiza kizazi chake chote; akageuza huzuni ya Wayahudi kuwa sherehe.
UNATAKA KIBALI TOKA KWA BWANA; MAOMBI LAZIMA YAWE NI MAISHA YAKO.
Maombi ya Leo;
Eh! Bwana Yesu naomba nijalie neema ya kufunga na kuomba; usiniache pasipo kibali chako. AMEN 🙏
GOD ANSWERS PRAYERS
+255 683477827