Kyela Mjini SDA Church

Kyela Mjini SDA Church Karibu Katika Page Ya Kanisa La Waadventisa wa sabato Kyela Mjini, Southern Highlands Conference.

24/01/2026
SIKU 10 ZA MAOMBI-KUFUNGULIWAFUNGAMANA NA VIPAUMBELE VYA YESU “Iliwapasa wanafunzi kuendelea mbele na kazi yao kwa jina ...
08/01/2026

SIKU 10 ZA MAOMBI-KUFUNGULIWA

FUNGAMANA NA VIPAUMBELE VYA YESU

“Iliwapasa wanafunzi kuendelea mbele na kazi yao kwa jina la Yesu Kila neno na tendo lao lilitakiwa kuwavuta watu kwenda kwa Kristo, k**a jina lenye nguvu za kuweza kumwokoa mwenye dhambi. Imani yao ilitakiwa kujikita Kwake aliye chimbuko la rehema na uwezo.
Kupitia jina Lake wangepeleka maombi yao kwa Baba nao wangejibiwa. Walikuwa wanatakiwa kuwabatiza watu kwa jina la Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Jina la
Kristo ndiyo ingekuwa kauli mbiu yao, kitambulisho kinachowatofautisha na wengine, kifungo cha umoja wao, mamlaka ya kila tendo lao na chanzo cha mafanikio yao. Chochote kisingetambuliwa katika ufalme Wake kisichochukua jina na neno hili kuu.” (Matendo ya Mitume, Sehemu ya Kwanza, uk. 22)

SIKU 10 ZA MAOMBI – KUFUNGULIWAKaribu katika KUFUNGULIWA. Tunaishi katika nyakati ambazo zinaashiria kwa wazi kwamba Yes...
07/01/2026

SIKU 10 ZA MAOMBI – KUFUNGULIWA

Karibu katika KUFUNGULIWA. Tunaishi katika nyakati ambazo zinaashiria kwa wazi kwamba Yesu anakuja hivi karibuni. Ndiyo maana, katika Siku 10 za Maombi mwaka huu, tunalenga kwa makusudi “kumwalika Roho Mtakatifu abadilishe maisha yetu binafsi pamoja na ulimwengu tunaouishi”. Hii ni safari ya siku kumi ya kumtafuta Mungu kwa unyenyekevu, maombi ya kina, na uamsho unaoongozwa na Roho Mtakatifu.
Kabla ya Yesu kuondoka duniani, aliwaachia wafuasi Wake ahadi kubwa sana. Aliwaambia kuwa angemwomba Baba awape Msaidizi mwingine, Roho wa kweli, ambaye angekaa nao hata milele. Baadaye tena, kabla hajapaa mbinguni, Yesu aliwaagiza wanafunzi Wake wasitoke Yerusalemu bali waingojee Ahadi ya Baba, yaani ubatizo wa Roho Mtakatifu. Hii inaonesha wazi kuwa maisha ya ushuhuda na ushindi hayawezekani bila nguvu ya Roho Mtakatifu.
Hata hivyo, ni jambo la kusikitisha kwamba zawadi hii iliyoahidiwa kwa watu wa Mungu mara nyingi imebaki katika kiwango cha mazungumzo tu. Tunaisoma, tunaijadili, na tunaifahamu kinadharia, lakini mara nyingi hatufikii hatua ya kuifungua na kuishi ndani ya uhalisia wake. Matokeo yake ni ukame wa kiroho, udhaifu wa imani, na kukosa nguvu ya kweli katika maisha ya Kikristo.
Ni muhimu kutambua kwamba ni Roho Mtakatifu pekee anayeweza kuifanya upya mioyo yetu yenye dhambi na kutupatia moyo mpya. Ni Yeye pia anayebadilisha watoto wetu, kuwalinda, na kuwalea katika baraka za Mungu. Zaidi ya yote, ni Roho Mtakatifu anayethibitisha ndani ya mioyo yetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu na kutuunganisha na familia ya mbinguni. Habari njema ni kwamba Mungu yuko tayari kabisa kutupatia Roho Mtakatifu kwa wote wanaomwomba kwa dhati.
Ellen G. White anaonya kwamba pale ambapo hitaji la Roho Mtakatifu linapochukuliwa kuwa jambo dogo, hujitokeza ukame, giza la kiroho, kushuka kwa hali ya imani, na hatimaye kifo cha kiroho. Anauliza kwa masikitiko kwa nini watu wa Mungu hawana njaa na kiu ya karama hii, kwa nini hawaombi, hawazungumzii, wala hawahubiri kwa uzito juu ya Roho Mtakatifu, ilhali hii ndiyo njia pekee ya kupokea nguvu kutoka juu.
Biblia inatupatia mfano wa kusisimua katika 1 Samweli 14 kupitia kisa cha Yonathani na mbeba silaha wake. Wakati Mfalme Sauli alikuwa amekaa bila kuchukua hatua, Yonathani alichochewa na imani yake kwa Mungu akaamua kutoka katika eneo la usalama na kukabiliana na jeshi kubwa la Wafilisti. Wakiwa wawili tu, lakini wakiwa wamejitoa kikamilifu kwa Mungu, Bwana aliingilia kati na kuleta tetemeko la Mungu lililotetemesha kambi yote ya adui. Imani ya watu wawili ilimpa Mungu sababu ya kuitikisa ardhi.
Mungu bado anatenda kazi hata leo. Swali ni hili: ni nini kitakachompa Mungu sababu, kwa siku kumi mfululizo, kufanya ardhi itetemeke tena? Miaka elfu mbili iliyopita, waumini wapatao 120 walikusanyika katika chumba cha juu huko Yerusalemu, wakathubutu kuamini ahadi ya Yesu na kuingojea kwa uvumilivu. Roho Mtakatifu alipomiminwa siku ya Pentekoste, waliibadilisha dunia kwa ushuhuda wao, upendo wao, ujasiri wao, na kujitoa kwao.
Roho Mtakatifu anapenda kufanya kazi kutoka ndani kwenda nje. Ndiyo maana Siku 10 za Maombi si tukio la kawaida tu, bali ni mwaliko wa kuanza mtindo mpya wa maisha ya maombi, utii, na uamsho wa kweli. Mungu bado yuko tayari kumimina Roho Wake—kinachohitajika ni mioyo iliyo wazi na tayari kupokea

KARIBU SIKU 10 ZA MAOMBI YA KUFUNGULIWA

Karibu sana Kyela Mjini SDA Church, Leo Ibada ya Maombi ya Siku kumi inaanza, Njoo Tushiriki kwa Pamoja Mibaraka Hii, Ha...
07/01/2026

Karibu sana Kyela Mjini SDA Church, Leo Ibada ya Maombi ya Siku kumi inaanza, Njoo Tushiriki kwa Pamoja Mibaraka Hii, Hakika Tutafunguliwa

Kwaya ya Kanisa la Waadventista wa Sabato Kyela mjini wakihubiri kupitia nyimbo na wahudumu wapo tayar wazee wa kanisa n...
03/01/2026

Kwaya ya Kanisa la Waadventista wa Sabato Kyela mjini wakihubiri kupitia nyimbo na wahudumu wapo tayar wazee wa kanisa na mchungaji wa mtaa Pastor

KYELA MJINI SDA CHURCH
03/01/2026

KYELA MJINI SDA CHURCH

1. Tunamwomba Mungu Atuongoze Kupitia Roho Mtakatifu ili Kupata Viongozi 2025/20262. Uongozi Ndani Ya Kanisa ni Upendele...
06/11/2025

1. Tunamwomba Mungu Atuongoze Kupitia Roho Mtakatifu ili Kupata Viongozi 2025/2026
2. Uongozi Ndani Ya Kanisa ni Upendeleo, ni Fursa, ni Wito, kutoka kwa Mungu.
3. Tusikatae Kazi, Vipingamizi Vya Kukataa Kazi Ni pamoja na K**a Utakufa, Utahama, Utaoa/Kuolewa Nje Ya Kanisa Lako, Utakuwa Mgonjwa Mwaka Mzima, vingine Naona watu Ni visingizio.
4. Kuna Kazi Kiukweli zinahitaji Ujuzi na Taaluma, na sio Mala Zote Utachaguliwa Kimakosa
5. Usiseme Nimefanya Miaka Mingi,Nataka Nipumnzike, Ni heri Kubadilishiwa Kazi, Kuliko Kukataa Kabisa
6. Usiseme Mmenionaje, Mbona mimi mdhambi sana, Tambua Uongozi ni kuongoza watu wenye dhambi k**a Wewe, wote Tunaongozana.
7. Omba Mungu uwe Mmoja wa Baraka Hio
8. Kanisa Dogo linapaswa kuwa na Nafasi Za Uongozi 60 Ila kulingana na Makanisa Yetu, mtu mmoja anafanya Kazi 3/4/5 Hii hudhoofisha Utendaji Bora wa Kazi, Mwaka Huu Majukumu yakiwa Mengi ni 1 au 2 tu
9. Ukichaguliwa, omba Maelekezo ikiwa Hujui ili Ufanye Kazi Kwa Ufanisi, Maana kila Kazi ina Mwongozo wake
🙏 🙏 🙏 🙏

Endelea Kuombea Uchaguzi Mkuu SHC 2025, Mwezi December pamoja na Uchaguzi katika Mtaa wa Kyela na Kasumulu
26/10/2025

Endelea Kuombea Uchaguzi Mkuu SHC 2025, Mwezi December pamoja na Uchaguzi katika Mtaa wa Kyela na Kasumulu

08/10/2025

KESHA LA ASUBUHI 2025

JUMATANO, OKTOBA 8, 2025

KUSUDI KUU KABISA

Bali tukienenda nuruni, k**a yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote. — 1 Yohana 1:7.

Umoja ni nguvu na Bwana anataka kwamba ukweli huu upate kufunuliwa kwa washiriki wote wa mwili wa Kristo. Wote wanapaswa kuwa wamoja katika upendo, upole na katika unyenyekevu wa akili. Wakiwa wameunganishwa katika jamii ya waumini kwa ajili ya kusudi la kuunganisha na kueneza mvuto wao, wanalazimika kufanya kazi k**a Yesu alivyofanya. Wanapaswa daima kuonesha uungwana na heshima kwa kila mmoja. Kila talanta ina mahali pake na inapaswa kusalimishwa chini ya utawala wa Roho Mtakatifu.

Kanisa ni jamii ya Kikristo iliyoundwa kwa ajili ya washiriki wanaoliunda, ili kwamba kila mshiriki aweze kufurahia msaada wa neema na talanta zote za washiriki wengine na utendaji wa Mungu juu yao, kulingana na karama na vipawa vyao kadhaa. Kanisa linaunganishwa katika vifungo vitakatifu vya ushirikiano ili kwamba kila mshiriki aweze kufaidika kwa mvuto wa mwingine. Wote wanapaswa kujifungamanisha kwenye agano la upendo na mapatano. Kanuni za Kikristo na neema ya jamii yote ya waumini wanapaswa kukusanya nguvu na uwezo katika uwiano wa kazi. Kila muumini anapaswa kufaidika na kuimarishwa na mvuto uadilishao na ubadilishao wa vipawa tofauti vya washiriki wengine, ili kwamba yale yanayokosekana kwa mmoja yaweze kufunuliwa kwa upana kupitia kwa mwingine. Washiriki wote wanapaswa kuwa na umoja, ili kanisa liweze kuwa tamasha kwa ulimwengu, kwa malaika, na kwa wanadamu.

Agano la makubaliano katika ushirika wa kanisa ni ili kila mshiriki atembee katika nyayo za Yesu, ili wote wajitie nira Yake na wajifunze Kwake Yeye aliye mpole na mnyenyekevu wa moyo. Wakifanya hivi, anasema Mwokozi mpendwa, “Mtapata raha nafsini mwenu. kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi” (Mathayo 11:29, 30).

Wale waliojitia nira ya Yesu watavuta pamoja. Watakuza huruma na ustahimilivu na katika uigaji Mtakatifu watajitahidi kuwaonesha wengine wingi wa huruma na upendo ambao wao wenyewe wanauhitaji mno. Yeye ambaye ni dhaifu na asiye na uzoefu, ijapokuwa ni dhaifu, anaweza kuimarishwa na tumaini zaidi na wale walio na uzoefu mkubwa. Ajapokuwa mdogo kuliko wote, bado yeye ni jiwe ambalo lazima ling’ae jengoni. Yeye ni mshiriki wa muhimu mno katika mwili uliounganishwa, ameunganishwa kwa Yesu kiongozi aliye hai na kupitia kwa Kristo anatambuliwa pamoja na ukamilifu wote wa tabia ya Yesu kiasi kwamba Mwokozi haoni haya kumwita ndugu yake.... Kanisa, lililojitenga na kuwa tofauti na ulimwengu, katika tathmini ya mbinguni linahesabiwa kuwa kitu kikuu kuliko vyote duniani.... Kanisa linapaswa kuwa k**a vile Mungu alivyokuwa amepanga liwe, kiwakilishi cha familia ya Mungu katika ulimwengu mwingine (Selected Messages 3:15-17).

MUNGU ALIYE HAI NA AKUBARIKI

06/10/2025

Kazi imekamlika Tarazo tayari jina la Mungu Litukuzwe.

Tunamshukuru Mungu kwa Makambi ya Baraka!Tunapenda kutoa *shukrani za dhati* kwa wote mliojumuika nasi katika *Makambi y...
06/10/2025

Tunamshukuru Mungu kwa Makambi ya Baraka!

Tunapenda kutoa *shukrani za dhati* kwa wote mliojumuika nasi katika *Makambi ya Mtaa wa Kyela Mjini na Kasumulu*. Bila shaka lilikuwa ni *kambi la kipekee, la kufaana,* na lililojaa *uwepo wa Mungu.*

Kwa kweli, Mungu alitukuzwa na kuinuliwa kupitia huduma ya *Dr. & Pr. Lekundayo* pamoja na wanenaji wote walioshiriki. Kazi waliyoifanya ilikuwa ya kugusa mioyo na kuimarisha imani—*Mungu azidi kuwatumia zaidi!*

*Ni somo gani bado linagusa moyo wako hadi leo?*
Tuchangie kwenye comments — tujengeane kiroho na tukumbushane yale tuliyojifunza.

Asanteni kwa ushirikiano, maombi, na upendo mlioonesha.
*Tunaendelea mbele tukiwa na moto wa kiroho ukiwaka! 🔥*
* TUKIMTUMAINI YESU

Address

Kyela

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kyela Mjini SDA Church posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share