Efatha Church Mbinga

Efatha Church Mbinga NENO EFATHA LILITAMKWA MARA MOJA TU NA BWANA YESU KATIKA KITABU CHA MARKO 7:34. MBINGA FUNGUKA. Nini kinafanyika? Kuwafanya watakatifu wawe na umoja.
6. HALELUYA!

Saa imefika ya kuileta injili halisi ya YESU KRISTO wilayani Mbinga. Mungu alipomuita Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira kwa kazi ya kuliandaa kanisa lenye NGUVU ili hatimaye Injili iwaokoe waliokusudiwa, kwa wakati na majira yake sasa tumefika Mbinga. Kuikomboa Mbinga na watu wake Kutoka madhalimu yote ya shetani Kupitia mahubiri ya Neno la Imani, k**a Biblia isemavyo "Imani chanzo chake ni k

usikia na kusikia huja kwa Neno la Kristo" WARUMI 10:17. Kwa kuwa wengi wanampenda Yesu Kristo hivyo tunafundisha mafundisho maalum ya kukulia wokovu, na jinsi ya kuishi na Nguvu ya ROHO MTAKATIFU ambaye ndiye chanzo cha Hekima, maarifa na Mafinikio Yote ya Mwanadamu. Huduma ya Efatha ni maono aliyopewa Mtumishi wa Mungu, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira ambayo ndani yake kuna kusudi la Kiungu. Ili kufanikisha kusudi hilo, MUNGU alimpa Mtume na Nabii vipengele 10 vya kutekeleza ambavyo kwa pamoja ndivyo vinavyoumba Huduma ya Efatha.
1. Kuikomboa Tanzania ili iweze kusimama mbele za kiti cha hukumu na kupokea baraka za MUNGU.
2. Kuliandaa kanisa la YESU KRISTO kwa ajili ya kunyakuliwa lisilo na mawaa wala makunyazi.
3. Kufanya Kanisa la YESU KRISTO liwe na Mamlaka.
4. Kudhihirisha uweza katika KRISTO YESU, kwa Ishara, Miujiza, Uponyaji na Ukombozi wa Roho, Nafsi na Mwili.
5. Kumzalia BWANA matunda yaani kuwaleta watu kwa YESU.
7. Kupokea vipawa vya MUNGU k**a mahitaji yetu, ROHO MTAKATIFU, lugha mpya na kuvigawa.
8. Kusimamia kazi ya MUNGU na kuruhusu maongozi ya ROHO MTAKATIFU yaweze kutenda kazi.
9. Kuhakikisha kuwa malango ya kuzimu yananyamazishwa.
10. Kuwa tayari wakati unaofaa na usiofaa kuhubiri NENO la MUNGU

Usisite, njoo ukutane na Neno lenye kukutoa shimoni yaani dhambini. MBINGA MBINGUNI NI KUWA NA YESU.

Haleluya!!  Wapendwa katika Bwana, tunapenda kuwajulisha kuwa tumefungua Page yetu mpya ya Facebook yenye jina la Efatha...
25/02/2024

Haleluya!!

Wapendwa katika Bwana, tunapenda kuwajulisha kuwa tumefungua Page yetu mpya ya Facebook yenye jina la Efatha church mbinga.
Muonekano wake ni k**a kwenye picha hii.
Mungu wa Efatha awabariki sana.
Amen!!

Kwa msaada zaidi: 0754711034/0753028805
ICT: 0625858883/0687804040

FOLLOW, LIKE AND COMMENT

11/02/2024

TAREHE 11/02/2024 -

MAPOKEZI YA MCHUNGAJI
KANISA LA EFATHA MBINGA

Unapopigania Ufalme wa Mungu unasababisha moyo wake uwe pamoja na wewe. Kwa nini Daudi hakuuawa na adui zake? Kwa sababu...
26/11/2023

Unapopigania Ufalme wa Mungu unasababisha moyo wake uwe pamoja na wewe. Kwa nini Daudi hakuuawa na adui zake? Kwa sababu moyo wake ulikuwa tayari kupambana kwa ajili ya Bwana. Unapoupigania Ufalme wa Mungu ndipo Mungu anakupigania na wewe.
1 Samweli 17:1-27 “……….Yule Mfilisti akasema, Nayatukana leo majeshi ya Israeli; nipeni mtu tupigane. Basi Sauli na Israeli wote waliposikia maneno hayo ya Mfilisti, wakafadhaika na kuogopa sana…….….”

Hapa unaona majeshi ya Israel chini ya Sauli yalikuwa tayari kusalimu amri kwa majeshi ya Wafilisti; lakini kijana mdogo aitwaye Daudi aliposikia aliingiwa na wivu wa Mungu ndani yake na akawa tayari kupambana kwa ajili ya Mungu. Hauwezi kupigania Ufalme wa Mungu ikiwa haumpendi.

Matendo 13:22 “Na alipokwisha kumwondoa huyo, akamwinua Daudi awe mfalme wao ambaye alimshuhudia, akisema, Nimemwona Daudi, mwana wa Yese, mtu anayeupendeza moyo wangu, atakayefanya mapenzi yangu yote.”

Huwezi kuupigania Ufalme wa Mungu isipokuwa mapenzi ya Mungu yapo juu yako. Ukiwa tayari kupigana kwa ajili ya Ufalme wa Mungu utamfanya Yeye ajivunie wewe, Mungu alifanya hivyo wakati wa Ayubu, Musa na Daudi.

Ukiwa na mapenzi na Mungu utakuwa tayari kupambana kwa ajili yake na kamwe hautapoteza mpambano kwa maana Yeye atakuwa pamoja na wewe wakati wote. Yabebe mapenzi ya Mungu ndani yako nawe utakuwa mshindi usiku na mchana na utasababisha watoto na wajukuu zako wafanikiwe.

Ukipigana kwa ajili ya Mungu wako, taa yako haitakoma, watoto wa watoto wako watang’aa milele na milele. Mahali pa kazi utang’aa, dukani kwako, biashara na hata shuleni kwako utang’aa.

MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA Kuna mambo unayofanya na matokeo yake unamsababisha Mungu aseme na kufanya  jambo...
26/11/2023

MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Kuna mambo unayofanya na matokeo yake unamsababisha Mungu aseme na kufanya jambo kwako. Isaya 65:24 “Na itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.” Hii ina maana gani? Mungu hajibu kwa sababu umesema, Bali ni kwa sababu umefanya jambo ndipo unamsababisha Yeye aseme au atende kwako. Kumsababisha Mungu asimame kwa ajili yako lazima umchokoze kwanza, mfanye Yeye atende kwako kwa kufanya jambo katika ufalme wake.

Mungu anasikia maombi ya wengi wakiomba lakini anawajibu wachache, kwa nini? Kwa sababu kuna mambo ambayo unapaswa kufanya.

K**a unataka kumgusa Mungu na kumfanya atende kwa ajili yako unapaswa kufanya yafuatayo:-

1. Utoaji wa kupitiliza matarajio au kilichotarajiwa.
Kwa nini malkia wa sheba utoaji wake unakumbukwa mpaka leo? Kwa sababu alitoa kuliko matarajio yaliyotarajiwa. Utoaji wa ziada ndio unaomchokonoa Mungu na humsababisha akuulize unataka nikutendee nini? Kuna mambo mengine unaweza kuomba sana lakini Mungu hatajitokeza mpaka utoe zaidi ndipo utamsababisha ajitokeze kwako na kukuuliza unataka nikutendee nini?
• 2 Nyakati 1:7-13 “Usiku ule Mungu akamtokea Sulemani, akamwambia, Omba utakalo nikupe. Sulemani akamwambia Mungu, Umemfanyia baba yangu Daudi fadhili kuu, nawe umenimilikisha mimi badala yake. Basi sasa, Ee Bwana Mungu, na limyakinie baba yangu Daudi neno lako; maana umenitawaza niwe mfalme juu ya watu wengi k**a mavumbi ya nchi..........”

Suleiman alitoa zaidi na hata akaugusa moyo wa Mungu ndipo Mungu akauliza unataka nikufanyie nini? Usimtolee Mungu kwa sababu unacho cha kutoa bali toa zaidi ili kuugusa moyo wa Mungu na kusababisha Mungu atende kwa ajili yako.

2. Unapoijenga nyumba ya Bwana Mungu wako utukufu unakuwa ni wa kwako. 2 Mambo ya Nyakati 7:1-3 “ Basi Sulemani alipokwisha maombi hayo, moto ukashuka kutoka mbinguni, ukateketeza sadaka ya kuteketezwa na dhabihu; utukufu wa Bwana ukaijaza nyumba. Wala makuhani hawakuweza kuingia nyumbani mwa Bwana, kwa kuwa utukufu wa Bwana umeijaza nyumba ya Bwana………..”

Unapoacha kila kitu ili kuijenga nyumba ya Bwana Yeye atakutakasa wewe na kila kitu kinachokushika na kukusumbua na kukutoa katika kuwa mateka na hata kukufanya uwe utukufu kwake. Ukitaka kuuona utukufu wa Mungu kwako hakikisha unaijenga nyumba ya Mungu. Utukufu wa Mungu ni ulinzi wako. Ukielewa hili hakuna anayeweza kukuangamiza kwa maana utukufu wa Mungu unakuwa upo juu yako ili kukulinda.

ASKOFU THABO MASENYA KUTOKA AFRIKA YA KUSINI: Zaburi 30:11 “Uligeuza matanga yangu kuwa machezo; Ulinivua gunia, ukanivi...
26/11/2023

ASKOFU THABO MASENYA KUTOKA AFRIKA YA KUSINI:

Zaburi 30:11 “Uligeuza matanga yangu kuwa machezo; Ulinivua gunia, ukanivika furaha.” Watu wengi wanapitia katika magumu au mabaya lakini huo sio mpango wa Mungu; kila aina ya ubaya, huzuni au maumivu uliyokutana nayo acha Bwana akayaondoe na akuletee furaha na mashangilio katika maisha yako.

Neno la Mungu linasema “Uligeuza matanga yangu kuwa machezo;” Katika matanga yoyote uliyokutana nayo katika maisha yako Mungu akalete mazuri kwako.

Biblia inasema kuwa “Bwana hufurahia katika ustawi wa watumishi wake” Mungu anafurahia ustawi wa watumishi wake, ustawi wowote utakaokutana nao fahamu kuwa utamfurahisha Mungu, Mungu kamwe hafurahii unapoteseka, Bali anafurahi pale ambapo wewe unastawi.

Ibilisi amewaaminisha wengi ya kuwa kumtumikia Mungu ni mateso, lakini Biblia inasema kuwa “Yesu alipitia mateso ili sisi tuweze kuwa na furaha” Ni mapenzi ya Mungu juu yako ya kuwa upitie katika mazuri na ustawi na siyo magumu. Mungu anataka upitie katika ustawi na siyo umaskini, nia ya Mungu katika maisha yako ni kwamba uweze kuona mazuri yake mahali unapoishi na sio kupitia katika maumivu na huzuni.

Hakuna sababu ya wewe kusherekea ustawi wa Mungu utakapofika mbinguni, la! Bali utafurahia hapa hapa duniani kwa maana Yesu amekwisha kulipa gharama yake ili wewe uishi maisha mazuri huku duniani.

K**a ustawi wako umeshikiliwa kuzimu, leo Baba yangu wa mbinguni akakufanye ukawe huru kutoka katika kila mtego wa ibilisi; kwa maana sio mpango wa Mungu wewe ung’ang’ane; acha baraka za Mungu alizokuwekea zikafunuliwe kwako kwa Jina la Yesu na ukazifurahie.

USHUHUDA:MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRAMimi pamoja na mke wangu tunapenda kumshukuru sana Mungu kwa kutujalia ku...
26/11/2023

USHUHUDA:

MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA
Mimi pamoja na mke wangu tunapenda kumshukuru sana Mungu kwa kutujalia kutimiza miaka 30 ya ndoa. Mungu amekuwa mwema sana kwetu kila iitwapo leo na ameyafanya maisha yetu kuwa baraka kwa wengi.

Kuachana ni jambo baya sana lakini kupendana ni kuzuri. Ili muweze kusameheana na kuchukuliana; upendo unahitajika, bila upendo kamwe hamtaweza. Ukiona mtu hawezi kusamehe fahamu kuwa hana upendo.

Mungu ni pendo na ukiona mtu anasamehe fahamu kuwa anaupendo na k**a anasamehe jua kuwa ana Mungu. Ukiona mtu ameshindwa kusamehe jua kuwa hana Mungu na k**a hana Mungu basi hana pendo.

MAMA ELIAKUNDA MWINGIRA:
Mungu ni mwema sana, namshukuru Mungu kwa pendo lake na fadhili zake kwetu mpaka kufikia siku hii ya leo tumefikisha miaka 30 ya ndoa.

Namshukuru sana Mungu kwa kunipa mume mzuri anayenipenda na kuniheshimu. Kitu kinachofanya watu wawe pamoja ni upendo.
Wengine wanapokaa miaka mingi wanachokana, mwanangu Mungu asikupe kumchoka mwenzi wako, k**a mlianza katika pendo maana pendo halihesabu mabaya halijivuni na halikosi kuwa na adabu. Mungu akupe neema ya hilo pendo.

Nawatakia wote mlioolewa mkawe na maisha mazuri ya ndoa na wale ambao hamjaolewa Mungu akawape wenza sahihi na mkafurahie maisha yenu ya ndoa.

MATUKIO KATIKA PICHA KWENYE SEMINA EFATHA CHURCH MBINGA.
09/11/2023

MATUKIO KATIKA PICHA KWENYE SEMINA
EFATHA CHURCH MBINGA.

MATUKIO KATIKA PICHAKIKAO CHA VIONGOZIEFATHACHURCH KILOSA,
09/11/2023

MATUKIO KATIKA PICHA
KIKAO CHA VIONGOZI
EFATHACHURCH KILOSA,

8/11/2023        SEMINA YA NENO LA MUNGU NA MTUMISHI WAMUNGU JOSIAH MGONJASOMO:MAFINIKIO*Mafanikio ni kufikia matarajio ...
08/11/2023

8/11/2023
SEMINA YA NENO LA MUNGU
NA MTUMISHI WAMUNGU JOSIAH MGONJA

SOMO:MAFINIKIO
*Mafanikio ni kufikia matarajio unapo timizamalengo hayo ndio mafanikio
*Mafanikio nikufikia malengo uliyo jiwekea

Waefeso 1:3
[3]Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;

USTAWI;
"USTAWI NIKUWANA MAFANIKIO YAKIROHO NA KIMWILI

AKILI TATU 3 UNAZOTAKIWA KUWANAZO

1,AKILI YA MOYONI
2,AKILI YA KICHWANI
3,MATOKEO YAMAKUBALIANO YAAKILI HIZO MBILI

Kutoka 35:35
[35]Amewajaza watu hao akili za moyoni, ili watumike katika kazi kila aina, ya mwenye kuchora mawe, na kazi ya werevu, na ya mwenye kutia taraza, katika nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri, na ya mwenye kufuma nguo; ya hao wafanyao kazi yo yote, na ya wenye kuvumbua kazi za werevu.

Mithali 3:1-4
[1]Mwanangu, usiisahau sheria yangu,
Bali moyo wako uzishike amri zangu.
[2]Maana zitakuongezea wingi wa siku.
Na miaka ya uzima, na amani.

[3]Rehema na kweli zisifarakane nawe;
Zifunge shingoni mwako;
Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.

[4]Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri,
Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu.

"Kipawa kinakupa kufanikiwa katika dam nanyama,

10/09/2023
IBADA YA JUMAPILI TAREHE 3/9/2023MCH. KASOLE MAYEYESOMO: MAJIRA NA WAKATIMwanzo 1Katika siku saba za uumbaji Mungu alifa...
03/09/2023

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 3/9/2023
MCH. KASOLE MAYEYE

SOMO: MAJIRA NA WAKATI

Mwanzo 1

Katika siku saba za uumbaji Mungu alifanya kila jambo kwa siku yake katika siku zote saba.

Kuna kusudi la kuumbwa kwetu ni lazima utambue kuwa Mungu amekuumba kwa kusudi gani.
Ukilijua kusudi la kuumbwa kwako utafanya kila jambo kwa majira na wakati wake.

Mhubiri 3:1
Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.

Ukifanya jambo lolote nje ya kusudi la kuumbwa kwako haliwezi kufanyikiwa.

Mathayo 11:12
Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.

Tangu miaka 2023 iliyopita hadi sasa katika ufalme wa Mungu kuna mvitano katika roho, hivyo wenye nguvu katika ulimwengu wa roho ndiyo wataweza kuteka ufalme wa Mungu.

Waefeso 5:14-17
Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza. Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si k**a watu wasio na hekima bali k**a watu wenye hekima; mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu. Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.

Wakolosai 4:5
Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati.

Wakati haurudi nyuma inatupasa kuukomboa wakati kwa kufanya mambo ndani ya kusudi ulilokusudiwa.

Zaburi 90:12
Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima.

Yakobo 4:13-16
Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida; walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka.Badala ya kusema, Bwana akipenda, tutakuwa hai na kufanya hivi au hivi. Lakini sasa mwajisifu katika majivuno yenu; kujisifu kote kwa namna hii ni kubaya.

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 20/2023/2023 MAMA MCHUNGAJI: CATHERENI MAYEYEISAYA 9:6[6]Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, ...
20/08/2023

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 20/2023/2023
MAMA MCHUNGAJI: CATHERENI MAYEYE

ISAYA 9:6

[6]Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa,
Tumepewa mtoto mwanamume;
Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake;
Naye ataitwa jina lake,
Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu,
Baba wa milele, Mfalme wa amani.

"Muamini mungu wako ili uishi maisha mazuli lazima uishi sawasawa nakusudi lamungu
"Inafika wakati majalibu lazima yaje ili uweze kufanikiwa
"Ukishamuamini mungu vyote unavyotaka anakupa

1 Samweli 2:8

[8]Humwinua mnyonge kutoka mavumbini,
Humpandisha mhitaji kutoka jaani,
Ili awaketishe pamoja na wakuu,
Wakakirithi kiti cha enzi cha utukufu;
Kwa maana nguzo za dunia zina BWANA,
Naye ameuweka ulimwengu juu yake.

Danieli 11:32
[32]Na wao wafanyao maovu juu ya hilo agano atawapotosha kwa maneno ya kujipendekeza; lakini watu wamjuao Mungu wao watakuwa hodari, na kutenda mambo makuu.

*Ukifanyavyema lazima upate kibali

Ezekieli 16:53
[53]Nami nitawarudisha watu wao waliofungwa; wafungwa wa Sodoma na binti zake, na wafungwa wa Samaria na binti zake na wafungwa wako waliofungwa kati yao;

Kutoka 23:25
[25]Nanyi mtamtumikia BWANA, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako.

Address

Precious Area, Kihaha
Mbinga
TZA

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 17:00
Sunday 00:00 - 17:00

Telephone

+255754711034

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Mbinga posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share