Mwl.Huruma Mwile, mwito mkuu - Greatest callings ministry

Mwl.Huruma Mwile, mwito mkuu - Greatest callings ministry Kutawanya Neno la Mungu kwa wenye mahitaji; wamjue Yesu - Luka 3:11 (Distributing Word of God to people- Luke 3:11)

30/07/2026

Bwana Yesu asifiwe!
Katika muendelezo wa kichwa Cha kijarida hicho, Cha KUKAMILISHWA KATIKA ROHO, pia Kuna:

KUZALIWA MARA YA PILI KWA MAJI NA KWA ROHO.
Ubatizo wote unahitajika katika maisha Yako, yaani kubatizwa Kwa MAJI na kubatizwa Kwa Roho, kwani ni ukamilifu wako katika roho Kwa agano jipya.(Yohana 3:5-6).

Warumi 6:4-5 inazungumzia ubatizo wa maji k**a ishara kufa na kufufuka pamoja na Yesu.

Katika kitabu Cha Luka 3:16, Yohana anazungumzia ubatizo wake wa maji Kwa watu, na ubatizo wa Yesu wa Roho mtakatifu, akisema, Mimi nawabatiza Kwa MAJI lakini yuaja mwenye nguvu kuliko Mimi ambaye Mimi sitahili kulegeza gidamu za viatu vyake, yeye atawabatiza Kwa Roho mtakatifu na moto.

Lakini pia katika kitabu cha matendo ya mitume, tunaona watu wakikamilishwa katika Roho Kwa kubatizwa, walipokutana na Paulo, "Ikawa Apolo alipokuwa korintho, Paulo akiisha kupita Efeso; akakutana na wanafunzi kadhaa wa huko; akawauliza, Je mlipokea Roho mtakatifu mlipoamini? Wakajibu, La, hata kusikia Kwamba Kuna Roho mtakatifu hatukusikia. Akawauliza, Basi mlibatizwa Kwa ubatizo Gani? Wakasema wa Yohana.
Paulo akasema, Yohana alibatiza Kwa ubatizo wa Toba, AKIWAAMBIA watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani Yesu.(matendo ya mitume 19:11-7)
Basi waliposikia HAYO , wakabatizwa Kwa JINA la Bwana YESU. Na Paulo alipokwisha kuweka mikono yake juu Yao; Roho mtakatifu akaja juu Yao; wakaanza kunena Kwa lugha na kutabili. Walikuwa wanaume 12.

Kwahiyo hapo:
1. Kuna ubatizo uliofanywa na Yohana (wa maji Yani kutubu na kumwamini Yesu ajaye.
2. Kuna ubatizo unaofanywa na Yesu) wa Roho mtakatifu.(Kubatizwa Kwa JINA la YESU)

N.B kutokana Neno Hilo hapo juu, Watu wengi, yaani mafarisayo, masadukayo, wakuu wa makuhani na wanasheria walikuwa wamebatizwa ubatizo wa maji ule wa Yohana, tatizo lilikuwa kukubali kubatizwa ubatizo wa Roho mtakatifu, yaani wa Yesu. Na hata Leo ndivyo ilivyo makanisani.

Kwahiyo hata Petro alipokuwa akisema tubuni, mkabatizwe kwa JINA la YESU, haukuwa ubatizo wa maji, sababu ubatizo wa Yohana wengi walikubali na kwenda Kubatizwa. Tatizo lilikuwa katika ubatizo wa Roho mtakatifu. Huku wakiamini Masihi aliyesemwa na Yohana yani Yesu bado kuja.

YESU ATUSAIDIE TUTAFUTE SANA KUKAMILISHWA NAYE!

BARIKIWA NA UWE NA SIKU NJEMA

25/07/2026

BWANA Yesu asifiwe!
Katika mfululizo wa mafundisho ya kijarida changu, kinachohusu kichwa KUKAMILISHWA KATIKA ROHO,
Moja katika vitu ambavyo Mungu amefanya juhudi Kwa wanadamu ni:

KUTURITHISHA JINA LAKE KWETU WOTE TUAMINIO (JINA YESU URITHI KWA WOTE WAAMINIO.)
Mungu ametoa JINA Hilo kutumika Kwa wote wanaoliamini, (Yohana 3:18), kwani JINA hili ni urithi Kwa wote wanao amini katika JINA hilo, Kwa kuwa ni JINA la Mungu mwenyewe (waebrania 1:1-4).

Kwahiyo ni mtu binafsi kuamini na kulitumia JINA lake Mungu(YESU)

Waebrania 9:16-19, inazungumzia namna urithi unavyofanya kazi, ni mpaka aliyetoa urithi afe.
INASEMA : "Maana agano la urithi lilipo, lazima iwepo mauti yake aliyelifanya. Maana agano la urithi Lina nguvu palipotukia kufa Kwa mtu; Kwa kuwa halina nguvu kabisa, ikiwa yu hai yeye aliyelifanya."

Mtume Petro aliwaambia watu waliochomwa na mioyo Yao baada ya kuwahubiri Neno, walioomuuliza yeye na mitume wengine tutendeje, akawaambia tubuni mkabatizwe kila mmoja Kwa JINA lake YESU KRISTO...(matendo ya mitume 2:38)
Nilitaka uone hapo alipowaambia tubuni mkabatizwe Kwa JINA la YESU KRISTO, ili JINA hilo lifanye na kwao pia KAZI k**a JINA la urithi.

WAWEZA KUOKOKA SASA, IKIWA UNAAMINI

BARIKIWA NA UWE NA SIKU NJEMA

23/07/2026

"But when it pleased God who separated me from my mother's womb, and called me by his grace,

To reveal his son in me, that I might preach him among the heathen; Immediately I conferred not with flesh and blood.

Neither went I up to Jerusalem to them which where apostles before me; but I went into Arabia, and returned again into Damascus."

(Galatians 1:15-17)

23/07/2026

"Alipoona vema kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu ili niwahubiri mataifa habari zake; mara sikufanya shauri na watu wenye mwili na damu; "

(Wagalatia 1:16)

"Wala sikupanda kwenda Yerusalemu Kwa hao waliokuwa mitume kabla yangu; bali nalikwenda zangu Arabuni, Kisha nikarudi tena Dameski."

(Wagalatia 1:17)

27/05/2026

UMPENDE JIRANI YAKO K**A NAFSI YAKO.
(MSITAZAME NAFSI ZA WATU KATIKA HUKUMU KWA KUWA HUKUMU NI YA MUNGU)
Bwana Yesu asifiwe, haya ni maneno utayakuta wagaratia 5:14 na kumbukumbu la torati 1:17-18.
Pia vifungu hivi vinafanana, vyote vinahusu maamuzi/kuamua mtu mmoja dhidi ya mwingine.

-Vyote vinazungumzia maamuzi HAYO k**a dhidi ya Mungu, kwani katika waraka wa Yohana, inazungumzia usipompenda JIRANI Yako huwezi kumpenda Mungu, kwahiyo ukimpenda JIRANI Yako (binadamu) ndio kumpenda Mungu asiyeonekana.

Na hio torati 1:16-17 inasema NIKAWAAGIZA WAKATI ULE WAAMUZI WENU, NIKAWAAMBIA, SIKIZENI NINYI MANENO KATI YA NDUGU ZENU, MKAAMUE KWA HAKI KATI YA MTU NA NDUGUYE, NA MGENI ALIYE PAMOJA NAYE. MSITAZAME NAFSI ZA WATU KATIKA HUKUMU; MWASIKIZE WADOGO NA WAKUBWA ; MSICHE USO WA MTU AWAYE YOTE, KWAKUWA HUKUMU NI YA MUNGU; NA LILE NENO LIWASHINDALO MNILETEE MIMI, NAMI NITAKISIKILIZA.
Hapo juu linasema,msiche USO WA MTU yeyote Kwakuwa HUKUMU ni ya Mungu.

Neno hili linafanana na LILE kitabu cha 2nyakati 19:5-7 linalosema "AKASIMAMISHA MAKADHI KATIKA NCHI, KATIKATI YA MIJI YOTE YENYE MABOMA YA YUDA, MJI KWA MJI; AKAWAAMBIA HAO MAKADHI, ANGALIENI MYAFANYAYO; KWAKUWA HAMFANYII MWANADAMU HUKUMU, ILA BWANA; NAYE YUPO PAMOJA NANYI KATIKA HUKUMU. BASI SASA HOFU YA BWANA NA IWE JUU YENU; ANGALIENI MKAIFANYE; KWA MAANA KWA BWANA MUNGU WETU, HAPANA UOVU WALA KUJALI NAFSI ZA WATU, WALA KUPOKEA ZAWADI.

-Na hapa pia linazungumzia juu ya maamuzi/kumfanyia mtu jambo LOLOTE ni kumfanyia Mungu,

Lakini linatoa angalizo kuwa Kwa Mungu(HUKUMU za Mungu/maamuzi ya Mungu yaliyo na usahihi) ni HAPANA UOVU, upendeleo wa NAFSI ZA WATU, Wala KUPOKEA ZAWADI.

Mfano : Kuna mfano mmoja katika kitabu cha mathayo 25:35-40) unasema hivi:
"Kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa MGENI, mkanikaribisha; nalikuwa uchi, mkanivika, nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia.
NDIPO wenye HAKI watakapomjibu, wakisema BWANA ni lini tulipokuona una njaa, tutakulisha, au una kiu tukakunywesha? Tena ni lini tulipokuona u MGENI, tukakukaribisha, au u uchi tukakuvika? Ni lini Tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?

Na mfalme atajibu, AKIWAAMBIA, Amini, nawaambia, kadri mlivyomtendea mmojawapo wa hao NDUGU zangu walio wadogo, mlinitendea Mimi.

Lakini 1nyakati 19:10, Neno linasema,
"Na kila mara, watakapowajia na teto NDUGU ZENU, wakaao mijini mwao, kati ya damu na damu, kati ya torati na amri, Sheria na hukumu, mtawaonya wasiingie hatiani mbele za BWANA, mkajiliwa na ghadhabu NINYI na NDUGU ZENU; FANYENI haya Wala hamtakuwa na hatia."

Kwahiyo tunapofanya jambo LOLOTE dhidi ya mtu, tunafanya dhidi ya Mungu sio mtu, (hivi huku ya kuwa mkimpokea mtumishi wa Yesu, na mmempokea Yesu Kristo, ndio hapo asemapo nalikuwa MGENI mkanikaribisha, wakati hakuwepo Duniani yeye Yesu NDIO KUOKOKA)

HUKUMU SAHIHI.
Kila maamuzi tunayoyafanya dhidi ya watu, ili yawe SAHIHI ni kuyafanya Kwa KUJIULIZA Neno la Mungu linasemaje juu ya jambo hili dhidi ya HUYU mtu, ninayetaka kumwendea, au kumfanyia Jambo.

K**A HUJAMKARIBISHA YESU K**A MGENI WAKO, MKARIBISHE SASA KUPITIA WATUMISHI WAKE WANAOKUJA KWAKO.

BARIKIWA NA UWE NA SIKU NJEMA

15/05/2026

NIMTUME NANI, NAYE NI NANI ATAKAYEKWENDA KWA AJILI YETU?

Bwana Yesu asifiwe, haya maneno utayakuta ndani ya mstari wa 8, katika kitabu cha Isaya sura ya 6.

Mstari wote unasomeka "KISHA NIKASIKIA SAUTI YA BWANA, AKISEMA , NIMTUME NANI, NAYE NI NANI ATAKAYEKWENDA KWA AJILI YETU? NDIPO NILIPOSEMA, MIMI HAPA, NITUME MIMI.

Bwana Yesu asifiwe, Ikiwa Mungu ni ROHO hivyo hutafuta watu hapa duniani ili kufanya KAZI yake au matendo mema Kwa niaba yake (yaani wawakilishi).
SWALI : Je hapa Duniani unamwakilisha nani?

Ikiwa hata shetani atafuta wawakilishi wake pia.
N.B : uwakilishi ni kufanya KAZI kwaniaba ya mtu mwingine/kitu kingine.

-Kwakuwa hapa Duniani tuna mwili na roho hivyo Mungu katika Yesu Kristo hutaka kutumia miili yetu kufanya KAZI yake k**a wawakilishi wake.
Neno la Mungu linasema Miili yetu ni hekalu la ROHO mtakatifu ( hivyo Mungu huweka ROHO yake ndani yetu, ili tumwakilishe katika matendo mema.

ISAYA ALISEMA: MIMI HAPA, NITUME MIMI.

Unaweza kusema hii ni Kwa watu Mungu aliowachagua, yaani watumishi k**a wachungaji, wainjilisti, waimbaji n.k na sio kila mtu.
SWALI: Je Mungu alikuleta Duniani Kwa kusudi gani? Kwasababu hakuna asiye na KAZI /uwakilishi hapa Duniani , usipokuwa upande huu unajikuta shetani amekupa mapepo yake umwakilishe hapa Duniani.

SADAKA:

Mfalme Daudi alisema: " Ee BWANA MUNGU WETU AKIBA HII YOTE TULIYOIWEKA ILI TUKUJENGEE NYUMBA KWA AJILI YA JINA LAKO TAKATIFU, YATOKA YOTE MKONONI MWAKO, NA YOTE NI YAKO WEWE. (1Mambo ya nyakati 29:16).

-Nilipokuwa nasoma hapa huu mstari, nikajua kuwa hivi tukiwa na Mali/fedha Mungu hutupa ili tumwakilishe pia katika KAZI ZAKE hapa Duniani, kwasababu fedha na dhahabu na Mali Zote Duniani ni ZAKE yeye.
Neno linasema: NIMTUME NANI NAYE NI NANI ATAKAYEKWENDA KWA AJILI YETU?

MUNGU KUTAFUTA MTU/SEHEMU YA KULIKALISHA JINA LAKE (YESU KRISTO) HAPA DUNIANI.
-Neno la Mungu linazungumzia juu ya Mungu kafuta mahali atakapoweka Jina lake (Jina la Yesu ) ndani yake, yaani Kwa mwanadamu aliye tayari, ili Mungu kuliweka Jina lake la Yesu ndani Huyo mtu.
-Yaani mtu wa kumwakilisha Mungu au ufalme wa mbinguni hapa Duniani.
1wafalme 5:3-4 inasema: " umemjua Daudi baba yangu jinsi asivyoweza kujenga NYUMBA Kwa Jina la BWANA, Mungu wake, kwa sababu ya vita vilivyomzunguka pande Zote, hata BWANA alipowatia watu chini ya nyayo ZAKE. Ila Leo BWANA, Mungu wangu amenipa amani kila upande; hakuna adui, Wala tukio baya. NAMI tazama nakusudia kujenga nyumba Kwa Jina la BWANA, Mungu wangu, k**a alivyomwambia Daudi baba yangu, AKISEMA, mwana wako, nitakaye mweka katika kiti Chake Cha enzi mahali Pako, ndiye atakayejenga NYUMBA Kwa Jina langu.

-Nilitaka uone hapo, sulemani alikuwa anaanza kujenga NYUMBA Kwa Jina la BWANA, Kwa namna nyingine tungesema, sulemani alipewa kufanya mambo Kwa muongozo wa Mungu, ili Mungu/Jina lake liwe ndani ya Israel, Yerusalem.

N.B: Hapo mwanzo hatukuweza kujenga NYUMBA Kwa Jina la BWANA kutokana na laana ya torati.

KUOKOKA

Ni kuamini Jina la Yesu ndani ya moyo wako, ili ROHO wa Mungu afanye KAZI NAWE katika Yesu Kristo (warumi 10:8-10).

N.B waongozwao na ROHO wa Mungu ndio Wana wa Mungu (Warumi 8:10)

KUMWAKILISHA YESU.

Yesu anasema katika Marko 16:15-16 :
" Enendeni ulimwenguni mwote mkaihubiri injili, Kwa kila kiumbe.
Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini atahukumiwa."

N.B MSAADA WA MAOMBI SALA YA TOBA, UPO BURE.

BARIKIWA NA UWE NA SIKU NJEMA!

05/04/2026

HERI YA PASAKA.

"Nao walipoingiwa na hofu na kuinama kifudifudi hata nchi, hao waliwaambia kwanini mnamtafuta aliye hai katika wafu."


Luka 24:5

Ni kweli SIKU ile Yesu alikuwa amefufuka, Kwani Petro na wenziwe waende kaburini kumtafuta, nasi tusimtafute Yesu Kwa waliokufa, Bali walio hai.
Ukitaka kuwa k**a mtu Fulani utamfuatilia njia ZAKE.

26/03/2026

AKAWAAMBIA LOLOTE ATAKALO WAAMBIA, FANYENI!(WHATSOEVER HE SAITH UNTO YOU, DO IT)
(Haya maneno utayakuta katika kitabu cha Yohana 2:5.)
Mstari wote unasomeka, " Mamaye AKAWAAMBIA watumishi, LOLOTE atakalowaambia, FANYENI.

Kwa lugha ya kingereza
"His mother saith unto the servants, whatsoever he saith unto you, do it." ( John 2:5)
Kuonesha msisitizo wa alichosema mama yake Yesu(Kwa lugha ya kingereza) ningesema
HIS MOTHER SAITH TO SERVANTS :"BE CAREFUL WITH WHAT HE SAITH TO YOU"
Hii ilikuwa harusi katika kana, mji wa Galilaya, na Yesu na mama yake Yesu (yaani Mariam) walikuwa wamealikwa huko (kila mtu kivyake Kwani Yesu alikuwa amealikwa na wanafunzi wake tofauti na mamaye).

SWALI KUJIULIZA
Mama yake Yesu alijuaje kuwa muujiza wa Divai, Yesu anaweza kuufanya. Na ni muujiza wa kwanza wa Yesu kwani hakuwa amefanya muujiza wowote.

Tena AKIWAAMBIA atakalowaambia fanyeni(Bila shaka alikuwa na Imani ya Yesu Kristo k**a mwana wa Mungu "NA NI NENO LA MUNGU")

Yesu angekuwa ni mtu tajiri, tungesema, mama yake alimfuata ili awasaidie fedha kwajili ya kununua Divai (kwani ALIMWAMBIA Yesu hawana Divai).

Katika mfulilizo wa mafundisho yangu ya Neno la Mungu kuhusu kichwa "NGUVU KATIKA KUTENDA NENO" NALO HILI NI MIONGONI MWA HAYO MASOMO.

UFUNUO KUHUSU MUNGU (ni Yesu).
Yohana 1:18, Neno linasema Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote; Mungu Mwana Pekee aliye katika kifua Cha Baba, HUYU ndiye aliyemfunua.
Kwahiyo tunakuwa makini na anayoeleza Yesu kwetu, kuhusu MUNGU, na anataka tufanye nini.

MWANZO WA KILA KITU.
Neno la Mungu linazungumzia MWANZO WA KILA KITU Kwa Neno la Mungu, ikiwa Huyo Neno alikuwako Kwa Mungu.
"Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwa Kwa Mungu. Huyo MWANZO alikuwako Kwa Mungu. Vyote vilifanyika Kwa Huyo; Wala pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika." (Yohana 1:1-3)

Kujua kuwa wanamzungumzia Yesu Kristo, pale mbele mstari wa 14, sura hiyo ya 1, inasema naye Neno alifanyika mwili , akakaa kwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu k**a wa Mwana Pekee wa Mungu.

UUMBAJI WA ULIMWENGU.
Hivi ebu fikiria Mungu, kuumba ULIMWENGU, angekuwa ndiye mfano wa fundi ujenzi ajengae nyumba kubwa Hadi kukamilika mfano wa Ghorofa, ingekuwa ni KAZI ngumu sana, Lakini Kwa Imani, twafahamu ya kuwa ULIMWENGU uliumbwa Kwa Neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa Kwa vitu vilivyo dhairi.(Waebrania 11:3)

Kwahiyo katika UUMBAJI Mungu alikuwa na Neno lake pamoja na Roho wake. K**a kitabu cha mwanzo 1:1-31 kinavyoonesha Mungu alikuwa akitamka kiwepo kitu Fulani nacho kinakuwepo.

UTIMILIFU WA MUNGU KATIKA MWILI.
Neno linasema "Angalieni mtu asiwafanye mateka Kwa elimu yake ya Bure na madanganyo matupu, Kwa jinsi ya mapokeo ya wanadamu, Kwa jinsi ya mafundisho ya awali ya ULIMWENGU, wala si Kwa jinsi ya Kristo." (Wakolosai 2:8)
-Kwa maana unapozungumzia UUMBAJI/kutokea Kwa ulimwengu lazima umzungumzie Yesu Kristo pia.
Neno linasema maana katika Yeye unakaa UTIMILIFU wote wa Mungu, Kwa jinsi ya kimwili. Inamaanisha unapozungumzia ULIMWENGU wa kimwili(ulimwengu tunaoishi), na utokeaji wa mambo ya Mungu katika ULIMWENGU wetu huu lazima umtaje Yesu/Neno.

CHAGUO LA UZIMA.
Katika Neno la Mungu, UZIMA umemanisha kumjua Yesu na Mungu aliyemtuma.
Na unajua ukimjua Yesu/Neno umemjua Mungu, kwani Yesu ni Neno litokalo Kwa Mungu.

MARIAM/MAMAYE ALIWAAMBIA:
"LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI" (Whatsoever he saith unto you do it.)

N.B Kwa hiyo Yesu ni Neno litokalo Kwa Mungu/Neno la Mungu.

K**A UMEAMINI NENO LA MUNGU KUPITIA YESU KRISTO NA UNATAKA AKUSAMEHE DHAMBI ZAKO (MSAADA WA MAOMBI INBOX)

BARIKIWA NA UWE NA SIKU NJEMA

Address

Mbeya

Telephone

+255754092142

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwl.Huruma Mwile, mwito mkuu - Greatest callings ministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share