Mkote global

Mkote global Taifa la Ufalme wa Mbinguni

20/01/2026

1. Kitu ambacho mwanadamu kapoteza katika maisha yake ni Ufalme wa Mungu.
- ufalme ndio msingi mkubwa zaidi wenye uwezo wa kumfanya mwanadamu ( a) aweze kuishi kuishi kwa amani ( b) aweze kumzalia Mungu matunda ,
anasema, "Yohana 15:16 Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.

huwezi mzalia Mungu matunda endapo ukiwa nje ya Ufalme wake.

kwasababu hizi.
1: Mtu ni roho ana Kaa ndani ya mwili na ana nafsi.
2: Nguvu ya kufanya kazi duniani na kuleta matokeo inatoka katika ulimwengu wa roho.
3: Mtu akiwa duniani, akitaka kufanikiwa kwa jambo lolote, lazima apate msaada katika ulimwengu wa roho, /
Mungu hakumuumba Mtu kufanikiwa duniani bila msaada wa rohoni/ ulimwengu wa roho.
anasema "Waebrania 11:3 Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri.

kwa hiyo Sasa Mtu kufanikiwa duniani pasipo msaada wa Mfumo wa ufalme wa Mungu ni ngumu, lakini pia hakuna mafanikio nje ya Mfumo wa Ufalme wa Mungu yatakayo mwacha Mtu salamaa, lazima yamwangamize tu;
anasema, "Mithali 1:32 Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.

Cha kufanya ni
kuutafuta Hadi tuupate Ufalme wa Mungu kwenye Kila eneo la maisha yetu, ndio suluhisho pekee alilo Baki nalo Mtu.
eg: Luka 15:4, 8
4 Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda nyikani, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone?

8 Au kuna mwanamke gani mwenye shilingi kumi, akipotewa na moja, asiyewasha taa na kufagia nyumba, na kutafuta kwa bidii hata aione?

10/01/2026

UFALME KWANZA - MATHAYO 6: 33

Ni somo ambalo tutajifunza kwa mfululizo na pointi, ambazo zitatupatia kulielewa hili somo, angalau kwa sehemu atakayo tujalia Mungu wetu wa Mbinguni.

1. Kuutafuta Ufalme wa Mungu na haki yake, ni agizo ambalo wanadamu wote tumepewa.

2. Mtu aliwekwa duniani kwa makusudi maalum ya Mungu mwenyewe,
-kusimamia ufalme wa Mungu na ukuaji wake hapa duniani / kuwa wakili wa Mungu hapa duniani.
- 1 Wakorintho 4:1-2
1 Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu.

tupo hapa duniani k**a mawakili wa alituweka, tupaswa kufanya Yale ya aliye tuweka sio ya kwetu.
-
Waebrania 13:21
awafanye ninyi kuwa wakamilifu katika kila tendo jema, mpate kuyafanya mapenzi yake, (naye akifanya ndani yetu lipendezalo mbele zake), kwa Yesu Kristo; utukufu una yeye milele na milele. Amina.

jambo analotaka Mungu ni kuona anatawala na dunia pia kupitia mtu.

3. Ni jambo Moja tu ambalo wanadamu tumeambiwa tulitafute, { nalo ni Ufalme na haki}
- lakini wanadamu tunatafuta maisha, pesa nk, ambavyo ni sio maagizo ya Mungu kwetu kuyatafuta.

4. Kinacho Fanya Ufalme na Haki vionekane ni vigumu kuvitafuta kwa wengibwetu, ni kwa sababu wengi tuna mambo mengi ambayo tunayatafuta,
lakini ametupatia jambo Moja tu la kulitafuta { Ufalme na Haki}
Bwana Yesu alisema hivi,
Mathayo 6:24
Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashik**ana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.
- tunayo yatafuta hayo yanatuweka kwenye huo utumishi wa tunacho kitafuta

5. Ufunuo wa Yohana 3:15-16
15 Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri k**a ungekuwa baridi au moto.

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

- Moja ya sababu inayo leta uvugu vuga katika Misha ya watu ni , mambo mengi tunayo yatafuta,
ni kwa sababu hayo mengine tunayo yatafuta yanataka mda wetu, nguvu, akili nk. na Mungu Naye anataka hivo pia,
- Sasa ni unawezaje kujigawa ukawarisha wote wawili, jua ni ngumu Sana, lazima mmoja atafurahi na mwingine utamkera tu.

6. Kumbuka uvugu vugu Hauna matokeo yanayo eleweka, hayatajulikana ni ya Ki Mungu au dunia kwa sababu hayatakuwa upande wa Mungu.
- kwa hiyo faida ambazo ulitakiwa uzipate kwa Mungu hutazipata, na uzuri wa kimahusiano baina Yako na Mungu hutauona,
...............

01/01/2026

Have a blessed year

10/08/2025

Warumi 5:12 Kwa hiyo, k**a kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi;

Mwanadamu siku zote anahofia kufa/ mauti, na mauti inamaanisha hivi Kwa mwanadamu, ni kwamba mwanadamu anaishu nje ya umilele.

Na kuishi nje ya umilele , Kuna tengeneza aina ya maisha yenye hofu, mashaka, mahangaiko/ masumbufu Kwa wanadamu, na hiyo unakuwa kubwa sana.

Waebrania 2:14-15
14 Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi,

15 awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa.

Je! Umewahi chunguza na ukajua hofu uliyo nayo ya kufa, imeku tengenezea aina gani ya maisha?
Ukichunguza Kwa makini utagundua kuwa una maisha yasiyo mzalia Mungu matunda, hata k**a utamzalia matunda Mungu, basi yatakuwa matunda yasiyo dumu.

Bwana wetu Yesu KRISTO, alikuja lengo Moja wapo ni kututoa katika hofu ya mauti.

-Tumwamini Bwana YESU, tumtegemee tukijua ndo mwamba ulio imara zaidi kuutegemea,
- tujifunze namna ya kujua kuwa hii amani imetoka Kwake Bwana YESU.
Ishara Moja wapo kuweza kutofatisha hizi amani ( Yohana 14:27 Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo k**a ulimwengu utoavyo.) ni…….
2 Wakorintho 7:9-10
9 Sasa nafurahi, si kwa sababu ya ninyi kuhuzunishwa, bali kwa sababu mlihuzunishwa, hata mkatubu. Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara kwa tendo letu katika neno lo lote.
10 Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti.

Amani toka kwa Mungu, inakupa juhudi, ya kuutafuta uso wa Mungu Kwanza

Amani toka duniani inakuweka mbali na uso wa Bwana

Ukiona unapata amani kwenye jambo lolote like, jaribu ufatili, kati ya hayo mawili lipi linatoka, ni je! Unakaa mbali na uso wa Bwana
Au inakupa kusogea/ kuufata uso wa Bwana.

08/08/2025

Yohana 14:27 Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo k**a ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.

Bwana YESU asifiwe watu wa Mungu.

Tuta tumia kitabu hiki cha Yohana kutazama kipengele cha amani katika somo letu la Leo.
Tunapo soma mistari hapo, inatupatia mambo ya kujifunza ndani yake.

1: mstari wa 27(b) Bwana Yesu anasema amani yake,
Tuanaona Kuna amani ya kwake Bwana YESU, lakini pia Kuna amani ya ulimwengu.
Hizi ni amani mbili tofauti kabisa, na utendaji kazi moyoni, ni tafsiri kabisa kabisa,

Ok. Kwanini kuwe na amani ya ulimwengu na amani ya Bwana YESU.
Ni Kwa sababu Kuna maeneoo mawili yaliyo tofautina haki na aina za maisha.
Kuna mbinguni juu, ambapo mda mwingine tunasema ni ulimwengu wa roho,
Hafu Kuna duniani

Mazingira ya mbinguni na duniani ni tafsiri kabisa, na Bwana wetu Yesu, asili/ alitoka mbinguni
-Yohana 16:28 Nalitoka kwa Baba, nami nimekuja hapa ulimwenguni; tena nauacha ulimwengu; na kwenda kwa Baba.

Kwa hiyo anasema anawapa amani yake, maana anataka anaowapa amani, waitumie amani ya kwake ambayo inatoka mbinguni kuwasaidia kuishi duniani, wasiitumie amani ya duniani kuishi.

Sifa ya amani ya mbinguni ni ya milele, lakini amani ya duniani ni ya kitambo kidogo/ haidumu.
Kwa hiyo haiwezi wasaidia wanadamu kuishi.

Kwa namna nyingine tuseme hivi, Mungu alipo iumba Dunia, alitaka Dunia itawaliwe na mifumo ya mbinguni, na aliwekeza mifumo ya mbinguni duniani Hadi pale mwanadamu/ Adam alipo amua kumuasi/ kumkataa Mungu, ndipo Mungu alipo iondoa mifumo yake duniani.

Kuanzia hapo mwanadamu akaanza kuishi duniani Kwa kutumia mifumo iliyopo duniani, ndipo unakuta wasiwasi na woga vinapo Anza kufanya kazi kwenye maisha ya mwanadamu, ni Kwa sababu pia anavyo vitumia kufanya kazi duniani ni vya muda/ havidumu.

Unajua hofu kubwa ya mwanadamu ipo kwenye mudaa?
tuseme hivii
Mungu alipomwumba mtu alimpa uzima wa milele, lakini dhambi ikamwondolea uzima huo.
:

Warumi 5:12 Kwa hiyo, k**a kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi;

Endelea kufuatana nasi.

07/08/2025

Ijumaa usiku saa 8:30, nitaweka mwendelezo wa somo la moyo.
Nitatazama kipengele cha amani k**a kifaa Moja wapo cha kuusaidia moyo kufanya kazi.
Usikose kufuatilia hiki kipengele Mungu akikupa neema ya kufuatilia.

Mungu wangu awabariki sana.

07/08/2025

K**a shetani anataka kuharibu jamii, huanza kwa kushambulia familia.

05/08/2025

Hebu tutazame kidogo Leo kuhusu moyo.

Warumi 14:17 Maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu.

Romans 14:17
[17][After all] the kingdom of God is not a matter of [getting the] food and drink [one likes], but instead it is righteousness (that state which makes a person acceptable to God) and [heart] peace and joy in the Holy Spirit.

Kwa mujibu wa huu mstari wa kitabu cha Warumi, Kuna jambo ambalo najifunza ndani yake, lonalo husu moyo ambalo ningependa kuwa shilikisha nanyi ndugu zangu.

Setting ambazo Mungu kaziweka katika moyo ili ufanye kazi yake vizuri ni,
haki
amani
furaha

Moyo unapo fanya kazi nje ya haya ma
mbo matatu(3) , moyo unaharibika.
Unaharibika Kwa namna ipi, maandiko yanasema Kwa lugha nyingine kuwa ni moyo mbovu.

Mithali 14:30 Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili;
Proverbs 14:30
[30]A calm and undisturbed mind and heart are the life and health of the body,

Moyo ukiharibika au kuwa mbovu matokeo yake tunayaona katika mwili au maisha ya kawaida,
Kunakuwa na maisha yaliyo jaa hofu, wasiwasi, taabu nk. Na ndio maana had
i inafikia mahali duniani panaoneka sio mahala salama pa kuishi, ni Kwa sababu ya matokeo ya mioyo iliyo haribika/ mibovu ya watu.
Ndugu yangu Mungu hafurahii aina hii ya maisha tunayoishi, ya wasi wasi, na taabu. Na ndio maana katuletea suluhusho la Kwanza na muhimu kuliko mengine yote, litakaloweza tibu hii changamoto tunayo kabiliwa nayo ya mioyo. Ambalo ni YESU KRISTO na UFALME WAKE MUNGU WETU.

Tumpokee na Tumwamini BWANA YESU KRISTO, Kwa mioyo yetu na kweli.
Hii ndo sehemu pekee ya kuanzia kutatua changamoto la tatizo la mioyo yetu

Moyo mbovu unatufanya tushindwe kumwamini Mungu kabisa/ unatufanya tukose Imani Kwa Mungu, au tunakuwa na wasiwasi hata na Mungu WETU jaman.

Ufunuo wa Yohana 3
20. Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.

Mungu akipa neema, wakati ujao ntaanza kuzielezea hizi setting( 3) za moyo ambazo ni ( haki, amani, furaha) namna zinavo Fanya kazi na moyo katika kufanya moyo uwe na mafanikio hapa duniani.

04/08/2025

Mhubiri 7:9
Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.

# hivi mpumbavu/ au wapumbavu ni watu wa aina gani?
Kwa mujibu wa maandiko yanasema,
Zaburi 14:1 Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu;

Ipo ivi, sababu zipi za msingi zinazo kufanya ukasirikee?
Au tujiulize hivi, kilicho kukasirisha au kufanya ukasirike ni nini/ au kitu gani?

Hicho kilicho kukasirisha, umekipimanisha na Mungu ukajua nani mkubwa?
Mpaka unakasirika, maana yake umekipimanisha na Mungu wa mbinguni ukaona ni kikubwa chenyewe kuliko Mungu wa Mbinguni,
Na ndio maana umeshindwa kumkabidhi Mungu akishughulikie, hafu umekasirika,.
Sawaa, na je baada ya kukasirika umebadili kitu gani, au umepata faida ipi kwenye kukasirika kwako?

Moja ya kitu hatari kwenye moyo wa bunadamu, ni kubeba kitu ambacho Mungu hakuweka setting zake ndani ya Moyo,

Nafasi ya Mungu kujifunua katika maisha yetu, ni sehemu ambazo Kuna udhaifu katika maisha yetu,
Kwa hiyo ukiona Kuna chochote ambacho kwenye moyo wako kinakupa,
Kutokuwa na amani
Kukasirika
Moyo kusumbuka
Moyo kutojua cha kufanya

Mkabidhi Mungu, usiishi k**a Mungu hayupo et,
Ishi k**a Kuna Mungu muumba mbingu na nchi na vyote vilivyomo ndani yake ambavyo ndio yeye mmiliki wa hivyo.

Tutoke kwenye upumbavu, ( kuona Mungu ni mdogo kuliko yanayo tusumbua)

Unajua nini:
Maandiko yanasema:
(1 Petro 5:6-7
6 Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;

7 huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.)

@ ntakuja na mwendelezo wake

2 Samweli 7:22  Kwa hiyo, wewe ndiwe mkuu, Ee Bwana Mungu, kwa maana hakuna k**a wewe, wala hapana Mungu mwingine ila we...
02/08/2025

2 Samweli 7:22
Kwa hiyo, wewe ndiwe mkuu, Ee Bwana Mungu, kwa maana hakuna k**a wewe, wala hapana Mungu mwingine ila wewe, kwa kadiri tulivyosikia kwa masikio yetu.

Yeremia 29:11  Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi...
31/07/2025

Yeremia 29:11 Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.

Address

Makambako

Telephone

+255769345986

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mkote global posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Mkote global:

Share