Efatha Tukuyu

Efatha Tukuyu KANISA LA EFATHA TUKUYU, KANISA LA UPONYAJI NA UKOMBOZI KWA DAMU YA YESU (MARKO 7:34)

Tunawakaribisha wote njooni tuabudu pamoja🙏🙏🙏
08/02/2025

Tunawakaribisha wote njooni tuabudu pamoja🙏🙏🙏

08/02/2025
VITA VYA ROHONIInashambulia mambo mawili kwa mwamini1. Hushambulia imani yake katika kristo  2 Timotheo 4:7Wakati unapig...
28/10/2024

VITA VYA ROHONI
Inashambulia mambo mawili kwa mwamini
1. Hushambulia imani yake katika kristo 2 Timotheo 4:7
Wakati unapigana vita vya kiroho hakikisha unailinda imani iliyopokea, kwasababu vita ina lengo la kuiondoa imani, kwanini imani? Kwasababu imani ndio inatupa kurithi uzima wa milele kwasababu imani inatupa namna ya kuenenda na kutuadabisha kutenda vyema

Imani yako inashambuliwa na ubaya
Yohana 15:16, wokovu ulionao sio kwasababu ya mapenzi yako bali Yesu ndio aliyekuchagua kwa mpenzi yake kwasababu una wito na wewe huo wito aliokuitia ndio unajenga mahusiano na yeye.
Ubaya wowote unakuja maishani mwako unalengo moja tuu kukuondole imani yako nakukutoa katika wito wako nakufanya ache kuamini kile unacho amini

Imani yako ikishambuliwa utaonaKiu ya Ibada inaondoka naUchumi unanza kupolomoka

2. Pendo la Mungu ndani yetu Mathayo 24:12 & 1 Wakorintho 13:1
Ili uweze kushinda vita za kiroho Isaya 52:2
Mhubiri 1: 4-9 Vifungo vinavyo tokana na kizazi ulichotoka, vifungo hivi vinaweza kukufanya ukaikana imani yako na pendo lako likapotea.

Mch. Lusajo Hezrone.

ADUI HUTUMIA VIFUNGO VYA KIROHO K**A SIRAHA YA KUTUKANDAMIZAVifungo vya kiroho vina vyanzo vyake ambavyo huusiana na;1. ...
27/10/2024

ADUI HUTUMIA VIFUNGO VYA KIROHO K**A SIRAHA YA KUTUKANDAMIZA
Vifungo vya kiroho vina vyanzo vyake ambavyo huusiana na;
1. Vizazi tulivyo toka , vifungo hivi vinakandamiza maeneo yafuatayo katika maisha ya mtu
Ndoa, Elimu, Familia, Afya, na Uchumi.
2. Vifungo vinavyo tokana na eneo au mji
3. Vifungo vinavyo tokana na Nguvu za giza, utenda kazi katika biashara huletwa na waganga na wachawi . Vifungo hivi tutavishinda kwa kutumia jina na damu ya yesu.
MAMBO YA MSINGI YA KUZINGATIA KATIKA VITA VYA KIROHO
1. Sio kila wakati ni vita , vita vina mda wake Luka 22:53. Lazima uelewe ni wakati gani kuzimu inapambana na wewe Luka 4:13. Watu wengi wanashambulia katika mda wasiodhani 1Wathesalonike 5:3
Kushinda vita vya kiroho kunahitaji
Ufahamu wako, Hekima, na Nguvu ndani yako
SIRAHA AMBAZO SHETANI HUTUMIA KUTUSHAMBULIA
Maneno, Rungu ( kukata tamaa), Shetani hutushambulia kutokana na matajio tulionao Mithali 13:12, na Udhaifu wako, ni mlango mkubwa ambao shetani anatumia kukushambulia hiyo tambua udhaifu wako.
SILAHA ZA KUZITUMIA KUSHINDA VITA VYA KIROHO
1. UPENDO, Warumi 12:21
2.AMANI, Yohana 14:27
3. UVUMILIVU
4. UTII
5.IMANI 1Yohana 5:4
6. MATOLEO

SUNDAY SERVICE
Mch LUSAJO HEZRONE

USHUHUDAAnaitwa Suzana Obadia, anamshukuru Mungu kwa kumponjwa mtoto Agnes amabe alikuwa anasumbuliwa na Matundu Mawili....
16/09/2024

USHUHUDA
Anaitwa Suzana Obadia, anamshukuru Mungu kwa kumponjwa mtoto Agnes amabe alikuwa anasumbuliwa na Matundu Mawili.
Namshukuru Mungu kwa kumtumia mtumishi wake mchungaji Lusajo Hezron ambae amekuwa karibu nami kipindi chote cha changamoto toka kipindi cha ujauzito nilipo pita katika changamoto za uzazi kwa njia ya upasuaji ambao nilifanyiwa mara mbili.
Baada ya kujifungua binti yangu Agnes alianza kuonekana mzaifu na hakuna maendeleo katika ukuaji wake ikabidi twende hospitali ndipo alipo gundulika kuwa mtoto ana Matundu kwenye moyo.
Hali hii ilinifanya nipite kwenye maumivu makali na kukata tamaa lakini namshukuru mtumishi wa Mungu alisimama nami kipindi chote hicho.
Kupitia maombi ya mfungo wa mwezi watano tulikuwa na maombi ya wagonjwa ndipo binti yangu aliombwa na mchungaji na kumtamkia kuwa amepona
Mwezi wa nane hali ya mtoto ilibadilika ikabidi turudi hospitali ya rufaa MBEYA ambapo tulilazwa tukiwa kwenye uangalizi kwajili ya kujiandaa kwenda MHUMBILI kwajili ya upasuaji wa mtoto ili kuziba matundu kwenye moyo.
Namshukuru Mungu vipimo vilifanywa kwa mara nyingine tena Mtoto alionekana hana tena matundu kwenye moyo.
NAMSHUKURU SANA MUNGU KWA UPONYAJI HUU MKUU AMBAO UMEBAKI UKIWASHANGAZA MADAKTARI NA KILA MTU ALIE JUA UGONJWA ALIKUWA NAO BINTI YANGU.

SUNDAY SERVICEMch. LUSAJO HEZRONESOMO: KUSUDI LA YESU KUJA DUNIANI1. Kurejesha Uumbaji wake(ukombozi) Wakorisai 1:13Tume...
15/09/2024

SUNDAY SERVICE
Mch. LUSAJO HEZRONE
SOMO: KUSUDI LA YESU KUJA DUNIANI
1. Kurejesha Uumbaji wake(ukombozi) Wakorisai 1:13
Tumeamishwa toka ufalme wa giza hivyo chochote kinacho husika na giza hakihusiani na wewe, lazima ulitambue hili ya kwamba umerejeshwa ibilisi hana haki juu yako.

Vitu gani Mungu amekurejeshea
1. NAFASI, baraka ya Mungu maisha mwanadamu inabebwa na nafasi ya mtu kwa Mungu.
2. MAMLAKA, Mungu alituumba tutawale na sio kutawaliwa kwa yeyote uliyemwanini Yesu unapewa mamlaka.
3. UTUKUFU, Wingi wa vitu vinavyo kuzunguka. Utukufu ndio unatufanya tusife mapema

Luka 4:18
Hivyo basi kwa kila aliye mwamini yesu amebeba habari njema za wokovu kwa ulimwengu.

Yohana 17:18
Kila amwaminie Yesu ametumwa kutangaza habari njema, k**a unahitaji usaidizi wa ufalme wa Mungu hakikisha unatangaza habari njema za Yesu.

Mathayo 10:7, Tumepewa mwongozo wa kuwaendea wanadamu
[7]Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.
[8]Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.

Isaya 42:22
Watu tunao wapeleke habari hizi za Yesu ni Mateka na Wafungwa
Kuhubiri kwetu kuwe na udhirisho wa Roho mtakatifu ili kuweza kushinda falme na mamlaka zinazo washirilia hawa watu

1Wakoritho 2:4-5
Watu wanaodumu katika wokovu ni wale walio guswa na roho mtakatifu.

SUNDAY SERVICETarehe: 08 September Mch. Lusajo MwakifumbwaSOMO: KUSUDI LA YESU KUJA DUNIANIMathayo 18:11 & Yohana 3:16Ye...
09/09/2024

SUNDAY SERVICE
Tarehe: 08 September
Mch. Lusajo Mwakifumbwa
SOMO: KUSUDI LA YESU KUJA DUNIANI
Mathayo 18:11 & Yohana 3:16
Yesu alikuja kwajili ya mimi na wewe kutuokoa kwasababu tulikuwa tumepotea.
Hakuna mtu atakaye weza kuokolewa pasipo kutafutwa, k**a unataka kutembea na Yesu hakikisha unawaendea walio potea.
Mathayo 28:19-20
Unapo anza kuwaeleza watu habari za Yesu wafikie toba , Yesu anakuwa na wewe.
Yesu anapokuwa na wewe
1. Una akikishiwa uzima kwenye mwili wako, magonjwa yanawekwa mbali na wewe
2. Unapata uhakika wa kurithi uzima wa milele "mti unao zaa matunda Mungu anausafisha na kufanya uzae zaidi"
3. Kazi za mikono yako zinakupa faida " Mungu anathibitisha kazi zako"
Yesu alikuja kulipa deni za dhambi zetu
Isaya 53:4 & Wakorisai 1:13-14
Kwasababu ya hili kusudi la yesu kulipa deni ya dhambi zetu sisi tuko huru, iwe wanadamu na mapepo hawana uwezo wa kuhukumu . Unakibali cha kuvunja kila laana inayo kushikilia
K**a bado unateswa na upo kifungoni
1. Kila unacho fanya hakiendi
2. Unakosa kibali
3. Harufu mbaya
Warumi 8:31-35
Yesu alikuja kuvunja kazi na mamlaka ya ibilisi
1Yohana 3b & Wakolosai 2:14-15
Kwenye hii dunia isipo kua kuivunja kazi za ibilisi utakuwa mhanga wa matukio ya kazi za giza.
Yesu alishughulikia enzi na mamlaka
Waefeso 6:12 & Luka 10:19
Yesu walishugulikia falme na mamlaka ni jukumu letu kushughulikia wakuu wa giza.

MATUKIO KATIKA IBADA
18/08/2024

MATUKIO KATIKA IBADA

SUNDAY SERVICEMch. Lusajo HezronSOMO: UMBA TABIA MPYA UPATE KUFANIKIWA 2Timotheo 2:20-21Katika nyumba ya Mungu kuna watu...
18/08/2024

SUNDAY SERVICE
Mch. Lusajo Hezron
SOMO: UMBA TABIA MPYA UPATE KUFANIKIWA
2Timotheo 2:20-21
Katika nyumba ya Mungu kuna watu wana heshima na wengine hawana heshima, na katika nyumba ya Mungu kuna watu ambao ni k**a vyombo vya Miti na udongo pia kuna vyombo vya dhahabu na fedha ambao ni watu wale wa thamani katika nyumba ya Bwana.
Ikiwa mtu akajitenga na nakujitakasa atafanyika kuwa chombo cha heshima katika nyumba ya Mungu.

TABIA AU SIFA
Tabia ulio nayo inaenda mbali na kuwa mbele yako ilikukutambulisha wewe ni mtu wa namna gani.
JINA
Pia jina huvuma kumtambulisha mtu .
Tabia inauwezo wakutengeneza na kuharibu Jina lako.
Mungu haumbi tabia ya mtu, tabia ya mtu huumbwa na mtu mwenyewe,
Tabia ulio nayo ndio iliyo kufikisha hapo ulipo, hivyo tunavyo kuona sasa ni matokeo ya tabia yako.
Ibilisi akitaka kumpata mtu anatumia tabia ya mtu hivyo hata Mungu akimtaka mtu anaingia katika tabia yake.

TABIA HUTOKANA NA
1. Asili ya kuzaliwa, hutokana na wale waliotangulia katikati familia zetu
2.Tabia unayo jifunze kwa wazazi wako, sawa na vile unavyo yaona maisha wanaoishi.
3. Tabia unayojifunza kutoka kwa marafiki ulionao
4. Tabia uyanayo jifunza Mwenyewe

WEKA MIKAKATI YA KUISHINDA TABIA
Tabia yako inakusababisha umkosee Mungu
Yohana 8:42 Mathayo 7:17-18

LAZIMA UBADILISHE TABIA ULIO NAYO KUPITIA.
1. Neno la Mungu au fundisho la Mungu, ndio njia ya kwanza ya badiliko la Tabia yako. 2Tihometheo 3:16
2. Maonyo, yana kazi ya kubadilisha na kulekesbisha tabia ya Mtu, Maonyo wakati wote hayafurahishi bali yana maumivu yake. Ufunuo 3:19
3. Maongozi ya namna ya kuenenda ili utambue kipi kipo kwajili yako na kipi sio kwajili yako.
4. Kuadabishwa na kutiishwa

UKITAKA MUNGU AKUINGIZE KWENYE USTAWI
Zi shinde tabia
1. Tabia ya kiburi, ukiwa na tabia ya kiburi adui yako sio shetani bali ni Mungu mwenyewe kiburi ni kitendo cha kujihesabia haki usio stahili Hufanyika k**a ulivyo elekezwa Ukionywa au kukemewa unakasirika.

SUNDAY SERVICEMch. Lusajo HezroneVita ya kiuchumi hupigana katika akili yako, ili kushinda vita hivi lazima ubadili mtaz...
14/08/2024

SUNDAY SERVICE
Mch. Lusajo Hezrone
Vita ya kiuchumi hupigana katika akili yako, ili kushinda vita hivi lazima ubadili mtazamo wako.
2 Wakorithonto 5:17
Mtu akiwa ndani ya Yesu mwonekano wake haubadiliki lakini Yesu anabadilisha mtazamo wake na anaanza kujiona tofauti na ukiri wake unabadilishwa. Matazamio ya Mungu ni kwamba baada ya mtu kuokoka mtamazo na matarajio yake yawe tofauti na mtu ambaye haja okoka.
Utofauti kati ya alie okoka na ambae hajaokoka ndio humpa ushindi yule alie okoka kwasababu mtazamo wake umebadilishwa na imani yake imeimarishwa.
Haijalishi ni nini unapitia katika maisha yako mtazamo wako ndio utakao kutoa katika hizo changamoto
2 Wakorintho 10:3
Japo kubwa tunaishi katika mwili lakini hatupigani vita katika mwili bali kwa Roho, shetani uinuwa mawazo ndani yetu ambayo hutukwamisha pia mtu huwa na mawazo ndani yake ambayo yana mzuuia mtu kuchukua hatua na kusonga mbele. Hivyo basi mtu anatakiwa kuwa na mtazamo wa Mungu ndani yake akijiwazia mambo mema na akikiri kuwa na kesho njema na kukiri ushindi wake katika yale unayo pitia
Warumi 1:28
Unakuwa na Mungu moyoni mwako na akilini mwako, ili kanisa lisonge mbele linahitaji Watu wa Mungu wawe na Mungu kwenye akili zao. Chochote kinacho inuka kinyume na elimu ya Mungu lazima uitiishe ili uweze kushinda changamoto za dunia ishi elimu na elimu ya Mungu
Yeremia 10:11
Unaona nini ?
Kile unacho kiona katika macho ya rohoni kitarajie kukiona katika macho ya damu na nyama
Mwanzo 13:14
Ni mwaka wetu wa kumiliki umeona kile unacho enda kumiliki?
UTABADILISHAJE MTAZAMO WAKO
Kwa kusikia na kuona kwako
Usiambatane na Watu ambao wameshindwa kwasababu watakujengea hali ya kushindwa kutokana na maneno watakayo kuwa wanakuambia kila siku. Kwasababu Mungu ametumba tofauti na kila mtu na majira na nyakati zake usijifananishe na mwingine.
Waebrania 4:12
Ruhusu neno la Mungu libadilishe mtazamo wako, ikiruhusu neno la Mungu litakutenga na kila hali ya kujiwazia mawazo mabaya . Neno la Mungu ni kweli
Mtazamo wako ukibalika unakuwa muumbaji unaumba kile anachotaka kukiona

SUNDAY SERVICEMAOMBEZI YA MTU MOJA MOJA
04/08/2024

SUNDAY SERVICE
MAOMBEZI YA MTU MOJA MOJA

SUNDAY SERVICEMch. MUSHISOMO : KANISAMungu ameruhusu nguvu yake, utukufu wake na mamlaka  itembee ndani ya kanisa hivyo ...
04/08/2024

SUNDAY SERVICE
Mch. MUSHI
SOMO : KANISA
Mungu ameruhusu nguvu yake, utukufu wake na mamlaka itembee ndani ya kanisa hivyo k**a kutakuwa na mtu mahiri na bora anatakiwa atoke ndani ya kanisa.
Kwakuwa Mungu ameachilia nguvu yake kanisa linatakiwa kuwa na utosherevu. Lakini Adui hutupofusha kwa kuchomeka hila zake ili tusiwe watu tuliojaa neema na utukufu.
Adui amepandikiza silaha zake kushambulia kanisa
1. MAJIVUNO
2. KUJIHESABIA HAKI
3. KUJITAFUTIA HESHIMA
4. UBINAFSI
5. HUKUMU ZISIZO HAKI
6. UCHUNGU MOYONI
7. TAMAA
Kunakuwa na mpasuko katika kanisa huadhihirisha utendaji wa hizi silaha
Unatambuaje Kuwa mtu ameshabuliwa na hizi silaha
1. ROHO YA KUKATALIWA
2. ANABEBA UCHUNGU
3. KUKATA TAMAA
4. HOFU
5. MKANDAMIZO

Address

Mbeya

Telephone

+255756656620

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Tukuyu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share