27/08/2024
IBADA NA IMANI
Kuna vitu vinatafakarisha kuhusu ibada na imani. Kuna kawaida ambayo ipo watu kuzifunika imani zingine, na hili wingu lipo kubwa kwa nyakati za sasa.
Sehemu kubwa sasa zinafanyika ibada zao tena kwa ushawishi mkubwa huku mioyo ya watu ikivutwa huko. Macaptain wao kabla ya kunyanyua kombe ibada kwanza. Uwe wa upande ule au ule kwa tendo hili umeshiriki ibada yao na usipokuwa na macho ya mbele utaona jambo hili ni la kawaida ila linaathiri sana upande huu.
Wasemaji wao wote ni wa imani na kila wanapoongea wanatumia salamu ya kiimani, bila kujali kuna imani tofauti tofauti. Wanaenda mbali zaidi wanatumia nafasi zao kuipa nguvu imani moja, wanatumia nafasi zao kutangaza mambo ya imani yao. Huwezi ona madhara sasa ila kwa baadaye ni hatari sana kwa imani nyingine.
Matajiri wa hizo timu wote wanaimani zao, na wanaziendesha hizo timu kwa imani yao, na wanapenyeza imani yao kwa kutumia nguvu kubwa na akili nyingi mno.
Wachezaji wao likifungwa goli imani mbele, wanapewa matangazo mengi kukuzwa majina yao, hata wakiwa wa kawaida ila tu kwa sababu wanatumika kiimani.
Wakiitwa sehemu hata k**a si za ibada huvaa mavazi ya kiimani na kutoa salamu za kiimani.
Wakati imani hii inayoshambuliwa kwa kiasi kubwa ikitumiwa kuwashambulia wale watoto wao waliowakuza kwa kuwachafua ili wadhohofike. Ile imani imeinua watu wenye akili sana na wameshawasambaza kila sehemu, wengi sasa ni viongozi wa imani hii inayoshambuliwa. Wamewawekea mtazamo kuwa washirika wenu wanahama wanahamia kwa watoto wenu, na sasa imani inayoshambuliwa. Inazishambulia imani zenzake ndogo, kwa kuwaonyesha kwa jamii kana kwamba hawafai na wasisikilizwe.
Kumekuwa na mahojiano ya viongozi wa imani ambayo inashambuliwa, yenye matamko ya ukakasi kwa imani inayoshambuliwa. Chakushangaza inatumika nguvu kubwa kutangaza matamshi ayo yanayoleta ukakasi. Ukijiuliza kwa nini? Jibu unakuja kupata imani moja inashambulia imani nyingine ili wajijenge kitaifa kila sehemu.
Hatutakiwi kulinda dhehebu tunatakiwa kulinda imani, hatutakiwi kuwalinda watu tunatakiwa kuzilinda imani zao. Hata k**a mtu alikuwa kwako akatoka, kuujenga mwili wa Kristo na bado yupo kwenye imani ile ile alindwe na asaidiwe na sio kuwapa nguvu wale wa ile imani.
Imani inapigwa, imani inatikiswa, imani inabomolewa na baada ya miaka 6 tu mbele hali itakuwa mbaya sana kwa hii imani inayopigwa.
MTU ALIKUWA ANANISIMULIA NIKIWA NIMELALA KWENYE SGR KUTOKEA MORO KUJA DAR ASUBUHI YA LEO.