10/11/2024
1 Samweli(1 Samuel) 2
Ombi la Hana
1 Naye Hana akaomba, akasema,
Moyo wangu wamshangilia BWANA,
Pembe yangu imetukuka katika BWANA,
Kinywa changu kimepanuka juu ya adui zangu;
Kwa kuwa naufurahia wokovu wako;
2 Hakuna aliye mtakatifu k**a BWANA;
Kwa maana hakuna ye yote ila wewe,
Wala hakuna mwamba k**a Mungu wetu.
3 Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo;
Majivuno yasitoke vinywani mwenu;
Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa,
Na matendo hupimwa na yeye kwa mizani.