06/09/2022
Mungu alipowaumba Adamu na Hawa, hapakuwa na maumivu, wala mateso, lakini kwa nini siku hizi watu wengi wanateseka sana? Je, unataka kujua kwa nini? Acha nishiriki nanyi nyote kifungu cha maneno ya Mungu.
📝📝📝Mungu anasema:
*“Uchungu wa kuzaliwa, kufa, magonjwa na uzee uliopo katika maisha yote ya mwanadamu ulitoka wapi? Ni kwa sababu ya nini ndio watu walikuwa na vitu hivi mwanzo? Je, mwanadamu alikuwa na vitu hivi alipoumbwa mara ya kwanza? Hakuwa navyo, sivyo? Hivyo, vitu hivi vilitoka wapi? Vitu hivi vilikuja baada ya wanadamu kujaribiwa na Shetani na miili yao ikasawijika. Uchungu wa mwili, mateso yake na utupu wake, na pia masuala yenye taabu sana ya dunia ya binadamu yote yalikuja baada ya wanadamu kupotoshwa na Shetani, kutoka wakati Shetani alipoanza kuwatesa watu; matokeo yalikuwa kwamba walisawijika zaidi na zaidi. Maradhi ya wanadamu yakawa makubwa zaidi na mateso yao yakawa makali zaidi. Watu zaidi walihisi utupu na tanzia ya dunia ya binadamu na vilevile kutoweza kwao kuendelea kuishi hapo, na walihisi matumaini madogo zaidi kwa dunia. Yote haya yalikuja baada ya kupotoshwa na Shetani. Kwa hiyo, mateso haya yaliletwa na Shetani kwa wanadamu, na yalikuja tu baada ya wao kupotoshwa na Shetani na wakasawijika. … Hii ndiyo maana haiwezekani kwako kuwa na magonjwa, matatizo na kuhisi mwenye kutaka kujitia kitanzi na wakati mwingine pia kuhisi huzuni ya dunia, au kwamba maisha hayana maana. Hiyo ni kusema, kuteseka huku bado kuko chini ya uongozi wa Shetani; ni mojawapo ya udhaifu wa kusababisha mauti wa mwanadamu”*