01/09/2015
MUENDELEZO WA SOMO LA NAMNA YA KUOMBA BY ASKOFU MWAKASEGE NILI WEKA PAGE MOJA KATI YA PAGE NNE NAMALIZIA PAGE TATU ZILIZO SALIA NA SOMO LETU LITAISHIA APO KAA TAYARI KWA SOMO LINGINE NA MUNGU AKUBARIKI WAWEZA KU COMENT POPOTE UNAPOHISI HAPAELEWEKI AMA KUNA LOLOTE ILI TUWEZE KUWEKANA SAWA SOMO JEMA-----Mweleze Mungu haja zako. Ongea na Mungu kwa uwazi na ukweli. Japo
anazijua haja zetu, lakini ameagiza kuwa tumwombe ndipo atafanya.
‘aombaye hupokea’ yaani; asiyeomba, hapati. Mungu anasema tumpelekee
hoja zenye nguvu (Isa 41:21). Omba vitu vizuri na mambo makubwa ili
upewe (pray for good things and big things)
5.FANYA MAOMBI YA VITA VYA ROHONI. *Efe 6:10-13 *2Kor 10:3-5
Baada ya kumwendea Mungu na kumweleza mahitaji yako, sasa simama k**a ‘mfalme’,
kwasababu wewe ni ‘mfalme’ (Ufu 5:8), tumia mamlaka yako ya kifalme, ongea na
hali/hitaji ulilokuwa unaliombea, na kwa mamlaka, amuru iwe k**a vile
ulivyoomba/unavyotamani. Ndio maana Bwana Yesu alipokabidhiwa mamlaka yote na
Mungu, naye akatukabidhi sisi (kanisa lake) “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga
nyoka na nge na nguvu zote za yule adui. Wala hakuna kitakachowadhuru” (Luk 10:19,
Yer 1:10, Yak 4:7). Tuma neno lenye mamlaka katika hali/jambo ulilokuwa unaliombea,
Amuru iwe vile ulivyokuwa unamwomba Mungu iwe. Kemea kila roho ya shetani
inayoweza kuwa inasababisha tatizo katika swala lako.
6.OMBEA ULINZI JUU YA ULIYOYAOMBEA. *Math 6:13a
Baada ya kupiga vita vya kiroho, weka ulinzi katika yale uliyoyaombea, ili shetani na
mapepo yake wasiweze kuirudia hali/jambo/mtu yule uliyemkomboa kwa maombi ya
vita. Yesu alisema shetani akifukuzwa mahali, haendi mbali, anasubiri kuona k**a
atapata upenyo wa kuparudia mahali pale alipokuwa kwanza. (Math 12:43-45). Kwahiyo,
usipoweka ulinzi, kuna uwezekano wa adui kurudi na kuliharibu zaidi lile jambo
uliloliombea na kulipata.
Kumbuka, unapoomba vizuri, unapokea papo hapo (katika ulimwengu wa roho), lakini
udhihirisho wake katika ulimwengu wa mwili, unaweza kuchukua muda fulani. Hivyo
katika muda huo wa kusubiri, shetani anaweza akapita na kuzuia au kuharibu kile
unachokisubiri kidhihirike katika ulimwengu wa mwili. Ndio maana Yesu alitufundisha
kuombea ulinzi, “tuokoe na yule mwovu” (Math 6:13a). Weka ulinzi juu ya mambo yako
yote. Jengea wigo wa moto wa mbinguni (2Fal 6:16-17), Yafunike kwa damu ya Yesu na
agiza malaika walinzi walinde mambo yako masaa yote. Omba hivyo kila siku. (Zab
34:7, Zab 91:9-11, Ebr 1:13-14)
MSIFU, MWABUDU NA KUMSHUKURU MUNGU. *Math 6:13b
Yesu alianza maombi kwa kumsifu Mungu na kumtukuza. Na ak**aliza maombi yake
kwa kumtukuza Mungu tena. Akasema “kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu ni zako,
sasa na hata milele” ak**aliza. Kwahiyo nawe kwa kumaliza maombi yako, msifu na
kumshukuru Mungu tena, kwa ukuu wake, uaminifu wake, na ahadi zake juu yetu. Ndipo
ufunge maombi yako.
MUHIMU: TUMIA MAANDIKO KATIKA KUOMBA *Kol 3:16
-Katika kuomba kwako, mara zote tumia maandiko kumkumbusha Mungu ahadi zake .(Isa
43:26). Mungu analiangalia neno lake ili alitimize. Sababu pekee itakayomfanya Mungu
akupe alichoomba, ni ili kulitimiza neno lake. Hivyo, baada ya kumweleza unachohitaji
(kwa ajili yako au kwa ajili ya mtu unayemwombea) mpe Mungu andiko/neno lake
linalokupa wewe uhalali wa kuomba hicho kitu mbele zake na kupewa.
-Hata unapompinga na kumkemea shetani, baada ya kutoa amri yako dhidi yake, shetani
atasubiri kusikia andiko/neno linalomnyima yeye uhalali wa kushika alichoshika. Ndio maana
Yesu alimshinda shetani kwa neno la Mungu. Alisema “imeandikwa” na shetani akashindwa.
“Nao wakmshinda (shetani) kwa damu ya Yesu na kwa Neno” (Ufu 12:11)
MBINU ZA KUKUSAIDIA KUOMBA VIZURI KWA MUDA MREFU
1. CHAGUA MAHALI PAZURI PA UTULIVU. *Mk 1:35
ili uweze kuomba kwa utulivu na kwa umakini, chagua au tafuta mahali pazuri
patakapokupa utulivu katika kuomba (concentration in prayer). Ndio maana Mungu
alipenda kuongea na Musa juu ya mlima. (K*t 24:12-18). Hata Yesu alizoea kwenda
kuombea mlimani, mahali palipo mbali na vurugu za watu, alipenda kwenda
mlimani.
(Math 14:22-23). Tafuta mahali patulivu; chumbani, kanisani, mlimani (Math 6:5-6)
2. CHAGUA MUDA MZURI. *Mhu 3:1,7
Ili uweze kuomba kwa umakini mzuri, chagua muda mzuri ambao akili yako ma mwili
wako viko fresh. Usilazimishe kuomba hata k**a akili yako au mwili wako
umechoka sana. Kila jambo lina wakati wake. K**a umechoka sana, huo si muda
wa kuomba, bali wa kupumzika. Usilazimishe ratiba. ni bora upumzike ili baadaye
uweze kuomba vizuri baadaye. Usije ukajikuta unamkemea Yesu badala shetani.
Penda kuomba wakati una nguvu ya akili na mwili, ili uwe makini kuongea na
Mungu kwa akili timamu. Ndio maana Yesu alipenda kuamka alfajiri sana kwenda
kuomba mlimani. (Mk 1:35, Luka 4:42)
3. OMBA KATIKA ROHO (NENA KWA LUGHA). *Efe 6:18, Rum 8:26-27
Mbinu nyingine nzuri ya kuomba kwa muda mrefu na kwa ufanisi, ni kuomba kwa
Roho; yaani kuomba kwa kunena kwa lugha. Tunapoomba kwa akili za kibinadamu,
Mungu anasikia pia, lakini maombi yako yanakuwa na mipaka / limited kwasababu
akili ya mtu haijui kila kitu. Bali Roho wa Mungu anajua kila kitu. Naye hutupa
kipawa cha kuomba kwa lugha ya mbinguni iliyo bora zaidi. (Yuda 1:20, Mk 16:17,
1Kor 14:1-4, 15-16,7)
4. OMBA KWA KUFUNGA WAKATI MWINGINE. *Math 6:16-18
Kufunga kula kunasaidia kudhoofisha mwili, ili roho iwe makini zaidi kuongea na
Mungu kwa kina zaidi. Mwili huu siku zote haupendi kufanya mambo ya Mungu.
Na mwili ukiwa umeshiba, unakuwa na uchovu na uzito wa kufanya mambo ya
kiroho. Mbinu mojawapo ya kuudhibiti, ni kuunyima/kuupunguzia posho yake ya
chakula. Mwili ukidhoofika kiasi, roho yako inapata nguvu na upenyo mzuri zaidi
(Zab 35:13). Mashujaa wote wa imani walifunga na kuomba. Ndio maana Yesu
anasema ‘mfungapo’ akimaanisha ratiba ya kufunga, ipo. Inasaidia.
5. OMBA NA RAFIKI (PRAYER PARTNER). *Mhu 4:9-10
Neno la Mungu linasema, ni heri wawili kuliko mmoja. Kuna faida ya kuomba
pamoja na rafiki yako. Kwanza, mnapokuwa wawili au watatu, inaleta hamasa na
ari ya kuomba zaidi. Si rahisi kujisikia mvivu unapokuwa na waombaji wenzako.
Pili; nguvu ya kiroho inaongezeka. Neno linasema, mwombaji mmoja anafukuza
adui elfu moja, bali wakiwa wawili, wanafukuza (sio elfu mbili) bali elfu kumi!
Shangaa! (Kumb 32:20) Hiyo ni kanuni ya mbinguni/kanuni ya Ki-Mungu. Kadri
mnavyoongezeka, nguvu ya Mungu huongezeka.
Kwahiyo, wakati mwingine, omba na rafiki yako, unayemwamini, unayeweza
kumshirikisha mambo yako ya binafsi. Mashujaa wengi wa imani, walikuwa na
marafiki wa kiroho. (Prayer Partners). Kwa Mfano:- Math 17:1-9
Musa - alikuwa na Joshua, Haruni na Huri
Eliya - alikuwa na Elisha
Daniel - alikuwa na Shadrack, Meshack na Abednego.
Yesu - alikuwa na Petro, Yakobo na Yohana.
Paul - alikuwa na Barnaba, Timotheo na Tito.
Wewe Je? Uko na nani katika urafiki wa kiroho?
K**a huna rafiki wa karibu wa kuomba naye, usikurupuke kujichaglia. Tulia
umwombe Mungu akupe mtu atakayekuwa wa msaada kwako. Mtu
mtakayefungamanishwa naye katika roho, hata k**a mmetengana kijiografia,
lakini katika roho, mko na umoja mzuri wa imani. (Math 18:18-19)
6. OMBA KATIKA MKAO UNAOKUPA UHURU NA NGUVU ZAIDI.
Katika kuomba kwa muda mrefu, mkao uliouzoea utakusaidia kwenda mwendo
mrefu. Yakupasa kujua nguvu yako na udhaifu wako (strong point and weak point).
Wakati wa kuomba, epuka mikao inayokuchosha haraka na tumia mikao inayokua
nguvu zaidi. Kwa Mfano:- Ukiwa umechoka, usipende kuomba kwa kupiga magoti
au kwa kuegemea kitandani. Ni bora uombe ukiwa umesimama au unatembea
tembea, ili kuepuka usingizi na uchovu. Waombaji hodari wanaujua mikao
inayowasaidia kuomba maombi marefu. Wengine hawana mikao maalum, bali
wakiwa katika maombi, huwa wanabadilisha-badilisha mikao ili wasichoke. Hiyo ni
mbinu nzuri pia.
Mifano ya Mashujaa wa imani;
Ibrahim – aliomba kwa kusimama (Mwa 18:22)
Daniel - aliomba kwa kupiga magoti (Dan 6:10)
Paul - aliomba kwa kupiga magoti (Efe 3:14)
Yesu - aliomba kwa kulala chini (Math 26:38-39)
Eliya - aliomba kwa kukaa chini na
kuweka kichwa kati ya miguu (1Fal 18:42)
Mimi - huwa napenda kuomba kwa kutembea tembea
Naweza kumaliza kilomita nyingi chumbani kwangu
Nikitembea huku nikiomba.
Wewe Je? Unaujua mkao wa nguvu? K**a hujui, Tafuta kujua.
OMBA NA MUZIKI LAINI KWA KUMWABUDU MUNGU.
Muziki wa kiroho, na wataratibu, unaweza kukutengenezea mazingira mazuri sana
ya kuomba kwa muda mrefu. Muziki wa kuabudu, unavuta uwepo wa Mungu kwa
namna ya pekee. Neno linasema, waimbaji na wanamuziki walipoimba na muziki
ukapigwa, nao wakawa k**a mtu mmoja, utukufu wa Mungu ukashuka na kulijaza
lile hekalu hata makuhani hawakuweza tena kuhudumu (2Nyak 5:12-14). Kule
mbinguni, kila malaika wa sifa, ana kinubi (zeze/gitaa). Elisha hakutoa unabii,
mpaka mpiga kinubi alipopiga kwa ustadi, ndipo mkono wa Bwana (Roho wa
Mungu) alipokija juu yake, naye akatabiri.
Najaribu kukuonyesha, kuna connection kati ya muziki wa kiroho na utukufu wa Mungu.
Kwahiyo, ukiweza kuomba huku umeweka kanda au CD ya nyimbo za kiroho za taratibu,
utapata (experience) hamasa ya kiroho (motivation) na utasikia una nguvu ya kuomba kwa muda
mrefu. K**a unaweza, tengeneza kanda au CD maalum yenye nyimbo nzuri unazozipenda
wewe, ili uwe unaipiga wakati wa maombi. Utajikuta unaweza kuomba kwa muda mrefu na kwa
bubujiko zuri zaidi