Nehemia Ministry

Nehemia Ministry Nehemia ni huduma ambayo inaendeshwa na Mwongozo wa Biblia inayowaweka watu waweze kutubu na kumfuata Yesu Kristo

06/04/2022

Najua umeomba sana haujaona mabadiliko yoyote, ushofu Wala isolate tamaa; unadhihakiwa na kutukanwa upo kanisani hujapona, hujafanikiwa, hujaolewa, uchumi wako hauko vizuri pamoja na maombi uliyoomba. usivunjike moyo MUNGU AMEJIBU,MAOMBI YAKO, NI SWALA LA MUDA TU, utafurahi utainuliwa. Soma MWANZO. 32 : 24 - 30 Yakobo aliingia kutafuta uso wa Mungu akiwa yuko vizuri, alikutana na Mungu uso kwa uso, na nafasi yake imeokoka. Ila amerika kwa maombi amevunjika mfupa wa paja lake hakuangalia watu watasema nini, alijua jambo moja tu, nimebarikiwa sitaitwa Yakobo tena bali Israel. Ktk ulimwengu wa umebarikiwa, ni swala la muda tu watakuheshimu, EV, Thomas Vuriva

06/04/2022
WATU WAKIFUATILIA MOJA KATI YA SEMINA ZA MTUMISHI THOMAS VURIVA
26/03/2014

WATU WAKIFUATILIA MOJA KATI YA SEMINA ZA MTUMISHI THOMAS VURIVA

26/03/2014

SIKU YA TATU
UREJESHO WA USHIRIKA KATI YA MWAMINI NA MUNGU.
UTANGULIZI
- Utakumbuka nilikuambia ni muhimu san kuwa na Ushirika na Mungu (Fellowship)
- Na usikubali kuupoteza kabisa Ushirika wako na Mungu.Ikatokea umepoteza Ushirika na Mungu tengeneza haraka.
- Vinginevyo gharama yake ni kubwa sana.

Andiko a Msingi ni LUKA 19:10.
- Nilikupa mifano kadhaa ya walipoteza Ushirika na Mungu lakini wakarejesha haraka huo Ushirika na Mungu.
- Na mambo yao yakawa mazuri mno.

MIFANO MINGINE.
1. YOHANA 4:1-26
YOHANA 4: 27-30
- Aliishi maisha mabaya kimaadili,lakini akapata neema ya kutengeneza Ushirika na Yesu.

YOHANA 4: 39-42
- Ushirika wako na Mungu ukiwa mzuri utawajibika kuwaambia wengine habari za Yesu.

Nikupe mifano:-
Habari za Mzee na Mkewe jaribu la mtoto tumboni hachezi.

2. HABARI ZA IBRAHIMU
MWANZO 18:16-22
-Walikuwa na Uhirika na ungu kwa kiwango ambacho Mungu alihitaji ushauri kwa Ibrahimu.

3. HABARI ZA HENOKO
MWANZO 5:22-24
- Ni sentensi ndogo sana au ni maneno machache sana lakini yanaisha kutudhihirishia uhusiano waliokuwa nao Henoko na Mungu – Henoko alienda na Mungu.
- Mungu hakuweza kuachana na Henoko walisindikizana mwisho akaamua kutwaa (Ushirika)

NA MWL THOMAS VURIVA
inaendelea,.......................................

26/03/2014

SIKU YA PILI
UREJESHO WA USHIRIKA KATI YA MWAMINI NA MUNGU.
UTANGULIZI
- Marudio machache ya somo la jana.
• Ushirika kati ya mtu na Mungu ni muhimu sana.
• Usikubali kupoteza kabisa uhusiano wako na Mungu.
• Unapopoteza Uhusiano wako na Mungu iyo swala la potelea mbali.
- Gharama yake ni kubwa kwako.
- Utakumbuka nilikuambia jana Adamu na mkewe walikuwa na uhusiano (Ushirika) mzuri na Mungu.
- Walipopoteza ule Ushirika iliwagharimu na hata sisi tunaonja hiyo gharama.
Na matokeo - Kifo
Magonjwa
Misukosuko
• Wanadamu tunapata shida sana kwa sababu ya kupoteza Ushirika wetu na Mungu.
LUKA 19:10
“ Kwa sababu Mwana wa Adamu amekuja…………………….”
• Nikakuambia ukiona Injili inahubiriwa mahali popote Lengo lake kurudisha Uhusiano kati ya mtu na Mungu.

UJUMBE WA LEO
I KORINTHO 1:9
- Mungu anatuita tuingie katika Ushirika na Mwanawe Yesu Kristo.
KOLOSAI 1:21-22
- Ametengeneza Mazingira ya kuwaleta watakatifu wasio na waa (Lawama)
KUMBUKUMBU 28:1-3
ISAYA 44:3

NJIA YA KUPATA HUO USHIRIKA
TUBU (TOBA)
Toba au kutubu ni njia sahihi ya kupata Ushirika na Mungu.Kama ambavyo dhambi inaharibu uhusiano na Mungu,hali kadhalika toba inaruisha ushirika kati ya Mtu na Mungu.

Nikupe Mifano
1. MIRIAM NA HARUNI
HESABU 12:1-10
11-16
- Dhambi yao iliharibu Ushirika kati yao na Mungu,matokeo yake WINGU LILIONDOKA.
- Miriam akapigwa na ukoma.Ikagharimu safari nzima ya wana wa Israel isimame siku 14.
- Mitaani wanasema “Mchuma janga hula na wakwao”
Tafuta Ushirika na Mungu.
MUSA
KUTOKA 3:1-6
KUTOKA 3:13

2. MWANAMKE MSAMARIA
YOHANA 4: 1-26
YOHANA 4: 27-30
- Aliishi maisha mabaya na Mungu,lakini akapata Neema ya kutengeneza Ushirika na Yesu.
YOHANA 4:39-42
- Ushirika wako ukiwa mzuri na Mungu,hutakaa kimya utawashuhudia watu.
NA MWL,THOMAS VURIRA
inaendelea.........................

26/03/2014

SIKU YA KWANZA
SEMINA YA NENO LA MUNGU
UREJESHO WA USHIRIKA KATI YA MTU NA MUNGU (Mwamini)
UTANGULIZI
- Ushirika kati ya mtu na Mungu ni kitu muhimu san asana.
- Usikubali kupoteza uhusiano wako na Mungu.
- Utakapopoteza uhusiano wako na Mungu siyo jambo la potelea mbali,gharama yake ni kubwa.

MWANZO 3:8-13
- Hawa watu walikuwa na Ushirikiano mzuri na Mungu,maisha yao yalikuwa mazuri Baraka na mafanikio yalikuwa makubwa.
- Walipoharibu ushirika wao na Mungu,mambo yakaharibika na kuwa magumu kwao.

MWANZO 3:21-24
- Wanafukuzwa kwenye bustani ya Edeni,wailime ardhi ndipo wale.
- Ndipo chanzo cha kifo,magonjwa na vurugu zote.

LUKA 19:1-10
- Chanzo cha maisha mabaya ya Zakayo,hatimaye kukosa kibali kwa majirani na watu wengine na kupoteza ushirika na Mungu.
“Yesu alisema ,Nimekuja kutafuta kile kitu kilichopotea”
- Ukiona Injili inahubiriwa kwa nguvu iwe:-
Redio
Television
Mikutano /semina.
- Mungu anatafuta kurejesha ushirika kati yako na yeye.Yesu alikuja kurudisha Ushirika kati ya Adamu na Mungu.

MIFANO
YOHANA 4:1-26
- Mwanamke aliyeishi maisha mabaya Kimadili amepoteza Ushirika na Mungu.
YOHANA 4:39-42
- Ushirika wako na Mungu ukiwa mzuri hata dhambi huwezi utenda tena.
- Utapata mzigo wa kuhubiri watu wengine juu ya kutengeneza Ushirika na Mungu.

EFESO 2:16 (11-16)
KOLOSAI 1:21-22
- Ametengeneza mazingira ya kuwaleta watakatifu wasio na waa (Lawama) wala uchafu.
- Ukianzisha ushirika na Mungu atakutembelea tu kila siku.masaa 24 siku 365.
- Yesu anatafuta Ushirika kati yako na yeye.

KUMBUKUMBU 28:1-14
UFUNUO 3:20
- Anatafuta apewe nafasi ndaniya Mwanadamu.
• Nitakula pamoja naye.
• Na yeye atakula pamoja name.
I KORINTHO 1:9
- Mungu anatuita tuingie katika ushirika na Mwanawe Yesu Kristo.
II KORINTHO 13:14
“Ushirika na Roho Mt ukae nanyi nyote”

NA MWL,THOMAS VURIRA
enaendelea...............

Moto wa Roho Mtakatifu
25/03/2014

Moto wa Roho Mtakatifu

Katika mafundisho ya Semina ndani ya Aglikana Korogwe
25/03/2014

Katika mafundisho ya Semina ndani ya Aglikana Korogwe

25/03/2014
ni moto wa Yesu unafanya kazi ya kufungua watu walio katika vifungo vya mapepo na majini,mila na n.k  PRAISE JESUS
25/03/2014

ni moto wa Yesu unafanya kazi ya kufungua watu walio katika vifungo vya mapepo na majini,mila na n.k PRAISE JESUS

NI MIUGIZA YA MUNGU WATU WAKIFUNGUKA KATIKA SEMINA YA WAOMBAJI ILIYOFANYIKA ANGLIKANA KOROGWE
25/03/2014

NI MIUGIZA YA MUNGU WATU WAKIFUNGUKA KATIKA SEMINA YA WAOMBAJI ILIYOFANYIKA ANGLIKANA KOROGWE

25/03/2014

MUNGU NI MWEMA KARIBUNI SANA KATIKA PAGE YETU.MUNGU AWABARIKI

Address

+255655702040
Lushoto

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nehemia Ministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Nehemia Ministry:

Share