06/07/2024
KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI JIMBO LA KILIMANJARO MASHARIKI USHARIKA WA HIMO
MAHUBIRI YA SIKU YA BWANA YA 6 BAADA YA UTATU, SIKUKUU YA VIJANA TAREHE 07/07/2024
MADA: BIDII YA KIJANA, MAFANIKIO YA KANISA
MASOMO: ZABURI 119:9 – 16, 1 YOHANA 2:13 – 17, *MITHALI 21:5
SHABAHA: Wasikilizaji watambue kuwa Kijana anayo matokeo mazuri kwa kanisa k**a akitumia juhudi alizopewa.
UTANGULIZI
Bwana Yesu asifiwe, leo 07/07/2024 ambayo ni kilele cha mwezi wa Vijana kwa mwaka huu wa 2024 tumepewa mada isemayo bidii ya Kijana, Mafanikio ya Kanisa. Ili kuweza kuchambua mada hii lazima tuanze kwa kuangalia maana ya maneno Kanisa, Kijana, Bidii na Mafanikio.
Kanisa linaweza kuelezwa katika maana mbili:-
a. Kanisa ni nyumba au jengo ambalo wakristo wanakutana kumwabudu Mungu wao. (
1Kor 11:18)
b. Kanisa ni jumuiya ya watu wote wanaomwamini Yesu Kristo ulimwenguni kote. (Mt 18:15 – 17, Mdo 12:5, Mdo 9:31, Mdo 2:41 – 42, Efe 2:20 – 22, 1Kor 12:28)
Kijana tunaweza kuangalia maana yake kulingna na vyanzo mbalimbali:-
a. Kijana kutokana na tafsiri ya kanisa ni mtu yeyote aliyepata kipaimara hadi miaka 35 na wengnine husema miaka 45.
b. Kulingana na mafundisho ya kijamii ni mtu yeyote aliyefikisha umri wa miaka 18 hadi miaka 35.
c. Kulingana na Wayahudi wao wanafundisha kuwa kijana ni yule mwenye miaka 20 hadi miaka 60. wayahudi walliwatambua vijana kwa umri huo kwa sababu walijua kuwa wao ndio watu wenye uwezo wa kuzalisha katika jamii na hata kulipa fidia na waliwatoza ghali kuliko makundi mengine yoyote.
Bidii (kutoka neno la Kiarabu) ni ile hali ya kuonyesha juhudi za dhati katika kufanya jambo fulani. Bidii ya mtu inaweza ikamfanya afikie malengo makubwa anayotaka na kujiona yeye ni wa juu.
Mafanikio ni ukamilishaji wa malengo yanayoipatia nchi, jamii au mtu binafsi ustawi, afya njema au hadhi. Mafanikio pia hujulikana k**a ufanisi, maendeleo au neema. Mafanikio hupatikana baada ya kumaliza shughuli fulani au kitu fulani.
Kijana akionyesha juhudi atakamilisha malengo yote yaliyowekwa na kanisa analolitumikia. Na katika kulitafakari hili tuepewa neno kutoka Kitabu cha Mithali 21:5
Mithali nyingi za Suleiman huwa na pande mbili ili kulinganisha na kutofautisha ili kupata somo kamili. Na katika mstari huu ameweka pande mbili ambapo upande wa kwanza zinamuelezea mtu mwenye lengo la kuwa tajiri na upande wa pili ni sifa ya mtu anayataka kuwa maskini.
Mtu mwenye bidii wakati wote anaelekea Utajiri kwa sababu anajua haya yafuatayo ( Mithali 10:4;Mithali 12:11; Mithali 13:4; Mithali 14:4; Mithali 22:29; Mithali 27:18; Mithali 28:19; Mhubiri 10:10)
Kujituma: Watu wanaotafuta utajiri wanajituma kwa bidii na wanafanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo yao ya kifedha.
Ubunifu: Wanaweza kuwa na uwezo wa kutafuta njia mpya na za ubunifu za kujipatia utajiri au kufikia malengo.
Kujiamini: Kujiamini ni muhimu sana katika kufanikiwa katika biashara na uwekezaji, na watu hawa mara nyingi wana imani kubwa katika uwezo wao.
Ujuzi wa Kifedha: Wanaweza kuwa na uelewa mzuri wa masuala ya kifedha na uwekezaji, na wanaweza kutumia maarifa haya kwa faida yao.
Uwezo wa Kuchukua Hatari(Risk takers): Watu wanaotafuta utajiri mara nyingi wanaweza kuchukua hatari kwa kufanya uwekezaji au kuanzisha biashara mpya na kufikia malengo.
Kujifunza na Kuboresha(Continuos Improvement): Wana uwezo wa kujifunza kutokana na makosa yao na kuboreka katika njia wanazotumia kutafuta utajiri.
Kujitolea/Kujinyima(Self Sacrifice): Wanaweza kuwa na nguvu ya kujitolea katika kufikia malengo yao.
Mtandao wa Kijamii(Network): Wanaweza kuwa na mtandao mzuri wa kijamii ambao unaweza kuwasaidia katika biashara zao na kutafuta fursa za kukamilisha malengo
Kujitambua(Self Awareness/Knowledge): Wanaweza kuwa na uelewa mzuri wa malengo yao na wanajua wanataka nini katika maisha.
Kujielekeza(Focus): Wana uwezo wa kujiwekea malengo na kuwa na mkakati wa kufikia malengo hayo.
Kufanya Kazi Kwa Bidii(Hard work): Wanaweza kuwa tayari kufanya kazi kwa saa nyingi na kwa bidii ili kufikia malengo yao.
Uwezo wa Kujisimamia: Wanaweza kuwa na uwezo wa kujisimamia wenyewe na kuwa na nidhamu katika matumizi yao ya muda na rasilimali.
Kufanya Maamuzi Bora ya Fedha: Wanaweza kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi bora ya kifedha kwa kuzingatia faida na hasara.
Mvivu ambaye anayeelekea kwa mhitaji huwa anajijali mwenyewe hapokei Ushauri na wala hana uvumilivu katika kukabiliana na mambo (Mithali 26:16, 20:21;28:20,22;) na wana sifa zifuatazo
K*tumia muda mwingi kuangalia TV, sinema au tamthilia. Dalili moja ya mtu kuwa masikini siku za mbeleni inatajwa kuwa utaratibu wa kutumia muda mwingi kuangalia TV badala ya kufanya shughuli za kuingiza kipato au hata shughuli za ziada zenye kuongeza manufaa fulani hata k**a sio pesa moja kwa moja.
Kununua chakula (Fast food) Hii ni tabia nyingine ambayo inatajwa ambayo k**a hairekebishwi hupelekea umaskini. K**a haukumbuki ni lini ulipika mwenyewe nyumbani kwako kwasababu unanunua chakula wakati wote basi hiyo ni dalili mbaya.
Kuchelewa kuamka. Tabia hii kufanyika katika umri wa ujana inaelezwa kuwa ni dalili ya kuukaribisha umaskini katika siku za mbeleni. Vijana ambao wanakuwa wazembe kufanya kazi kwa bidii kwenye kipindi chao cha ujana, hufanya kazi zaidi na kwa tabu wakifika umri wa kuanzia miaka 40 tena yawezekana bila malipo makubwa, na hii ni kwasababu hawakutumia vizuri muda wao wa ujana kufanya kazi na kuwekeza kwa ajili ya miaka ya mbeleni.
Kulaumu wengine kwa matatizo unayopitia. Wataalamu wa uchumi wanaeleza kuwa moja ya tabia zinazoweza kumfanya mtu awe maskini ni pamoja na kulaumu watu wengine kutokana na kutofanikiwa kwako.
K*toweka akiba. Akiba ni jambo la msingi sana katika mapato yoyote yanayopatikana. Akiba ya pesa husaidia pindi likitokea tatizo, inaweza kuwa ugonjwa, safari ya dharura na kadhalika. K**a huna akiba likitokea tatizo itakubidi uuze mali yako yoyote au uchukue mkopo ili kutatua tatizo hilo.
Kufanya manunuzi yasiyo kwenye mpangilio. Hii ni pamoja na kununua vitu ambavyo havikuwa kwenye bajeti au mpangilio. K*tokana na hili, wataalamu wanashauri kufanya manunuzi ukiwa tayari umeandika orodha ya vitu unavyotaka kununua na sio kwenda sokoni au dukani na kuangalia kilichopo ili ufanye manunuzi.
Kuzaa watoto wengi. K**a wewe ni kijana na una mpango wakuja kuwa na familia yenye watoto wengi, hakikisha hali yako ya uchumi iko imara kabla haujaanza kuzaa watoto hao.
K*topima afya mara kwa mara. Inawezekana ukaona sio suala la msingi kupima afya mara kwa mara lakini hili ni suala la msingi kwa watu matajiri, kwani kuishi ukiwa na uhakika wa afya ndio msingi wa kuishi maisha ya mafanikio.
K*tumia pesa kabla ya kuzipata. K**a una tabia ya kukopa pesa kipindi ambacho hauna pesa huku ukitarajia kuzilipa pindi utakapopata pesa, hiyo ni dalili ya umaskini kukunyemelea.
Kuwa na marafiki wasio na malengo makubwa. Marafiki huweza kukusaidia kufikia malengo yako uliyojiwekea, lakini pia huweza kufanya usifikie malengo yako hayo. Inashauriwa kuwa k**a unataka kufanikiwa hakikisha unatumia muda mwingi zaidi na marafiki ambao wana malengo makubwa ya maisha, wanawaza mambo chanya na sio mambo hasi muda wote, ambao wanakukumbusha kufanya vitu vya msingi.
Kuna jambo kubwa Zaidi linalotegemea bidii ya kijana ambayo ni kumpendeza Mungu kuzishika amri za Mungu ili kuurithi uzima wa milele. Hata mtume petro amesema wazi kuwa inahitaji bidii nyingi ili kuonyesha kuwa umekubaliwa (2 Petro 1:5 – 11) na hasa katika kipindi hiki kilichojaa mafundisho ya uongo na unabii wa uongo tunapaswa kujiadhari Zaidi na kuhakikisha kanisa linasonga mbele (Yohana 1:13, Warumi 9:15 – 16, Mathayo 7:21 – 23)
YANAYOMPASA KIJANA KWA KANISA
Kanisa k**a ilivyo maana yake kuwa ni jengo linaloabudiwa na wakristo na pia ni jumuiya ya wote wanaomwamini Yesu Kristo kuwa ni Bwana na Mwokozi wao.
Hivyo tunamuangalia kijana jinsi ambavyo anatakiwa kujihusisha katika hizi sehemu mbili.
YANAYOMPASA KIJANA KWENYE JENGO LA KUABUDIA
Nyumba ya ibada ni nyumba ya kuabudia na sio ya kufanyia kebehi na karaha ( Mt 2:12
– 13)
Unapokuwa katika jengo la ibada unapaswa kuvaa nguo za kujisitiri na safi ( Hes 8:21, Mwa 3:21, 1Tim 2:9 – 10, kumb 22;5, Mk 9:43, 1Kor 8:9, Lk 17:1)
Ukiwa kanisani unapaswa kuwa na nidhamu sio kutembea kwa “madoido”, unapaswa kutuliza macho, unapaswa kutulia usitoketoke hovyo, tusisome magazeti, sms, kutokusinzia, asiongee wa kunongonezana kanisani, asile chochote wala kutumia simu kanisani.
Kijana anapaswa kupanda maua, kufagia, kudeki, kufuta vumbi, na kuhakikisha mazingira yote ya ndani na nje ya Jengo la kanisa yanatunzika vizuri.
Kijana anapaswa kumsaidia mchungaji kazi k**a vile kusoma neno, kusoma matangazo, kugonga kengele, nk.
Kijana anapaswa kujiandaa kuwa kiongozi ( Law 19:30, Zab 29:2)
YANAYOMPASWA KIJANA KWA KANISA K**A JUMUIYA YA WAAMINIO (KWA WAKRISTO WENGINE)
Kuishi maisha ya ujamaa ( Mdo 2;44 – 45, Mdo 4:32) k**a vile kuwatembelea wagonjwa sababu wanahitaji kufarijiwa ( Lk 1:37)
Kijana anapaswa kuwahudumia wahitaji k**a vile kutoa damu, huduma ya kwanza, kuwasaidia wazee, vilema, kujihusisha na shunguli za maziko, harusi, kufundisha Sunday school, kushiriki kazi za kitaifa, kukaribisha wageni, kuandaa semina na mikutano ( Mt 25: 39 – 40)
Kijana anapaswa kutoa sadaka kwa kazi ya kanisa ( Kumb 16:17, 2Kor 8:12, Mt 3:
27, 1Kor 9:13 – 14, 2Kor 9:7, Mt 6:2)
Kijana anapaswa kufanya uinjilisti na kujitahidi kuyajua maandiko ( Mdo 18: 28) na kuwa wavumilivu ( Tito 3:9)
HITIMISHO
Sisi vijana tujiulize maswali haya:-
Mimi ni nani?
Je, baada ya muda Fulani ninataka kuwa nani?
Je, ninataka kuwa na ujuzi/utaalamu gani?
Je ninahitaji kujiajiri au kuajiriwa?
Je ninatamani kumiliki nini maishani?
Mungu atusaidie sote ili tuweze kumtumikia Mungu kwa bidii ili kuleta matokeo chanya kwa kanisa letu.
AMEN.