Efatha Church- MBEYA

Efatha Church- MBEYA Efatha Church Mbeya: Healing & Deliverance by the Blood of JESUS CHRIST. Administered by Pastor Joshua J. Mwingira. Joshua J.

Mwingira is our Senior Pastor at Efatha-Mbeya.

Kamwe Mungu huwa hadharau moyo uliopondeka mbele zake.MATUKIO KATIKA PICHAZIARA YA MCHUNGAJI ,JOSHUA  JOSEPHAT MWINGIRA....
10/06/2026

Kamwe Mungu huwa hadharau moyo uliopondeka mbele zake.

MATUKIO KATIKA PICHA

ZIARA YA MCHUNGAJI ,JOSHUA JOSEPHAT MWINGIRA.

MCHUNGAJI KIONGOZI ,KANISA LA EFATHA MBEYA.

MUNGU alipokuumba,aliweka taarifa  zako zote kuhusu wewe katika  Roho yako.Na taarifa  zote tayari zimeandikwa katika ki...
10/06/2026

MUNGU alipokuumba,aliweka taarifa zako zote kuhusu wewe katika Roho yako.

Na taarifa zote tayari zimeandikwa katika kitabu cha mbinguni, na ni mapenzi ya Mungu kuishi sawasawa na yale yaliyoandikwa.

Zaburi 139–16”Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado”.

Hivyo kila mtu aliyepo hapa duniani hayupo kwa bahati mbaya kila mtu ana kusudi.

Kusudi limeambatana na tabia yako.

Swali la kujiuliza Je, ndani ya moyo wako umebeba nini?

Umebeba neno au umebeba maumivu, mateso, mizigo, hofu na mashaka?

Haijalishi ulizaliwa na mganga wa kienyeji, ulizaliwa katika mateso na maumivu

isikuzuie kuishi kusudi lako na kufikia hatima yako.

Tumechelewa kufika kwenye hatima zetu kwa sababu ya maumivu, kukataliwa, na mateso tuliyobeba ndani ya mioyo yetu. Mara zote, haijalishi nini kilitokea katika maisha yako, usikubali kuishi katika dimbwi la mateso na maumivu.

ZINGATIA : Mungu ana kusudi na wewe, na ni lazima ufikie hatima yako.

Ziara Ya Kichungaji ,Kanisa La Efatha Mbalizi.

Mchungaji Joshua Josephat Mwingira.

Mchungaji Kiongozi,Kanisa La Efatha Mbeya.

Mungu ambaye ni Baba yetu, alitujua hata kabla ya kuwekwa kwenye matumbo ya mama zetu; alikutakasa na akakuweka kuwa nab...
10/06/2026

Mungu ambaye ni Baba yetu, alitujua hata kabla ya kuwekwa kwenye matumbo ya mama zetu; alikutakasa na akakuweka kuwa nabii wa mataifa.

Yeremia 1-5”Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.”

Nabii ni ofisi Lakini katika mfumo wa uumbaji wewe ni nabii wa maisha yako.

Kazi za nabii ni zipi?

NABII ANA KAZI ZIFUTAZO:

1. Kusikiliza maagizo anayopewa na Mungu.

2. Kusema kile alichokisikia, sawasawa na maagizo.

3. Kuhakikisha mapenzi ya Mungu yanatimia.,kukiwa na dhoruba mahali ana hakikisha mapenzi ya Mungu yanatimia.

4. Kuleta suluhu kwenye matatizo, analeta majibu kwenye maswali.

Ziara Ya Kichungaji Kanisa La Efatha Mbalizi.

Mchungaji ,Joshua Josephat Mwingira.

Mchungaji Kiongozi,kanisa La Efatha Mbeya.

Wewe ni asili yetu nguvu zetu,ngome yetu hatuna Mungu mwingine ila wewe pekee.Ziara ya Kichungaji Tarehe 10/6/2026.Kanis...
10/06/2026

Wewe ni asili yetu nguvu zetu,ngome yetu hatuna Mungu mwingine ila wewe pekee.

Ziara ya Kichungaji Tarehe 10/6/2026.

Kanisa La Efatha Mbeya.

10/06/2026

🔴 LIVE EFATHA CHURCH MBALIZI

ZIARA YA MCHUNGAJI JOSHUA JOSEPHAT MWINGIRA.

MCHUNGAJI KIONGOZI KANISA LA EFATHA MBEYA.

10/06/2026

Hakikisha unatengeneza na Mungu, kwa maana yeye hadhihakiwi; chochote apandacho mtu, atakivuna.

Mchungaji,Joshua Josephat Mwingira.

Mchungaji Kiongozi ,Kanisa La Efatha Mbeya.

NAIBARIKI JUMATANO YANGU.Ni siku ya kuchukua urithi wangu. Mimi nitamiliki kila ninachohitaji kumiliki.Asante YESU.
10/06/2026

NAIBARIKI JUMATANO YANGU.

Ni siku ya kuchukua urithi wangu. Mimi nitamiliki kila ninachohitaji kumiliki.

Asante YESU.

MATUKIO KATIKA PICHA.ZONI YA PAMOJA ENEO LA BETHLEHEMU.KANISA LA EFATHA MBEYA.
09/06/2026

MATUKIO KATIKA PICHA.

ZONI YA PAMOJA ENEO LA BETHLEHEMU.

KANISA LA EFATHA MBEYA.

Uzuri wako umeyazunguka maisha yetu; tumeona kutunzwa na kutetewa na wewe, Ee Mtakatifu.Zoni  ya  pamoja 8/6/2026.Eneo L...
09/06/2026

Uzuri wako umeyazunguka maisha yetu; tumeona kutunzwa na kutetewa na wewe, Ee Mtakatifu.

Zoni ya pamoja 8/6/2026.

Eneo La Bethlehemu.

Kanisa La Efatha Mbeya.

Mimi nitabaki na wewe, Mungu hata nikipita kwenye mabonde bado unabaki kuwa Mungu kwangu.Sikutafutii kwa sababu ya matat...
09/06/2026

Mimi nitabaki na wewe, Mungu hata nikipita kwenye mabonde bado unabaki kuwa Mungu kwangu.

Sikutafutii kwa sababu ya matatizo au kwa kuwa sina kitu,bali ninatambua wewe pekee ndiyo kila kitu kwenye maisha yangu.

Kimbilio langu, tegemeo langu ni wewe; vyote nilivyo navyo vinatoka kwako.

Nikila na kushiba, nikiwa na furaha, ninaponunua gari nzuri, nikiwa na fedha za kutosha, bado wewe ni kila kitu kwenye maisha yangu.

Chochote nilichonacho kimetoka kwako; nguvu nilizonazo ni wewe umenipa, kibali nilichonacho kinatoka kwako.

Mimi, nje yako, siwezi chochote.

Mchungaji,Joshua Josephat Mwingira.

Mchungaji Kiongozi,Kanisa La Efatha Mbeya.

Address

New Forest
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church- MBEYA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church- MBEYA:

Share