Tule Chakula Cha Kiroho

Tule Chakula Cha Kiroho MATHAYO 4:4
IMEANDIKWA,MTU HATAISHI KWA MKATE TU,ILA KWA KILA NENO LITOKALO KATIKA KINYWA CHA MUNGU.

Swali limeulizwa na mwalimu Damian Ndimbo
04/12/2016

Swali limeulizwa na mwalimu Damian Ndimbo

30/11/2016

*KATI YA YESU KRISTO NA MUHAMMAD (S.A.W.) NI NANI NABII YULE?*

*Katika Ulimwengu wa kimwili siyo rahisi kuweza kuelewa hiki ambacho nakizungumza, ila katika ulimwengu wa kiroho ni rahisi sana kuzitambua hila za muovu yule shetani! imekuwa ni kawaida sana kuwaona baadhi ya Waislamu wakijaribu kwa makusudi kabisa kuwapotosha waislamu wenzao na wakati mwingine kuwapotosha baadhi ya Wakristo, wale ambao kusoma neno la MUNGU kwao ni mtihani, wakifundisha yasiyowapasa! wakinukuu mistari hii 👇hii ndani ya BIBLIA.*

Yohana 1: 19 Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani?

20 Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo.

21 Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La.

22 Basi wakamwambia, U nani? Tuwape majibu wale waliotupeleka. Wanenaje juu ya nafsi yako?

23 Akasema, Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, Inyosheni njia ya Bwana! K**a vile alivyonena nabii Isaya.

*Wakishasoma mistari hii wanasema kuwa, hapo kuna watu watatu!*

(1) KRISTO
(2) ELIYA
(3) KRISTO

*Wanasema kuwa, YOHANA yeye amekataa kuwa siyo mmoja katika wale watatu! hivyo wanaendelea kudai kuwa, Kristo na Nabii yule ni wawili tofauti, kwa sababu Yohana ametajiwa watu watatu na amekiri kuwa yeye siye! Ila Yesu yeye alipoambiwa kuwa yeye ni Kristo alikubali.*

Yohana 4:25 Yule mwanamke akamwambia, Najua ya kuwa yuaja Masihi, (aitwaye Kristo); naye atakapokuja, yeye atatufunulia mambo yote.

26 Yesu akamwambia, Mimi ninayesema nawe, ndiye.

*Wanasema kuwa, Yesu yeye ni Kristo, hivyo siyo Nabii yule, wanasema "Ni lazima tumtafute Nabii yule" Katika kumtafuta kwao, wanamdumbukiza Muhammadi, ukiwaomba ushahidi wa andiko ndani ya QURAN lisemalo kuwa Muhammadi ndiye Nabii Yule, hawawezi kutoa ila wanalazimisha dhana zao na Ujuzi wa kutunga maneno na kuyapangilia kwa ustadi mkubwa, kiasi kwamba k**a hujazama katika maandiko basi wewe unaenda na Maji!*

*JE! NABII YULE NI NANI?*

*kabla hatujamwangalia na kumjua ni nani kwa mujibu wa maandiko, tuwatazame wale walioenda kumuuliza Yohana wao wenyewe Walitoka wapi?*

Yohana 1:24 Nao wale waliotumwa walikuwa wametoka kwa Mafarisayo.

25 Wakamwuliza, wakamwambia, Mbona basi wabatiza, ikiwa wewe si Kristo, wala Eliya, wala nabii yule?

26 Yohana akawajibu akisema, Mimi nabatiza kwa maji. Katikati yenu amesimama yeye msiyemjua ninyi.

27 Ndiye yule ajaye nyuma yangu, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya kiatu chake.

*Wale watu walikuwa wametoka kwa Mafarisayo, wakawa wanamshangaa Yohana ni vipi abatize wakati yeye siyo Kristo siyo Eliya wala Nabii yule? Inaonyesha wazi kuwa, wale nao pia hawakuwa wanamjua Yohana k**a Nabii aliyetabiriwa, Wao walijua atakaenza kubatiza ni Kristo na Nabii yule, Yohana akawajibu Amesimama yule wasiyemjua, huyo ambae atakuja nyuma yake ndiye Nabii yule ndiye Kristo. 👇*

Yohana 1:29 Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!

30 Huyu ndiye niliyenena habari zake ya kwamba, Yuaja mtu nyuma yangu, ambaye amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu.

*Yohana 👆 Anawafahamisha kuwa huyu Yesu ndiye Muhusika ambae ninyi mlikuwa mkimuuliza, nikawapa habari zake, lakini wao hawakumjua pamoja na kwamba walijua ujio wake lakini bado hawakumjua kuwa ni Yesu, hawakutaka kukubali kuwa Yesu ni Kristo.*

Yohana 7:25 Basi baadhi ya watu wa Yerusalemu wakasema, Je! Huyu siye wanayemtafuta ili wamwue?

26 Na kumbe! Anena waziwazi, wala hawamwambii neno! Yamkini hao wakuu wanajua hakika ya kuwa huyu ndiye Kristo?

27 Lakini huyu twamjua atokako; bali Kristo atakapokuja hakuna ajuaye atokako.

*Watu hao 👆🏻 Bado hawakutaka kuamini kuwa Yesu ni Kristo, kwa sababu wao hawakujua kuwa Kristo ndiye huyo huyo Nabii yule, wao walijua kuwa Kristo na Nabii yule ni wawili tofauti, Swali la Kujiuliza Je! ni kweli Yesu ndiye NABII yule?*

Yohana 6:11 Basi Yesu akaitwaa ile mikate, akashukuru, akawagawia walioketi; na kadhalika katika wale samaki kwa kadiri walivyotaka.

12 Nao waliposhiba, aliwaambia wanafunzi wake, Kusanyeni vipande vilivyobaki, kisipotee cho chote.

13 Basi wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili, vipande vya mikate mitano ya shayiri vilivyowabakia wale waliokula.

14 Basi watu wale, walipoiona ishara aliyoifanya, walisema, Hakika huyu ni nabii yule ajaye ulimwenguni.

*Yesu Kristo ️👆 Ndiye Nabii yule, kwa nini ni Nabii yule kwa sababu, Ishara na dalili zake zipo sawa, unaweza kujiuliza, hao watu walijuaje kwamba, atakuja Nabii? ni hapa. 👇*

Kumbukumbu la torati 18:18 Mimi nitawaondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe, nami nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.

*MUNGU 👆🏻alishawaambia Kuwa atawaondokeshea Nabii mfano wa Musa, japo katika andiko hili Waislamu hujaribu pia kumpachika Muhammadi wakisema, Musa alioa Muhammad nae alioa, Musa alipigana Vita Muhammadi nae alipigana Vita, hivyo ni vigezo vya kawaida visivyoendana kwani Kuoa kupigana Vita, siyo Vigezo vya Unabii mfano wa Musa, Daudi alioa na alipigana Vita, lakini yeye siyo mfano wa Musa! (NITAKUJA KUANDAA SOMO LA JE! MUHAMMADI NI NABII MFANO WA MUSA?) hapa tuendelee kuyaangazia maandiko ndani ya BIBLIA yamemtaja nani kuwa ndiye Nabii Mfano wa Musa?*

Matendo 3:19 Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana;

20 apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamani;

21 ambaye ilimpasa kupokewa mbinguni hata zije zamani za kufanywa upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu tokea mwanzo wa ulimwengu.

22 Kwa maana Musa kweli alisema ya kwamba, Bwana Mungu wenu atawainulieni nabii, katika ndugu zenu, k**a mimi; msikieni yeye katika mambo yote atakayonena nanyi.

23 Na itakuwa ya kwamba kila mtu asiyemsikiliza nabii huyo ataangamizwa na kutengwa na watu wake.

24 Naam, na manabii wote tangu Samweli na wale waliokuja baada yake, wote walionena, walihubiri habari za siku hizi.

25 Ninyi mmekuwa watoto wa manabii na wa maagano yale, ambayo Mungu aliagana na baba zenu, akimwambia Ibrahimu, Katika uzao wako kabila zote za ulimwengu zitabarikiwa.

26 Mungu, akiisha kumfufua mtumishi wake Yesu, alimtuma kwenu ninyi kwanza, ili kuwabarikia kwa kumwepusha kila mmoja wenu na maovu yake.

*Mtume Petro anatuambia kuwa, huyo nabii mfano wa Musa, ni Yesu Kristo, na Yesu alijithibitisha kwa kusema.👇🏼*

Yohana 3:14 Na k**a vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa;

15 ili kila mtu aaminiye awe na uzima wa milele katika yeye.

*Maandiko yanazidi kutuonyesha kuwa aliye mfano wa Musa ni YESU. 👇*

Waebrania 4:1 Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye kuushiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini sana Mtume na Kuhani Mkuu wa maungamo yetu, Yesu,

2 aliyekuwa mwaminifu kwake yeye aliyemweka, k**a Musa naye alivyokuwa, katika nyumba yote ya Mungu.

*Hivyo watu wakawa wanamtazamia nabii huyo yaani Nabii yule ambaye alisemwa na Musa kuwa atakuja, Na alipokuja Yesu walinena. 👇*

Yohana 7:37 Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.

38 Aniaminiye mimi, k**a vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.

39 Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.

40 Basi wengine katika mkutano walipoyasikia maneno hayo, walisema, Hakika huyu ndiye nabii yule.

*Waliotambua Utimilizo wa maandiko waliendelea kumtambua Nabii yule, 👇*

Mathayo 21:10 Hata alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu?

11 Makutano wakasema, Huyu ni yule nabii, Yesu, wa Nazareti ya Galilaya.

*YESU NDIYE NABII YULE HAKUNA MWINGINE ALIYETAJWA KATIKA MAANDIKO KUSEMA KUWA NI NABII YULE WANAOSEMA NI NABII YULE NJE YA YESU WANASEMA KWA VINYWA VYAO PASINA USHAHIDI WA MOJA KWA MOJA K**A ULIVYO KWA KRISTO YESU!*

*Quran inamtumbua kuwa Muhammadi ni Nabii lakini haijawahi kusema ni Nabii yule, k**a kuna mtu ambae anao ushahidi ndani ya quran kuwa kuna aya imesema kuwa Muhammadi ni Nabii yule toa ushahidi hapa*

BY ABEL SULEIMAN SHILIWA.

Usikose tarehe 25 Mbezi mwisho, mbezi Luis
14/09/2016

Usikose tarehe 25 Mbezi mwisho, mbezi Luis

30/08/2016

Bwana Yesu asifiwe sana!
Wiki iliyopita tuliangalia mfano wa 1 ili kujifunza jinsi Roho Mtakatifu anavyotumia “Uhuru wa Kristo”, ili kumsaidia mtu aweze kutembea katika mapenzi ya Mungu.
Mfano huo wa 1, ulihusu namna ya kuyajua mapenzi ya Mungu, kuhusu “mahali pa kuhubiri neno la Mungu”.
Leo – nataka tuangalie mfano wa 2, unaohusu Roho Mtakatifu kutumia “Uhuru wa Kristo”, kumjulisha mtu juu ya “hatari liyopo mbele yake, ili aweze kukuepusha nayo!”
Nakumbuka miaka kadhaa iliyopita, mama mmoja alinisimulia jinsi Mungu alivyomuepusha na ajali, alipokuwa anatoka mji mmoja, na kwenda mji mwingine alipokuwa anafanya kazi.
Mama huyo alisema, alipokuwa kwenye kituo cha basi akisubiri usafiri, lilikuja basi la kwanza lililokuwa linaelekea alikokuwa anataka kwenda, lakini alisikia moyoni “kufungika” na “kukosa uhuru” wa kulipanda
Kwa hiyo, akaamua kutopanda lile basi, na kuamua kusubiri basi lingine. Lile basi baada ya kupakia abiria – likaondoka! Yeye akasubiri hadi basi lingine lilipokuja, na baada ya kusikia “uhuru moyoni” wa kulipanda – akapanda na kuondoka nalo.
Baada ya kusafiri k**a mwendo wa lisaa limoja hivi ….wakakuta lile basi alilosikia moyoni – mwake “uzito” wa kulipanda, limepata ajali – na limeanguka, na kuua karibu robo tatu ya abiria waliokuwa wamepanda humo!
Yule mama akamshukuru Mungu kwamba, alitii ile hali aliyoisikia moyoni mwake – na kuamua kutolipanda lile basi! Mimi nikamwambia ya kuwa ni Roho Mtakatifu wa Mungu aliyemwekea ishara ile moyoni mwake, ili apate kumwepusha na hatari iliyokuwa mbele yake!
Yule mama asingetii vile viashiria vya Roho Mtakatifu moyoni mwake – vya “kusikia kufungika moyoni na kukosa uhuru wa kupanda” lile basi la kwanza, ina maana angekuwemo na yeye katika ile ajali mbaya iliyotokea!
Tunaona msaada huu wa Roho Mtakatifu, akipewa pia mtume Paulo katika safari zake. Kuna wakati mtume Paulo alipewa tahadhari ya hatari, katika safari ya kwenda Yerusalemu, iliyokuwa mbele yake.
Mtume Paulo aliwambia wenzake hivi: “Basi sasa, angalieni, nashika njia kwenda Yerusalemu hali nimefungwa rohoni, nisiyajue mambo yatakayonikuta huko; isipokuwa Roho Mtakatifu mji kwa mji hunishuhudia akisema, ya kwamba vifungo na dhiki vyaningoja” (Matendo ya Mitume 20:22,23).
Mtume Paulo aliposema “Roho Mtakatifu….hunishuhudia akisema….”; alitaka wenzake wajue ya kuwa aliwekewa kiashiria cha “kufungika rohoni” mwake, kwa ajili ya kumjulisha hatari zilizokuwa mbele ya safari yake – ikiwa ataendelea na mpango wa kusafiri k**a alivyopanga.
Lakini ukisoma Matendo ya Mitume 20:24, utaona ya kuwa, mtume Paulo aliamua kupuuzia lile onyo la Roho Mtakatifu, na kuamua kuendelea na safari k**a alivyopanga!
Roho Mtakatifu hakumkatia tamaa – bali alisema naye tena, na kumwonya juu ya hatari zilizokuwa mbele yake, ikiwa angeendelea na safari yake ya kuelekea Yerusalemu!
Onyo la pili alipewa akiwa amefika Tiro (Matendo ya Mitume 21:3, 4), akiwa njiani akielekea Yerusalemu. Onyo la tatu alipewa akiwa amefika Kaisaria akitokea Tiro kwa kupitia Tolemai (Matendo ya Mitume 21:7 – 14).
Onyo la nne alipewa akiwa amefika Yerusalemu, na wakati ghasia zikiwa zimeanza mjini pale kwa ajili yake (Matendo 22:17 – 21).
Kutokutii huko kwa mtume Paulo, kulivuruga sana maisha na huduma yake – kiasi cha kuondolewa hapo “akiwa mfungwa” ili apelekwe Rumi kwa ajili ya kusikilizwa kesi yake!
Ndani ya shuhuda hizi mbili nilizokushirikisha – juu ya yule mama aliyepona ajali na juu ya mtume Paulo – tunajifunza yafuatayo:
(i) Unaposikia moyoni mwako “uhuru wa kusafiri” umeondoka, na badala yake unasikia “kufungika”, au “kukinai” au “uzito” kusafiri – wakati ulikuwa unajiandaa kusafiri – ina maana Roho Mtakatifu anakupa ishara ya kuwa, ukisafiri k**a ulivyopanga, kuna jambo litakalotokea ambalo si zuri kwako. Tafadhali usipuuzie!
(ii) Ikiwa utapewa ujumbe k**a huo wa (i) hapo juu, na ukauelewa, lakini mazingira hayakuruhusu kuahirisha – basi – ingia katika maombi ili Mungu akusaidie kubadilisha mazingira hayo ili usisafiri! Au hata k**a ukisafiri, basi Mungu apate kukulinda na hatari zilizoko mbele yako! Hivi ndivyo ilivyotokea katika safari ya mtume Paulo, ya kutoka Yerusalemu akipelekwa Rumi kwenye kesi yake (Soma Matendo ya Mitume 27:9 – 44).
(iii) Si kila wakati ukisikia “kufungika” moyoni na kupoteza “uhuru” wa kusafiri – ina maana usisafiri kabisa! Kuna wakati mwingine ina maana – badili usafiri unaotaka kuutumia; au badili siku unayotaka kusafiri; au badili njia uliyokusudia kupita!
Ukijizoeza kuomba ushauri na ufafanuzi kwa Mungu, unaposikia viashiria vya Roho Mtakatifu k**a hivyo moyoni mwako, uwe na uhakika Mungu atakupa maelekezo sahihi wakati huo, juu ya kile utakachotakiwa kukifanya!
La msingi ninalokushauri – usipuuzie viashiria k**a hivi unapotaka kusafiri – hata k**a sababu inayokufanya usafiri ni ya muhimu sana! Gharama ya kupuuzia inaweza ikawa kubwa sana kwako!

Na mwalimu Christopher Mwakasege.

15/08/2016

NENO LA LEO KUTOKA KATIKA BIBLIA

Ulinisukuma sana ili nianguke;
Lakini Bwana akanisaidia.
Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu,
Naye amekuwa wokovu wangu

Zaburi 118:13-14
Psalms 118:13-14

The Holy Bible, Divine Book

09/08/2016

NENO LA LEO KUTOKA KATIKA BIBLIA

Mnifuate mimi k**a ninavyomfuata Kristo. Basi nawasifu kwa sababu mmenikumbuka katika mambo yote, nanyi mmeyashika yale mapokeo vile vile k**a nilivyowatolea.
Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanaume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanaume, kichwa cha Kristo ni Mungu

1 Wakorintho 11:1-3
1 Corinthians 11:1-3

The Holy Bible, Divine Book

27/07/2016

MITHALI 22;1

Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi; Na neema kuliko fedha na dhahabu.

18/05/2016

Neno la LEO.... Yakobo 4 👇

1 Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu?

2 Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi!

3 Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.

4 Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu.

5 Au mwadhani ya kwamba maandiko yasema bure? Huyo Roho akaaye ndani yetu hututamani kiasi cha kuona wivu?

6 Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.

7 Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.

8 Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.

14/05/2016

Kwa neema ya Mungu leo naomba niendelee na utaratibu wa kutoa dondoo kutoka katika mafundisho ya Kikristo..Yesu ni Kristo siyo Kristu ,soma TITO 2.13 ,Hivyo sisi ni Wakristo siyo Wakristu,Marko 9.38-42.Tumsifu Yesu Kristo

Source: Biblia ni Jibu

Ufufuo na Uzima imekuwa nyumba ya Uponyaji wa watu, kurudishwa kwa watu, kufarijiwa kwa watu, kufufuliwa kwa watu, kuwek...
10/05/2016

Ufufuo na Uzima imekuwa nyumba ya Uponyaji wa watu, kurudishwa kwa watu, kufarijiwa kwa watu, kufufuliwa kwa watu, kuwekwa huru kwa watu, na wengine kuoa na kuolewa. Ugonjwa wa kansa matibabu hugharimu mamilioni ya Hela lakini Ufufuo na Uzima wanaponywa bure.

Nyumba hii sasa ndio inahitaji kujengwa utaipa nini? Tumekuwa tukitoa lakini sasa ni wakati wa kujitoa. Na k**a Mungu alivyoahidi kwa kinywa cha baba yetu nyumba hii itakapojengwa kila kitu kitaongezeka zaidi...

Hizi ni account za Bank:
CRDB:Glory of Christ (T) Church
01J2096061900
Equity Bank
Glory of Christ (T) Church
3004211197855


Share na wengine habari njema hizi..

Address

Mbeya

Telephone

+255657919450

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tule Chakula Cha Kiroho posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share