02/06/2020
SOMO:MAISHA YA IBADA KATIKA ROHO
MWALIMU:SALOME .U. MWAKAFWILA
SEHEMU YA 1
Namshukuru Mungu Mungu muumbaji wa mbingu na nchi kwa nafasi ya kukufundisha Jambo hili ili upate maarifa Mungu akubariki Sana utakayejifunza pamoja nami
Mtu yoyote anayemcha Mungu maisha ya ibada Ni sehemu ya maisha yake mda wowote kwa sababu ibada kwake Ni K**a kupumua huwa hai ndani yake mda wowote humuwaza Mungu na kumuona Mungu katika Kila Jambo tunamuona ayubu alikuwa mtu anayemcha Mungu tukisoma Ayubu1:1
Ayubu alikuwa mtu aliyemcha Mungu alikuakimtolea Mungu Kila wakati tunaona Ayubu 1:6
Tunaona Ayubu alimwona Mungu maeneo yote hata kwenye magumu yake tunaona Ayubu 1:21 ,Ayubu 2:10
NINI MAANA YA IBADA
Ibada Ni kitendo Cha kumwabudu Mungu kumuweka mbele kuliko chochote katika roho MAANA pasipokuwa mtu wa rohoni kumwabudu Mungu Ni ngumu Sana bila kuingia na kuwa na roho mtakatifu hakuna ibada halisia biblia inasema tukisoma
Yohana 4:21-24
Inasema MUNGU Ni ROHO na wamwabuduo imewapasa kumwabudu katika ROHO na kweli tunamuona Mungu na kumsikia KUPITIA ulimwengu wa ROHO nje ya kuwa rohoni na kuwa na ROHO MTAKATIFU
Hutokaa kuweza katika maisha yako ya wokovu kwa sababu tunakutana na Mungu KUPITIA ulimwengu wa roho
Tukimwabudu Mungu kwa kutanguliza Mambo yetu tunakuwa tayari tumeingia kwenye ibada ya sanamu
Ambayo Ni ibada ya sanamu Ni chukizo kwa Mungu
Tukisoma
Kutoka 20:1-5
Kwa Nini tunamwabudu Mungu katika roho
Tunaendelea wakati mwingine
Mubarikiwe