ROCK FM RADIO

ROCK FM RADIO ROCK FM RADIO

🌍 Injili ya Milele Iwahi kwa Ulimwengu WoteLeo tunaungana na Waadventista duniani kote katika Sabato Maalumu ya Adventis...
14/03/2026

🌍 Injili ya Milele Iwahi kwa Ulimwengu Wote

Leo tunaungana na Waadventista duniani kote katika Sabato Maalumu ya Adventist World Radio (AWR).

Kupitia redio na vyombo vya mawasiliano, injili inaendelea kufika mahali ambapo wahubiri hawawezi kufika — vijijini, milimani, jangwani, na hata katika maeneo ambayo kuhubiri hadharani ni vigumu.

✨ Watu wengi wamepata tumaini
✨ Vijiji vimebadilika
✨ Maelfu wamekubali Kristo

Na yote haya yanawezekana kwa sababu watu wa Mungu wameamua kushiriki katika utume huu.

🙏 Sadaka yako leo inaweza kusaidia mtu kusikia injili kwa mara ya kwanza.

Hebu tushiriki pamoja kupeleka tumaini kwa ulimwengu.

📻 AWR – Sauti ya Matumaini kwa Ulimwengu








TANZIAMwenyekiti wa kanisa la Waadventista wa Sabato Nyanda za juu kusini mwa Tanzania Mch.Toto Ndege Bwire kusaga.Anata...
07/03/2026

TANZIA
Mwenyekiti wa kanisa la Waadventista wa Sabato Nyanda za juu kusini mwa Tanzania Mch.Toto Ndege Bwire kusaga.Anatangaza kifo cha Mch.Joseph T Msambwa wa Mtaa wa Malangali Wilaya ya Rungwe mkoa wa Mbeya, kilichotokea tarehe 06/03/2026 mkoani Mbeya.
Mwenyekiti anaungana na familia,waumini na wote walioguswa na msiba huo.Mazishi yatafanyika siku ya Jumatatu tarehe 09/03/2026 Mkoani Njombe.
"Naye atafuta kila chozi katika macho yao"

Katika jiji la St. Louis, Missouri, Marekani, Mkutano Mkuu wa 62 wa Konferensi Kuu ya Kanisa la Waadventista wa Sabato U...
05/07/2025

Katika jiji la St. Louis, Missouri, Marekani, Mkutano Mkuu wa 62 wa Konferensi Kuu ya Kanisa la Waadventista wa Sabato Ulimwenguni umemchagua Erton Köhler kuwa Kiongozi Mkuu wa Kanisa hilo Ulimwenguni kwa kipindi cha miaka mitano.

Ni utaratibu wa kawaida kwa Kanisa la Waadventista wa Sabato Duniani kufanya mkutano wa Konferensi Kuu kila baada ya miaka mitano. Mkutano huu huwaleta pamoja wajumbe kutoka mataifa mbalimbali duniani kote, ambapo miongoni mwa shughuli zake kuu ni uchaguzi wa viongozi wa Kanisa kwa ngazi ya Konferensi Kuu yenye makao yake makuu Marekani, pamoja na viongozi wa Divisheni 13 duniani.

Kabla ya kuchaguliwa kwake, Erton Köhler alikuwa Katibu Mtendaji wa Kanisa la Waadventista wa Sabato Duniani nafasi aliyoianza rasmi Aprili 14, 2021. Kabla ya hapo, aliwahi kuwa Kiongozi wa Divisheni ya Amerika ya Kusini, akihudumu katika eneo hilo lenye nchi nane tangu mwaka 2007, alipochaguliwa akiwa na umri wa miaka 36 na kuwa mmoja wa viongozi vijana zaidi kwa jukumu hilo katika historia ya Divisheni hiyo.

Köhler alizaliwa kusini mwa Brazil na tangu utotoni alitamani kufuata nyayo za baba yake ambaye alikuwa mchungaji wa Waadventista. Alipata Shahada ya Kwanza ya Theolojia mwaka 1989 katika Taasisi ya Mafunzo ya Waadventista, ambayo sasa ni Chuo Kikuu cha Waadventista cha Brazil. Mwaka 2008, alihitimu tena kutoka chuo hicho akiwa na Shahada ya Uzamili katika Theolojia ya Kichungaji. Kwa sasa, anaendelea na masomo ya Shahada ya Udaktari wa Huduma ya Kichungaji katika Chuo Kikuu cha Andrews nchini Marekani.

Kati ya mwaka 1990 hadi 1994, alikuwa mchungaji wa kanisa mahalia huko São Paulo. Baadaye, mwaka 1995, alichaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Vijana wa Konferensi ya Rio Grande do Sul, kisha mwaka 1998 akawa Mkurugenzi wa Huduma za Vijana wa Unioni ya Kaskazini-Mashariki mwa Brazil. Mwaka 2002, alirejea katika Konferensi ya Rio Grande do Sul k**a Katibu Mtendaji, na mwaka uliofuata akachaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Vijana kwa nchi nane za Divisheni ya Amerika ya Kusini (SAD) kabla ya kuwa Kiongozi wa Divisheni hiyo mwaka 2007.

Köhler amemuoa Adriene Marques, ambaye ni muuguzi, na wamejaliwa watoto wawili. Pamoja, wamekuwa mstari wa mbele katika huduma ya kanisa, wakihudumu bega kwa bega na kutembelea waumini duniani kote. Amekuwa akisisitiza mitazamo thabiti kuhusu athari za michezo ya kompyuta kwa vijana, upendeleo wa muziki unaojenga imani, na umuhimu wa kushikilia imani kuliko kuhusika kisiasa.

Katika nafasi yake mpya, Köhler ataongoza Kanisa la Waadventista wa Sabato Duniani akiwa ni kiongozi mkuu wa kiutawala. Atasaidia kuunda maono ya kimkakati ya utume wa Kanisa hilo lililoko katika nchi zaidi ya 200 duniani, kutoa mwongozo wa mafundisho, na kuunganisha maeneo mbalimbali kupitia utume wa pamoja. Atakuwa mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Utendaji ya Konferensi Kuu, mabaraza kadhaa ya kanisa, na atashirikiana kwa karibu na viongozi wa Divisheni, akiwakilisha kanisa katika matukio makubwa ya kimataifa.

Pia anatarajiwa kuhamasisha mipango ya utume wa dunia, kuhakikisha uthabiti wa mafundisho ya Waadventista, na kuimarisha taasisi za elimu, afya, na vyombo vya habari vya kanisa hilo.

Kanisa la Waadventista wa Sabato limekuwa dhehebu la Kiprotestanti la kimataifa tangu mwaka 1863, likiwa na zaidi ya waumini milioni 23 kote duniani. Biblia inatambuliwa kuwa mamlaka kuu ya mafundisho ya kanisa, na ujumbe wake ni kuwasaidia watu kupata uhuru, uponyaji, na tumaini katika Yesu Kristo.

08/01/2025
Siku 10 za Maombi, Wakati wa kipekee kusogea karibu na Mungu kuweka mipango yetu ya mwaka huu 2025 miguuni pake na kuruh...
08/01/2025

Siku 10 za Maombi, Wakati wa kipekee kusogea karibu na Mungu kuweka mipango yetu ya mwaka huu 2025 miguuni pake na kuruhusu atawale maisha yetu.

Wanenaji katika siku 10 za Maombi ni Mch. PAUL SEMBA na MRS. DEBORA URIO.

Shiriki pamoja nasi kupitia Hope channel Tanzania, AWR Tanzania na Rock FM Mbeya, kila siku saa 11.00 -01.00 Jioni.

Heri ya Mwaka mpya 2025, tunaanza mwaka na Bwana k**a ilivyo kawaida kwa kuwa na Siku 10 za Maombi, Wakati wa kipekee ku...
05/01/2025

Heri ya Mwaka mpya 2025, tunaanza mwaka na Bwana k**a ilivyo kawaida kwa kuwa na Siku 10 za Maombi, Wakati wa kipekee kusogea karibu na Mungu kuweka mipango yetu ya mwaka huu 2025 miguuni pake na kuruhusu atawale maisha yetu.

Shiriki pamoja nasi kupitia Hope channel Tanzania, AWR Tanzania na Rock FM Mbeya, kila siku saa 11.00 -01.00 Jioni.

Repost by  Tunamshukuru Mungu kwa Kuanza Vyema Mwaka 2025 kwa ibada ya kujiweka wakfu mbele za Mungu kwa mwaka mzima huu...
05/01/2025

Repost by

Tunamshukuru Mungu kwa Kuanza Vyema Mwaka 2025 kwa ibada ya kujiweka wakfu mbele za Mungu kwa mwaka mzima huu!

Pamoja na hiyo kulikuwa na huduma ya kuwaweka mikono viongozi wa Mwaka huu na kuweka wakfu watendakazi wa Kanisa 2025, ibada hii iliendeshwa na Mchungaji wa Mtaa Mch. Christopher Mk**a.

Tunawatakia Heri na Nguvu watendakazi wote wa Mwaka huu Mungu awe nanyi!

Tunakutakia baraka za BWANA kwa mwaka 2025, Asante kwa kuwa nasi, tunaendelea kukuletea kilichobora zaidi, ili kuilisha ...
31/12/2024

Tunakutakia baraka za BWANA kwa mwaka 2025, Asante kwa kuwa nasi, tunaendelea kukuletea kilichobora zaidi, ili kuilisha roho yako na akili yako kwa vipindi maridhawa.

Idara ya Huduma za Wanawake na Watoto Konferensi ya Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania imeendesha semina kwa Vijana wa k*...
25/12/2024

Idara ya Huduma za Wanawake na Watoto Konferensi ya Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania imeendesha semina kwa Vijana wa k**e na wa kiume yenye lengo la kuwakumbusha Maadili na Mwenendo wa Mkristo.

Semina hiyo imefanyika katika Kanisa la Waadventista Wasabato Mbeya Kati imeongozwa na Mkurugenzi wa Idara hiy Madam Stela Baravuga akishirikiana na wakufunzi wengine

Semina imehusisha Mitaa Mitano ambayo ni Mtaa wa Ituha,Ikulu,Uyole,Rwanda na Itezi

Rai imetolewa kwa Wazazi na Walezi kutenga muda wa ziada wa kuzungumza na Vijana ili kujua na kutatua changamto zinazowakabili.

Jumatano ya Maombirepost by Usinipite tena Mwokozi Jumatano hii 🙏Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.Yoha...
18/12/2024

Jumatano ya Maombi

repost by

Usinipite tena Mwokozi Jumatano hii 🙏

Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.
Yohana 14:14

Karibu tena Jumatano ya Maombi Kumwita Bwana

⏰ 12:30-01:00 ASUBUHI
11:30-12:00 JIONI

⛪ MBEYA KATI SDA

Thamani ya maisha ya Mwanadamu, iligharimu uhai wa Mwana pekee wa Mungu, Damu yake ya Thamani ndiyo pekee iliweza kununu...
18/12/2024

Thamani ya maisha ya Mwanadamu, iligharimu uhai wa Mwana pekee wa Mungu, Damu yake ya Thamani ndiyo pekee iliweza kununua gharama za wokovu wa Mwanadamu.


Karibu katika wiki ya shukrani na maombi ikiletwa kwako na Kanisa la Waadventista wa Sabato Nyarugusu, Geita. Utabarikiwa na Mahubiri, Shuhuda, Shukrani na Maombi ya kipekee kwa juma zima, Kuanzia Tar 21-28 Disemba 2024, kuanzia saa 12.00 hadi saa 02.00 Usiku, Ibada hizi za kipekee zitarushwa Mbashara kupitia Hope Channel Tanzania | AWR Tanzania na Rock Fm Mbeya, huu utakuwa wakati wa pekee kumshukuru Mungu katika wiki ya mwisho ya kumaliza mwaka 2024.

Address

Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ROCK FM RADIO posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share