Efatha Church Makambako

Efatha Church Makambako Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Efatha Church Makambako, Religious organisation, Kivavi/Mashujaa, stand daladala Along makambako/Njombe Road, Makambako.

The Official Efatha Church page
YouTube: youtube.com/efatha church https://youtube.com/?si=_K0eJQRstCm1WEg-
Website: efathachurch.org

24/05/2026

Somo:Maisha ya Utukufu
Mchungaji Fahamuel Mndeme

24/05/2026

IIBADA YA JUMAPILI | TAREHE 24 MAY 2026
NENO: MAISHA YA UTUKUFU
MCHUNGAJI MNDEME

IBADA YA JUMAPILI| TAREHE 24/05/2026Mchungaji Fahamuel Mndeme2 Nyakati 5:13-14sifa za Mungu hazitokei wakati ule tunapoi...
24/05/2026

IBADA YA JUMAPILI| TAREHE 24/05/2026
Mchungaji Fahamuel Mndeme

2 Nyakati 5:13-14

sifa za Mungu hazitokei wakati ule tunapoimba na kucheza tu, bali ni kule kukubalika kwangu mbele zake, kwa sauti ninayoitoa nikisifia matendo yake makuu na heshima yake katika maisha yangu.

Unapokuja mbele za Mungu, haangalii umevaa nguo ya gharama kiasi gani, wala elimu yako bali anaangalia moyo wako na hapo ndipo unapata kibali.

Mungu anampa mtu maisha ya kiwango fulani kwa kusudi, usimdharau mtu kutokana na elimu yake, wala kazi yake, ukifanya hivyo utapoteza heshima ya Mungu

Yohana 11:4

Hata k**a ukiombea mgonjwa na akapona, usionyeshe kiburi, yawezekana ni Mungu tu anataka kuonyesha uwezo wake.

Ukishaona jambo lina sifa na heshima ya Mungu, wewe lifanye bila kuangalia wanadamu wanakuona vitu.

Kila unapomuendea mtu na akaokoka, hiyo ni sifa ya Mungu, hivyo tambua uwepo wa Mungu unakua na wewe.

Ayubu 16:19

Hali yako ya maisha isikufanye umkane Bwana. Usijiunge na mtu anaekejeli na kukufuru matakatifu ya Mungu.

Matendo 8:20

Kumbuka kuna mtu alitaka kununua nguvu za Mungu, je si una heri wewe unaepata bure?

Chochote ulichonacho angalia usitukanishe jina la Bwana.

IBADA YA JUMAPILI| TAREHE 24/05/2026Mchungaji Fahamuel MndemeAINA MBILI ZA UTUKUFU1.Utukufu wa MunguHii ni ile hali ya k...
24/05/2026

IBADA YA JUMAPILI| TAREHE 24/05/2026
Mchungaji Fahamuel Mndeme

AINA MBILI ZA UTUKUFU
1.Utukufu wa Mungu

Hii ni ile hali ya kuzibeba sifa za Bwana kwa maneno, mwenendo wangu kila siku mbele za Mungu na wanadamu. Ni utukufu unaomuheshimisha Mungu.

Je? ninapoongea na watu, na mahusiano yangu na jamii na ndugu zangu, wanaona nini kwangu? fika mahali hata familia yako imuone Mungu kupitia wewe, si lazima mchungaji afike.

je? Mumeo, Mkeo au watoto wanajivunia wewe na wokovu wako?

Utukufu wa Mungu ni mimi kuzingatia ninachofanya, iwe ni kazi, maneno yangu, mwenendo wangu, muonekano wangu na maisha ya kila siku, yanakua na sifa na heshima ya Mungu.

2.Utukufu wa mwanadamu

Haya ni maisha ya mashindano, sehemu yoyote iliyo na mashindano, hapo unatakiwa utukufu wa binadamu. hivyo usiishi maisha ya mashindano kwani hapo utukufu wa Mungu hautaonekana.

Usifanye jambo kwasababu fulani anafanya. Fanya kazi au biashara ambayo Mungu anahusika, usishindane na watu.

1 Samweli 4:21

Chochote utakachozalisha au kupata faida nje ya mapenzi ya Mungu, elewa kitaondoa mapenzi ya Mungu kwako, na wala mapenzi ya Mungu yaliyo katika agano lako na Yeye [Mungu] hayatoonekana tena.

Linda utukufu wa Mungu uonekane kwako.

IBADA YA JUMAPILI| TAREHE 24/05/2026Mchungaji Fahamuel MndemeHakikisha katika maisha yako unayoyaishi, unaonesha utukufu...
24/05/2026

IBADA YA JUMAPILI| TAREHE 24/05/2026
Mchungaji Fahamuel Mndeme

Hakikisha katika maisha yako unayoyaishi, unaonesha utukufu wa Mungu hapo ulipo.

Utukufu ni ule muonekano wa sifa na heshima na uweza wa Mungu mahali alipo. Utukufu ni ile sifa, heshima, uweza wa Mungu kwangu. Hakikisha huo utukufu unaonekana kwenye maisha yako.

k**a Mungu hataona sifa, heshima na uweza wake kwangu, hawezi kukaa pamoja na Mungu. Kinachomvuta Mungu awe na mimi, ni zile sifa, heshima na uweza wake nilionao.

Hakikisha kila jambo, kazi, maneno yako, na mwenendo wako, unabeba utukufu wa Mungu.

Unaweza ukavaa nguo, au namna yako ya kutembea na kuongea watu wakamkosa Mungu kwako

jiulize, maneno unayoongea kwa siku, ni kwa kiasi gani yamebeba sifa, heshima na uweza wa Mungu.

24/05/2026

Yale Ametenda Ndani Yangu - Efatha Church Makambako

24/05/2026

Hata sasa nauona wema wako

24/05/2026

Efatha Nakupenda - Efatha Makambako Choir

24/05/2026

Efatha Makambako Choir

Address

Kivavi/Mashujaa, Stand Daladala Along Makambako/Njombe Road
Makambako

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Makambako posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church Makambako:

Share