PENDO LIsilo Kifani

PENDO LIsilo Kifani Tunajifunza kweli za msingi kwa ajili ya umilele

Yohana 8:32
tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kwel

SADAKA ISIYO NA KIFANI YA MJANE MASKINIKristo aliwakaripia wenye kuharibu mali, lakini alikuwa mwangalifu kwa watu wanao...
23/07/2025

SADAKA ISIYO NA KIFANI YA MJANE MASKINI

Kristo aliwakaripia wenye kuharibu mali, lakini alikuwa mwangalifu kwa watu wanaotimiza wajibu wao kuhusu kutumia mali. Matumizi mabaya ya matoleo ya Mungu yasingelizuia mibaraka ya Mungu kutoka kwa mtoaji.

Yesu alikuwa ukumbini, akiwatazama waliokuwa wakitoa sadaka zao. Matajiri walileta fedha nyingi kwa majivuno. Yesu aliwatazama kwa masikitiko ila hakusema neno kuhusu sadaka zao kubwa. Mara moja uso wake uling'aa alipomwona mjane mmoja maskini akija kwa kusitasita kana kwamba anawaogopa watoaji.

Aliangalia sadaka yake katika mikono yake. Ilikuwa ndogo sana kulinganisha na sadaka za wengine, walakini ilikuwa ndiyo yote aliyo nayo. Aliweka vipande viwili vya fedha kwa haraka, akaondoka. Alipofanya hivyo alikutanisha macho na Yesu aliyekuwa akimwangalia kwa makini.

Mwokozi aliwataka wanafunzi wake wamwangalie mjane huyu maskini. Kisha maneno yake ya sifa yakasikika masikioni mwa yule mjane. "Hakika nawaambia huyu mjane maskini: ametia zaidi kuliko wote." Machozi ya furaha yakamlengalenga, alipofahamu kuwa sadaka yake imekubalika. Watu wengi wangalimshauri kuwa aache kutoa, atumie tu maana isingelitambulikana miongoni mwa sadaka nyingi za thamani kubwa zilizoletwa katika hazina. Lakini aliamini kuwa huduma ya hekaluni imeamuriwa na Mungu, naye alitaka kuisaidia huduma hiyo kwa kadiri awezavyo. Alitenda alivyoweza, na sadaka yake ilikuwa ukumbusho wakati wote, na furaha yake ya milele. "Ametia zaidi kuliko wote." Sadaka kubwa ya matajiri haikuwa ya kujinyima, kwa hiyo haikuweza kuhesabika kwa thamani k**a ile ya mjane maskini.

Nia huongoza matendo yetu, ikiyafanya yawe mazuri au yawe mabaya. Matendo madogo yatendwayo kwa furaha, na sadaka zitolewazo bila majivuno, huwa ya thamani mbele za Mungu. Mjane maskini alijinyima chakula chake ili kutoa senti mbili hizo kwa kazi aliyoipenda sana. Alifanya hivyo kwa imani, akiamini kuwa Baba wa mbinguni hawezi kumnyima riziki yake. Huduma hii isiyokuwa ya ubinafsi, na imani k**a ya mtoto mdogo, ilisifiwa na Mwokozi.

Watu wengi miongoni mwa maskini hutamani kuonyesha shukrani zao kwa Mungu kwa ajili ya neema yake na kweli yake. Watu k**a hao hebu na wakusanye senti zao chache na kuziweka katika hazina ya mbinguni. Ikiwa watazitoa kwa moyo mkunjufu, uliyojaa upendo wa Munngu, vitu vidogo hivi vikitolewa sadaka, Mungu huvifurahia na kuvibariki.

Yesu aliposema kwa mjane yule kuwa, "Ametia zaidi kuliko wote", maneno yake yalikuwa ya kweli, siyo kwa nia tu, bali pia kwa matokeo ya sadaka yake. Zile senti mbili hizo zilizoletwa hazinani, zilizidi matoleo ya Wayahudi matajiri. Sadaka ndogo hiyo imekuwa kijito kilicho panuka na kuzidi kima kwa karne zote. Kwa njia elfu elfu mbali mbali imekuwa msaada kwa wenye dhiki, na kuitegemeza injili. Kielelezo chake cha kutoa kwa kujinyima kimeigwa katika nchi zote na watu maelfu katika kila karne.

Mbaraka wa Mungu kwa sadaka ile ya mjane umeifanya kuwa na matokeo makubwa sana. Ndiyo ilivyo na kwa sadaka zote zitolewazo kwa utukufu wa Mungu. Matokeo yake hayahesabiki na mwanadamu
"Ole wenu Waandishi na Mafarisayo, wanafiki, kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani adili na rehema na imani, hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache." Yesu hakuacha kuhimiza mambo ya lazima. Kulipa zaka kuliamuriwa na Mungu nako kulitekelezwa tangu mwanzoni. Ibrahimu alilipa zaka katika mali zake zote. Mpango wa kulipa zaka jinsi Mungu alivyouweka ulikuwa safi na wa haki, lakini Makuhani na Walimu walikuwa wameufanya kuwa mzigo wa kusumbua.

Mafarisayo walikuwa wakilipa zaka kamili ya mazao ya bustani zao, k**a bizari, jira na mboga. Vitu hivyo viligharimu kidogo sana, na hivyo kuwapa sifa kwamba ni waaminifu kweli kweli. Lakini mambo makuu ya sheria, k**a vile adili, rehema, na ukweli waliyaacha. Kristo alisema: "hayo imewapasa kuyafanya wala yale mengine msiyaache.

"Mambo mengine ya sheria yalikuwa yamepotoshwa kwa jinsi hiyo na Walimu. Maagizo aliyoagizwa Musa, k**a kula nyama ya nguruwe, na wanyama wengineo waliokatazwa yalitolewa ili kuepukana na maradhi na hivyo kufupisha maisha. Lakini Mafarisayo walipita kiasi. Watu waliambiwa wachuje maji yote yasije yakawa na wadudu, ambao wangehesabiwa sawa na wanyama wachafu. Yesu akilinganisha haya mambo madogo madogo na dhambi zenyewe hasa aliwaambia Mafarisayo "Viongozi vipofu, wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia."

"Mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu, na uchafu wote." Makaburi meupe yaliyopambwa yalificha maozea yaliyomo ndani yao. Ndivyo ilivyokuwa kwa makuhani na wazee waliokuwa wakionekana kwa nje k**a wanyofu, walificha uovu ndani yao.
Yesu aliendelea kusema: "Mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki, na kusema: K**a sisi tungalikuwepo zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao katika (kumwaga) damu ya manabii". Hivyo mwajishuhudia wenyewe kuwa ninyi ni wana wa wale waliowaua manabii".

Ushirikina wa kuheshimu makaburi ya watakatifu ulidumishwa na fedha nyingi zilitumika katika kuyapamba. Machoni pa Mungu hii ilikuwa ni ibada ya sanamu. Ilionyesha kuwa hawakumpenda Mungu hata kidogo, wala jirani zao k**a nafsi zao. Leo watu wengi hawawajali wajane, na yatima, wagonjwa na maskini, ili kutoa gharama ya kujenga minara ya kumbukumbu kwa ajili ya watu. Wajibu kwa waliohai,wajibu ambao Kristo ameuagiza kwa dhati umeachwa bila kutendeka.

Mafarisayo walisema wao kwa wao: K**a sisi tungaliishi siku za baba zetu, tusingalishirikiana nao kumwaga damu za watumishi wa Mungu. Lakini wakati ule ule walikuwa wakipanga kumwua Mwana wa Mungu. Jambo hili linapasa kufunua macho yetu tuone jinsi Shetani anavyowadanganya watu na kuwatoa katika njia ya kweli. Wengi hushangaa kwa upofu wa Wayahudi wa kumkataa Kristo. Husema: K**a sisi tungaliishi siku hizo za Kristo, tusingelishiriki katika hatia ya wale waliomkataa Mwokozi, lakini watu hawa wanapotakiwa kumtii Mungu na kuishi maisha yasiyokuwa ya ubinafsi, hukataa kufanya hivyo. Hudhihirisha roho ile ile ya Mafarisayo.

Wayahudi hawakutambua hata kidogo matokeo ya kutisha ya kumkataa Kristo. Katika kila kizazi manabii walipaza sauti zao kuwaonya watawala, wakuu, na watu, na hivyo wakihatarisha maisha yao katika kumtii Mungu. Kumekuwako na kurundikana kwa adhabu ya kufisha wale walioikataa nuru na kweli. Kwa kumkataa kwao Mwokozi makuhani na watawala walijihusisha na damu ya watakatifu wote kutoka Habili mpaka hadi Yesu mwenyewe. Wayahudi walikuwa karibu kukijaza kikombe chao cha uovu. Na karibu kitamwagwa vichwani mwao katika kulipiza haki. Kwa ajili ya hayo Yesu aliwaonya akisema: "hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki hata damu ya Zakaria na bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu Amini nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.

"Waandishi na Mafarisayo walijua jinsi nabii Zakaria alivyouawa. Wakati alipokuwa akinena onyo kutoka kwa Mungu, ghadhabu ya kishetani ilimchochea mfalme mwovu na kwa amri yake nabii akauwawa. (Tazama 2 Nyakati 24:18-22). Damu yake ilikuwa imejigandisha katika mawe ya hekalu, na kuwa ushuhuda wa uasi wa Israeli. Kadiri hekalu litakavyodumu kuwako, doa la damu hiyo itakuwa ikilia mbele za Mungu ili ilipiziwe kisasi. Yesu alipozighusia dhambi hizi, hofu kuu iliwajaza watu.

Yesu alipoona ugumu wa mioyo ya Wayahudi, alisema kuwa hali yao ya ugumu wa moyo itakuwa sawa k**a ilivyokuwa wakati uliopita.
"Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii, na wenye hekima, na Waandishi: na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulubisha; na wengine wao mtawapiga masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji. "Yesu alitamka maneno haya ya adhabu hali mikono yake ikiwa imeinuliwa mbinguni, na nuru ya Uungu ikimfunika, Kristo alinena hayo k**a jaji katika kukemea na hukumu. Wasikilizaji wake walitetemeka sana. Hali ya mvuto na maneno yake ilikuwa ya nanma isiyoweza kufutika kabisa.

Chuki ya Kristo hasa iliekezwa kwa dhambi zinazotendwa na watu wakijiharibu wenyewe, na kuwadanganya wengine na kumdharau Mungu. Lakini hakunena maneno ya kulipiza kisasi. Hakudhihirisha hasira yo yote. Huruma ya kimbingu ilionekana usoni pa Mwana wa Mungu, alipolitazama mara moja hekalu na kisha wasikilizaji wake. Kwa sauti iliyojawa na huzuni na majonzi mazito alitamka, "'Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! ni mara ngapi nimetaka kuwa kusanya Pamoja watoto wako, k**a vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka." Katika maombolezo ya Kristo, moyo wa Mungu uliguswa. Hivyo ilikuwa kwaheri ya kisirisiri ya uvumilivu wa upendo wa Mungu.
Mafarisayo na Masadukayo walinyamazishwa kimya. Yesu aliwakusanya wanafunzi wake wakatoka hekaluni, akiwa siyo k**a mtu aliyeshindwa, bali k**a ambaye ametimiza kazi yake. Aliondoka akiwa mshindi kutoka katika pambano.

Katika siku hiyo yaajabu, katika mioyo mingi mawazo mapya yalichipuka, na, historia mpya ikaanza. Baada ya kusulubishwa na kufufuka, watu hawa walijitokeza mbele wakiwa na hekima na bidii. Walikuwa na ujurnbe uliowavutia watu. Mbele ya ushuhuda wao dhana na falsafa za wanadamu zilikuwa hadithi za kubuni.

Lakini Israeli k**a taifa lilikuwa limejitenga kutoka kwa Mungu. Akiangalia ndani ya hekalu kwa mara ya mwisho, Yesu alisema kwa huruma na kuomboleza! "Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa. Kwa maana nawambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana." K**a vile Mwana wa Mungu alivyozitoka zile kuta, Utukufu wa kuweko Mungu utaondolewa milele kutoka, katika hekalu lililojengwa kwa ajili ya utukufu wake. Tamasha zake hazitakuwa na maana, huduma zake zitakuwa dhihaka

YESU AZURU HAKALU MARA YA MWISHOIlikuwa siku ya mwisho ya Yesu kufundisha hekaluni. Kijana wa Kigalilaya alisimama, akiw...
22/07/2025

YESU AZURU HAKALU MARA YA MWISHO

Ilikuwa siku ya mwisho ya Yesu kufundisha hekaluni. Kijana wa Kigalilaya alisimama, akiwa hali ya kawaida tu. Akizungukwa na makuhani wenye hali ya kitajiri sana, na wakuu wenye mavazi ya fahari sana na mapambo ya kila hali, na Waandishi wakishikilia mkononi mwao magombo waliyoyafunua kila mara. Yesu alisimama kimya k**a mwenye kuvikwa uwezo wa kimbingu.
Aliwakodolea macho adui zake, waliokuwa na uchu wa uhai wake. Mitego yao ya kutaka kumnasa ikiwa imeshindwa. Alikuwa amekutana na maswali mbali mbali, akitoa majibu safi ya hakika, kinyume cha giza la makosa ya Mafarisayo na Makuhani. Maonyo yalitolewa kwa uaminifu. Walakini ilibakia kazi nyingine kwa Kristo, kufanya.

Watu walikuwa wamefurahishwa na mafundisho yake, ingawa walikuwa na wasiwasi. Walikuwa wakiwatumaini Makuhani na Waalimu, lakini sasa wanawaona watu hawa wakimwinda Yesu, kumdhalilisha ambaye maarifa yake yalitoa nuru ya kila shambulio. Walishangaa kwa kuwa Makuhani na Marabi hawakumwamini Yesu, ambaye mafundisho yake yalikuwa dhahiri na rahisi kueleweka. Wao wenyewe hawakujua njia ya wima ya kufuata.

Katika mifano, lilikuwa kusudi la Kristo kuwaonya wakuu na kuwafundisha watu ukweli. Lakini ilikuwa ni lazima kusema kwa wazi zaidi. Kutokana na imani yao duni kwa ukuhani, uliopotoshwa, watu walikuwa wametekwa. Kristo lazima akate minyororo hii. Alisema: "Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa, basi yo yote watakayowaambieni myashike na kuyatenda, lakini msiwaige jinsi wanavyokuwa, maana kwao hunena tu, wala hawatendi hivyo wanavyonena."

Waandishi na Mafarisayo waliamua kukichukua kiti cha Musa, wakiwa k**a ndio wenye kufundisha sheria, lakini hawakufanya k**a sheria isemavyo. Na walifundisha mengi yaliyo kinyume cha Maandiko Matakatifu. Wao hufunga Mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitende wenyewe kugusa kwa kidole chao. Hufundisha sheria, na kuwalazimisha watu wazishike, wao hujidai kusamehewa wasitenda hivyo.

"Tena matendo yao yote huyatenda ili kutazamwa na watu; kwa kuwa hupanua hirizi zao, huongeza matamvua yao; hupenda viti vya mbele katika karamu, na kuketi mbele katika masinagogi, na kusalimiwa masokoni, na kuitwa na watu Rabi. Bali ninyi msiitwe Rabi, maana mwalimu wenu ni mmoja, nanyi nyote ni ndugu. Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoia, aliye wa mbinguni. Wala msiitwe viongozi; maana kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo."

Katika maneno ya wazi k**a hayo Mwokozi alidhihirisha tamaa ya ubinafsi iliyokuwa inajikweza kutaka makuu kila mahala, huku ikionyesha kejeli ya unyofu, na huku moyo umejaa wivu na choyo. Mafarisayo walikuwa wakitafuta kwa kila hali kujionyesha na kujipendelea. Mambo k**a hayo yalikemewa na Yesu.
Alikemea ubatili uliyoonyeshwa katika kutamani kuitwa Rabi, au Bwana. Makuhani, Waandishi na Wazee, wote walikuwa ni ndugu, watoto wa Baba mmoja. Watu hawakupaswa kumpa mtu ye yote heshima ya kuwafanya watawaliwe nia zao, au imani yao.

K**a Kristo angelikuwako ulimwenguni leo, akizungukwa na watu wenye majina ya heshima k**a vile Mstahiki (Reverend), au Mstahiki Sana (Right Reverend), je, asingaliurudia usemi wake kwamba Msiitwe bwana, kwa kuwa mnaye Bwana mmoja ndiye Kristo?" Maandiko Matakatifu humtaja Mungu kuwa, jina lake ni Takatifu na la kuogopwa." (Zaburi 119:9). Watu wangapi hujiita kwa jina hilo linalomhusu Mungu na huku wakiwakilisha vibaya jina na tabia yake. Mara ngapi tamaa za kidunia na dhambi mbaya kabisa zimefichwa ndani ya vazi la cheo cha juu na kitakatifu!

Mwokozi aliendelea kusema: "Atakaye kuwa mkubwa wenu, atakuwa mtumishi wenu. Atakaye-jikuza atashushwa, na atakayejidhili atakuzwa." Kristo alifundisha mara nyingi kwamba, ukuu wa kweli hupimwa katika hali ya unyofu. Mbele ya mbingu ukuu halisi hupimwa kwa jinsi mtu anavyowahudumia wanadamu wenzake. Kristo ambaye ni Mfalme wa utukufu alikuwa mtumishi wa wanadamu wenye dhambi.

"Mnawafungia watu wasiingie katika ufalme wa mbinguni, ninyi wenyewe hamwingii, na wanaotaka kuingia mnawazuia." Kwa njia ya kuyapotosha Maandiko Matakatifu makuhani na wanasheria waliwazuia watu wasielewe njia ya kuingia katika ufalme wa mbinguni.

"Mnakula nyumba za wajane, na kwa unafiki mnaomba sala ndefu; kwa hiyo mtapokea hukumu iliyo kubwa zaidi." Mafarisayo walipata heshima ya wajane watauwa, na walifanya kuwa ni kawaida yao kuchukua vitu vyao kwa ajili ya makusudi ya dini. Baada ya kupata fedha zao walizitumia kwa faida yao. Ili kujificha na upotovu wao waliomba sala ndefu sana na kujionyesha kuwa ni watu wa dini kamili. Makaripio ya aina hiyo yanawahusu watu wa sasa pia. Maisha yao yamejaa ubinafsi na uovu, walakini hujifunika na vazi la dini, waonekane kana kwamba ni wenye dini halisi.

UFUFUO WA WAFU, FUNDISHO LENYE UTATABaina ya Mafarisayo na Masadukayo, fundisho la ufufuo wa wafu lilikuwa jambo la utat...
29/08/2024

UFUFUO WA WAFU, FUNDISHO LENYE UTATA

Baina ya Mafarisayo na Masadukayo, fundisho la ufufuo wa wafu lilikuwa jambo la utata mkubwa. Mafari-sayo waliamini kabisa fundisho la ufufuo wa wafu, lakini fikara zao kuhusu hali ya baadaye ya wafu zilikuwa na kasoro. Mauti ilikuwa siri isiyoelezeka. Mabishano baina ya makundi hayo mawili yalizusha ubishi wenye hasira.

Watu wa kawaida hawakuvutiwa na Masadukayo. Lakini wengi wa Masadukayo walikuwa na mvuto uletwao na utajiri wa mali. Katika hao ndio alichaguliwa kuhani mkuu. Kule kustahili kushika wadhifa huo kulitoa mvuto kwa mafundisho yao yenye makosa.

Masadukayo waliyakataa mafundisho ya Yesu; mafundisho yake kuhusu maisha ya baadaye yalikuwa kinyume na dhana zao. Waliamini kuwa baada ya kuumbwa na Mungu mwanadamu aliachwa tu ajitawale. Walichukulia kuwa mwanadamu alikuwa huru kumudu mambo yake duniani, na hali yake ya baadaye imo mikononi mwake.

KRISTO AKABILIANA NA ADUI ZAKEMakuhani na wazee hawakuweza kukanusha madai ya Kristo, ila tu walinuia kumtega. Walimtumi...
25/07/2023

KRISTO AKABILIANA NA ADUI ZAKE

Makuhani na wazee hawakuweza kukanusha madai ya Kristo, ila tu walinuia kumtega. Walimtumia majasusi “waliojifanya kuwa waaminifu kwake, ili wapate kumka-mata katika maneno yake, na kumsh*taki kwa watawala.” Vijana hao wenye juhudi walifuatana na wafuasi wa Herode kusudi wasikie maneno yake wapate kumnasa na kumsh*taki.

Mafarisayo waliudhiwa na kodi za Warumi wakidai kuwa kulipa kodi ni kinyume cha sheria ya Mungu. Sasa majasusi walimjia Yesu wakijifanya wanataka kujua wajibu wao, wakisema: “Bwana, twajua kuwa wewe hufundisha ukweli mtupu, wala hujali cheo cha mtu, ila hufundisha sheria ya Mungu tu: Je, ni halali kumlipa kodi kwa Kaisari?”

Wale waliomwuliza Yesu swali hilo walidhani kuwa wameficha kusudi lao, lakini Yesu alisoma nia yao kana kwamba ni kitabu. Akasema: “Mbona mnanijaribu?” Alisema hayo kuonyesha kuwa anafahamu nia yao. Walikuwa bado wangali katika mtataniko, aliposema: “Nionyesheni dinari.” Walimletea. Naye aliwauliza: “Sanamu hii ni ya nani?” Wakasema, “Ni ya Kaisari.” Yesu akisonda dinari hiyo alisema: “Mpeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu.”

Wapelelezi walijiona kuwa duni katika mtego wao na kushindwa. Ufasaha wa majibu ya maswali yao uliwafanya wasiwe na la kusema zaidi. Majibu ya Kristo hayakuwa ya kupiga chenga, bali majibu adilifu kwa maswali yao. Akishikilia dinari ya Kirumi mkononi aliwaambia kuwa kwa kuwa wanaishi chini ya ulinzi wa Warumi, ni haki kabisa kulipa kodi kwao. Lakini wakiwa chini ya sheria ya Warumi lazima utii wao kwanza uwe kwa Mungu.

K**a Wayahudi kwa uaminifu wangalitimiza wajibu wao kwa Mungu, wasingalitawaliwa na watu wa mataifa mengine. Bendera ya Warumi isingalipepea katika Yerusalemu; wala mtawala wa Kirumi asingelitawala humo.

Mafarisayo walishangazwa na majibu ya Yesu. Hakuwakemea tu bali alieleza kanuni zinazohusu wajibu wa watu kwa Mungu wao na wajibu wao kwa serikali inayotawala. Ingawa wengi hawakuridhika, lakini waliona kanuni ilivyo kwa majibu ya maswaii yao. Walishangazwa kwa uwezo wa Kristo wa kujibu.

Haukupita muda mara baada ya Mafarisayo kunyamazishwa Masadukayo nao wakajitokeza na maswali ya ujanja. Ingawa hawakumwamini Kristo kwa ujumla, lakini baadhi yao walikuwako waaminifu katika mafundisho ya Kristo. Masadukayo walikiri kuwa Wanaamini sehemu kubwa ya Maandiko Matakatifu, lakini kimaisha walikuwa wenye mashaka na wapenda utajiri.

JINSI YA KUJENGEKA BAADA YA KUVUNJIKAKwa wale wanaomwamini, Kristo ni msingi ulio imara. Wameanguka mwambani na “wamevun...
14/07/2023

JINSI YA KUJENGEKA BAADA YA KUVUNJIKA

Kwa wale wanaomwamini, Kristo ni msingi ulio imara. Wameanguka mwambani na “wamevunjika”. Kuanguka mwambani na kuvunjika, maana yake ni kuacha hali ya kujiona kuwa mwenye haki, ni kumwendea Kristo kwa unyenyekevu, k**a mtoto na kutubu makosa yetu yote, na kuamini upendo wake wa msamaha. Kwa imani na utii hujenga juu ya Kristo, ambaye ni msingi imara.

Juu ya msingi huu ambao jiwe hai kuu la pembeni ni Yesu watu wote hujenga kwake, yaani Wayahudi na watu wa mataifa pia. Unawatosha wote, na kuchukua uzito wa ulimwengu wote. Wote wanaojiunga naye na kujenga juu ya msingi huu huwa mawe yaliyo hai. (Soma 1 Petro 2:5).

Kwa wale wanaojikwaa kwa neno, huasi. Kristo ni mwamba wa kujikwaa. K**a jiwe lililokataliwa, alichukua aibu zote. “Alidharauliwa na kukataliwa na watu, wala hakuhesabiwa kuwa ni kitu.” (Soma Isaya 53:3.) Lakini kwa kulufuka kutoka kwa wafu alihesabiwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu. (Tazama Warumi 1:4.) Atakaporudi ataonekana kuwa Bwana wa mbingu na nchi, jiwe lililokataliwa na waashi, sasa ni jiwe kuu la pembeni, mfalme wa ulimwengu.

Mtu ambaye ataangukiwa na jiwe hili atasangwasagwa. Waliomkataa Kristo, walishuhudia maangamizo ya mji wao na nchi yao. Utukufu wao ukatawanyika k**a mavumbi. Mwamba ambao wangalijengea ungekuwa usalama wao. Zilikuwa ni rehema za Mungu zilizodharauliwa na wema uliodhihakiwa. Watu walijiweka wenyewe kuwa kinyume na Mungu, na yote yale yaliyokuwa yawe wokovu wao yakawa maangamizi yao.

Kusulubishwa kwa Kristo na Wayahudi kulichanganyikana na kuangamizwa Yerusalemu. Damu ya Yesu waliyomwaga ndiyo iliyokuwa uzito uliowazamisha kwa maangamizi.

Hivyo katika siku ya mwisho wakati hukumu ya Mungu itakapowakalia walioikataa neema ya Mungu, Kristo ataonekana k**a mlima wakulipiza kisasi. Utukufu wake, ambao kwa watakatifu ni uzima, kwa waovu utakuwa ni moto wa kuteketeza. Kwa ajili ya upendo uliokataliwa, neema iliyodharauliwa, wenye dhambi wataangamizwa. Hekalu lililochafuliwa, mwana mkaidi, wakulima waovu, wajenzi wakorofi, wote hupata mfano katika njia ya kila mwenye dhambi. Asipotubu hukumu iliyowakabili itakuwa yake.

JIWE GANI LILOKUWA MFANO WA KRISTO Mwokozi akiwaangalia kwa masikitiko, alisema: “Hamkusoma kwamba jiwe lililokataliwa n...
24/06/2023

JIWE GANI LILOKUWA MFANO WA KRISTO

Mwokozi akiwaangalia kwa masikitiko, alisema: “Hamkusoma kwamba jiwe lililokataliwa na waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni? Hii ni kazi ya Bwana, nayo imekuwa ajabu machoni mwetu?” Kwa hiyo nawaambieni, ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, litapewa taifa jingine lenye kuzaa matunda yake. Na ye yote aangukaye juu ya jiwe hili atavunjika vipande vipande; lakini yeye yule jiwe hili litakayemwangukia, litamsagasaga kuwa unga.”

Unabii huu ulikaririwa na Wayahudi mara kwa mara masinagogini mwao, ukimhusu Masihi ajaye. Kristo alikuwa Jiwe kuu la pembeni katika itikadi ya Wayabudi, na katika mpango mzima wa wokovu. Jiwe hili la msingi sasa lilikuwa linakataliwa na wajenzi wa Kiyahudi. Kwa kila njia na kwa bidii yote, Mwokozi alijitahidi kuonyesha maana ya matendo waliyokuwa wanataka kutenda. K**a wakishindwa kutubu kutokana na maonyo hayo yote, basi hukumu itawakumba, ajali ya Mungu katika kuwanyang’anya nafasi ya taifa lao na kisa cha kuwaacha na siyo tu kuliacha hekalu lao liharibiwe lakini kwa taifa lao kutawanywa.

Wasikiaji wake walifahamu maonyo hayo, lakini hukumu waliyojikatia wenyewe, licha ya makuhani na wakuu walikuwa tayari kujaza kikombe chao kwa kusema: “Huyu ndiye mrithi wa yote, haya na tumwue; “Lakini walipotaka kumk**ata, waliogopa makutano, maana walikuwa upande wa Kristo.”

Kristo alipotaja juu ya unabii wa jiwe la msingi, lililokataliwa, alikuwa akisemea hekalu la kwanza. Jambo hili lilikuwa na maana kuhusu kuzaliwa kwake Yesu, lakini pia lina umuhimu na kwetu pia. Wakati hekalu la Sulemani lilipojengwa, mawe makubwa yaliandaliwa katika machimbo yake. Yalipoletwa mafundi waliyatia tu katika mahali pake. Kuhusu msingi, jiwe moja lilikuwa limeletwa na wajenzi hawakupata mahali pa kulitia. Jiwe hilo lililokosa mahali pake lilisumbua kuachwa tu pembeni. Hilo likabaki k**a jiwe lililokataliwa.

Lakini wajenzi walipotafuta jiwe lifaalo katika hekalu la pili, iliwalazimu watafute na kuchagua jiwe lenye kufaa. K**a watatia jiwe lisofaa wangalileta uharibifu katika jengo. Lakini mwishowe walilirudia jiwe la kwanza walilolikataa. Lilipigwa na jua na baridi bila kupata nyufa. Baada ya kulijaribu lilionekana kuwa ndilo lifaalo. Jiwe hilo ni mfano wa Kristo.

Isaya asema: “Naye atakuwa ni mahali patakatifu bali ni jiwe la kujikwaza, na Mwamba wa kujikwaa kwa nyumba za Israeli zote mbili .... Na wengi watajikwaa juu yake, na kuanguka na kuvunjika, na kunaswa na kuk**atwa.” Kristo atachukua majaribu yote ambayo jiwe la pembeni katika hekalu la Sulemani alikuwa mfano wake. “Tazama naweka jiwe katika Sayuni liwe msingi, jiwe lililojaribiwa, jiwe la pembeni lenye thamani, msingi ulio imara, yeye aaminiye hatafanya haraka.” Isaya 8:14, 15; 28:16.

Mungu alichagua jiwe kuu la pembeni akaliita, “Msingi ulio imara.” Ulimwengu mzima unaweza kuweka juu yake uzito wake wote na matatizo yake yote. Vyote vya ulimwengu vitakaa juu yake bila kuuharibu. Wale wanaomtegemea hatawakatishwa tamaa. Yeye amejaribiwa katika mambo yote, akashinda. Amebeba kila mzigo uliowekwa juu yake na kila mtu atubuye. Wote wanaomtegemea yeye, hukaa salama kabisa. Kristo ndiye “Basi heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini, Jiwe walilolikataa waashi, Limekuwa jiwe kuu la pembeni. Tena, Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha. Kwa maana hujikwaza kwa neno lile, wasiliamini, nao waliwekwa kusudi wapate hayo” 1 Petro 2:7, 8.

MAKUHANI NA WAKUU WANYAMAZISHWAWakisimama katika hali ya kutahayari, makuhani, wakuu na waandishi walikosa jambo la kuse...
20/06/2023

MAKUHANI NA WAKUU WANYAMAZISHWA

Wakisimama katika hali ya kutahayari, makuhani, wakuu na waandishi walikosa jambo la kusema mbele ya Kristo. Watu wengine walisimama kando wakiwacheka watu hawa wenye kiburi na majivuno wakiwa wameshindwa.

Mambo yote ya Kristo yalikuwa ya maana tupu na mvuto wake ulikuwa, uendelee kukumbukwa kwa kiasi kikubwa hata baada ya kusulubiwa kwake, na kupaa mbinguni. Watu wengi waliamini na kumfuata kwa ajili ya mambo ya siku hiyo. Tofauti baina ya Yesu na Kuhani Mkuu ilionekana wazi kwa jinsi walivyokuwa wakizungumza. Mkuu wa hekalu alijivika kwa heshima na fahari sana. Kichwani alivaa taji lililong’ara, nywele na ndevu zikiwa na mvi kutokana na umri wake. Mbele ya huyu mwenye majivuno, alisimama Mtukufu wa mbinguni bila mapambo yo yote, uso wake umefadhaika, wenye kuonyesha uvumilivu, na uaminifu. Huku akionyesha heshima na huruma. Watu wengi walioyasikia maneno yake na kuona matendo yake siku ile hekaluni walimwamini moyoni mwao kuwa ni nabii wa Mungu. Lakini kadiri watu walivyomfuata, ndivyo chuki ya Makuhani ilivyozidi juu yake.

Halikuwa kusudi la Kristo kuwaaibisha adui zake jinsi hiyo. Alikuwa na fundisho muhimu la kuwafundisha. Kule kudai kutotambua ubatizo wa Yohana Mbatizaji, kulimpa nafasi ya kusema mengi zaidi kwao na kuwadhihirishia hali zao, na kuongeza onyo jingine. “Mnafikiri nini?” Mtu mmoja alikuwa na wana wawili. Akamwambia mtoto wa kwanza: “Mtoto nenda leo shambani ukalime. Akajibu, nitakwenda, wala asiende. Akamwambia na mwingine: Mwanangu, nenda leo shambani ukalime, akakataa, lakini baadaye akajuta na kwenda. Ni yupi katika hao aliyefanya mapenzi ya babaye?”

Swala hili liliwatupa wasikilizaji wake kando ya ngome yao. Mara moja walijibu “Yule aliyekwenda kulima.” Yesu akawakazia macho akawajibu kwa ujasiri na kusema: “Amini nawaambieni, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu katika kuingia kwenye ufalme wa Mungu. Maana Yohana alikuja kwenu kwa njia ya haki, wala hamkumwamini, ila watoza ushuru na makahaba walimwamini, nanyi mlipoona hivyo hamkutubu, ili mmwamini baadaye.”

Makuhani na wakuu hawakuweza kumjibu Kristo isipokuwa k**a ipasavyo; na hivyo alipata jibu kuwa mwana aliyekataa kulima, walakini baadaye akaenda. Na ambaye alikuwa mfano wa watoza ushuru na makahaba. Yohana alipokuja na kuhubiri toba, watoza ushuru walimwamini na kubatizwa.

Mwana wa pili asiyekwenda kulima ni mfano wa waongozi wa Wayahudi ambao hawakukiri kuwa Yohana alitumwa na Mungu. Walipinga “shauri la Mungu juu yao, kwa kuwa hawakubatizwa naye.” Luka 7:30. Wayahudi walikuwa sawa na mwana aliyekataa kulima, wakijidai kukubali, lakini wakitenda kinyume cha maungamo yao.

Makuhani na wakuu waliendelea kuwa kimya. Lakini Kristo alisema: “Sikieni mfano mwingine: Mkulima mmoja alifanya bustani yake, akaizungushia ugo, akachimba shinikizo ndani yake, akajenga mnara, akawakabidhi watunzaji wake, akasafiri katika nchi za mbali. Wakati wa matunda watunzaji wakawak**ata watumishi wale, wakampiga mmoja, na kumwua mwingine, na kumpiga mawe mwingine. Tena akatuma watumishi wake zaidi ya wale wa kwanza, wakawatenda k**a walivyowatenda wa kwaaza. Mwisho wa yote alimtuma mwanawe, akisema kuwa huyu watamjali. Lakini watunzaji walipomwona, waliambiana. Huyu ndiye mrithi wa yote, basi na tumwue na kutwaa urithi wake. Walimshika na kumtupa katika shinikizo na kumchinja. Je, Bwana wa shamba hili atawatendaje waangalizi wale?”

Makuhani na wazee wakajibu: “Atawaangamiza waovu hao, na kuwaweka watunzaji wengine, ambao watatoa matunda kwa wakati wake.” Wasemaji hao waliona kuwa sasa wametoa hukumu inayowahusu wao wenyewe. Jinsi ambavyo watunza shamba walivyopaswa kutoa matunda kwa wakati wake, vivyo hivyo na watu wa Mungu walipaswa kuishi maisha ya kweli kufuatana na hadhi takatifu waliyo nayo. Lakini k**a wale watunza shamba walivyowaua watumishi wa Bwana, ndivyo Wayahudi walivyowaua manabii waliotumwa kwao na Mungu ili kuwatubisha.

Hivyo maana ya mfano wa wakulima wale, haukuweza kubishiwa. Mwana mpendwa ambaye alitumwa na Mungu mwishowe, kwa watumishi wakaidi wakamk**ata na kumwua, makuhani waliona wazi yaliyokuwa yanamkabili Yesu. Katika adhabu iliyowafika watumishi wasiyo na shukurani Kulidhihirika yaliyokuwa yanawasubiri wale ambao.

HEKALU LATAKASWA TENAMwanzoni mwa huduma yake, Kristo alikuwa amewafukuza hekaluni watu waliokuwa wakifanyia biashara ya...
16/06/2023

HEKALU LATAKASWA TENA

Mwanzoni mwa huduma yake, Kristo alikuwa amewafukuza hekaluni watu waliokuwa wakifanyia biashara yao batili hekaluni. Ujasiri na mwenendo wake mtakatifu viliwatia hofu wafanya biashara wenye hila.

Panapo mwisho wa huduma yake alikuja tena hekaluni akaona hali ya uchafuzi wa hekalu ingalipo k**a hapo kwanza. Milio ya wanyama na kelele za ubadilishaji wa, fedha, na fujo ya kila aina vilifanyika humo. Wakuu wa hekalu ndio waliokuwa wenyewe, wakinunua na kuuza. Wao wenyewe ndio walikuwa wachoyo kabisa, wala mbele za Mungu hawakuwa na afadhali kupita watu wezi.

Kila wakati wa Pasaka na Sikukuu ya vibanda, wanyama maelfu walichinjwa, damu zao zilichukuliwa na makuhani na kumwagwa madhabahuni. Wayahudi walikuwa wamesahau umuhimu wa kuchinja wanyama hao kwamba ni kwa ajili ya dhambi. Hawakufahamu kwamba kuchinja wanyama ni mfano wa kumchinja Kristo kwa, ajili ya dhambi za ulimwengu.

Yesu aliona jinsi Wayahudi walivyofanya mikutano hii kuwa tamasha za kumwaga damu na ukatili. Walikuwa wamezidisha wanyama wa kafara kana kwamba Mungu hupendezwa na huduma za juu juu tu. Makuhani na watawala walizifanya kafara zinazoelekeza kwa Mwana Kondoo wa Mungu kuwa njia za kujipatia mapato. Kwa hiyo utakatifu wa kafara kwa kiasi kikubwa uliharibiwa kabisa. Yesu alijua kuwa damu yake ambayo karibu itamwagwa kwa ajili ya dhambi za ulimwengu, nayo ingehafifishwa na makuhani na wazee k**a walivyofanya damu ya wanyama!

Kristo alikuwa amepinga matendo ya jinsi hii kupitia kwa manabii. Isaya, akiona kwa njozi Wayahudi walioasi aliwaambia. “Huu wingi wa sadaka zenu mnazonitolea una faida gani? asema Bwana. Nimejaa mafuta ya kafara ya kondoo waume, na mafuta ya wanyama walionona, mimi siifurahii damu ya ng’ombe wala ya wana kondoo wala ya mbuzi waume. Jiosheni, jitakaseni, ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu.” Isaya 1:11-16.

Yeye aliyetoa unabii huu, sasa kwa mara ya mwisho anarudia maonyo haya. Katika utimizo wa unabii huu watu walikuwa wamemtangaza Yesu kuwa mfalme wa Israeli. Alikuwa amekubali heshima yao, na kukubali uteuzi wa kuwa mfalme. Katika tabia hii lazima atende. Alifahamu kuwa katika kujitahidi kuwarekebisha makuhani itakuwa kazi bure; Hata hivyo ushahidi wa utume wake mtakatifu lazima utolewe kwa taifa lisiloamini.

Mara hii tena mtazamo wa kutisha wa Yesu ulieneza ukumbi wote wa hekalu. Watu wote walimtazama. Uungu uliwaka k**a umeme katika ubinadamu na kumwangaza, Kristo, kwa utukufu na heshima, ambavyo hakupatwa kuwa navyo kabla ya hapo. Watu waliokuwa karibu naye walisogea mbali kadiri ilivyowezekana. Alisimama peke yake isipokuwa wanafunzi wake wachache. Kukawa kimya kabisa. Kristo alizungumza kwa uwezo mkuu uliotikisa watu k**a tufani; Akisema: “Imeandikwa, Nyumba yangu itakuwa ya sala, lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.” Sauti yake ilitoka k**a tarumbeta ndani ya hekalu. “Yaondoeni haya ...” Yohana 2:16.

Miaka mitatu iliyopita wakuu wa hekalu walikuwa wameaibishwa na kukimbia kwao mbele ya agizo la Yesu. Hawakutaka tena hali yao ya kudhalilishwa kurudiwa tena mara ya pili. Walakini hata hivyo wakati huu waliogofishwa zaidi kuliko hapo kwanza, na wakaharakisha kutii amri yake. Makuhani na wenye biashara walikimbia na wakiwaswaga ng’ombe wao.

Walipokuwa njiani kutoka hekaluni, walikutana na watu wengi wakileta wagonjwa wao kwa Mganga Mkuu. Habari walizoambiwa na watu waliokimbizwa hekaluni ziliwaogopesha, hata wengine wakarudi, lakini kundi kubwa zaidi walisonga mbele wakitamani kumfikia. Mara ukumbi wa hekalu ulijaa watu wenye maradhi, na waliokuwa karibu kufa na Yesu akawahudumia wote.

Baada ya muda, makuhani na wakuu walithubutu tena kurudi hekaluni. Walikuwa wakidhani kuwa Yesu atatawazwa kuwa mfalme na kuchukua kiti cha Daudi. Walipoingia hekaluni walisimama hali wakiduwaa. Waliwaona wagonjwa wa kila aina wakiponywa, vipofu wakiona, vilema wakiruka kwa furaha, viziwi wakisikia na kadhalika. Watoto ndio waliokuwa wakishangilia zaidi. Yesu alikuwa amewaponya maradhi yao; na kuwakumbatia mikononi mwake. Na sasa wanamsifu kwa sauti zao za shangwe. Walirudia kuimba Hosana na kupunga matawi, k**a walivyofanya siku ya jana yake.

Sauti za hawa wenye shangwe ziliwachukiza wakuu na waangalizi wa hekalu. Wakawaambia watu kuwa nyumba ya Mungu inadharauliwa sana kwa kelele za shangwe na mirukoruko ya furaha za watoto. Wakuu wakamwambia Kristo: “Husikii hayo yote?” Yesu akawaambia: “Je, hamjasoma kwamba: Kwa midomo ya watoto na kwa midomo ya wanyonyao utakamilisha sifa?” Unabii ulitabiri kuwa Kristo atatangazwa k**a mfalme, na Mungu aliwainua watoto hawa wawe mashahidi wake. K**a sauti za watoto zingenyamaza kimya, nguzo za hekaluni zingemsifu Mwokozi.

Mafarisayo walifadhaishwa kabisa. Yesu alikuwa hajajichukulia mamlaka ya kifalme jinsi hivyo. Alikuwa ametenda maajabu, lakini kamwe, alikuwa hajatukuzwa k**a wakati huo. Ingawa alikuwa amewachukiza na kuwafedhehesha makuhani na wakuu, lakini hawakufanya lo lote siku ile. Kesho yake tena baraza la Sanhedrin lilikutana ili lione nini cha kumtendea Yesu. Kwa miaka mitatu wakuu walishuhudia kuwa Yesu ni Masihi. Sasa hawakuwa na haja kutaka ishara, ila walitaka akiri au kutamka ili wapate sababu ya kumk**ata na kumhukumu.

Ndani ya hekalu walimwuliza: “Unafanya haya yote kwa uwezo gani? Nani amekuruhusu?” Yesu aliwakabili na majibu yenye masharti ya kujibu swali lake: “Ubatizo wa Yohana ulitoka wapi, mbinguni au kwa wanadamu?”

Makuhani waliona kuwa wamo mtegoni. K**a wakisema kuwa ulitoka mbinguni, Yesu atawaambia: Mbona hamkumwamini? Yohana alishuhudia akisema: “Tazama Mwana Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu.” Yohana 1:29. K**a makuhani waliukubali ujumbe wa Yohana kwa hiyo wangewezaje kuukataa Umasihi wa Kristo?

K**a wangekubali kuwa ubatizo wa Yohana ulikuwa wa wanadamu, watajiamshia fujo na vita kutoka kwa makutano. Maana waliamini kuwa Yohana ni nabii. Watu walijua kuwa makuhani walimkiri Yohana kuwa nabii, na kukubali kuwa alitumwa na Mungu. Lakini baada ya kushauriana kwa siri, walikata shauri kujitosa wenyewe. Kwa unafiki wakidai hawafahamu, walisema “Hatujui.” Kristo naye alisema: “Hata mimi siwaambii kwamba kwa uwezo gani ninatenda haya.”

Address

Tukuyu
Mbeya
53515

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when PENDO LIsilo Kifani posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to PENDO LIsilo Kifani:

Share