Pastor Ulenje

Pastor Ulenje HII NI ZAIDI YA PAGE
NI MADHABAHU YA KUPOKEA UAMSHO WA MAOMBI NA MIUJIZA.
2025 Mungu anataka sana Kanisa kurejesha Matumaini yao katika Maombi.

Karibu Tujifunze na Tuombe Pamoja.

NewDay-NewPower Prayer Devotion Thu 28 MayESTA MWANAMKE SHUJAA WA MAOMBISijui unawaza nini unaposikia jina Esta; ila mim...
28/05/2026

NewDay-NewPower

Prayer Devotion
Thu 28 May

ESTA MWANAMKE SHUJAA WA MAOMBI

Sijui unawaza nini unaposikia jina Esta; ila mimi huwa nawaza dada fulani mnyenyekevu ila shujaa wa imani ndani yake; dada aliyekuwa na shauku ya Mungu ya kila siku.

🫶 Esta alimpenda Mungu na alimwamini Mungu; na alikuwa na shuhuda za kutosha kuhusu Mungu; kufunga na kuomba ilikuwa ni sehemu ya maisha yake.

🏹 Alikuwa na ufahamu kuhusu vita vya kiroho; alijua chochote mbele yake ni Mungu anakiongoza; ila pia alijua ili kuishinda mizimu ya Umedi na Uajemi basi ilihitaji kufunga na kuomba.

💥 Alitoa uzoefu wa maombi kwa Mordekai ambaye aliposikia habari mbaya akavaa magunia ishara ya kunyenyekea mbele za Bwana; ila Esta alienda mbali zaidi; alijumrisha na kufunga; tena alifundisha wajakazi wake wote; nina hakika na watoto wake; kuhusisha maombi na kufunga.

🧨🔥 Haleluya, maombi yamebeba nguvu; maombi yamebeba kibali; kwa maombi esta akapa kibali toka kwa Bwana; kibali ambacho hakiwezi shindwa popote na hakiwezi zuiliwa na yoyote.

🧡♥️ Kwenye maombi tunakusanya harufi nzuri kutokea kwa Bwana (Ufunuo 8:1-5) na hapo tunapata neema toka kwa Bwana (Ebra 4:12) hiyo inazalisha kibali kwenye maisha yetu.

🎻🎉 kwa kibali hiko; Esta akapita mbele ya mfalme; kinyume cha sheria; akamsh*taki yule adui wa Wayahudi Hamani; akaangamiza kizazi chake chote; akageuza huzuni ya Wayahudi kuwa sherehe.

UNATAKA KIBALI TOKA KWA BWANA; MAOMBI LAZIMA YAWE NI MAISHA YAKO.

Maombi ya Leo;

Eh! Bwana Yesu naomba nijalie neema ya kufunga na kuomba; usiniache pasipo kibali chako. AMEN 🙏


GOD ANSWERS PRAYERS

+255 683477827

NewDay-NewPowerPRAYER DEVOTION Tue 26 May🔥 UKIONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU UTAFANIKIWA 🔥Watu wengi wanatafuta mafanikio kup...
26/05/2026

NewDay-NewPower

PRAYER DEVOTION
Tue 26 May

🔥 UKIONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU UTAFANIKIWA 🔥

Watu wengi wanatafuta mafanikio kupitia nguvu zao, akili zao, elimu, au mahusiano yao; lakini mafanikio ya kweli yanapatikana pale mtu anapoongozwa na Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu si nguvu tu, bali ni uwepo wa Mungu unaomwelekeza mwanadamu katika kusudi, amani, ushindi, na uhusiano wa kweli na Yesu Kristo.

1️⃣ Roho Mtakatifu ni wa zamani sana zaidi yako — alikuwepo kabla ya Adamu na kabla ya misingi ya dunia kuwekwa.

📖 Mwanzo 1:2 SUV
“Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.”

Kabla mwanadamu hajaumbwa, kabla dunia haijakamilika, Roho wa Mungu tayari alikuwepo. Anaijua mwanzo na mwisho kwa sababu alikuwa pale tangu mwanzo.

2️⃣ Roho Mtakatifu ana ufahamu wote kuhusu maisha yetu na kusudi la Mungu juu yetu.

📖 1 Wakorintho 2:10-11 SUV
“Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu.”

Roho Mtakatifu anajua hatima yako, wito wako, mapambano yako, na mpango kamili wa Mungu juu ya maisha yako. Ukimruhusu akuongoze, lazima ufikie hatima yako.

3️⃣ Roho Mtakatifu anajua namna ya kutimiza kusudi la Mungu ndani yetu,

📖 Warumi 8:14 SUV
“Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu.”

📖 Yohana 14:26-27 SUV
“Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote…”

Unataka kufikia kusudi la Mungu huwezi kwepa kutengeneza nidhamu ya kuongozwa na Roho Mtakatifu kwenye maisha yako.

4️⃣ Furaha ya kweli inapatikana katika Roho Mtakatifu.

📖 Warumi 14:17 SUV
“Maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu.”

Furaha ya Roho Mtakatifu haitegemei mazingira. Ni furaha inayotoka kwa Mungu mwenyewe, inayobaki hata wakati wa majaribu. Haleluya.

5️⃣ Uhusiano wetu na Kristo unashikiliwa na Roho Mtakatifu.

📖 Yohana 16:13-14 SUV
“Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote…”

“Yeye atanitukuza mimi…”

Bila Roho Mtakatifu, mtu hawezi kutembea kwa ukaribu wa kweli na Kristo. Yeye ndiye anayemfunua Yesu ndani yetu, anatubadilisha kufanana naye, na kuweka mioyo yetu karibu na Kristo.

✨ Ukijisalimisha kwa Roho Mtakatifu kila siku, atakuongoza kwenye maamuzi sahihi, atakulinda, atakutia nguvu, na atakupeleka kwenye mafanikio ya kweli katika kila eneo la maisha yako. Maisha salama na yenye ushindi ni maisha yanayoongozwa na Roho wa Mungu.

📖 Wagalatia 5:16 SUV
“Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.”

Maombi ya Leo:
Roho Mtakatifu nakupenda sana; naomba uongoze maisha yangu katika amani ya kweli, na kwenye njia ya kufikia kusudi la Mungu. Amen 🙏

pastorUlenje
GOD ANSWERS PRAYERS
+255 683477827

NewDay-NewPower PRAYER DEVOTION Wed 20 MayWEWE AMINI TU.Mk 9:23 SUVYesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aamin...
20/05/2026

NewDay-NewPower

PRAYER DEVOTION
Wed 20 May

WEWE AMINI TU.

Mk 9:23 SUV
Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.

Hakuna neno zuri na gumu kwenye Biblia k**a hili; maana unaweza fikiri umelielewa kumbe "hapana"

🤔 Kwa uelewa Yesu hakusema Yote yanawezekana; bali kasema "Yote yanawezekana kwake aaminiye.

Kuamini hapo ndiyo mada kuu ya Yesu.

🙆‍♂️ Tatizo ni moja Yesu anataka kuamini pasipo mashaka.

Mk 11:23 SUV
"...wala asione shaka moyoni mwake...

😞 Fikiri Petro mbele ya Yesu mashaka yalimzamisha.

Mbele ya Yesu Kristo, Petro alianza vizuri kutembea juu ya maji baada ya kuamini neno la Yesu; lakini alipoona shaka; akazama - Math 14:30.

🤔 Mashaka yanakuja pale unapoanza kuwaza itakuwaje/itatokeaje?

Unapoanza kuwaza itakuwaje/itatokeaje hapo ndipo unaanza kuona ugumu na ukubwa wa hitaji na mapito yako; hapo ndipo mashaka yanakuja na kuvamia moyo wako - 2 Wafalme 6 na 7.

🤨 Unamkumbuka yule akida wa mfalme mwenye mashaka?

Alimwambia Elisha _"...Tazama, k**a BWANA angefanya madirisha mbinguni, je! Jambo hili lingewezekana?_ 2 Fal 7:2; kwanini alisema hivi? Ni kwa sababu alitazama uwezekano wa jambo hakumtazama Mungu.

🙌 Itawezekanaje/Itatokeaje ni sehemu ya Mungu siyo yako.

Wengi wanakonda na kuwa wanyonge sababu wanatazama itatokeaje/itawezekanaje; hiyo ipo kwenye kiwango cha akili ya Mungu siyo yako; yeye ndiye anajua muujiza wako utatokeaje.

👉 Haina maana usitumie akili zako.

Kuna yale ambayo Mungu anataka kutumia akili ambayo amekupatia; katika hayo ni utukufu kwa Mungu ukitumia akili; ila tazama usizitegemee akili zako hapo utavuka mipaka ya makusudi ya Mungu kukupatia akili na utaingia kwenye mashaka.

Nakushauri

Badala ya kuumiza kichwa itakuwaje; wewe nyenyekea Kwake Mungu Yeye atakupa akili ya kufanya na atakusaidia majibu kutokea.

Maombi ya Leo;

Nakuombea sana Bwana akupe moyo wa utulivu wa kuamini; hata eneo unaona shaka leo Roho wa imani akujaze imani.


GOD ANSWERS PRAYERS
+255 683 477827

🔥

NewDay-NewPowerPRAYER DEVOTION Tue 19 MayMSTARI HUU UKIUTENDEA KAZI UNA MAJIBU YAKO.📚 Mt 21:22 SUV_Na yo yote mtakayoyao...
19/05/2026

NewDay-NewPower

PRAYER DEVOTION
Tue 19 May

MSTARI HUU UKIUTENDEA KAZI UNA MAJIBU YAKO.

📚 Mt 21:22 SUV
_Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea._

Kuna vitu vitatu vya kujifunza kwenye huu mstari.

🙏 Mtakayo-yaomba

Yesu alimaanisha kitu pekee utakachoomba; kuna msemo unasema "Mungu ni mwenye zote ila hawezi kujibu maombi ambayo hayajaombwa"

🎻 Anasema katika "Sala"

Yesu alitaka si tu maombi (deēsis) bali alitaka sala (proseuchē) kwa maneno mengine sala ni jumla ya ibada nzima; maombi yakiwa ndani yake - Mungu anataka umwimbie tenzi, na zaburi, nyimbo za rohoni, anataka ushirika na wewe; hapo sasa weka na maombi yako ya kumsihi sana Mungu - Efeso 5:19-20.

🫶 Anasema "mkiamini"

Hapa ndipo sehemu muhimu sana; wengi wanasahau "si tu kuomba bali kuomba na kuamini" sababu maombi pasipo kuamini ni maneno tu ya kawaida; imani ndiyo inafanya maneno ya kawaida kuwa maombi.

🤔 Kuamini ni kuamini ulichoomba umekipokea; hapo utapokea.

Weka kumbukumbu katika yale uliomba alafu ukaamini kuwa yametokea; na ukaanza kuwa na furaha hata kabla hujaona; ukashangilia kabla hata hayajatokea; ukawatangazia watu bila woga kana kwamba unayo tayari - kumbuka - kwa imani ile "yalitokea" hata hili la sasa jitie wazimu wa imani k**a ule utaona hakika utakuwa na majibu yako - Marko 11:23-24

👍 Imani ni Practical siyo theoretical.

Imani ni vitendo vya moyo; siyo majaribio ya mawazo; hatuwazi kutokea tukasema ni imani; bali tunatenda kuwa imetokea hiyo ndiyo imani- utaona matendo yako na hisia zako za moyo zimebadirika hapo utajua umeamini.

🔥 Nakushauri.

Ukiingia kuomba usiseme amina mpaka hisia za moyo wako zimebadirika kutoea mashaka kuwa imani - Flp 4:6-7 haina maana imani ni hisia bali ukiamini amani inakuja.

Ukifanya haya Yesu anasema "Majibu yako yatakuwa yako. Hallelujah.

Maombi ya Leo;

Nakuombea leo yule Roho wa imani; azalishe imani ndani yako isiyotikiswa na dhoruba yoyote; imani yenye kukupa matokeo kwa Jina la Yesu - 2 Kor 4:3


GOD ANSWERS PRAYERS
+255 683 477827

🔥

NewDay-NewPower Prayer DevotionMon 18 May👏🔥KUWA JASIRI KUSUBIRI.⏰️Natamani leo kushare nawe mambo kumi nimejifunza kuhus...
18/05/2026

NewDay-NewPower

Prayer Devotion
Mon 18 May

👏🔥KUWA JASIRI KUSUBIRI.⏰️

Natamani leo kushare nawe mambo kumi nimejifunza kuhusu kusubiri;

> “Umngojee Bwana; uwe hodari, moyo wako upate nguvu; Naam, umngojee Bwana.” — Psalms 27:14

👑 Uwe jasiri kusubiri.

Mungu bado anatenda kazi hata katika nyakati ambazo inaonekana hakuna kinachoendelea.
— Isaiah 64:4

😞 Kusubiri si udhaifu.

Ni imani inayochagua kuutumainia wakati wa Mungu kuliko plesha ya maisha.
— Ebr 10:36

🫶 Uwe jasiri kumngoja Mungu.

Majibu yaliyochelewa si maombi yaliyokataliwa; Bwana siku zote hawezi kutoa ambacho haja-kikamilisha.
— Filp 1:6

🥰 Wakati mwingine Mungu hukuza roho yako katika msimu wa kusubiri.

Kabla hajabadilisha hali yako, kwanza huimarisha moyo wako.
— Rum 5:3-4

⏰️ Chumba cha kusubiri cha Mungu hakijawahi kuwa tupu bila kufanya chochote.

Unahisi hakupi chochote wakati unasubiri kumbe anakupa tabia mpya, ufahamu mpya, misuri mipya wakati unasubiri
— Yer 33:3

🎵 Uwe jasiri kubaki mwaminifu wakati unasubiri.

Abudu unapongoja, imba nyimbo na tenzi; Omba unapongoja. Tumaini unapongoja. Mungu huheshimu watu wa namna hiyo
— Gal 6:9

♥️ Unapomngoja Bwana, husubiri peke yako.

Uwepo wake hutembea pamoja nawe katika kila wakati; akikubeba pale nguvu zako zinapoonekana kuwa ndogo.
— Kumb 31:8

⏰️ Ahadi za Mungu haziishi kwa sababu ya muda.

K**a amesema, atatimiza. Ujasiri ni kuendelea kuamini hata pale mchakato unapokuwa mrefu; mchakato mrefu kwa Mungu si adhabu ni kutufanya bora zaidi.
— Hes 23:19

🤔 Uwe jasiri kusubiri ukiwa na tumaini.

Mungu aliyefungua milango hapo kabla anaweza kuifungua tena. Hadithi yako bado ipo mikononi mwake.
— Ufu 3:8

🤴 Kusubiri pamoja na Mungu siku zote kuna kusudi.

Kuna watu wanasubiri sababu si Mungu anataka kukupa ulichoomba bali a ataka akupe kusudi lake.
— Mhu 3:11

Maombi ya Leo;
Nakuombea kwa Jina la Yesu Bwana akupe ujasiri na uhodari katika wakati wako huu wa kusubiri; sababu majibu yanakuja hakika. Amen 🙏


GOD ANSWERS PRAYERS
+255 683 477827

🔥

NewDay-New PowerPRAYER DEVOTIONSun 17 MayUSIHANGAIKE, OMBA 🙌“Kamwe Mungu hakukusudia ubebe mizigo yako peke yako. Maombi...
17/05/2026

NewDay-New Power

PRAYER DEVOTION
Sun 17 May

USIHANGAIKE, OMBA 🙌

“Kamwe Mungu hakukusudia ubebe mizigo yako peke yako. Maombi ni badilishano la kiungu ambapo unampa Mungu mahangaiko yako na kupokea amani Yake.”
— Kenneth E. Hagin

Wafilipi 4:6 inatukumbusha kuwa wasiwasi haupaswi kutawala moyo wako bali maombi ndiyo uyape nafasi kuteka moyo wako.

“Imani hukua unapozungumza na Mungu zaidi kuliko unavyozungumza kuhusu matatizo yako.”
— Kenneth Copeland

Watu wengi hutumia muda mwingi kuyakuza matatizo yao kuliko kumkuza Mungu; hii inakuzalishia hofu na kuondoa nguvu yako ya kuomba.

“Maombi si chaguo la mwisho kwa mwamini; ni mwitikio wa kwanza wa imani.”
— Kenneth E. Hagin

Usianze kwanza kujisumbua kutatua tatizo ndipo uombe; omba kwanza Mungu ndiye akupe mbinu ya kutatua tatizo; hapo utakuwa na amani na ushindi utapatikana.

“Shukrani hufungua mlango wa amani kutawala ndani ya roho yako.”
— Kenneth Copeland

Wafilipi 4:6 haisemi tu kuhusu maombi na dua, bali pia inaagiza kushukuru. Sababu shukrani ina nguvu sana kubadirisha hari ya moyo na kuupa nguvu mpya ya kuendelea kuomba na kushindana hata kushinda.

“Maombi yenye imani yanapopaa mbinguni, mioyo yenye amani huzaliwa duniani.”
— Kenneth E. Hagin

Mungu hajaahidi kuwa waamini hawatapitia changamoto, lakini ameahidi amani na ushindi na kuwa pamoja nao katikati ya changamoto hizo; na kuwa utukufu wa mwisho kuwa mkubwa zaidi.

Asante
kcm.org
Kenneth Copeland Ministry

Ulenje
GOD ANSWERS PRAYERS

🔥

04/07/2025
25/06/2025

SIKILIZA MPAKA MWISHO UPATE SIRI YA KUJIBIWA MAOMBI YAKO YA MUDA MREFU.

21/06/2025

Haya Unayakosa k**a Utakata tamaa

17/06/2025

KWANINI WENGI WANAOMBA HAWAPATI
Sikiliza kwa makini utapata majibu kwanini wengi wanaomba na hawapati majibu ya maombi yao.

Utapata kujua mambo ya msingi ili kuanzia leo uanze kupokea majibu ya maombi yako.

Kujiunga na kundi la maombi ingia link hii https://chat.whatsapp.com/JBDpnf9X9R5DtRxuHw5MO0

10/06/2025

Swali kubwa naulizwa kila sehemu “Pastor mimi naomba sana ila sioni matokeo; Karibu kujifunza siri hii hakika utaenda viwango vingine. Karibu Darasa la Maombi kila siku ya Jumatatu, Jumatano, na Alhamisi Tutajifunza na Kuomba Pamoja. # #

Address

Kihonda Viwandani
Morogoro

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Pastor Ulenje posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share