Love Living WORD

Love Living WORD RESIDENCE OF CHRIST AMBASSADORS

UPENDO NI NJIA YA KUISHINDA DHAMBI Warumi 5:8 " Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo...
05/12/2024

UPENDO NI NJIA YA KUISHINDA DHAMBI

Warumi 5:8 " Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi."
Upendo wa Mungu ulifanya dhambi iliyokuwa juu yangu kuondolewa na kuokolewa na adhabu ya mauti. Kila mtu aliyewahi kuzaliwa katika Dunia hii alistahili kufa ,kwa kuwa wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.

Hakuna mtu angeweza kusimama kwa ujasiri mbele za Mungu . Lakini Upendo wa Mungu unaushinda dhambi iliyoleta mauti katika ulimwengu, Ungali ukiwa mwenye dhambi Kristo alikuja kufa kwaajili ya dhambi zako!! Hili ni pendo linalopita fahamu ,biblia inasema ni rahisi kwa Mtu kufa kwa ajili ya mtu mwema lakini si mtu mdhambi. Katika hili Mungu ametuonyesha Upendo wake kwetu upitao ufahamu.

Mungu baada ya kutuokoa sisi pia alitupatia nguvu hiyo hiyo ya Upendo wake ndani yetu
Warumi 5:5 "na tumaini halitahayarishi; kwa maana pendo la Mungu limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Mtakatifu tuliyepewa sisi."
Kupitia hili twajua ya kuwa nguvu kuu ya Upendo katika ulimwengu unapatikana ndani ya Moyo wa mkristo halisi aliyemwamini Mungu. K**a wakristo tuliojawa na pendo la Roho wa Bwana basi ni jukumu letu kuumimina Upendo huu katika ulimwengu huu ,tuwe kielelezo katika Jamii kwa Kuudhihirisha Upendo wa Kiungu ,Maana kupitia hili tutajuliwa kuwa tu wanafunzi wa Bwana wetu Yesu Kristo.
1 Petro 4:7 Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala.
1 Petro 4:8 Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.

TAIFA TAKATIFU LA MUNGU Warumi 8:17 "na k**a tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; n...
28/11/2024

TAIFA TAKATIFU LA MUNGU

Warumi 8:17 "na k**a tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye."

Ikiwa wewe ni mrithi wa Mungu unarithi pamoja na Kristo ni kwamba yote yaliyo ya Kristo ni yako pia. Anasema yeye ni mzabibu na sisi ni matawi hivyo akaaye ndani yake huyo huzaa sana. Yesu anakutaka uzae matunda; yaani uwaongoze wengi kwa Mungu kupitia Yesu Kristo,wewe ni taifa kubwa na takatifu la Mungu kwa kuwa kupitia wewe Mtu mmoja mwenye Roho mtakatifu unaweza kuwaongoza maelfu ya watu kuwa wenye haki wa Mungu. Hivyo Mungu akikutazama anakuona k**a taifa kubwa lililo takatifu.

Yeye asema anakuja kuchukua Kanisa lisilo na ila wala kunyazi kanisa lililo takatifu na lisilo na lawama , wa kuwaandaa watu watakatifu ni wewe taifa takatifu.

Wewe ni kichwa Wala si mkia ,hivyo kwa neema uliyo ibeba hupaswi kubuluzwa wewe ni kichwa Cha taifa litakalo mwamini Mungu na kumtukuza katika kizazi hichi. Chukua jukumu la kuinui kizazi Cha watu wanao mcha Bwana kwa mioyo yao yote, Usiogopeshwe na Jinsi mambo yanavyo endelea kwenye Dunia hii kwa kuwa aliye ndani yako wewe k**a taifa takatifu ni mkuu kuliko aliye katika Dunia. Amekufanya kuwa mshirika wa tabia yake Mungu.

2 Petro 1:4 "Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa."

AMANI YAKE MUNGU Wafilipi 4:6-76 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kus...
20/11/2024

AMANI YAKE MUNGU

Wafilipi 4:6-7
6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.

7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.

Mara nyingi Wanadamu hujikuta kwenye matatizo ambayo hupelekea kutoweka Kwa amani katika maisha yao. Na nidhahili kuwa hakuna mtu ambaye atakuwa na ujasiri wa kusema Kwamba yeye hayuko na changamoto au hawezi kupata changamoto. Kumbuka maneno ya Bwana Yesu “Ulimwenguni mnayo dhiki” Hivyo huwezi kukwepa dhiki iliyo ulimwenguni humu. Lakini k**a Mungu mwenyewe anajua kuwa ipo dhiki hasa kwa wale wanao mwamini Kristo mwana wa Mungu. Anasema “... jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.”

Nini maana ya kuushinda ulimwengu? Kwanini Bwana Yesu alisema yeye ameushinda ulimwengu!? Cha kwanza ni Kwamba amekubali kuwa ulimwenguni mnayo dhiki lakini kauli yake inakuwa na radha zaidi pale anaposema “jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.”- Yesu alikuja katika hali ya ubinadamu Ili ajaribiwe sawasawa na Wanadamu, akaishi kwenye dunia tunayo ishi akakutana na majaribu ambayo tungekutana nayo, na upinzani ambao tungekutana nao. Lakini alishinda yote hayo na ushindi wake ulikuwa kwenye kauli yake “ Mimi nalishuka kutoka juu” Alikuwa anakiri asili yake, Kwamba yeye si wa dunia hii japo amezaliwa na anaishi duniani. Aliishi duniani kwa mamlaka ya Ki-Mbinguni kitu ambacho kilimfanya aushinde ulimwengu.

Aliishi duniani kwa mfumo wa Ki-Mbinguni. Sikia hii ndugu mpendwa, ulimwenguni humu yupo mkuu wa ulimwengu huu ambaye ni adui yetu ( Ibilisi shetani) ambaye hawezi kuruhusu wewe kufanikiwa Wala kuwa na furaha, na yeye ndiye aliye tawala mfumo wa ulimwengu huu, hivyo Kwa wewe kutawala katika maisha ni lazima “uishi duniani kwa mfumo na kanuni za Ki-Mbingu”

1 Yohana 4:4 “Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia.”

Kwanini anasema aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika Dunia?
Ni kwasababu anajua kwa yanayo endelea duniani unaweza kuona shetani ana nguvu na uweza mwingi. Ndio maana neno la Mungu ni kioo ambacho tunajitazama Uhalisia wetu ulivyo. Kuna kitu Mungu amekifanya ndani yetu kinacho tufanya kuwa washindi juu ya upinzani wa mwovu, na hii ni Mungu - ndani ya mwamini.

Mungu anatuonyesha kupitia neno lake Kwamba anaye kaa ndani yetu ni mkuu kuliko mkuu wa Dunia hii. Hivyo kushinda kushindako ulimwengu ni kwa Imani ya kutambua asili tuliyo nayo ambayo ni ya mbinguni. Mungu mwenye nguvu anaishi ndani yangu hallelujah. Ishi Mifumo ya mbinguni ukiwa duniani; na huu ndio u kristo wa kweli, Uungu kutokea ndani ya mwili.

Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.”

Kupitia Imani katika maneno ya Yesu Kristo tunajipata ndani ya amani yake. Ulimwenguni kunayo dhiki, kweli kabisa lakini anasema kwa yale ameyasema tuwe na amani “ndani” yake ndipo tunaona vizuri katika mstari wetu wa ufunguzi Mtume Paul anasema “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.”
Unapo jikuta umezungukwa na changamoto katika maisha yako kumbuka kauli hii

“Msijisumbue kwa neno lo lote; “ Hii ni kanuni ya Ki-Mbingu huwa hatu-panic bali muitiko wetu huwa katika KUOMBA KUSALI & KUSHUKURU. Ndio Mungu anatimiza ahadi ya neno lake Kwa kukuhifadhi ndani ya amani yake.
“Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.” Wafilipi 4:7
Amani hii ya Mungu - huleta Furaha, huleta connection za ki mbingu, huleta majibu ya maswali ya moyo wako. Roho ya Bwana Mungu ndani yako anakuhifafhi katika eneo ambalo hakuna akili katika dunia hii inaweza kufahamu. Hii ina maana Kwamba katika dhiki utakayo kuwa unapitia Bwana atakubeba katika mbawa zake mwenyewe. Hallelujah!! 🙌

SIO SWALA LA WEWE KUJITAHIDI KUSHINDA DHAMBI, HAPANA! BALI NI WEWE KUMUAMINI ALIYEISHINDA DHAMBI NA MAUTI. Nini tafsiri ...
13/11/2024

SIO SWALA LA WEWE KUJITAHIDI KUSHINDA DHAMBI, HAPANA! BALI NI WEWE KUMUAMINI ALIYEISHINDA DHAMBI NA MAUTI.

Nini tafsiri ya mtu mwenye dhambi? huyu sio yule Mtu mwenye matendo au maneno mabaya au mwenye kutenda maovu mengi, ni hapana. Mwenye dhambi ni yule ambaye dhambi zake hazijafunikwa Kwa damu ya Yesu. Usidanganywe Kwamba Kuna Mtu ana ubabe juu ya dhambi.

Warumi 3:23-24
23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;

24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu;

Ni Kwa neema tu tumekombolewa, kuwa mnyenyekevu, hubiri injili Kwa Upendo acha kufoka juu ya dhambi za watu. Upendo wa Mungu pekee waweza kumtoa mwanadamu kwenye dhambi. Mungu mwenyewe alitambua kuwa Kwa kuwapa Sheria watu wake walizidi kufanya maovu. Lakini Kwa neema iliyo kuja na Yesu Kristo tunaona Uhalisia wa Mungu katika Pendo lake.

Warumi 5:8 "Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.

ITIKIA PENDO LAKEMungu anawapenda watu wote. Alimtoa mwanae wa pekee kwaajili ya watu wote kuokolewa. Yohana 3:16 Lakini...
07/11/2024

ITIKIA PENDO LAKE

Mungu anawapenda watu wote. Alimtoa mwanae wa pekee kwaajili ya watu wote kuokolewa. Yohana 3:16
Lakini ni muhimu kufahamu Kwamba mbali na Mungu kuonyesha Pendo lake la kiujumla, Mungu anampenda Mtu mmoja mmoja na ndio maana anahitaji kuwa na uhusiano na Kila mmoja wetu; uhusiano wa maisha yako ya Kila siku pamoja na Mungu.

Hivyo liko pendo ambalo Mungu analionyesha kwako wewe k**a wewe. Anahitaji mwitikio wako katika Pendo lake. Mwitikio wako juu ya Pendo lake, kutamfanya adumishe mahusiano yake na wewe, ndio maana anasema
"Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.Mithali 8:17 Hapa akiwa na maana wale walio itikia Pendo lake.

Mungu ndiye aliyejifunua Kwa mwanadamu na si mwanadamu kumpata Mungu Kwa juhudi zake. Hivyo anavyosema nawapenda wale wanipendao ni Kwamba " amelifunua pendo lake kwako na je! ni nani aliye itikia Pendo lake. Mungu anakupenda wewe k**a wewe, itikia Pendo lake kwako . Mahusiano yako na yeye yatajengwa katika Pendo halisi la Mungu na kuwa na maisha imara ya kiroho. Hallelujah!!

1 Yohana 4:20 "Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona."

VAZI LA ARUSI Mathayo 22:11-1211 Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa...
30/10/2024

VAZI LA ARUSI

Mathayo 22:11-12
11 Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi.

12 Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa.

Tunajiandaje kuingia arusini? Lazima tujitafakari, tumepewa neno k**a kioo Ili tuweze kujitazama na kujitathimini. Huwezi ingia arusi ya mwana kondoo K**a hujavaa vazi la Arusi. Kumbe sio swala la kuinga tu bali inahitajika kuwa na vazi husika.

Kwenda tu kanisani na kushikilia dini yako vizuri hakuwezi kukupa uhakika wa kuvikwa vazi la Arusi ya mwana kondoo. Ntakupa mfano mmoja mzuri

Mathayo 7:22-23
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.

Hawa ni watu ambao wameishi wakijishughulisha na mambo ya kanisa, lakini kwanini anasema hakuwajua!? Ni kwasababu hawana/hawakuwa na vazi la utambulisho walilo takiwa kuwa nalo. Vazi hutambulisha cheo au nafasi ya Mtu. Kuna mavazi ya kifalme, kiaskari ki daktari na pia kuna vazi la Arusi.

Ndugu haimaanishi kutumika tu kanisani ndio kutakupa tiketi ya kuingia kwenye Raha ya Mungu bali ni vazi lililo wekwa tayari Kwa kuchovya kwenye damu ya mwana kondoo kwaajili ya kuingia arusini.

Ufunuo wa Yohana 3:18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

Liko vazi ambalo wa kristo tunatakuwa kuwa nalo, vazi ambalo limesafishwa Kwa damu ya mwana kondoo, jeupe lisilo na doa.

Wagalatia 3:27 Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo.

Kristo ni vazi letu la Arusi, katika kumvaa Kristo ndiko Kuna kufanywa Mtu mpya anaye mlingana Mungu. Kristo ni vazi lililo chovywa kwenye damu ya mwana kondoo aliyeshinda. Kubatizwa katika Kristo ndipo tuna maanisha kuzikwa pamoja naye na kufufuliwa pamoja naye Kwa kuziamini nguvu za Mungu aliye mfufua kutoka katika wafu. Ambapo huzikwa Mtu wa kale na matendo yake, Lakini anafufuka Mtu mpya mwenye vazi jipya liitwalo Kristo.

Kuna wale ambao wanamtumikia Mungu lakini tabia na mienendo yao havimlingani Mungu. Hivyo watu hawa wanakosa kuwa na vazi la Arusi. Wanaoneka k**a wako ndani lakini hawana vazi linalo wakilisha tabia za Kristo.

Ufunuo wa Yohana 3:4-5
4 Lakini unayo majina machache katika Sardi, watu wasioyatia mavazi yao uchafu. Nao watakwenda pamoja nami hali wamevaa mavazi meupe, kwa kuwa wamestahili.

5 Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake.


DS

KWANINI NIZALIWE MARA YA PILIWarumi 3:23-24 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;wanahes...
24/10/2024

KWANINI NIZALIWE MARA YA PILI
Warumi 3:23-24
kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;
wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu;

Kupitia Adamu wa kwanza wote tulikuwa na dhambi ya asili ambayo kwa hiyo tulistahili hukumu ya kifo.Wote wanaozaliwa kwa asili ya Adamu ni wa dhambi kwa mujibu wa maandiko ,hivyo kwa wewe kushikiria asili ya kale ,maana ake unaishi kwenye mauti ya laana ya dhambi.

Kwa wale ambao huwa wana hoji jinsi ya kuzaliwa mara ya pili , ni kwamba huwezi ukawa mwenye haki wa Mungu kwa kutumia akili zako mwenyewe ,haya ni mambo ya kiroho haya hitaji akili yako ,bali yanahitaji moyo wenye kuamini. Usipo amini wokovu wa kuzaliwa mara ya pili kwa roho yako hautawezekana. Kwamaana pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu.

1 Wakorintho 15:45 ndivyo ilivyo andikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha.
Nafsi ya Adamu wa kwanza ilihukumiwa kifo kwa ajili ya dhambi. Lakini mauti ya bwana Yesu kristo nguvu ya mauti imeondolewa kwa wale wanao mwamini.

Waebrania 2:14-15
Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi,awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa.

Hivyo kwa wewe kuondolewa katika hofu ya mauti ni lazima umwamini mwana wa Mungu (Adamu wa pili) ,ni lazima utangaze ya kwamba unaamini juu ya Ukombozi wa Yesu kristo. Kilicho zaliwa kwa mwili ni mwili na kilicho zaliwa kwa roho ni roho. Usipo zaliwa mara ya pili utaishi kwa matendo ya mwili ambapo hamna uzima wa milele bali mwili hutawaliwa na hisia zipelekeazo mauti.

Kuzaliwa mara ya pili kuna kupa uhusiano wa roho yako na uzima wa Mungu. Neno la Mungu linasema roho ndiyo itiayo uzima mwili haufai kitu. Ikiwa roho yako haijapokea uzima ,wewe ni wa mauti tu.Kwa maana mwili ulio nao utakufa wakati wowote kwa sababau roho yako haina uzima wa Mungu ndani yake.

WEWE NI HARUFU NZURI KWA MUNGU 2 Wakorintho 2:15 BHN"Maana sisi ni k**a harufu nzuri ya ubani ambayo Kristo anamtolea Mu...
16/10/2024

WEWE NI HARUFU NZURI KWA MUNGU

2 Wakorintho 2:15 BHN
"Maana sisi ni k**a harufu nzuri ya ubani ambayo Kristo anamtolea Mungu, harufu nzuri inayofikia wote, wanaookolewa na wanaopotea."

Kwa wale wanaopotea, harufu hiyo ni kifo; lakini kwa wale wanaookolewa, harufu hiyo ni uhai. Nani basi, awezaye kushiriki katika kazi ya namna hiyo? "

Biblia inasema wewe k**a mkristo uliye zaliwa mara ya pili ndani ya Kristo Yesu ni harufu nzuri ya ubani ambayo Kristo anamtolea Mungu ,na hii ni kwasababu ya damu yake ya dhamani ambayo ilikusafisha na wewe kuwa harufu nzuri kwa Mungu.

Harufu hii nzuri ya ubani ni lile Neno la Imani tulilo nalo katika Mioyo yetu na katika vinywa vyetu,ambalo Neno hili tukilihubiri katika ulimwengu linakuwa uzima kwa wale wanao okolewa lakini harufu ya kifo au mauti kwa wale wanaopotea. Wanaopotea ni kina nani? Ni wale wasio muamini Yesu Kristo Mwana wa pekee kutoka kwa Mungu . Yohana 3:16

2 Wakorintho 2:17" Kwa maana sisi si k**a walio wengi, walighoshio neno la Mungu; bali k**a kwa weupe wa moyo, k**a kutoka kwa Mungu, mbele za Mungu, twanena katika Kristo."

Wewe k**a harufu nzuri ya ubani Kwa Mungu ,usiwe mtu wa kulighoshi Neno la Mungu k**a wengi wanavyo fanya katika kanisa la Leo ,wakihuburi Yale yaliyo mapendeleo ya wanadamu na sio ukweli wa Mungu hivyo imepelea kudhihika kwa harufu isiyo nzuri kwa kanisa ktika Dunia hii. K**a mtu wa Mungu yakupasa ulitafakari hili na ruhusu Neno likubadilishe kwanza wewe Kisha libadilishe na wengine , usisome Neno la Mungu kwa madhumuni ya kuhubiri tu.

NI MAHALI GANI UNAISHI ?2 Wakorintho 5:17 "Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepit...
09/10/2024

NI MAHALI GANI UNAISHI ?

2 Wakorintho 5:17 "Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya."

Swali la kujiuliza ni mahali gani unaishi?

Wakristo wengi walio zaliwa mara ya pili wanateseka na magonjwa ,mawazo na hisia mbaya pamoja na umasikini kwasababu hawajajua ni mahali gani wanaishi.

Biblia inasema k**a "mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya;" Wewe sasa ni kiumbe mpya wa kiroho sio wa kimwili , sisi sio watoto wa Mwili ,sisi ni watoto wa Rohoni, Wewe upo ndani ya Kristo ambaye ni Roho.

Lakini mbali na kuwa kiumbe kipya ,biblia inasema ni kiumbe kipya ndani ya "Kristo"
Kristo ni nini basi ? Kristo ni mpakwa mafuta na mmiliki wa mafuta, pia Kristo ni sehemu au mahali, na hapo ndipo unapo ishi k**a Mwana wa Nuru. Waefeso 2:6 "Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu;"
Amekuketisha , maana yake upo mahali Fulani una starehe kwa amani katika uwepo wake. Mahali hapa magonjwa ,mateso ,vifungo ,umasiki havitutawali Wala havina nguvu juu yetu. Swala ni kwamba una yasadiki haya ?

Waebrania 12:22 "Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi,"

K**a kweli wewe umekiri Imani na kumwamini Yesu Kristo, ni kwamba umeufikilia Mlima sayuni Mji wa Mungu aliye hai . Ikiwa upo ndani ya Mji wa Mungu aliye hai kwanini unateswa na magonjwa?? Ndugu Shetani asikudanyanye ukadhani ni Jambo la kawaida kuumwa ,kwa wewe mtoto wa Mungu Hilo sio jambo la kawaida na ukiona dalili hizo ndani yako mpinge Shetani naye ata kukimbia .(Yakobo 4:7)

Usiishi katika matunaini yaliyo kufa ya kuendeshwa na elimu ya upotevu ya mwovu anayo ihubiri kupitia mawazo yako " angusha ngome za mawazo mabaya kwa silaha ya Neno la Mungu" wewe sio wa kutawaliwa na magonjwa.

Wewe upo katika Mji wenye majeshi elfu elfu ya malaika , na Bwana Mungu wako ndiye Bwana wa Hayo majeshi,na wewe ndo mtoto wake , mrithi sawasawa na ahadi , pamoja na kristo (Warumi 8:17) . Mahali unapo ishi ni mahali pa amani, utulivu ,nguvu , utukufu, ukamilifu, utoshelevu , mahali hapa tunaimba nyimbo za kumsifu na kumtukuza Yeye aliye shinda.

RESIDENCE OF CHRIST AMBASSADORS ( MAKAO YA MABALOZI WA KRISTO )Waefeso 2:22  "Katika yeye ninyi nanyi mnajengwa pamoja k...
02/10/2024

RESIDENCE OF CHRIST AMBASSADORS

( MAKAO YA MABALOZI WA KRISTO )

Waefeso 2:22 "Katika yeye ninyi nanyi mnajengwa pamoja kuwa maskani ya Mungu katika Roho.

We are a dwelling place of God in the spirit/ Sisi ni makao ya Mungu katika roho hivyo ni mabalozi wa Kristo katika mwili.

Karibu sana Residence of Christ Ambassadors
JUMAPILI
MUDA: SAA 3ASB - 7:30 MCHANA
G/ MBOTO ULONGONI A - KWA MADIBA

SOMO : NJIA NA  KWELI NA UZIMASt. John 14:6KJV: Jesus saith unto him, I am the way, the truth, and the life: no man come...
25/09/2024

SOMO : NJIA NA KWELI NA UZIMA

St. John 14:6
KJV: Jesus saith unto him, I am the way, the truth, and the life: no man cometh unto the Father, but by me.

Swahili: Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

Maneno haya aliyasema Yesu akiwa na wanafunzi wake ,na ukweli kwamba maneno aliyo yatamka hapo hakuna Mtu mwenye ujasiri wa kuyasema k**a Yesu alivyo yatamka.

" Mimi ndimi njia na Kweli na uzima " Wengine wanapenda kunukuu mstari huu k**a Mimi ndimi njia ya Kweli na uzima ...hayo ni makosa ! lazima usome ilo andiko vizuri Yesu siyo Njia ya Kweli Bali yeye ni Njia na Kweli .

Nikisema kwamba yeye ni Njia ya Kweli maanake Kuna weza kuwa na njia nyingi za Kweli lakini ninaposema Yesu ni Njia na Kweli na uzima ,Ina maanisha hakuna uzima mwingine nje yake ,Wala hakuna Kweli mbali na Yesu na hakuna Njia nyingine isipokuwa kupitia Yesu.

Njia unayo iendea ni ipi ? Je umeisha upokea uzima utokao kwake ? Je Kweli yake inaishi ndani yako.?

Kuokoka au kuzaliwa mara ya pili ni kutii kwa kumwamini Mwana wa Mungu na hapo unakuwa umeingia katika Familia ya Mungu .
Ndani ya familia hii Kuna Kweli ambayo inakuongoza na ndo chakula chako Cha Kila siku.
Ikiwa maisha yako unasema umeokoka ,lakini matendo yako hayaendeshwi na Kweli ya Mungu, wokovu wako umekufa ndani yako.
Ndani ya familia ya kristo kazi kubwa ni kui-ishi Kweli ya Mungu ambayo ni kristo.

Je maisha yako yakipimwa katika mizani ya Kweli ya Mungu ,utaweza kusimama mbele zake.?
Je utumishi wetu ukipimwa katika maandiko tutakuwa na ujasiri mbele zake.?
Je kazi yako ikipimwa katika moto hutaona aibu mbele zake?
Yesu ni Njia na Kweli na uzima , Mafundisho yako lazima yaweke wazi kuwa Yesu ndio Njia na hakuna nyingine. Fundisha kuwa Yesu ndie Kweli na hubiri maneno ya uzima ya Yesu Kristo yakaishi ndani ya mioyo ya watu.

Address

Masaki

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Love Living WORD posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Love Living WORD:

Share