Neno La Mungu Ni Uzima

Neno La Mungu Ni Uzima Kwa maana jinsi hii mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwana wake wapekee ili kila mtu amwaminie asipotee bali awe na uzima wa milele.(Yoh 3:16).
(1)

21/02/2026

🙏 Sala ya Kuvunja Roho ya Manung’uniko

Baba wa Mbinguni,
Nakuja mbele zako kwa unyenyekevu.
Nakiri kwamba mara nyingi nimekuwa nikilalamika, kunung’unika, na kukata tamaa.
Nimesahau wema wako na baraka zako ulizonipa.
Leo ninaomba unisamehe.
Safisha moyo wangu na unifundishe kuridhika katika hali yoyote.
Nisaidie kuona mema katikati ya changamoto.
Nipe roho ya shukrani badala ya kulalamika.
Nipe amani badala ya hasira.
Nipe imani badala ya hofu.
Naamini kwamba wewe bado una mpango mwema kwa maisha yangu.
Kuanzia leo nachagua kushukuru, kuamini, na kusonga mbele.
Katika jina la Yesu,
Amina.

21/02/2026

Hizi ni hatua za vitendo za kuondokana na roho ya manung’uniko:

1️⃣ Tambua Chanzo Chake

Jiulize kwa uaminifu:

Naumia kwa sababu gani hasa?

Nimevunjika moyo kwa nani au kwa nini?

Nimeweka matarajio makubwa kupita hali halisi?

Mara nyingi manung’uniko ni dalili ya maumivu ya ndani.

2️⃣ Badilisha Maneno Yako

Biblia inasema katika Wafilipi 2:14:

> “Fanyeni mambo yote pasipo manung’uniko…”

Jaribu:

Badala ya kusema: “Kwa nini mimi kila wakati?”

Sema: “Nitajifunza nini kupitia hili?”

Maneno hubadilisha mtazamo.

3️⃣ Jenga Tabia ya Shukrani

Kila siku andika mambo 3 ya kushukuru — hata madogo sana:

🙏Uhai

🙏Afya

🙏Fursa ya kuanza upya

Shukrani huua manung’uniko polepole.

4️⃣ Epuka Mazingira ya Kulalamika

Ukikaa na watu wanaolalamika kila wakati, roho hiyo inakua ndani yako. Tafuta watu wenye mtazamo wa matumaini.

5️⃣ Omba kwa Moyo wa Unyenyekevu

Mwambie Mungu wazi:

> “Baba, nisaidie nione mema hata katikati ya changamoto.”

Mungu hubadilisha moyo kabla hajabadilisha mazingira.

6️⃣ Chukua Hatua Ndogo za Mabadiliko

Manung’uniko hupungua unapochukua hatua:

✍️Panga bajeti

✍️Tafuta kazi ndogo ya ziada

✍️Jifunze ujuzi mpya

SOMO; KUTOKA KWENYE VIFUNGO VYA FAMILIA. Mwanzo 12:13"Tafadhali useme, wewe u ndugu yangu, iwe heri kwangu kwa ajili yak...
21/11/2024

SOMO; KUTOKA KWENYE VIFUNGO VYA FAMILIA.

Mwanzo 12:13
"Tafadhali useme, wewe u ndugu yangu, iwe heri kwangu kwa ajili yako, na nafsi yangu iishi kwa ajili yako."

Familia unayotoka wewe na ukoo unaotoka unahusiana na maisha yako, ndiyo maana Biblia inasema adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake, na unapoyaangalia maisha yako ya kila siku upo k**a ulivyo ni kwa sababu ya familia uliyotokea.

2Timotheo 1:5
"nikiikumbuka imani uliyo nayo isiyo na unafiki, ambayo ilikaa kwanza katika bibi yako Loisi, na katika mama yako Eunike, nami nasadiki wewe nawe unayo."

Utaona hapa kwamba imani imeanzia kwa bibi ikaja kwa mama na inaenda kwa mtoto, kwa hiyo unaweza kuona kwamba kumbe kwenye familia kuna vitu vinaweza vikasafiri mtu hadi mtu. Ukija kuangalia kwenye familia yenu utaona kwamba kuna mambo yanayosafiri ambayo si mazuri utaona kwamba hamuwezi kukaa mahali pamoja kwenye familia, ama kufanya biashara kati ya ndugu na ndugu, yote ni kwa sababu ya roho iliyo nyuma ya familia kwa maana kila familia ina roho nyuma inayoiongoza.

Si kwamba wanaofanikiwa kwenye familia zao ndiyo wanaakili zaidi hapana, ila kuna roho iko nyuma ya familia ambayo inasababisha wafanikiwe ila kufanikiwa ama kutokufanikiwa kuna roho inayosimama badala yao. K**a hutaweza kufungua vifungo vinavyoikabili familia yenu tambua kwamba hutaweza kufanikiwa kwenye familia yenu.
Unaweza kuona kwenye familia mama aliolewa mke wa pili na mtoto anakuja kuolewa mke wa pili lakini kumbe sababu kubwa ni kwamba nyuma yake kuna roho inasababasha wawe hivyo walivyo.

MAMBO 4 AMBAYO NI MISINGI YA VIFUNGO VYA FAMILIA

1.Uchawi wa kifamilia
Familia nyingi leo zinateseka kwa sababu mwanzo wa familia hizo zilianza kichawi au kishirikina au kuna mkoba wa familia. Vitu k**a hivi vinasababisha familia ikae kwenye Kongwa la uchawi. Unaweza ukaona ndani ya familia kuna mtu mmoja amenunua uchawi, au amerithi kutokea mahali fulani. Vitu k**a hivi vinasababisha familia ikae kwenye vifungo vizito. Unaposema kuna mchawi kwenye familia yetu tambua kwamba kwenye hiyo familia kuna madhabahu ya kishetani na kuna njia ya kwenda kwa shetani. Ndani ya familia kukiwa na mtu ambaye ameokoka au ni mchungaji basi ujue madhabahu ya Mungu iko ndani ya familia na hakuna uchawi utakayoiweza.

2Wafalme 17:17
"Wakawapitisha watoto wao, waume na wake, motoni, wakapiga ramli, wakafanya uchawi, wakajiuza nafsi zao wapate kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, hata kumkasirisha."

Hakuna kitu kibaya k**a Mungu akasirike kwa ajili ya familia yenu, tunamwona Samweli anamwomba Mungu kwa ajili ya Sauli ila Mungu anamwambia Samweli, Sauli simtaki nilishamkataa. Mungu akiona mchawi kwenye familia yenu anachukizwa na familia hiyo na utaanza kuona mabaya yanaanza kuwapata, utaona huyu aliye mchawi wa familia utaona kwamba akienda mahali kwenye kikao anang'ang'ania awe kiongozi ili aifunge familia na moja kwa moja anaitoa familia kwenye mikono ya Mungu, jambo la Muhimu ni kuung'oa uchawi na ushirikina kwa jina la Yesu. Ili ufanikiwe ni mahusiano yako mazuri na Mungu. Unakuta mabaya yanawapata ni kwa sababu ya kujichanganya na mambo ya kishetani, ni lazima utambue kwamba Mungu hajichanganyi na wabaya.

Kumbukumbu la Torati 18:10-12
10 Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,
11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.
12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.

Unaanza kujiuliza, Kwanini Mungu hatendi nikimwomba?, ni kwa sababu ndani ya familia kuna waabudu sanamu, kuna wachawi na washirikina kuna waenda kwa waganga, lakini leo amua kuwaondoa wote waendao kwa waganga, na wachawi, sema leo asionekane mchawi ama mshirikina ama muenda kwa mganga ili Mungu akae kwenye familia yenu kwa jina la Yesu.

Usiwe na ndugu muenda kwa mganga kwa sababu utakuwa maskini kila siku. Kila kitu unachokiona duniani leo chanzo chake ni kwenye ulimwengu wa roho, lazima utambue kwamba kila tatizo linalokupata nyuma yake kuna mkono wa mtu unaotenda kazi ili usifanikiwe. Familia inapokaa pamoja ni uzima na baraka lakini shetani hataki mkae pamoja kwa sababu anajua mtafanikiwa.
Kwa kadri wachawi wanapokaa ndani ya familia yenu ndivyo milango ya baraka inafunga, ila kwa kadri unavyowaondoa wachawi kwenye familia yako ndivyo milango ya familia unavyozidi kufunguka kwa sababu Mungu amesema asionekane mchawi kwenu hivyo asipoonekana neema ya kufanikiwa inaonekana. Amua leo kuwaondoa wachawi, washirikina ama waenda kwa waganga kwenye familia yenu kwa jina la Yesu.

Nahumu 3:4
"Kwa sababu ya wingi wa ukahaba wa yule kahaba mzuri, yule bibi wa mambo ya uchawi, auzaye mataifa kwa ukahaba wake, na jamaa za watu kwa uchawi wake."

Unapoviona vifo vyenye utata kwenye familia amini kwamba kwenye familia kuna mchawi wa familia. Mwanadamu ni k**a mashine hawezi kufa ghafla lazima kuwe na sababu ama mkono wa Mtu, uwo mkono wa mtu leo ukatwe kwa jina la Yesu. Haya matukio yasiyoeleweka lazima utambue kwamba kuna bibi wa kichawi, mtoto wa kichawi, mwanaume wa kichawi ama mwanamke wa kichawi ambao wanasababisha hayo yatokee. Wewe hujafanikiwa sio kwamba huna nyota ya kufanikiwa hapana ila kuna mchawi anayesababisha usifanikiwe, usimuache mchawi kutaabisha familia yako.

Mambo ya Walawi 20:27
"Tena mtu mume au mtu mke aliye na pepo, au aliye mchawi, hakika atauawa; watawapiga kwa mawe; damu yao itakuwa juu yao."

Tumepewa maelekezo kwamba tuwapige kwa mawe, wewe umeacha wafilisti waendelee kukutesa leo achia jiwe limpate mchawi yeyote aliye kwenye familia, kwenye biashara aliye mahali popote pale kwa jina la Yesu. Yupo mchawi anayeng'ang'ana kuiangusha familia, ukiangalia kwenye familia kuna matabaka kwamba kuna wengine wanafanikiwa sana lakini wengine hawafanikiwi.

2.Mizimu/Mungu ya Kifamilia
Lazima uelewe kwamba tangu babu wa babu kuna ibada na pia kuna vitu huwa vinaabudiwa na ibada hizi ni za kishetani moja kwa moja zinamfanya shetani aimiliki familia yenu.

Mwanzo 31:30
"Basi sasa, umetoka kwa sababu umetamani sana nyumba ya baba yako. Mbona basi umeiiba miungu yangu?"

Kwa asili familia inaweza ikawa na Miungu ya kishetani, ama kuna vitu vinatuunganisha na shetani bila kujua. K**a familia yenu ina misingi ya kishetani lazima uwe na matatizo, Unakuta kuna mganga anaitwa ndani ya familia anaitwa ili aizindike familia na huku ndiko kuabudu mashetani na familia inakuwa na vifungo. Ki-mila cha kiafrika kina mahusiano moja kwa moja na mashetani. Misingi yetu ya kiafrika chimbuko lake limetokana na mashetani, Unakuta kwenye familia kinachotupinga sisi ni ile misingi ya kishetani ya familia.

Luka 3:23
"Na Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa amepata umri wake k**a miaka thelathini, akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusufu, wa Eli,"

Unaweza ukaona familia ya Yesu imeanza vizuri kabisa kwamba ukoo wake kuanzia huko nyuma kuna uhusiano na Mungu moja kwa moja lakini ukija kuangalia kwenye familia yako chimbuko la familia yako utakuta babu wa babu alikuwa anaabudu mizimu. Ukijikuta unapenda mila au ndani yako kuna aina fulani za mila mila utambue kwamba ndani yako kuna chembechembe za ushetani. Kinachofunga sana maisha yetu sisi ni mila za kifamilia, Unakuta kuna mtu mmoja kwenye familia anaenda kwa waganga anasababisha familia ifungwe iwekwe chini ya mamlaka ya giza. Unajikuta kwenye familia hamfanikiwi kwa sababu familia imekabidhiwa kwenye madhabahu za mizimu ya ukoo.
Kuna minyororo ya giza ndani ya familia ambayo inaleta matatizo, inaleta laana, inaleta mikosi kwenye familia kwa sababu ya uchawi uliyoko ndani ya familia na Mungu anaamua kutengana na nyinyi tambua kwamba hamtaweza kufanikiwa kamwe kwa sababu Mungu ameondoka kwenu.

Waamuzi 6:25-26
25 Ikawa usiku uo huo Bwana akamwambia, Mtwae ng'ombe wa baba yako, yaani ng'ombe wa pili, wa miaka saba, ukaiangushe madhabahu ya Baali, aliyo nayo baba yako, ukaikate Ashera ile iliyo karibu nayo;
26 ukamjengee Bwana, Mungu wako, madhabahu juu ya ngome hii, kwa taratibu zake; ukamtwae yule ng'ombe wa pili na kumtoa awe sadaka ya kuteketezwa, kwa kuni za ile Ashera uliyoikata.

Mungu anataka kukutumia wewe lakini akiangalia anaona madhabahu nyingine iko ndani yako anaghairi kukutumia. Lakini unapoamua kuondoa madhabahu ya kishetani kwenye familia yako utaona Mungu anaanza kukutumia. Kuna watu wanakaa kwenye familia, kwenye maisha yetu na Tunaona wako vizuri lakini bila kujua huyo/hao ndiyo wanaoharibu familia. Unapoleta ndugu kwa pamoja unatafuta ugomvi na shetani, kwamba shetani hapendi kuona mnapiga hatua kwa sababu anajua mkikaa pamoja lazima maendeleo ya familia yataonekana. Utaona kwenye familia yule anayejitahidi familia ikae kwa pamoja, anayefanya mambo ya kuleta maendeleo kwa pamoja lazima shetani asababishe jambo baya limpate ama afe au augue kwa muda mrefu. Unakuta familia yenu hamuendi vizuri ni kwa sababu hamjamng'oa yule anayeleta kizuizi kwenye familia. Kwenye familia yako k**a hujafanikiwa kushinda vita ya ndani tambua kwamba hata vita ya nje hutaweza. Mafanikio yako, ushindi wako na baraka zako huanzia kwenye familia, k**a hujawashinda wachawi na waganga wa familia tambua kwamba hutaweza kushinda kamwe amua kuwaondoa wachawi na waganga wa kifamilia ndipo mtafanikiwa kwa jina la Yesu.

Ukiri
Damu ya Yesu imeniosha, damu ya Yesu imetakasa, damu ya Yesu imeniweka huru, leo nashindana na mamalaka zote za giza, mamlaka zote za mizimu, na mamlaka zote za balaa na mikosi nazipiga kwa damu ya Yesu, mahali popote nilipounganishwa na familia za giza, mizimu, uganga, mshirikina toka kwa damu ya Yesu, leo naingia kwenye familia yetu nateketeza kila vyanzo vya uovu, kila vyanzo vya giza, kila vyanzo vya kishetani, vyanzo vya kuzimu navipiga kwa damu ya Yesu, naviharibu kwa damu ya Yesu, navipasua kwa damu ya Yesu, Amen.

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.Mathayo 17:21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]Kuna mam...
22/10/2023

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

Mathayo 17:21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]

Kuna mambo ambayo kamwe hayawezi kutokea bila kufunga…Neno “kufunga” maana yake ni “kutokuruhusu kitu kiingie wala kitoke sehemu fulani”…..kwamfano kuku ili aweze kuwa na Watoto hana budi kupitia kipindi cha mfungo wa siku 21, kutaga mayai sio kuwa na Watoto, bado kuna kazi nyingine ya ziada…itambidi, ajizuie kula, ajizuie kuzurura-zurura mitaani…ajizuie kucheza na wenzake..ili asilipoteze lile joto, vinginevyo akiwa mzembe mayai yatakuwa viza..na ndege wote wa angani ni hivyo hivyo, upo wakati itawabidi waliache anga kidogo, wajifungie ndani kutamia mayai yao.

Na sio tu mfungo wa kutokujizuia kula unahitajika ili kuumba jambo jipya…bali pia mfungo wa Maisha…kwamfano ili mwanafunzi aweze kufanya vizuri katika mitihani yake…hana budi kufunga milango fulani fulani…atakwenda shule ya bweni (huko tayari ni kifungoni)..atakaa huko miezi hata 6 bila kutoka hata nje ya uzio wa shule, mbali na wazazi wake na ndugu zake, na mafariki zake wa mtaani…ni k**a tu kuku aliyeko bandani, sio hilo tu peke yake, itamlazimu aache matumizi ya simu, tv, aache kuangalia tamthilia hizi au zile, movie, aache kabisa kuzurura…itambidi kila siku za muda wake wa masomo aishi Maisha ya kuitumikia elimu..ataamka mapema asubuhi, atachelewa kulala…Sasa anafanya hayo ili asilipoteze lile joto…

Kwasababu anajua akishika mambo mawili au Zaidi kwa wakati mmoja…hatafaulu…kichwa hicho hicho kimoja akikijaza tamthilia, movie na miziki na wakati huo huo masomo…HATAFAULU!…Kwahiyo ni bora aache kimoja afuate kingine…Na Zaidi ya yote anakuwa radhi kuvumilia vyakula vibovu vya shuleni mpaka anahitimu ili tu apate anachokitafuta…

Vivyo hivyo…na katika Imani…hatuna budi kufunga baadhi ya mambo ili TUPATE YALIYO BORA!…Utasema mimi miaka yote nimeshindwa kuushinda uasherati…ni kwasababu haujaamua kuutoa maishani mwako…bado hujafunga baadhi ya milango!…Mbona wengine waliookoka wanaweza kwanini wewe ushindwe?..maana yake tatizo lipo kwako sio kwa Mungu wako!….Hujafunga hiyo milango ya uasherati…bado kuna vimelea vinavyokuchochea wewe kuendelea kuwa hivyo ulivyo…na hivyo si vingine Zaidi ya kampani ulizonazo, au picha unazoziangalia, au mazungumzo unayoyazungumza kila wakati yenye maudhui ya kizinzi, au mitandao unayoitembelea, au mtu unayeishi naye…K**a ukifunga kweli kweli na uk**aanisha kuutafuta uso wa Mungu…hayo mambo hayatakuendesha kamwe!!…

Kwanini hulielewi Neno la Mungu unapolisoma na huku umeshaokoka?… ni tabia tu uliyonayo!…na sababu zake ni zile zile za kwanini mwanafunzi haelewi anaposoma…Ni kwasababu hajaamua kuacha kila kitu na kuongeza umakini kwa kile anachokisoma….Utaona anafungua tu kitabu na kusoma Mada iliyopo katikati ya kitabu, halafu analalamika haelewi…sasa ataelewa vipi?..na wakati mada za kwanza zilipokuwa zinafundishwa darasani yeye alikuwa anacheza huko nje wakati wenzake wanasoma?…



Hali kadhalika utaelewa vipi kitabu cha Yeremia wakati madarasa ya biblia yanayofundishwa makanisani huudhurii??..Hujawahi hata kukisoma kitabu cha Mwanzo peke yako na kukimaliza…utakielewa vipi kitabu cha kutoka?…wakati wa asubuhi au jioni wa utulivu ambao ungetakiwa kukaa chini kwa bidii yako mwenyewe kusoma Biblia…wakati huo ndio unafungua whatsapp na facebook?, kusoma Habari za kidunia??…halafu unalalamika hulielewi neno?…Nakuambia ukweli biblia ni kitabu kirahisi sana kukielewa kuliko vitabu vyote endapo tu, tutaamua kumtii Mungu na kuzingatia kulisoma Neno lake kwa bidii…

kwasababu Roho Mtakatifu yupo kutusaidia kulielewa, kwahiyo kazi inakuwa rahisi sana…

Lakini k**a Maisha yako hutajishughulisha kutenga muda kusoma Neno lako mwenyewe, angalau kuanzia kitabu cha Mwanzo, ukatulia, ukasoma hatua kwa hatua..bila kutegemea kufundishwa na mtu…utajikuta ufahamu wako unakuwa kwa haraka sana…na KUZALISHA KITU KIPYA KATIKA MAISHA. Lakini ukipalilia tabia ya kutolisoma kwa bidii Neno, hautazalisha chochote…

Hivyo funga leo vitu ambavyo ulikuwa umeviachia mlango wazi katika Maisha yako, ambavyo vinazuia wewe kutoivisha kitu chochote kipya!…matamthilia ya Kikorea, ya ki-Nigeria, ya-Kifilipino, ya Ki-hindi na mamovie yote pamoja na MIPIRA!…ni mambo yanayoondoa joto la Maisha yako ya kiroho, Jitenge achana nayo Jiondokee..…Wewe utaona unajifurahisha tu, lakini katika roho mayai uliokuwa unayatamia yanazidi kupoa na kuwa viza!…kwasababu tulivyoumbwa hatuwezi kushikilia mambo mawili kwa wakati mmoja.

Je Umewahi kuwasikia watu wanaosema “Ngoja nikatazame tamthilia fulani nipoteze mawazo au ngoja nikatazame movie au mpira nipoteze mawazo au kupunguza stress?”…. umewahi kujiuliza kwanini wanahusisha na neno “kuondoa stress au kupunguza mawazo”?….Ni kwasababu ni kweli wanapokwenda kutazama hayo mambo yanasababisha kile kitu ambacho kilikuwa kimeingia ndani ya mioyo yao kipotee, hivyo k**a wakiendelea kujiburudisha hivyo kwa kipindi fulani hatimaye kile kitu ambacho kilikuwa kinawaumiza kichwa kinamezwa na zile burudani….Hali kadhalika k**a mtu alikuwa ametoka kusoma Neno vizuri na kulielewa…ile ni mbegu inakuwa imepandwa ndani yake….Lakini sasa anapotoka na kwenda kutazama vichekesho, au mipira, au movie, au tamthilia wakati wote au kuhudhuria hudhuria party party zisizo za muhimu, kidogo kidogo kile kilichopandwa ndani yake kinaanza kujizika….hata k**a hapendi! Kitapotea tu!..na baada ya kipindi kupita atajikuta kakisahau kabisa….

Hivyo tunajukumu zito la kulinda kile kilichowekwa ndani yetu na Mungu ili tupate kile tunachokitafuta kumbuka biblia tena hili Neno.

“namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga”.

Nyakati hizi ni za mwisho. Tukaze mwendo tuufikie mwisho mwema wenye mafanikio.

Kwani biblia inasema.. “Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako. (Ufunuo 3:11)

Bwana atubariki.

JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.Mhubiri 7:20 “Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ...
21/10/2023

JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.

Mhubiri 7:20 “Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ambaye afanya mema, asifanye dhambi.

21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.

22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine”.

Kitabu cha Mithali na Mhubiri ni vitabu vilivyojaa mafunzo mengi ya maisha ya kawaida, tukiachilia mbali yale ya rohoni. Vitabu hivi vimeandikwa na mtu mmoja ambaye ni Sulemani. Hivyo leo tutaangalia jambo moja la kujifunza kwenye maisha yetu ya kawaida sisi k**a wakristo.

K**a tunavyosoma hapo katika mstari wa 21 na 22 inasema “usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa”… Sasa ni jambo la kawaida kwa kadiri tunavyoishi hapa duniani, kupitia katika hali tofauti tofauti, kuna wakati utapitia hali ya kuzungumziwa vibaya, kusengenywa, haijalishi utakuwa ni mwema, au umefanya mazuri kiasi gani, hilo haliepukiki, hata k**a wewe ni mtakatifu vipi?.

Sasa biblia inatuambia, tunapokuwa katika mazingira k**a hayo, tusitie moyoni kila kitu tunachokisikia, au kwa namna nyingine tuvipuuzie, haijalishi tulichoambiwa kinachoma kiasi gani, hiyo ni kwa faida yetu wenyewe..

Lakini tatizo linakuja kwetu pale ambapo tunakisikia kidogo tu tumezungumziwa vibaya, na sisi hapo hapo tunaanza kutafuta, ni nani huyo kasema, ni nani kamwambia, na k**a hiyo haitoshi tunaendelea kutafiti na yule aliyemwambia ni nani kamweleza, na yule aliyeelezwa katolea wapi taarifa hizo, na kwanini wamefanya hivyo, hivyo tunaendelea, mpaka unazalika mlolongo mrefu ambao hauna mwisho.

Sasa ukisoma mstari wa 22 utaona unatupa madhara ya kufanya hivyo na kutuambia ikiwa mtu ataendelea kutafuta tafuta hivyo, kuchunguza chunguza hivyo.., kutafuta mchawi ni nani,.mwisho wa siku atashangaa kusikia mambo ambayo asingetazamia kusikia kutoka kwa watu wake ambao hawategemei kabisa.. Ukisoma hapo anatumia mfano wa “mtumwa”, mtu ambaye ni mjakazi wake anayekuheshimu atasikia anamtukana..

“21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana”.

Hivyo kabla hujaanza kuyafikiria mambo ya wanadamu, utakapoona habari fulani inakujia ya kusemwa vibaya, ikwepe, au ipuuzie kabisa kwa usalama wa moyo wako, kisha endelea na shughuli zako za kawaida, Watu wengi (hususani wakristo) wanaohangaika huku na huko kutafuta ni nani aliyewasengenya au Yule anazungumzia nini kuhusu mimi, mwisho wa siku wanakuwa na vinyongo na watu wote, wanakuwa na chuki zisizokuwa na sababu, wanapoteza hata imani na Mungu na kuanza kuishi maisha ya visasi, maisha ya kutokusamehe, na Maisha ya uchungu, hata maombi yao yanakuwa ni ya kuwalenga tu maadui zao, mawazo yao ni kukomoa tu, nipate hiki nimfundishe yule adabu n.k. kisa tu alimsikia Fulani akimcheka.. Na pia kamwe hawawezi kuwa na maombi ya unyenyekevu mbele za Mungu, bali ya kunung’unika tu na kulalamika.

Na kumbe hajui yule mtu aliyemsengenya pengine hata hakuwa na chuki na yeye kwa kiwango hicho anachokifikiri yeye, alizungumza tu k**a mwanadamu ambaye hawezi kuuzuia ulimi wake, na pengine alishatubu na akawa anamuombea, lakini yeye kwa kuwa alishasikia fulani alimzungumzia vibaya, hilo jambo ataendelea nalo moyoni mwake kwa miaka na miaka..Atasema kwanza yule nilishawahi kumsikia akinisema hivi au vile.

Hivyo kabla hatujamkasirikia fulani kwasababu ya kutuzungumzia vibaya, tunapaswa tujiulize je na sisi hapo nyuma hatujawahi kumsengenya mtu yeyote katika maisha yetu?. Kwasababu Ule mstari wa 22 unasema;

“21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.

22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine”.

Unaona? Imetumia neno “mara nyingi”. Pengine hata wewe ulishawahi kuzungumza maneno ambayo usingeweza kuyasema mbele ya huyo jirani yako, Lakini akija mbele yako humwekei vinyongo.

Hivyo na sisi pia tunapaswa tuachilie, tusiwe wapelelezi sana kwa yale tunayoyasikia kuhusu sisi, ukisikia mtu anakuambia fulani kakuzunguzia hivi au vile, usitake kujua zaidi ya hapo.. Kwasababu utajikuta una chuki na kila mtu, pengine hata mke wako, au dada yako, au mwanao, kwa sababu hiyo tu ya udadisi.

Tunapaswa tufahamu tu, kuzungumziwa vibaya au kusengenywa ni sehemu ya maisha yetu maadamu tupo hapa duniani. Hivyo hakuna haja ya kufuatilia fuatilia. Hiyo kazi tumwachie shetani, Sisi tutafute mambo msingi ya imani yetu. Na kamwe hutapata mtu mkamilifu asilimia mia moja hapa duniani, k**a unayemtaka wewe, tukilielewa hilo tutaishi Maisha ya upendo na furaha sana.

Bwana atusaidie katika hilo kwenye safari yetu ya wokovu.

Je! Umeokoka? Je! Unajua kuwa hizi ni nyakati za mwisho? Na kwamba hatutakuwa na muda mrefu sana Unyakuo utapita, na mwisho wa dunia utafika? umejiandaaje? Je! Bado upo vuguvugu? Ikiwa hujamkabidhi Yesu maisha yako ni heri ufanye hivyo sasa. Na wokovu unakuja kwa kutubu dhambi zako na kwa kubatizwa ipasavyo hivyo, zingatia hayo na uyakamilishe. Kwani hizi ni dakika za majeruhi. Bwana yupo mlangoni kurudi.

Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;Waefso 6:...
21/10/2023

Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;

Waefso 6:18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote
👇🏾
Yuda 1:20 Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu

Watu wengi wanaamini kuomba katika Roho ni kuomba kwa “kunena kwa lugha tu”. Nje ya hapo sio kuomba kwa Roho. Lakini tukiwa na mtazamo huo basi tutakuwa na uelewa finyu kuhusu Roho Mtakatifu.

Ukweli ni kwamba hiyo ni namna mojawapo kati ya nyingi ambazo Roho wa Mungu anamjalia mtu kuomba.

Maana ya ‘kuomba katika Roho’ Ni kuomba ‘ndani ya Roho ya Mtakatifu/ ndani ya utaratibu/ uwepo wa Roho Mtakatifu’. Na hiyo ni zaidi ya kunena kwa lugha, Hii ikiwa na maana Mtu anaweza kuomba lakini asiwe katika uwepo huo. Na matokeo ya hivyo ni maombi kuwa makavu sana, yasiyo na nguvu.

Sasa mstari mama unaotufundisha juu ya uombaji wa Roho Mtakatifu ni huu;

Warumi 8:26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA”

Hapo anasema “kuugua kusikoweza kutamkwa” . Maana ya kuugua hapo ni kuweka uzito, au presha, au shauku ya kuomba ndani ya mtu isiyokuwa ya kawaida. Tofauti na angejitahidi kwa nguvu zake yeye mwenyewe. Sasa mtu akifikia hatua hiyo, basi tayari kuanzia huo wakati anaomba katika Roho hata k**a maneno yake ni ya kawaida anayoyatumia. Maombi hayo yana nguvu na yanasikika sana mbele za Mungu.

Kwamfano, ndio hapo utakuta mtu anaomba, lakini mara anasikia kububujika machozi ndani yake, mwingine anazidi kuona kiu ya kuendelea kuombea jambo lile lile kwa muda mrefu tofauti na sikuzote. Mfano wakati ule Bwana Yesu alipokuwa Gethsamane anaomba.

mwingine anajisikia wepesi usio wa kawaida, uchovu wote umeondoka ijapokuwa alikuwa amechoka sana, anaanzafurahia maombi, anafurahia kuendelea kubaki palepale muda mwingi kuendelea kuomba,

Sasa hali k**a hizi ukizifikia, ujue tayari umeshazama katika Roho, umeshawezeshwa na Roho, maombi yako yanakuwa na nguvu sana,

Mwingine anasikia raha Fulani moyoni, akiwa anaomba, mwingine ndio anazama katika kunena kwa lugha (kwa kusukumwa na Roho), na sio kwa akili. Mwingine anasindikizwa na kuusikia uwepo wa Mungu umemfunika, nguvu za Mungu zinashuka mwilini mwake, anasikiswa, n.k. na unajikuta unafurahia sana maombi..

Kusudi la sisi kuomba sio kwenda kujitesa au kujiumiza, hapana bali ni mahusiano, tena ya k**a mtu anazungumza na Baba yake. Kiasi kwamba ukitoka kwenye maombi unaona umetoka kweli kuwasiliana na mtu, sio umetoka kuusemesha ukuta, usiokuwa na mrejesho wowote, umeomba hewani hewani tu

Sasa ni mapenzi ya Mungu kwamba sisi watoto wake kila tuombapo tuombe katika Roho Mtakatifu. Tuzame, tuyafurahie maombi yetu. Sasa tunawezaje kufikia hatua hiyo?

Kabla ya kuona namna ya kufikia hicho kilele. Tuone kwanza vikwazo vinavyomzuia mtu asiombe kwa Roho.

*VIKWAVYO VINAVYOPINGANA NA MTU KUOMBA KATIKA ROHO.*

1) Mwili
2) Shetani

Hawa ndio maadui wawili wakubwa wa mtu kuzama. Ndio maana wewe k**a mwombaji ni lazima uwafahamu, na ujue kabisa huna budi kushindana nao na ni lazima ukutane nao. Vinginevyo usipowatilia maanani kila siku maombi yako yatakuwa ni ya “kawaida sana” na kila utakapofikiria kitu kinachoitwa maombia utaona k**a vile unapelekwa gerezani.

Ndugu Mungu hajakusudia tujihisi hivyo sisi watoto wake tunapomkaribia yeye, tuwe k**a tunaliomba sanamu lisilonena, amekusudia kutupa mrejesho, na ndio hiyo zawadi ya Roho kuugua ndani yetu. Lazima atupe mrejesho wake kwamba yupo nasi.

Sasa uanzapo, hakikisha unaunyima mwili wako, raha zote, zinazokinzana na wewe kuomba. Kuwamfano, ukijiona mwili unasinzia au unapoa wakati wa kuomba usipende kukakaa kwenye kiti, ni heri upige magoti, ukishindwa tembea-tembea. Tena ni vizuri ukanyoosha na mikono yako juu, huku umefunika macho. Kisha anza kuomba.

Usiogope adhabu hizo za mwanzoni hazitadumu muda mrefu sana utaingia katika Roho, ni mwili tu unakuambia wacha, kunitesa, wewe ulazimishe tu, ukikuambia leo siku nzima umefanya kazi legea-legea, pinga hayo mawazo. Hivyo ukiwa Sasa katika hali hiyo. Anza kuomba lakini pia tumia ahadi za Mungu zilizopo kwenye biblia ni muhimu sana, kulingana na jambo unaloliombea, mkumbushe Bwana, ulisema hivi, na hivi kwenye Neno lako,, Ulisema ni nani aliye Baba, mtoto wake akimwomba mkate atampa jiwe, mkumbushe mwambie ulisema, k**a ungetazama dhambi zetu ni nani angesimama,..mwambie ulisema niite nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa na magumu usiyoyajua n.k..Tumia njia hiyo, kujimimina kwa Bwana

Omba huku umetilia ukamini (concentrate), mawazo yako ukiyalazimisha yasiende nje ya Mungu. Tengeneza picha halisi Mungu amesimama mbele yako kukusikia, fumba macho. Usiruhusu kufikia mambo ya nje, kwasababu akili yako itakuwa shapu kukutoa, ukitoka rudi, endelea kuomba. Ndio ni kipindi kifupi utataabika , lakini hatimaye utazama tu.. Sasa ukiendelea kudumu kwa kung’ang’ania huko kwenye maombi hayo kwa kipindi fulani. Hayo mazingira rafiki ya Roho Mtakatifu kuyaingilia maombi yako. Utashangaa tu, wepesi usio wa kawaida umezuka ndani yako. Tangu huo wakati endelea kuomba kwa jinsi usikiavyo rohoni, kwani hayo maneno unayoyaomba mengine hutaelewa unayatolea wapi, huyo ni Roho Mtakatifu anaomba na wewe.

Ndio maana akasema msifikiri-fikiri, kwasababu Roho mwenyewe atawajalia. Wengine kabla ya kuomba wanasema sijui nitaomba nini? Ndio hujui kwasababu bado hujazama, ukishazama utaweza tu kuomba kwasababu ni yeye ndio anayekujalia. Wengine wanasukumwa kunena kwa lugha n.k.

Adui wa pili ni shetani. Huyu anapaswa apingwe kwa kukemewa. Kabla ya kuanza maombi, hakikisha unayateka mazingira yako ya kimaombi. Ukimwomba Mungu, afukuze uwepo wote wa mapepo, hapo ulipo. Dalili ya shetani, ni pale unashangaa ukiwa unataka kuomba kichwa kinauma au tumbo, au hali Fulani isiyo ya kawaida inakuvaa katika mwili wako. Huyo ni shetani, mpinge kwa kukemea kisha endelea na maombi. Au mwingine anaona mazingira ya kusumbuliwa, mara kelele Fulani za nje, au simu zinaingia, ambazo si kawaida sikuzote kuwepo. Ndio maana ni vizuri katika kuomba kwako uzime simu. Ukae mbali na mazingira yenye mwingiliano, hiyo itakufanya umpe adui wakati mgumu kukusumbua.

Zingatia tu: Shetani haogopi sana maombi ilimradi maombi, anaogopa sana maombi yaliyo katika Roho, Hata k**a ni ya muda mfupi, hayapendi, na ndio atakayoyapiga vita sana. Hivyo usiwe mwepesi mwepesi kupenda kuomba juu juu.

Kwahiyo ukizingatia mambo hayo mawili kutakufanya uzame rohoni katika maombi yako yote. Na utayafurahia na utaona matokeo pia.

Bwana akubariki.

Je maombi ya mlimani yana ulazima wowote kwa mkristo?Swali: Je sisi watu wa agano jipya ni lazima kuwa na vipindi vya ku...
18/10/2023

Je maombi ya mlimani yana ulazima wowote kwa mkristo?

Swali: Je sisi watu wa agano jipya ni lazima kuwa na vipindi vya kuombea mlimani?. Na je huko mlimani Mungu ndioko anakosikia Zaidi maombi kuliko chini?.. msaada!

Jibu: Hakuna agizo lolote katika biblia la mahali rasmi pa kuombea!, k**a ni mlimani au k**a ni chini.. Lakini tunaweza kujifunza kupitia watu kadhaa katika biblia jinsi walivyoomba na kisha tunaweza kujifunza kitu.

BWANA YESU MWENYEWE.

Mathayo 14:22 “ Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng’ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano.

23 Naye alipokwisha kuwaaga makutano, ALIPANDA MLIMANI FARAGHANI, KWENDA KUOMBA. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake”.

Na pia…

Luka 6:12 “Ikawa siku zile aliondoka AKAENDA MLIMANI ILI KUOMBA, akakesha usiku kucha katika kumwomba Mungu”.

Soma pia Marko 6:46 na Yohana 6:15, utaona jambo hilo hilo la Bwana kupanda mlimani kuomba, na pia utaona sehemu nyingine alipanda na wanafunzi wake, soma Luka 9:28.

Umeona?.. K**a Bwana Yesu kuna nyakati alikuwa akienda mlimani kuomba, yeye pamoja na wanafunzi wake maana yake si bure!.. Kuna kitu cha ziada katika milima.

Na kitu hiko si kingine Zaidi ya UWEPO WA MUNGU. Milimani kunakuwa na Uwepo wa Mungu zaidi ya mabondeni?. Na kwanini milimani kunakuwa na Uwepo wa Mungu Zaidi ya sehemu nyingine nyingi?.

Ni kwasababu kule juu kunakuwa na utulivu,.. na siku zote utulivu unavuta uwepo wa Mungu, na milimani ni sehemu ambazo hazina usumbufu hivyo ni rahisi mtu kuzama katika roho kuliko akiwa chini penye masumbufu mengi na mwingiliano wa Sauti nyingi.

Umewahi kujiuliza ni kwanini minara ya simu huwa inapelekwa juu katika milima na haiwekwi mabondeni?.. Ni kwasababu kule juu network inapatikana vizuri Zaidi ya chini, kwasababu hakuna vizuizi vingi vya kuzuia mawimbi kusafiri. Sasa k**a wanadamu wameiona hiyo siri iliyopo juu ya milima, vipi kwetu sisi wakristo?

Si kwamba Mungu hatakusikia ukiomba mabondeni, atakausikia lakini ule uwepo wa Mungu kwako unaweza usiupate vizuri kuliko k**a ungeenda kuomba sehemu iliyoinuka (Milimani). Ndio maana utaona mtu anakuwa mzito kuomba, pasipo kujua chanzo ni nini?.. Wakati mwingine si mapepo!, bali ni mazingira tu!… Badili mazingira na utaona jinsi utakavyozama katika roho na maombi!.

Kwahiyo k**a wakristo ambao pia ni mwanafunzi wa biblia, ni lazima tuwe na vipindi vya kupanda mlimani kuomba!. K**a mahali ulipo hapana milima, basi linaweza lisiwe jambo la lazima sana, lakini k**a ipo basi tenga muda wa kufanya hivyo mara chache chache na utaona matokeo makubwa sana na vile vile utaona utofauti na utafungua mlango mpana sana wa kupokea mafunuo kutoka kwa Baba.

Bwana akubariki

Address

84
Longido
84LONGIDOARUSHA

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Neno La Mungu Ni Uzima posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share