26/03/2026
AKAWAAMBIA LOLOTE ATAKALO WAAMBIA, FANYENI!(WHATSOEVER HE SAITH UNTO YOU, DO IT)
(Haya maneno utayakuta katika kitabu cha Yohana 2:5.)
Mstari wote unasomeka, " Mamaye AKAWAAMBIA watumishi, LOLOTE atakalowaambia, FANYENI.
Kwa lugha ya kingereza
"His mother saith unto the servants, whatsoever he saith unto you, do it." ( John 2:5)
Kuonesha msisitizo wa alichosema mama yake Yesu(Kwa lugha ya kingereza) ningesema
HIS MOTHER SAITH TO SERVANTS :"BE CAREFUL WITH WHAT HE SAITH TO YOU"
Hii ilikuwa harusi katika kana, mji wa Galilaya, na Yesu na mama yake Yesu (yaani Mariam) walikuwa wamealikwa huko (kila mtu kivyake Kwani Yesu alikuwa amealikwa na wanafunzi wake tofauti na mamaye).
SWALI KUJIULIZA
Mama yake Yesu alijuaje kuwa muujiza wa Divai, Yesu anaweza kuufanya. Na ni muujiza wa kwanza wa Yesu kwani hakuwa amefanya muujiza wowote.
Tena AKIWAAMBIA atakalowaambia fanyeni(Bila shaka alikuwa na Imani ya Yesu Kristo k**a mwana wa Mungu "NA NI NENO LA MUNGU")
Yesu angekuwa ni mtu tajiri, tungesema, mama yake alimfuata ili awasaidie fedha kwajili ya kununua Divai (kwani ALIMWAMBIA Yesu hawana Divai).
Katika mfulilizo wa mafundisho yangu ya Neno la Mungu kuhusu kichwa "NGUVU KATIKA KUTENDA NENO" NALO HILI NI MIONGONI MWA HAYO MASOMO.
UFUNUO KUHUSU MUNGU (ni Yesu).
Yohana 1:18, Neno linasema Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote; Mungu Mwana Pekee aliye katika kifua Cha Baba, HUYU ndiye aliyemfunua.
Kwahiyo tunakuwa makini na anayoeleza Yesu kwetu, kuhusu MUNGU, na anataka tufanye nini.
MWANZO WA KILA KITU.
Neno la Mungu linazungumzia MWANZO WA KILA KITU Kwa Neno la Mungu, ikiwa Huyo Neno alikuwako Kwa Mungu.
"Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwa Kwa Mungu. Huyo MWANZO alikuwako Kwa Mungu. Vyote vilifanyika Kwa Huyo; Wala pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika." (Yohana 1:1-3)
Kujua kuwa wanamzungumzia Yesu Kristo, pale mbele mstari wa 14, sura hiyo ya 1, inasema naye Neno alifanyika mwili , akakaa kwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu k**a wa Mwana Pekee wa Mungu.
UUMBAJI WA ULIMWENGU.
Hivi ebu fikiria Mungu, kuumba ULIMWENGU, angekuwa ndiye mfano wa fundi ujenzi ajengae nyumba kubwa Hadi kukamilika mfano wa Ghorofa, ingekuwa ni KAZI ngumu sana, Lakini Kwa Imani, twafahamu ya kuwa ULIMWENGU uliumbwa Kwa Neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa Kwa vitu vilivyo dhairi.(Waebrania 11:3)
Kwahiyo katika UUMBAJI Mungu alikuwa na Neno lake pamoja na Roho wake. K**a kitabu cha mwanzo 1:1-31 kinavyoonesha Mungu alikuwa akitamka kiwepo kitu Fulani nacho kinakuwepo.
UTIMILIFU WA MUNGU KATIKA MWILI.
Neno linasema "Angalieni mtu asiwafanye mateka Kwa elimu yake ya Bure na madanganyo matupu, Kwa jinsi ya mapokeo ya wanadamu, Kwa jinsi ya mafundisho ya awali ya ULIMWENGU, wala si Kwa jinsi ya Kristo." (Wakolosai 2:8)
-Kwa maana unapozungumzia UUMBAJI/kutokea Kwa ulimwengu lazima umzungumzie Yesu Kristo pia.
Neno linasema maana katika Yeye unakaa UTIMILIFU wote wa Mungu, Kwa jinsi ya kimwili. Inamaanisha unapozungumzia ULIMWENGU wa kimwili(ulimwengu tunaoishi), na utokeaji wa mambo ya Mungu katika ULIMWENGU wetu huu lazima umtaje Yesu/Neno.
CHAGUO LA UZIMA.
Katika Neno la Mungu, UZIMA umemanisha kumjua Yesu na Mungu aliyemtuma.
Na unajua ukimjua Yesu/Neno umemjua Mungu, kwani Yesu ni Neno litokalo Kwa Mungu.
MARIAM/MAMAYE ALIWAAMBIA:
"LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI" (Whatsoever he saith unto you do it.)
N.B Kwa hiyo Yesu ni Neno litokalo Kwa Mungu/Neno la Mungu.
K**A UMEAMINI NENO LA MUNGU KUPITIA YESU KRISTO NA UNATAKA AKUSAMEHE DHAMBI ZAKO (MSAADA WA MAOMBI INBOX)
BARIKIWA NA UWE NA SIKU NJEMA