21/05/2026
SIKU YA ISHIRINI NA MOJA YA KUFUNGA NA KUOMBA.
Leo tunakumbushwa kuwa kuishi kwa haki na uaminifu hutuweka chini ya ulinzi wa Mungu. Katika dunia yenye maadili yaliyopotoka, Mungu anatafuta watu wa kweli katika maneno na matendo yao.
Chagua leo kuishi kwa haki na uaminifu, ili uendelee kufurahia ulinzi wa Mungu na kumpendeza kwa maisha yako ya kila siku.
Mithali 12:21-22 (SUV) “Mwenye haki hatapatikana na msiba wo wote; Bali wasio haki watajazwa mabaya. Midomo ya uongo ni chukizo kwa Bwana; Bali watendao uaminifu ndio furaha yake.”