27/04/2022
UPENDO WA MUNGU KWETU “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”
— Yohana 15:13 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”
— Yohana 3:16 UPENDO WETU KWA MUNGU NI AMRI “nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.”
— Marko 12:30 tena Kutoka 20 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
² Mimi ni Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.
³ Usiwe na miungu mingine ila mimi.
⁴ Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
⁵ Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
⁶ nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu. UPENDO WA SISI KWA SISI NAO NI AMRI Yohana 13 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
³⁴ Amri mpya nawapa, Mpendane. K**a vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.
³⁵ Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.1 Wakorintho 13 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, k**a sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
² Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, k**a sina upendo, si kitu mimi.
³ Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, k**a sina upendo, hainifaidii kitu.
⁴ Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
⁵ haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
⁶ haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;
⁷ huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
⁸ Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
⁹ Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;
¹⁰ lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika.
¹¹ Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema k**a mtoto mchanga, nalifahamu k**a mtoto mchanga, nalifikiri k**a mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto.
¹² Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana k**a mimi nami ninavyojuliwa sana.
¹³ Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.MBARIKIWE WAPENDWA