14/04/2021
JE, MTU ALIYEOKOKA ANAWEZA KUFUATILIWA NA NGUVU ZA GIZA AU MIZIMU YA KWAO?
Zaburi 11:1-3
Zaburi 11:3 K**a misingi ikiharibika, Mwenye haki atafanya nini?
Hii misingi ni mifumo au maagano na mapatano na nguvu za vita kwenye familia zetu, koo zetu, jamii zetu na makabila yetu. Kumbuka mwenye haki ni yule aliyepata neema ya Mungu kuwa mjoli wake au mtumishi wake au mtu wake.
Yohana 17:14-15, " 14 Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa si wa ulimwengu, k**a mimi nisivyo wa ulimwengu 15. Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu".
Mizimu ni nini? Mizimu ni miungu iliyoabudiwa na inayoabudiwa na hujifunua kwa sura za wahenga{ ancestors) au mtu yoyote toka upande wa baba au mama aidha yu hai sasa au alishafariki.
Hii mizimu/miungu inaweza kuonekana kiuhalisia au kwa ndoto pia katika maumbo ya aina mbalimbali k**a vile nyoka, simba, chui, na kadhalika au babu, bibi ,shangazi, baba, mama na kadhalika aidha wako hai au hapana.
Ni kweli kuwa mtu aliyeokoka anaweza kifuatiliwa na nguvu za giza au mizimu. Kivipi? Kumbuka mwanadamu yuko katika utatu pia maana aliumbwa kwa mfano wa Mungu maana naye Mungu yuko katika utatu. Biblia inasema roho itendayo dhambi ndio itakayohukumiwa, so mtu anapoamua kumpokea Yesu awe Bwana na Mwokozi wake, roho yake ndo inaokoka bali nafsi na mwili wake unabaki katika hali ileile ya mwanzo. So nguvu za giza na hii mizimu inabaki na uhalali na kuishikilia nafsi yake, so maombi ya ukombozi( Deliverance) yanahitajika kuinunua nafsi yake, kuitakasa na kufuta kila hati ya madai, uhalali na vitu vyote visivyohitajika na mwili huwa unatiishwa tu kwa Neno la Kristo maana biblia inasema mtu akiipenda dunia hawez kumpenda Mungu.
Na kwa nini tunaziita nguvu za giza? Kumbuka nguvu za giza ni halisi ila zinatenda kazi nyuma ya pazia( bila mtu kujua/kufahamu, kwa kujificha) na ndo maana tunaziita giza. Giza ni kutokujua, kutokutambua kile kinachoendelea au kinachotokea au kinachotakiwa kujiri!