12/08/2025
Shallom Shallom Mwana Ngomeni
JUMANNE YAKO IMEBARIKIWA
SOMO: CHOCHOTE KISICHOKUBALIANA NA MAPENZI YA MUNGU JUU YAKO HAKITOSIMAMA.
Neno: Isaya 7:7 Bwana MUNGU asema hivi, Neno hili halitasimama wala halitakuwa.
Ukiisoma vyema hii sura utagundua mfalme Ahazi mwana wa Yothani na mwana wa Uzia alipokuwa mfalme wa YUDA kuna wafalme wawili waliopanga njama kinyume na Yuda nao ni Resini wa Shamu na Peka wa Remalia. Walipanga njama za kuiangamiza Yuda na watu wake. Ahazi mfalme wa Yuda akawa katika kuugua aliposikia habari hii. Moyo wake ulimuuma saana. Alikuwa ni mwenye maumivu na kuvunjika moyo ndipo Mungu akamtuma Isaya kwake na Isaya hakuwahi kupepesa macho kwa ujasiri akamwambia Mfalme Ahazi kuwa Jambo hili halitasimama wala halitakuwa. Unaposikia jambo kusimama maana yake ni *kuonekana* na kuwa maana yake ni *kuthibitika*
Mtu wa Mungu wakati natafakari Mungu juu yako Mwana Ngomeni nikasikia hili neno ndani yangu kuwa niseme nawe. Sijui unapitia nini au umesikia nn kinachouumiza moyo wako ila nsikia kukwambia hili neno unalolisikia k**a utisho kwako halitakuwa na halitasimama. Halitaonekana wala halitathibitika.
Na kwao wanaokupangia mashauri ya kigeni yenye asili ya Rasini na Peka kwamba upigwe katika biashara zako, Maisha yako, kazi zako, mifugo yako, Uzao wako, Afya yako nk nk nk hawataweza na kwamba jambo hili halitathibitika wala kuonekanani dauti za mfano wa simba aungurumaye.
Isaya 8:10
“Pangeni shauri, nanyi mtaangamizwa; semeni neno, neno hilo halitasimama, maana Mungu yu pamoja nasi.”
K**a ilivyokuwa kwa Ayubu 5:12
“Yeye huvunja shauri la hila, mikono yao isitimize makusudi yao.” Atavunja shauri lolote ambalo limefanya na kusimama kinyume nawe. Na kila mkono wenye kusudi ovu hautafanikiwa
Mithali 19:21
“Mawazo mengi yako mioyoni mwa wanadamu; lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.
Waweza omba hivi
Baba yetu uliyembinguni. Tunalitukuza na kuliinua jina lako takatifu. Ahsante kwa sababu ya asubuhi hii njema. Ahsante kwa sababu ya hakikisho la ushindi na ubatilisho wa mashauri yanayopangwa kinume nami na uzao wangu. Nakuomba neno hili likathibitike kwangu kuwa hakuna mipango ya kunisambaratisha itakayosimama au kuwa
Shallom