05/06/2023
*Sasa unaweza Kudhamini uchapishaji na usambazaji wa nakala hizi za rhapsodi ya Uhakika kupitia code namba: 8177098*
*ANZA NA UJUMBE WA UPENDO*
Jumatatu, 05
Mchungaji Chris Oyakhilome, PhD
_*“Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”*_ Yohana 3:16
Wakati wa kuhubiri Injili, baadhi ya Wakristo hukazia hasa somo la dhambi, wakikazia uhitaji wa watu kutubu dhambi zao. Ujumbe wa toba uliwafaa Wayahudi kwa sababu walikuwa chini ya Sheria. Kilichotakiwa kutoka kwao ni kugeuka kutoka katika uovu walipofanya dhambi, na kumwelekea Mungu.
Hata hivyo, wasio Wayahudi—yaani Mataifa—hawakuwa na kitu chochote cha kugeuka kwa sababu hawakuwa kamwe chini ya Sheria, ambayo (Sheria) yenyewe, ilikuwa hukumu yao. Biblia inasema, _*“Maana kabla ya sheria dhambi ilikuwamo ulimwenguni, lakini dhambi haihesabiwi isipokuwapo sheria”*_ (Warumi 5:13).
Ndiposa, Biblia inasema, _*“Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu”*_ (Warumi 3:23). Hii inajumuisha Wayahudi na Wamataifa. Ikiwa watu wa mataifa mengine hawakuvunja Sheria kwa sababu hawakupewa, je, dhambi yao ilikuwa wapi?
Tunajifunza katika kitabu cha Mwanzo kwamba Mungu alipowaumba Adamu na Hawa, walikuwa kwenye uwepo wa Mungu mtakatifu. Waliishi katika utukufu Wake. Lakini walikatiliwa mbali na utukufu huo Adamu alipomtenda Mungu dhambi.
Warumi 5:19 inasema, _*“Kwa sababu k**a kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki.”*_ Kupitia kosa la mtu mmoja, watu wote walipungukiwa na utukufu, lakini sasa, katika Kristo, utukufu unarejeshwa. _*“…Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu”*_ (Wakolosai 1:27). Haleluya!
Hii ndiyo sababu mkakati wako wa Injili hupaswi kuanza na suala la dhambi; badala yake, unapaswa kuanza na ujumbe wa upendo. Huo ndio ufunguo; hivyo ndivyo Yesu alivyoiweka katika mstari wetu wa ufunguzi. Upendo ulikuwa msukumo Wake.
Tazama katika mstari huo kwamba hakusema lolote kuhusu dhambi. Hiyo ndiyo Injili ya Kristo. Ni ujumbe wa upendo na ujumbe wa uzima—uzima na asili ya Mungu—ambao mauti yake na kuzikwa Kwake na kufufuka Kwake kumefanya iwezekanike na kupatikanika kwa uzima huu kwa kila mtu anayeamini.
*| SALA*
*Baba Mpendwa, ahsante kwa upendo Wako ambao umedhihirishwa, kufunuliwa, na kukumbatiwa kwa vile ambavyo wengi ulimwenguni kote wanasikia na kupokea Injili ya kweli ya Yesu Kristo, na matokeo ya zawadi ya haki. Leo, wanaupata udhihirisho kamili wa upendo Wako thabiti na wa milele, utukufu wa neema Yako, katika Jina la Yesu. Amina.*
*Jifunze Zaidi:*
** Yohana 3:16 AMPC; 2 Wakorintho 5: 19-21 **
*SOMA MAANDIKO KILA SIKU*
_*MPANGO WA KUSOMA BIBLIA MWAKA-1:*_
Yohana 19:17-42 & 1 Nyakati 17-19
_*MPANGO WA KUSOMA BIBLIA MIAKA-2:*_
Marko 15:1-14& Kumbukumbu la Torati 3
*Imetolewa kutoka: Rhapsody of Realities Daily Devotional*
*Weka maoni kuhusu utenzi wa leo kwenye _www.rhapsodyofrealities.org_*