Spiritual reborn ministry

Spiritual reborn ministry Huduma ya kuzaliwa upya kiroho
"Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili."

08/06/2026

YESU KRISTO NI MSHAURI WA AJABU.

Hallelujah!
Ukisoma biblia katika kitabu cha Isaya 9:6 kinasema hivi;

"Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani."

Ukisoma vizuri mstari huo hapo juu mtoto anaye ongelewa hapo ni Bwana wetu Yesu kristo ambaye jina lake moja wapo ni mshauri wa ajabu.

Ukiangalia kwa makini maisha yetu ya Kila siku yamejaa changamoto nyingi sana ambazo kwa namna ya kibinadamu huwa ni ngumu kuzitatua, wakati mwingine huwa tunaangaika kwa wanadamu wenzetu ili watushauri namna ya kuzitatua changamoto zetu lakini tunijikuta Bado tunakwama.

Sina maana ya kwamba ni vibaya kupokea ushauri kwa watu ila kabla ya kuomba ushauri kwa watu muombe kwanza Bwana wetu Yesu kristo maana yeye ni mshauri wa ajabu anaweza kukushauri vizuri namna ya kutatua changamoto yako.

24/05/2026

MUDA WA MUNGU NI SAHII KABISA.

Bwana wetu Yesu kristo asifiwe milele!!

Mungu amepanga Kila kitu kwenye maisha yetu kifanyike katika mda ambao ametaka yeye, sawasawa na Mhubiri 3:1 inayosema hivi;

"Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu."

Na ikumbukwe pia mda ambao Mungu anataka akufanyie kitu fulani kwenye maisha yako ni sahii kabisa, ijapokuwa kwa namna ya kibinadamu inaweza kuonekana k**a Mungu anachelewa kufanya.

Inawezekana umeomba sana hilo jambo lako kwa Mungu na ajajibu, unachotakiwa kujua Mungu anafanya vitu kwa wakati wake na wakati wa Mungu ni sahii kabisa kuliko wakati ambao unataka wewe, hivyo uwe mvumilivu kumsubili Mungu maana atafanya kwa wakati wake.

10/05/2026

ACHA KUMPENDA MUNGU KWA SABABU YA VITU.

Bwana Yesu kristo asifiwe milele!!

Ukiangalia na kuchunguza kwa makini watoto wengi wa Mungu leo hii, utaona wazi kabisa wengi wanampenda Mungu kwa sababu ya vitu ambavyo anawapa kwa mfano wapo wengine wanampenda Mungu kwa sababu ya baraka anazowapa, uponyaji, na mambo mengine mengi mazuri kutoka kwa Mungu.

Unachotakiwa kujua upendo wa kweli ni ule ambao hauna sababu, yaani haijalishi Mungu anatupa mema au mabaya bado tunatakiwa kumpenda Mungu kwa mioyo yetu yote.

Tujifunze kitu kutoka kwa Ayubu hata katika hali ya majaribu aliyokuwa anayapitia bado upendo wake na Mungu ulibaki vile vile, ukisoma kitabu cha Ayubu 2:9-10 kinasema hivi;

"Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washik**ana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe.Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena k**a mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake."

25/02/2026

MUNGU HAWEZI KUKUSAHAU KAMWE.
Bwana Yesu kristo asifiwe milele!!

Ukisoma biblia katika kitabu Cha isaya 49:14-16 kinasema hivi;

"Bali Sayuni alisema, YEHOVA ameniacha, Bwana amenisahau. Je! Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe. Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako ziko mbele zangu daima."

Ikiwa umesoma vizuri mistari hiyo, na k**a ulikuwa hujui basi unachotakiwa kujua Mungu hawezi kukusahau kamwe hata iweje.

Ijapokuwa Kuna wakati huwa tunakutana na changamoto mbalimbali za maisha, ambazo zinaweza kutufanya tuone k**a Mungu ametusahau na ayupo pamoja nasi, lakini kulingana na Neno la Mungu hawezi kukusahau na hata k**a itatokea wamekusahau watu wote lakini Mungu hawezi kamwe kukusahau na kukuacha pekee yako.

12/02/2026

KUADHIBIWA NA MUNGU.

Bwana wetu Yesu kristo asifiwe milele!

Je? Unajua ya kuwa Mungu huwa anatoa adhabu kwa watoto wake, pale ambapo wanakuwa wamefanya kinyume na Neno lake au maagizo yake.

Ikiwa hujui hili basi unachotakiwa kujua Kuna wakati tunapatwa na mabaya kwenye maisha yetu lakini ukiangalia kwa umakini utaona chanzo Cha hayo mabaya inakuwa sio shetani ila inakuwa ni Mungu anakuwa anatuadhibu kwa ajili ya dhambi zetu.

Ukisoma biblia katika kitabu Cha Mithali 3:11-12 kinasema hivi:

"Mwanangu, usidharau kuadhibiwa na BWANA, Wala usione ni taabu kurudiwa naye.Kwa kuwa BWANA ampendaye humrudi, K**a vile baba mwanawe ampendezaye."

Ikiwa umesoma vizuri mstari huo, utaona wazi kabisa adhabu kutoka kwa Mungu ni upendo wake kwetu sisi k**a watoto wake, pia lengo la Mungu kutuadhibu tunapokuwa tumefanya dhambi ni ili tutubu na kugeuka na kuziacha njia zetu mbaya.

Na ndio maana njia pekee ya kutoka kwenye adhabu ya Mungu ni kutubu na kuacha njia mbaya.

31/01/2026

NENDA kWA MUNGU AKUSAFISHE DHAMBI ZAKO.
Bwana Yesu kristo asifiwe milele.
Ukisoma biblia katika kitabu cha isaya 1:18 kinasema hivi;

"Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe k**a theluji; zijapokuwa nyekundu k**a bendera, zitakuwa k**a sufu."

Ikiwa unajiona k**a ni mwenye dhambi nyingi mbele za Mungu, basi usichojua bado Mungu anakuita na anataka uende kwake ili akusafishe dhambi zako zote na ndio maana anasema "njoni tusemezane"

Mtu ambaye anamkimbia Mungu kwa ajili ya dhambi zake, ni sawa na mgonjwa ambaye hataki kwenda hospitali kutibwa, Mungu anayo dawa kwa ajili ya dhambi zetu, hivyo basi mkimbilie Mungu ili akusafishe na kukuponya dhambi zako.

Usichokijua Mungu anatusamehe na kutusafisha dhambi zetu kwa ajili yake mwenyewe na sio sisi,
Na jambo hili unaliona ukisoma biblia katika kitabu cha Isaya 43:25 inasema hivi;

"Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako."

Usiogope kwenda kwa Mungu kwa ajili ya wingi wa dhambi zako.

02/01/2026

USIKUBALI SHETANI AJUE NA KUHARIBU ASILI YA NGUVU ZAKO.

Bwana wetu Yesu kristo asifiwe milele!

Ukisoma biblia katika kitabu cha Waamuzi 16:15-20 utaona jinsi ambavyo Delila akitafuta kujua chanzo au asili ya nguvu za Samsomi.

Ukiendelea kusoma habari hii utaona Samsoni hakusema kwa haraka asili ya nguvu zake, lakini Delila aliendelea kumsumbua hata ikifika mahali Samsoni akaweka wazi siri yake juu ya asili ya nguvu zake ukisoma Waamuzi 16:17 inasema hivi;

"Ndipo alipomwambia yote yaliyokuwa moyoni mwake, akamwambia, Wembe haukupita juu ya kichwa changu kamwe; maana mimi nimekuwa Mnadhiri wa Mungu, tangu tumboni mwa mama yangu; nikinyolewa, ndipo nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa dhaifu, nitakuwa k**a wanadamu wenzangu."

Na baada ya Delila kujua asili ya nguvu zake, utaona aliweza kumnyoa nywele zake na nguvu zake zikamtoka na ukiendelea mbele zaidi kusoma habari hii utaona wafilisti waliweza kumshika na kumtoboa macho yake na kisha kumuingiza gerezani.

Ukisoma Waamuzi 16:21 inasema hivi;

"Wafilisti wakamk**ata, wakamng’oa macho; wakatelemka naye mpaka Gaza, wakamfunga kwa vifungo vya shaba; naye alikuwa akisaga ngano katika gereza."

Ni kitu gani ? Cha kujifunza katika habari hii ya Samsoni na Delila, kitu kikubwa unachotakiwa ujifunze katika habari hii wewe k**a mkristo usikubali shetani akajua asili ya nguvu zako, kwani akijua atatafuta kila namna ya kuweza kuziondoa ili uwe dhaifu kwake.

Unaweza kujiuliza swali na kusema asili ya nguvu zako maana yake ni nini? Tunaposema asili ya nguvu zako inaweza kuwa ni maisha yako ya maombi, ibada, kumtolea Mungu sadaka au kitu chochote kinachofanya Mungu akupe nguvu zake ambazo zinakupa ushindi ziidi ya shetani.

Lakini ikiwa hujui asili ya nguvu zako basi tafuta na hakikisha unaijua asili ya nguvu zako, na usikubali shetani ajue na kuharibu hiyo asili yako.

21/12/2025

NJIA ZA KUKUSAIDIA KUWA MSAFI KATIKA MAISHA YAKO YA KIROHO.

Bwana wetu Yesu kristo asifiwe milele!!

Kati ya kitu kimoja wapo ambacho ni muhimu sana kwa watoto wa Mungu, basi ni pamoja na kuwa wasafi kiroho kwani usafi wa roho zetu ndio ambao unavuta uwepo wa Mungu kwenye maisha yetu.

Ukiangalia maisha ya watoto wengi wa Mungu tuko makini sana kusafisha miili yetu ya nyama na si roho zetu, tunaposema kuwa mchafu kiroho maana yake ni kuwa na dhambi ndani yako, vifungo vya kiroho, mapepo na mengine mengi.

Zipo njia nyingi ambazo ukijifunza kuzifuata zinaweza kukusaidia kuyafanya maisha yako ya kiroho kuwa masafi, moja wapo ya njia hizo ni hizi:

Njia ya kwanza;
Jifunze kufanya maombi ya toba au kuungama au kutubu dhambi zako mara kwa mara.

Ukisoma biblia katika kitabu Cha 1 Yohana 1:9 kinasema;

"Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote."

Unapofanya maombi ya toba unakuwa k**a unaoga ndani ya roho yako.

Njia ya pili;
Jifunze kusikiliza mafundisho ya Neno la Mungu mara kwa mara.

Ukisoma biblia katika kitabu Cha Yohana 15:3 kinasema;

"Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia."

Hayo ni maneno ya Yesu kristo aliwaambia wanafunzi wake wamekuwa wasafi kwa sababu ya Neno la Mungu alilowaambia, hivyo basi hata wewe ukijifunza kusikiliza mafundisho ya Neno la Mungu mara kwa mara yatakufanya kuwa msafi kiroho.

Njia ya tatu;
Jifunze kuwa mtendaji wa Neno la Mungu au jifunze kuepuka dhambi.

Ikumbukwe dhambi ndio ambayo inachafua roho zetu, hivyo ukijifunza kuwa mtendaji wa Neno la Mungu au kuikwepa dhambi kwenye maisha yako basi utakuwa msafi kiroho.

Na ndio maana biblia inasema tufanye vita na dhambi Kwenye maisha yetu na tuishinde jambo hili unaliona ukisoma biblia katika kitabu cha Waebrania 12:4 kinasema hivi;

"Hamjafanya vita hata kumwagika damu, mkishindana na dhambi;"

09/12/2025

SHETANI NI MWIZI.

Bwana wetu Yesu kristo asifiwe milele!!

Ukisoma biblia katika kitabu Cha Yohana 10:10 kinasema hivi;

"Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele."

Ikiwa umesoma vizuri mstari huo hapo juu, utaona vitu vitatu ambayo shetani anaweza kufanya kwetu, shetani ni mvivi ambaye anaiba vitu vyetu lakini pia anachinja na kuharibu vitu vyetu.

Mambo mengi mabaya ambayo yanayoweza kutupata kwenye maisha yetu ni matokeo ya shetani ambaye anaweza kuiba baraka, afya, na pia anaweza kuchinja au kuua na kuharibu vitu vyetu vizuri kutoka kwa Mungu.

Kitu cha muhimu unachotakiwa kujua huwezi kulinda vitu vyako au kujilinda mwenyewe ziidi ya uharibifu unaotoka kwa shetani na ndio maana ukisoma Zaburi 127:1 inasema hivi;

".....BWANA asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha bure."

Hivyo basi Mungu pekee yake ndiye anayeweza kukupa ulinzi ziidi ya uharibifu unaotoka kwa shetani.

Ukisoma Ayubu 1:9-10 inasema hivi;

"Ndipo Shetani akamjibu BWANA, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha BWANA bure? Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi."

25/11/2025

USIACHE KUJIFUNZA NENO LA MUNGU.

Jina la Bwana wetu Yesu kristo lisifiwe milele!

Ikiwa umeokoka au umemwani Yesu kristo kwenye maisha yako, basi unakuwa umefanyika kuwa mwanafunzi wa Yesu kristo.

Na moja wapo ya jukumu kubwa la mwanafunzi ni kufundishwa, hivyo basi ikiwa wewe ni mwanafunzi wa Yesu kristo unachotakiwa ni kufundishwa Neno la Mungu siku zote.

Na moja wapo ya agizo kubwa ambalo Yesu kristo aliwaagiza wanafunzi wake wa kwanza ni kuwafanya watu kuwa wanafunzi wake na kuhakikisha wanafundishwa Neno la Mungu.

Jambo hili unaliona Ukisoma Mathayo 28:18-20 biblia inasema hivi;

"Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa daharI"

Address

Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Spiritual reborn ministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share