25/07/2022
MUNGU AMEWEKA HAZINA NDANI YAKO ILI IWE MSAADA NA FAIDA YA WENGINE.
🟣Ivi unatambua kuwa kilichoko Ndani yako si kwaajili yako pekee Bali ya watu wengine?.
➖K**a Ndani yako umewekwa uwezo wa kufundisha unahitaji watu Ili utumie uwezo huo kufundisha,na unapo fundisha wale unaowafundisha wananufaika na mafundisho yako.
➖Umewekewa uwezo wa kuimba?,Bado kupitia kuimba unaweza gusa maisha wengine kwa kuwatia moyo,kuonya,kuwavuta wamjie Mungu pia kuwajenga.
⭕Jichunguze; Chochote ambacho Mungu ameweka Ndani yako anataka kimletee yeye Utukufu kwa wewe unapo kitoa kuwahudumia wengine.
Warumi 12
5 Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.
6 Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani;
7 ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake;
8 mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha.
JIULIZE...
🟥Umekuwa unatumia kile ambacho Mungu ameweka Ndani yako kwaajili ya kuwahudumia wengine?,Ili Mungu aendelee kupata Utukufu kupitia kile ameweka Ndani yako!!!!!.
➖Kumbuka usipo tumia kile kilichopo Ndani yako kuwahudumia wengine unasababisha jambo flani ambalo haliko sawa.
➖Tambua thamani ya mda katika kuachilia kile kilichoko Ndani yako,Usifikiri unao mda zaidi k**a unaupoteza mda ulio nao Sasa.
🟥Jikumbushe kuwa Kuna siku utatoa hesabu kwake yeye aliyeweka Ndani yako Ili utumie kuwagusa wengine.
Mathayo 25
15 Akampa mmoja talanta tano, na mmoja talanta mbili, na mmoja talanta moja; kila mtu kwa kadiri ya uwezo wake; akasafiri.
19 Baada ya siku nyingi akaja bwana wa watumwa wale, akafanya hesabu nao.
FAIDA ZA KUTUMIA KILICHOKO NDANI YAKO.
🟣Kupata furaha ya kweli na bubujiko la amani ikitokea Ndani na kuleta ustawi wa maisha ya kiroho na kimwili.
3 Yohana 1
2 Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, k**a vile roho yako ifanikiwavyo.
➖Wakati mwingine madhara ya kiafya yanaweza mpata mtu pale anapo acha kutumia kile ambacho Mungu ameweka Ndani yake.
🟣Inaleta furaha na Ustawi kwa wale ambao utawahudumia kupitia kilicho Ndani yako.
🟥MUNGU HUTUKUZWA SANA PALE AMBAPO WEWE UNATUMIA KILE AMEWEKA NDANI YAKO, NA KUTUMIA KILE MUNGU AMEWEKA NDANI KWA UONGOZI WAKE HUO NI UTII.
USHAURI.
Jijengee tabia ya kujitathimini mara kwa mara kuwa kile ambacho Mungu ameweka Ndani yako kwaajili ya kuwahudumia wengine umekuwa unakitumia sawa na Kusudi lake yeye aliye kuumba.
Neema ya Mungu iwe juu yako.