20/01/2026
1. Kitu ambacho mwanadamu kapoteza katika maisha yake ni Ufalme wa Mungu.
- ufalme ndio msingi mkubwa zaidi wenye uwezo wa kumfanya mwanadamu ( a) aweze kuishi kuishi kwa amani ( b) aweze kumzalia Mungu matunda ,
anasema, "Yohana 15:16 Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.
huwezi mzalia Mungu matunda endapo ukiwa nje ya Ufalme wake.
kwasababu hizi.
1: Mtu ni roho ana Kaa ndani ya mwili na ana nafsi.
2: Nguvu ya kufanya kazi duniani na kuleta matokeo inatoka katika ulimwengu wa roho.
3: Mtu akiwa duniani, akitaka kufanikiwa kwa jambo lolote, lazima apate msaada katika ulimwengu wa roho, /
Mungu hakumuumba Mtu kufanikiwa duniani bila msaada wa rohoni/ ulimwengu wa roho.
anasema "Waebrania 11:3 Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri.
kwa hiyo Sasa Mtu kufanikiwa duniani pasipo msaada wa Mfumo wa ufalme wa Mungu ni ngumu, lakini pia hakuna mafanikio nje ya Mfumo wa Ufalme wa Mungu yatakayo mwacha Mtu salamaa, lazima yamwangamize tu;
anasema, "Mithali 1:32 Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.
Cha kufanya ni
kuutafuta Hadi tuupate Ufalme wa Mungu kwenye Kila eneo la maisha yetu, ndio suluhisho pekee alilo Baki nalo Mtu.
eg: Luka 15:4, 8
4 Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda nyikani, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone?
8 Au kuna mwanamke gani mwenye shilingi kumi, akipotewa na moja, asiyewasha taa na kufagia nyumba, na kutafuta kwa bidii hata aione?