Efatha Church Babati

Efatha Church Babati Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Efatha Church Babati, Christian church, Babati Town, Babati, Magugu.

03/11/2023
18/10/2023
MKUTANO  MKUBWA WA INJILI KILIMANJAROMwana wa Mungu mkazi wa  Mkoa wa Kimanjaro na maeneo ya jirani, karibu katika mkuta...
01/08/2023

MKUTANO MKUBWA WA INJILI KILIMANJARO

Mwana wa Mungu mkazi wa Mkoa wa Kimanjaro na maeneo ya jirani, karibu katika mkutano mkubwa wa injili utakaofanyika katika viwanja vya MASHUJAA Moshi mjini, mkutano huu utaongozwa na Mtumishi wa Mungu Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira kuanzia tarehe 2 mpaka 5 mwezi wa 8 mwaka 2023. Walete wagonjwa na wenye shida mbalimbali wataombewa bure kabisa. Ukipata tangazo hili sambaza kwa wengine ili wakutane na mkono wa Bwana.

Ni zamu ya Kilimanjaro, kila goti litapigwa na kila ulimi utakiri Yesu Kristo ni Bwana.

NENO LA SIKUNa Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira - Kanisa la Efatha.Tarehe  20/6/2023SOMO:  NAMNA YA KUEPUKA MATAMA...
20/06/2023

NENO LA SIKU

Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira - Kanisa la Efatha.

Tarehe 20/6/2023

SOMO: NAMNA YA KUEPUKA MATAMANIO YAKO.

Zabari 27:4 "Neno Moja nimelitaka kwa Bwana, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa Bwana Siku zote za maisha yangu, Niutazame uzuri wa Bwana, Na kutafakari hekaluni mwake."

Kila wakati tamani kukaa na kutulia mbele za Bwana, ili upate mafunuo yake ambayo yatakusaidia kukutoa mahali na kukupeleka sehemu yenye baraka zako, epuka kuhubiriwa na mazingira au maumivu unayoyapitia kwani mwisho wake utaishia kwenye majuto.

Ili Mungu akubariki lazima ataanglia k**a kuna hekima ndani yako. Kwasababu bila hekima kuwa ndani yako, itakupelekea kutamani yale ambayo yanamchukiza na hatimaye utafanya k**a watu wa dunia wanavyofanya, hakikisha unaepuka mambo yote ambayo macho yako yanatamani na uzingatie yale ambayo Neno la Mungu na Roho wa Bwana wanayaridhia, ili upate kuziona baraka za Mungu kwenye maisha yako.

MCHUNGAJI KIONGOZI EBEN MSHIU.SOMO: MKULIMA MWEMA.Yohana 15:1-3  "Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkuli...
08/06/2023

MCHUNGAJI KIONGOZI EBEN MSHIU.

SOMO: MKULIMA MWEMA.

Yohana 15:1-3 "Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima. Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa.Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia."

Mkulima ni MUNGU, Mzabibu ni YESU na wenye kubeba Matunda au tawi ni sisi. Mwenye shamba ama Mkulima ndio mwenye maamuzi ya kuchagua mazao gani ya kulima, na alime kwa kiasi gani, na anajua kwa zao alilopanda aweke mbolea gani ili mazao yastawi.

Lakini ili tawi listawi na kuzaa Matunda kuna kanuni za kufuata, hivyo MUNGU anapokutangazia ustawi, baraka na utajiri ili upokee unatakiwa ufuate utaratibu na kanuni za MUNGU. Mzabibu mwema ni wale wanaozaliwa wakiwa ndani ya YESU.Wewe k**a huwezi kuzaa bila shina lenye virutubisho unavyotakiwa kwa ajili ya Matunda.

MAMBO YA KUZINGATIA ILI KUZAA MATUNDA

1.Hakikisha unazingatia kanuni za MUNGU, taratibu na maelekezo ya MUNGU.

2. Hakikisha unajitambua kuwa wewe ni nani, wewe ni sura na mfano wa MUNGU, kuwa unaweza kutawala na kumiliki vyote vilivyoumbwa na MUNGU.

3. Shika Neno lake na Amri zake, maisha yako ishi k**a Neno linavyosema, hakikisha moyoni mwako umeliweka Neno na tendea kazi Amri za MUNGU.

NENO LA SIKU.Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha.Tarehe 5/6/2023.SOMO: KABLA HUJAFANYA CHOCHOTE ...
05/06/2023

NENO LA SIKU.

Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha.

Tarehe 5/6/2023.

SOMO: KABLA HUJAFANYA CHOCHOTE MSHIRIKISHE MUNGU.

Tunatakiwa kuomba kabla hatujafanya maamuzi yoyote. Je ulimpataje mume wako au mke wako, je uliomba kwanza ndipo ukampata au uliomba baada ya kumuona? Je ulipataje watoto wako, je uliomba kwanza au ulibeba tu ujauzito? Namna tunavyoishi inatuonesha ni jinsi gani maisha yetu yanamilikiwa na sisi wenyewe.

Ni wangapi wenu mnamshirikisha Mungu nini mnataka kula? Leo hii watu wengi wana magonjwa k**a kisukari, lehemu (cholesterol) n.k, kwa nini? Kwa sababu ya vyakula wanavyokula. Ukikabidhi maisha yako kwa Mungu Yeye anakuongoza na atakupa kujua nini ufanye na nini usifanye na hata vyakula vya kula pia atakujulisha ili usipate magonjwa. Hakikisha unaitunza afya yako kwa maana afya yako ni ya muhimu sana kuliko hata kazi yako kwa maana k**a unaumwa hauwezi kwenda kazini.

Wakati mwingine watu wanakufa sio kwa sababu muda wao umefika, la! Bali ni kwa namna wanavyoishi. Kuvaa miwani sio fasheni bali ni kuonyesha kuwa ndani yako kuna kitu kimekufa. Kabidhi maisha yako kwa Bwana, k**a unaona kuna kitu kinakufa ndani yako maana yake ni kuwa katika roho kuna kitu kimekufa, inaanza kwanza katika ulimwengu wa roho ndipo inajidhihirisha katika damu na nyama, ndipo utaona mtu anangoa meno, anavaa miwani, hasikii vizuri n.k.

NENO LA SIKU.Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha.Tarehe 3/6/2023.SOMO: SADAKA YA AMANI.Mambo ya ...
03/06/2023

NENO LA SIKU.

Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha.

Tarehe 3/6/2023.

SOMO: SADAKA YA AMANI.

Mambo ya Walawi 3: 1-5 "Na matoleo yake kwamba ni sadaka za amani; kwamba asongeza katika ng'ombe, mume au mke, atamtoa huyo aliye mkamilifu mbele ya Bwana............"

Sadaka ya amani inakupatanisha na Mungu na kuweka mahusiano mazuri naye ili muwe katika nia moja na kufanya mambo kwa pamoja. Unamheshimu naye anakuwa karibu nawe na kukupa uwepo wake uweze kustawi. Unastawi kwa sababu unapata neema, huruma na upendo wake.

Hii ni kwa sababu unapopata mahitaji yako moyo wako huwa na amani lakini ukipungukiwa inatoweka. Katika nyakati hizi matoleo yanayowakilisha sadaka ya amani ni Ile sadaka ya upendo kwa Mungu na ndiyo inayoitwa sadaka ya thawabu. Unapochukua sehemu katika ile tisini (90%) iliyobaki katika mapato yako baada ya kutoa fungu la kumi (10%) kwa Mungu inamaana kuwa inakupatanisha naye na kwa kufanya hivyo anakustawisha.

Mungu alimwambia Musa watoe sadaka ya kuteketezwa na ya amani ili watu waweze kupatana na Mungu na kumpa Yeye nafasi anayostahili maishani mwao. Katika utaratibu huu sadaka ya kuteketezwa yaani fungu la kumi na malimbuko huanza kutolewa ndipo hufuata sadaka ya amani. Ukifanya hivyo, utamshinda Shetani kwa urahisi ikiwemo umaskini na maradhi.

NENO LA SIKU.Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha.Tarehe 1/6/2023.SOMO: TIMILIZA LEO YAKO  ILI  K...
01/06/2023

NENO LA SIKU.

Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha.

Tarehe 1/6/2023.

SOMO: TIMILIZA LEO YAKO ILI KESHO USIINGIE KWENYE MAJARIBU.

Mathayo 6:13a “Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu.”

Kwa sababu ya kutokuitimiza jana yako leo ni rahisi kuingia majaribuni, lakini ukiitimiliza leo yako kesho siyo rahisi kuingia majaribuni, itimilize leo yako ili kusababisha majaribu yakae mbali na wewe. Majaribu yapo k**a wewe hautimizi majukumu yako. Kwa maana Biblia inasema Mwanzo 4:7a “ K**a ukitenda vyema, hutapata kibali?” Wale wanaofanya vyema wanapata kibali kwa Mungu.

1 Yohana 5:18 “ Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi.” Muovu hawezi kuja na kukujaribu kwa sababu wewe ni mkamilifu, kwa nini Yesu alijaribiwa? Alijaribiwa kwa ajili yetu, na jaribu halikuja lenyewe bali Roho Mtakatifu alimchukua na kumpeleka kujaribiwa inamaana kuwa ni Mungu mwenyewe ndio alitaka ajaribiwe. Watu wakamilifu majaribu yanawakimbia.

Mwanzo 4:7b “ Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.” Wewe ni mshindi, na ndio maana akasema jaribu lipo linakusubiri lakini yakupasa ushinde. Ni kweli hukutimiliza siku yako na ikafungulia mlango wa ibilisi kukujaribu lakini ili uweze kushinda simama imara na umkemee shetani naye atakimbia. Ukiikamilisha siku una kuwa mtu mkamilifu na unajilinda mwenyewe na yule mwovu atakimbia mbele zako.

NENO LA SIKU.Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha.Tarehe 31/5/2023.SOMO: MFANYE BWANA AWE MSIRI W...
31/05/2023

NENO LA SIKU.

Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha.

Tarehe 31/5/2023.

SOMO: MFANYE BWANA AWE MSIRI WAKO ILI KESHO YAKO IWE BORA.

1 Wakorintho 4:1-5 "Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu".

Uchawi hauwezi kukuondolea baraka zako hatak**a wanaloga usiku na mchana, wewe ndiye unayeuza baraka zako, kivipi? Pale unapoanza kuongea na kila mtu na kutoa siri zako hapo ndipo unauza baraka zako. Biblia inasema sisi ni Wasiri wa siri za Mungu na sio wasiri wa rafiki zetu. Linda siri zako na ukiweza kuzitunza basi umeshinda.

Angalia watu unaochangamana nao ni watu wa aina gani kwa sababu unapokutana na watu kila saa unajifunza tabia za wanadamu, ndipo unaweza kujikuta zile tabia ambazo baba na mama yako hawakuwa nazo au hawakukufundisha unakuwa nazo kwa maana unazipata kwa kuiga na matokeo yake unamkosea Mungu.

Kitakacho sababisha kesho yako na ustawi wako kuwa nzuri ni kile unachokifanya leo. Kitakachofanya jina lako liwe na nguvu, lionyeshe tofauti na maisha yako yawe ya kushangilia ni kile unachokifanya leo, hicho ndicho kinatengeneza kesho yako. Ndio maana Yesu akasema “utavuna ulichokipanda". K**a unapitia hali ambayo sio nzuri amua kuitengeneza leo yako kwa kuacha kuongea siri zako kwa watu na siku zote mfanye Bwana awe Msiri wako. Ukiulizwa swali jibu swali tu usiongeze maneno mengi utamkosea Mungu.

Mathayo 5: 37 "Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu".

Address

Babati Town, Babati
Magugu

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Babati posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share