23/08/2026
: chanzo cha baraka za mtu ni kuisikia sauti ya Mungu.
Ibrahimu kilichomfanya apate baraka ni kuisikia sauti ya Mungu. huwezi fanya baraka zozote pasipo kuisikia sauti ya Mungu,.
Kusudi la kufanyika mwana lina sifa mbili mhimu sana
1. Upekee wa kuzaliwa huyu mwana
2. Kibali Cha kuingia mahali ambapo mwingine hawezi kuingia ila TU huyu mwana.
Kumbuka wana Israel walitembea safari ndefu sana lakini walichelewa kwa kutosikia sauti ya Bwana.
Kusudi la kuwa mwana ni kuturithisha Mali na vyote alivyoviumba kuwa sawasa
Mwanzo 1:28
Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.
Kumbukumbu la Tolati 28
Biblia haisemi atabarikiwa mchungaji Wala muimbaji Wala mwenye wadhifa flani.
Bali inasema utakapoisikia sauti ya bwana
ISAYA 9:6
Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.
Natangaza kwamba Dunia isikie na mbingu zikisie kwamba Mimi ni mwana wa Mungu. Na kwaa ajili yangu Yesu alizaliwa ili niwe Amani.
Yesu kristo alizaliwa katika uweza wa roho mtakatifu ndivyo na Mimi nilivyo, nimezaliwa katika uweza wa roho mtakatifu.