Forest Lutheran Church Mbeya

Forest Lutheran Church Mbeya Evangelical Lutheran Church, in Mbeya West church district, of the konde Diocese in Mbeya

Mkuu wa Jimbo la la Mlimba, KKKT Dayosisi ya Ulanga Kilombero, Mchg. Piana Mwenda akiweka wakfu vifaa vya kuwekea mishum...
01/09/2026

Mkuu wa Jimbo la la Mlimba, KKKT Dayosisi ya Ulanga Kilombero, Mchg. Piana Mwenda akiweka wakfu vifaa vya kuwekea mishumaa madhabahuni pamoja na vitambaa vya ibada za Jumuiya, vilivyotolewa na Jumuiya ya Meta.
Jumuiya ya Meta walitoa vyombo vya kuwekea mishumaa madhabahuni kwaajili ya matumizi ya ibada usharikani na pia vitambaa vya ibada za jumuiya kwaajili ya kuwekwa wakfu tayari kwa matumizi ya ibada.
Haya yalifanyika kwenye Ibada ya Jumapili tarehe 30/08/2026, Siku ya Bwana ya 13 Baada ya Utatu.

Mchungaji Mwenda aliambatana na Kwaya ya Uinjilisti usharika wa Ruaha waliotembelea usharika wa Forest katika siku hiyo ya Jumapili.

IBADA YA JUMAPILI 30/08/2026Tumpende na Kumjali Jirani Wetu - Zaburi 112:5-10 - 1Yohana 4:7-9 - 1Samweli 24:16-17Praise ...
01/09/2026

IBADA YA JUMAPILI 30/08/2026
Tumpende na Kumjali Jirani Wetu
- Zaburi 112:5-10
- 1Yohana 4:7-9
- 1Samweli 24:16-17

Praise Team wakiongoza Nyimbo za Sifa na Kuabudu.
Zaburi 100:4 Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake;

UGENI WA KWAYA YA UINJILISTI KUTOKA USHARIKA WA RUAHA.Jumapili tarehe 30/08/2026 usharika ulipokea ugeni wa Kwaya ya uin...
01/09/2026

UGENI WA KWAYA YA UINJILISTI KUTOKA USHARIKA WA RUAHA.
Jumapili tarehe 30/08/2026 usharika ulipokea ugeni wa Kwaya ya uinjilisti kutoka Dayosisi ya Ulanga-Kilombero, Jimbo la Kilombero usharika wa Ruaha. Ugeni huo uliokaa kwa siku mbili uliongozwa na Mkuu wa Jimbo la Mlimba Mchg. Piana Mwenda.

Ibada ya Jumapili ilipokea neno la Mungu kutoka kwa Mchg. Mwenda pamoja na huduma ya nyimbo mbalimbali kupitia Kwaya ya wageni kutoka Ruaha.

Usharika unawashukuru sana wageni wetu kwa upendo waliouonesha wa kufika Dayosisi ya Konde na unawaalika tena wakati mwingine wakaribie k**a Usharika, kwaya au mtu mmoja mmoja.

Awali akiwapokea wageni hao siku ya Jumamosi 29/08/2026 Mkuu wa Jimbo la Mbeya Magharibi, Mchg. Nancy Maro aliwashukuru kwa moyo wa amshirikiano hata kuwa tayari kusafiri umbali mrefu ili kuja kushirikiana na sisi kwenye huduma ya Kristo.

03/08/2026

Kwaya ya Usharika wakiimba wimbo wa utamaduni kwenye ibada ya Uimbaji Dayosisi tarehe 02/08/2026

03/08/2026

Kwaya ya Usharika wa Forest wakiimba kwenye Ibada ya Uimbaji Kidayosisi siku ya Jumamosi 01/08/2026 kanisa kuu Tukuyu.

02/08/2026

Kwaya ya Watoto katika ibada leo Jumapili 02/08/2026

Ni kesho Jumapili tarehe 26/07/2026
25/07/2026

Ni kesho Jumapili tarehe 26/07/2026

Ibada ya Jumapili tarehe 19/07/2026 ilihudumiwa na kwaya ya Usharika, Kwaya ya Uinjilisti Forest, kwaya ya vijana na Pra...
25/07/2026

Ibada ya Jumapili tarehe 19/07/2026 ilihudumiwa na kwaya ya Usharika, Kwaya ya Uinjilisti Forest, kwaya ya vijana na Praise Team.

Ibada iliongozwa na Mth. Yusufu Fungo na Neno lilitolewa na Mchungaji Kiongozi Lutengano Mwaijande.

Karibu uabudu nasi kesho Jumapili tarehe 26/07/2026. Ibada itaambatana na Sikukuu ya Idara ya Malezi ya Vijana

Zaburi 119:105 Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.Ibada ya Jumapili tarehe 19/07/2026Ujumbe: Neema...
23/07/2026

Zaburi 119:105 Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.

Ibada ya Jumapili tarehe 19/07/2026
Ujumbe: Neema ya Mungu Yatosha,
Mchg. Lutengano Mwaijande

Usharika wa Forest Wafanya Huduma ya Udiakonia.Usharika wa Forest wamefanya huduma ya udiakonia kwenye Hospitali ya Rufa...
23/07/2026

Usharika wa Forest Wafanya Huduma ya Udiakonia.

Usharika wa Forest wamefanya huduma ya udiakonia kwenye Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kwa kutoa sadaka mbalimbali kwa watoto wetu wenye changamoto ya utapiamlo.
Sadaka hiyo imetolewa kupitia Idara ya Malezi ya Vijana katika kuelekea kwenye kilele cha maadhimisho ya Sikukuu ya Vijana kidayosisi.

Akiongea baada ya kuwasilisha sadaka hiyo Katibu wa Idara ya Malezi ya Vijana Usharika wa Forest Bi. Ushindi Mwanyambo amesema kuwa Idara ya Vijana wamesukumwa kugusa maisha ya watoto kwa njia ya sadaka k**a Biblia inavyotuagiza kuwa tusichoke kutenda mema, na kuwa wanaamini kwa sadaka hiyo watoto hao watakuwa na afya njema hata kufikia umri wa ujana ambapo watakuwa na nguvu za kumtumikia Mungu, kusaidia jamii na kujenga nchi yetu.

Baadhi ya vitu vilivyowasilishwa k**a sadaka ni pamoja na sabuni, mchele, maziwa, mafuta ya kupaka, wipes, diapers, sukari na mafuta ya kula.

"Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho. Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio."

Address

Forest
Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Forest Lutheran Church Mbeya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Forest Lutheran Church Mbeya:

Shortcuts

Share

Category