Kondoa Catholic Diocese

Kondoa Catholic Diocese Official Page for Kondoa Catholic Diocese

SALA YA KUOMBEA MIITO. Ee Yesu, ulivumilia mateso makali mpaka kufa kwa ajili ya kutuokoa sisi binadamu. Tunakuomba utuj...
11/04/2026

SALA YA KUOMBEA MIITO.

Ee Yesu, ulivumilia mateso makali mpaka kufa kwa ajili ya kutuokoa sisi binadamu. Tunakuomba utujalie tupate Mapadre, Watawa wa kiume na k**e, Makatekista wengi walio Watakatifu.

Tunawahitaji sana katika Parokia yetu, Jimbo letu, nchini mwetu na katika Kanisa lote.

Uwajalie vijana wetu, wavulana na wasichana, neema ya kuitikia wito wako Mtakatifu. Uwape hamu ya kueneza neno lako.

Uwajalie pia neema ya kuwa wasikivu wakati wa malezi yao katika Seminari, katika nyumba za kitawa na mahali popote watakapoishi.
Hatimaye wafikie wito wao. Amina

Baba yetu...x1, Salama Maria...x1, Atukuzwe...x1

Kwa moyo uliojaa upendo na mshik**ano wa Kikristo, tunakuomba leo umkumbuke kwa namna ya pekee katika sala zako, ukimwom...
09/04/2026

Kwa moyo uliojaa upendo na mshik**ano wa Kikristo, tunakuomba leo umkumbuke kwa namna ya pekee katika sala zako, ukimwombea baraka nyingi na heri katika utume wake, Padre Zefrin Shakijuu. Paroko wa Parokia ya Yosefu Mfanyakazi, Lalta, Jimbo Katoliki Kondoa.

KWANINI TAREHE YA PASAKA HUBADIRIKA BADIRIKA? Kwanza kabisa, msingi wake unatoka katika uhusiano wa karibu kati ya Pasak...
06/04/2026

KWANINI TAREHE YA PASAKA HUBADIRIKA BADIRIKA?
Kwanza kabisa, msingi wake unatoka katika uhusiano wa karibu kati ya Pasaka ya Kikristo na Pasaka ya Wayahudi. Kwa mujibu wa Injili, Yesu Kristo aliteswa, akafa na kufufuka wakati wa kipindi cha Pasaka ya Wayahudi (rej. Mt 26:17–19; Yoh 19:14). Pasaka ya Wayahudi hufuata kalenda ya mwezi, si kalenda ya jua. Hivyo, tangu mwanzo Kanisa lilihifadhi uhusiano huu wa kihistoria na kibiblia kwa kuunganisha maadhimisho ya Pasaka na mzunguko wa mwezi. Hii ndiyo sababu ya kwanza na ya msingi inayofanya tarehe ibadilike.

Pili, Kanisa liliweka kanuni rasmi kupitia Mtaguso wa Nisea. Mtaguso huu uliamua kuwa Pasaka iadhimishwe Jumapili ya kwanza baada ya mwezi mpevu unaofuata tarehe 21 Machi (machipuko ya majira ya jua). Hapa kuna mambo matatu muhimu: lazima iwe Jumapili (siku ya ufufuko), lazima iwe baada ya mwezi mpevu (kuheshimu kalenda ya mwezi), na lazima iwe baada ya machipuko (kuweka mpangilio wa pamoja kwa Kanisa lote). Ndiyo maana Pasaka haisimami tarehe moja k**a Krismasi, bali huzunguka kati ya tarehe 22 Machi na 25 Aprili.

Tatu, sababu ya ndani kabisa ni ya kiteolojia: Pasaka si tu kumbukumbu ya tarehe, bali ni fumbo hai la wokovu. Kwa mujibu wa Sacrosanctum Concilium (n. 102–106), Pasaka ndiyo kitovu cha mwaka mzima wa liturujia. Vivyo hivyo, Katekisimu ya Kanisa Katoliki inaeleza kuwa fumbo la pasaka ndilo msingi wa imani ya Kikristo 1168–1171). Kwa hiyo, Kanisa lilichagua mfumo huu ili Pasaka ibaki imeunganishwa na historia ya wokovu, si tu kufungwa katika tarehe ya kalenda ya kawaida.
©️Vox Magazine

Jimbo Katoliki la Kondoa linawatakia waamini wote pamoja na watu wote wenye mapenzi mema Pasaka njema iliyojaa neema na ...
04/04/2026

Jimbo Katoliki la Kondoa linawatakia waamini wote pamoja na watu wote wenye mapenzi mema Pasaka njema iliyojaa neema na baraka tele. Katika fumbo hili kuu la Ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo, tuhuishwe mioyo yetu kwa mwanga wa imani, tuimarishe tumaini letu, na tuendelee kudumisha upendo wa kweli katika maisha yetu ya kila siku. Kwa kufuata mfano wa Kristo Mfufuka, tuwe mashuhuda wa amani, upendo na mshik**ano katika familia zetu na jamii nzima.

Heri njema ya Pasaka!

TANZIA
04/04/2026

TANZIA

JE WAKATOLIKI WANAABUDU MSALABA SIKU YA IJUMAA KUU? Hapana, Wakatoliki hawaabudu msalaba; wanauheshimu (wanauenzi) msala...
03/04/2026

JE WAKATOLIKI WANAABUDU MSALABA SIKU YA IJUMAA KUU?
Hapana, Wakatoliki hawaabudu msalaba; wanauheshimu (wanauenzi) msalaba k**a ishara ya wokovu. Ili kuelewa hili kwa kina, ni lazima kutofautisha kati ya kuabudu na kuheshimu, kwa mwanga wa mafundisho rasmi ya Kanisa.

Katika Ijumaa Kuu, Kanisa linafanya ibada maalum iitwayo Ibada ya Msalaba (Veneration of the Cross), si ibada ya Misa. Kwa mujibu wa Roman Missal, waamini wanakaribia msalaba na kuupigia magoti au kuubusu k**a ishara ya heshima (Roman Missal, Good Friday, Adoration of the Holy Cross). Neno linalotumika hapa si “adoration” kwa maana ya kumwabudu Mungu, bali “veneration”, yaani heshima ya kidini.
Kwa mujibu wa Katekisimu ya Kanisa Katoliki, ibada ya kweli (latria) inamstahili Mungu peke yake “Mungu peke yake ndiye anayeabudiwa” (2096–2097). Hii ina maana kuwa msalaba, sanamu, au picha yoyote haiwezi kuabudiwa k**a Mungu. Hata hivyo, Katekisimu inaendelea kufundisha kuwa picha na alama takatifu zinaheshimiwa kwa sababu zinatuongoza kwa Kristo:
“Heshima inayotolewa kwa picha inaelekezwa kwa anayewakilishwa” (2132).
Kwa hiyo, heshima inayotolewa kwa msalaba inaelekezwa kwa Yesu Kristo aliyekufa juu yake, si kwa mbao yenyewe. Aidha, mafundisho haya yana mizizi ya kale katika Kanisa, hasa katika Mtaguso wa Pili wa Nisea, ambao ulifafanua wazi tofauti kati ya ibada ya Mungu (latria) na heshima ya vitu vitakatifu (dulia). Mtaguso huu ulifundisha kuwa picha na alama takatifu, ikiwemo msalaba, zinaweza kuheshimiwa, lakini si kuabudiwa k**a Mungu.
Kwa upande wa liturujia, Paschalis Sollemnitatis inaeleza kuwa katika Ijumaa Kuu, Ibada ya Msalaba ni sehemu kuu ya maadhimisho, ambapo waamini wanaitwa kuutazama msalaba k**a ishara ya ushindi wa Kristo juu ya dhambi na kifo (PS, n. 68–71). Hivyo, tendo la kuubusu au kuupigia magoti si ibada ya kuabudu kitu, (kuheshimu) bali ni tamko la imani katika wokovu.
©️Vox Magazine

FAHAMU KUHUSU SIKU AMBAYO KANISA  KATOLIKI HALIADHIMISHI MISA TAKATIFUKatika maisha ya Kanisa Katoliki, Misa Takatifu nd...
03/04/2026

FAHAMU KUHUSU SIKU AMBAYO KANISA KATOLIKI HALIADHIMISHI MISA TAKATIFU
Katika maisha ya Kanisa Katoliki, Misa Takatifu ndiyo kitovu cha ibada na kilele cha maisha ya Kikristo. Kwa mujibu wa Katekisimu ya Kanisa Katoliki, Ekaristi ni “chemchemi na kilele cha maisha yote ya Kikristo” (1324). Hata hivyo, ndani ya mpangilio wa kina wa mwaka wa liturujia, kuna siku moja ya pekee ambayo Kanisa haliadhimishi Misa Takatifu: siku hiyo ni Ijumaa Kuu. Ukweli huu hauonyeshi upungufu wa Ekaristi, bali unaonyesha utajiri wa fumbo la wokovu ambalo Kanisa linataka kuishi kwa kina zaidi.

Kwa mujibu wa Roman Missal, badala ya Misa, Kanisa linaadhimisha ibada maalum iitwayo Liturujia ya Mateso ya Bwana (Celebration of the Passion of the Lord). Ibada hii ina sehemu kuu tatu: Liturujia ya Neno (ikiwa na simulizi la mateso ya Yesu Kristo), Ibada ya Msalaba, na Komunyo Takatifu kwa kutumia hostia zilizo takatifuzwa (Consecrated) siku ya Alhamisi Kuu (rej. Roman Missal, Good Friday). Hii inaonyesha kuwa hata bila Misa, Kanisa bado linaishi neema ya Ekaristi kwa namna ya pekee.

Sababu ya kwanza ya kutoadhimisha Misa siku ya Ijumaa Kuu na Jumamosi kuu ni ya kiteolojia. Kanisa linafundisha kuwa sadaka ya Kristo msalabani ni tukio la kipekee na kamili. Kwa mujibu wa Sacrosanctum Concilium, liturujia inaadhimisha fumbo la Pasaka mateso, kifo, na ufufuko wa Kristo kwa namna mbalimbali katika siku tofauti (SC, n. 5–6). Ijumaa Kuu ni siku ambayo Kanisa haliongezi “adhimisho la sadaka” kwa njia ya Misa, bali linaelekeza macho yake moja kwa moja kwenye sadaka halisi iliyotolewa na Yesu Kristo msalabani. Hapa Kanisa linaingia katika ukimya wa kushuhudia, si kufanya upya.

Sababu ya pili ni ya kiliturujia. Kwa mujibu wa Paschalis Sollemnitatis, siku ya Ijumaa Kuu inaadhimishwa kwa hali ya ukimya, huzuni, na unyenyekevu mkubwa (PS, n. 59–60). Alutare hubaki wazi bila mapambo, hakuna sala ya Ekaristi inayosomwa, na Kanisa linajikita katika Neno la Mungu na Ibada ya Msalaba. Hii ni lugha ya ishara: Kanisa linaonyesha kwa vitendo kuwa Mchungaji wake ametoa uhai wake kwa ajili ya watu wake.

Sababu ya tatu ni ya kiimani na kiroho. Kwa mujibu wa Katekisimu ya Kanisa Katoliki, sadaka ya msalaba na sadaka ya Ekaristi ni moja (1366–1367). Hivyo, kwa kutoadhimisha Misa siku hii, Kanisa halikatai Ekaristi bali linaonyesha chanzo chake yaani msalaba wa Kristo. Ni siku ambayo waamini wanaitwa kusimama chini ya msalaba, k**a Bikira Maria, wakitafakari upendo unaojitoa bila kipimo.

Katika mtazamo wa kina zaidi, kutokuwepo kwa Misa siku ya Ijumaa Kuu ni fundisho lenye nguvu ya kiroho. Ni k**a Kanisa linanyamaza ili Neno la msalaba lisik**e zaidi. Ukimya huu si tupu, bali umejaa maana ni ukimya wa upendo, wa sadaka, na wa matumaini.

Kwa hiyo, Ijumaa Kuu ni siku ya pekee ambapo Kanisa Katoliki haliadhimishi Misa Takatifu, kwa sababu linaingia moja kwa moja katika fumbo la sadaka ya Kristo msalabani. Ni siku ya ukimya unaozungumza, huzuni yenye tumaini, na imani inayotazama mbele kwa sababu baada ya msalaba, mwanga wa Pasaka hauwezi kuzuilika.
©️Vox Magazine

MKATOLIKI NA  MAADHIMISHO YA ALHAMISI KUU: EKARISTI TAKATIFU, DARAJA NA HUDUMAAlhamisi Kuu, Kanisa Katoliki linaingia ka...
02/04/2026

MKATOLIKI NA MAADHIMISHO YA ALHAMISI KUU: EKARISTI TAKATIFU, DARAJA NA HUDUMA
Alhamisi Kuu, Kanisa Katoliki linaingia katika fumbo la kina la upendo wa Mungu unaojifunua kwa njia ya sadaka, huduma, na uwepo wa kudumu. Hii ni siku ambayo Yesu Kristo aliweka msingi wa Sakramenti ya Ekaristi, akaanzisha Daraja Takatifu, na kutoa amri ya upendo kwa njia ya huduma ya unyenyekevu. Kwa hiyo, Alhamisi Kuu si kumbukumbu ya kihistoria tu, bali ni ufunuo hai wa imani ya Kanisa katika liturujia yake.

Kwa mujibu wa Roman Missal, Misa ya jioni ya Alhamisi Kuu (Mass of the Lord’s Supper) inaadhimisha kuanzishwa kwa Ekaristi Takatifu. Katika Karamu ya Mwisho, Kristo alichukua mkate na divai na kusema: “Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu” (Lk 22:19). Hapa ndipo Kanisa linapokea agizo la kuendeleza sadaka hii katika historia. Kwa mujibu wa Katekisimu ya Kanisa Katoliki, Ekaristi ni “chemchemi na kilele cha maisha yote ya Kikristo” (Katekisimu ya Kanisa Katoliki 1324), kwa sababu ndani yake Kristo mwenyewe anajitoa k**a chakula cha uzima wa milele.

Katika siku hii hiyo, Kanisa linaadhimisha pia kuanzishwa kwa Daraja Takatifu. Kwa maneno ya Kristo, “Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu,” aliwakabidhi Mitume wake mamlaka ya kuadhimisha Ekaristi. Hivyo, upadre haujitokezi k**a cheo cha kibinadamu, bali k**a zawadi ya huduma inayotokana na Kristo mwenyewe. Kwa mujibu wa Lumen Gentium, maaskofu na mapadre wanashiriki katika ukuhani wa Kristo kwa namna ya pekee ili kuongoza, kufundisha, na kutakatifuza watu wa Mungu (LG, n. 10–11). Hivyo, Alhamisi Kuu ni siku ya shukrani kwa zawadi ya ukuhani ndani ya Kanisa.

Aidha, ishara yenye nguvu sana katika liturujia ya siku hii ni tendo la kuosha miguu (Mandatum), linalotokana na Injili ya Yohane (Yoh 13:1–15). Yesu Kristo, Bwana na Mwalimu, aliinama na kuwaosha wanafunzi wake miguu, akitoa mfano wa huduma ya unyenyekevu. Kwa mujibu wa Sacrosanctum Concilium, liturujia hutufundisha kwa ishara zinazoonekana ili kuunda maisha ya waamini (SC, n. 33). Hivyo, tendo hili si maigizo bali ni mwaliko wa kweli kwa kila Mkristo kuishi upendo wa kujitoa kwa wengine.

Kwa upande wa tafakari ya imani, Alhamisi Kuu inatuingiza katika fumbo la upendo unaojitoa. Ekaristi Takatifu ni sadaka na chakula cha kiroho; Daraja Takatifu ni huduma na uwakilishi wa Kristo; na tendo la kuosha miguu ni agizo la kuishi upendo kwa vitendo. Haya yote yanaunganika katika ukweli mmoja: kwamba maisha ya Kikristo ni maisha ya kujitoa kwa Mungu na kwa jirani.

Kwa mujibu wa Ecclesia de Eucharistia, Kanisa linaishi kwa Ekaristi (n. 1), na bila Ekaristi, utambulisho wake hauwezi kueleweka kikamilifu. Hivyo, Alhamisi Kuu inakuwa siku ya kutafakari si tu juu ya ibada, bali juu ya utambulisho wa Kanisa lenyewe k**a jumuiya inayokula, kuabudu, na kuishi sadaka ya Kristo.

Kwa hiyo, kwa Mkristo Mkatoliki, maadhimisho ya Alhamisi Kuu ni mwaliko wa kuingia kwa kina katika imani, kuithamini liturujia, na kuishi huduma kwa vitendo. Ni siku ya kukumbuka kuwa tunaitwa kushiriki katika meza ya Bwana, kuongozwa na wachungaji waliowekwa wakfu, na kuonyesha upendo wa Kristo kwa unyenyekevu. Katika fumbo hili, Kanisa linaona chanzo cha maisha yake na nguvu ya utume wake, yote yakitoka kwa Yesu Kristo anayejitoa kwa ajili ya wokovu wa ulimwengu.
©️Vox Magazine

Heri ya kumbukizi ya siku mfanano ya  kuzaliwa kwako Mhashamu Baba Askofu  Bernadin Francis Mfumbusa, Askofu wa Jimbo ka...
01/04/2026

Heri ya kumbukizi ya siku mfanano ya kuzaliwa kwako Mhashamu Baba Askofu Bernadin Francis Mfumbusa, Askofu wa Jimbo katoliki la Kondoa.
Umefanyika baraka kwetu, nasi tuna kuombea heri katika maisha yako, Mwenyezi Mungu azidi kukujalia afya ya mwili na roho.
Wapendwa…..karibuni tumtakie heri na matashi mema Baba Askofu Bernadin Mfumbusa anapofanya Kumbukizi ya siku mfanano ya kuzaliwa kwake.

MAFUTA YA KRISMA HUTUMIKA WAPI KANISA KATOLIKI? Mafuta ya Chrisma (Sacred Chrism) ni kati ya mafuta matakatifu zaidi kat...
31/03/2026

MAFUTA YA KRISMA HUTUMIKA WAPI KANISA KATOLIKI?
Mafuta ya Chrisma (Sacred Chrism) ni kati ya mafuta matakatifu zaidi katika Kanisa Katoliki, yakibarikiwa na Askofu wakati wa Misa ya Krisma. Mafuta haya yanachanganywa na manukato (balm) na hutumika kuashiria utakatifu, kuwekwa wakfu, na kupokea Roho Mtakatifu. Matumizi yake yameelezwa wazi katika mafundisho ya Kanisa, hasa katika Katekisimu ya Kanisa Katoliki (rej. Katekisimu ya Kanisa Katoliki 1241, 1289, 1294).

Kwanza, mafuta ya Chrisma hutumika katika sakramenti ya Ubatizo. Baada ya kubatizwa, mtu hupakwa mafuta kifuani k**a ishara ya kushiriki katika ukuhani wa Kristo, utume wake wa kinabii, na ufalme wake (rej. Katekisimu ya Kanisa Katoliki1241). Hii inaonyesha kuwa Mkristo mpya amewekwa wakfu kwa Mungu na ameanza maisha mapya ndani ya Kristo.

Pili, hutumika katika sakramenti ya Kipaimara. Hapa ndipo matumizi yake yanaonekana kwa uzito zaidi, kwa sababu anayepokea kipaimara hupakwa mafuta ya Chrisma kwenye paji la uso. Mafuta haya yanakuwa ishara ya Roho Mtakatifu na kuimarishwa kwa imani (rej. Katekisimu ya Kanisa Katoliki 1289–1294). Ndiyo maana sakramenti hii huitwa pia sakramenti ya kukomaza imani.

Tatu, mafuta ya Chrisma hutumika katika sakramenti ya Daraja Takatifu (Upadre na Uaskofu). Katika kuwekwa wakfu kwa padre, mikono yake hupakwa mafuta haya, na katika kuwekwa wakfu kwa askofu, kichwa chake (utosini) hupakwa mafuta ya Chrisma. Hii inaonyesha kuwa wamewekwa wakfu kikamilifu kwa huduma ya Mungu na Kanisa (rej. Pontificale Romanum).

Nne, hutumika katika kuweka wakfu vitu vitakatifu, hasa madhabahu (altare) na kanisa jipya. Wakati wa kuwekwa wakfu, madhabahu hupakwa mafuta ya Chrisma k**a ishara kuwa imewekwa wakfu kabisa kwa ibada ya Mungu (rej. Pontificale Romanum, Rite of Dedication of a Church and an Altar). Hii inaonyesha kuwa si watu tu wanaowekwa wakfu, bali hata mahali pa ibada.
©️Vox Magazine

Kwa namna ya pekee mpendwa leo unaalikwa kumtakia neno la baraka na matashi mema katika Utume wake Padre Lucas Racha, Pa...
31/03/2026

Kwa namna ya pekee mpendwa leo unaalikwa kumtakia neno la baraka na matashi mema katika Utume wake Padre Lucas Racha, Paroko wa Parokia ya Kristo Mfalme - Huruvi, Jimbo Katoliki Kondoa.

DOMINIKA YA MATAWI ILIANZAJE KANISA KATOLIKI ?Historia ya Dominika ya Matawi katika Kanisa Katoliki ina asili yake moja ...
28/03/2026

DOMINIKA YA MATAWI ILIANZAJE KANISA KATOLIKI ?
Historia ya Dominika ya Matawi katika Kanisa Katoliki ina asili yake moja kwa moja katika Injili na imejengwa kwa kina kupitia mapokeo hai ya liturujia ya Kanisa. Siku hii inaadhimisha tukio la Yesu Kristo kuingia Yerusalemu kwa ushindi, akipokelewa na umati uliotandaza matawi na kupaza sauti za “Hosana” (rej. Mt 21:1–11; Mk 11:1–10; Lk 19:28–40; Yoh 12:12–16). Tukio hili lina maana ya kifalme na ya kinabii: Kristo anaingia k**a Mfalme mnyenyekevu, lakini pia anaelekea kwa hiari katika mateso yake. Ndiyo maana Kanisa linaunganisha tukio hili na mwanzo wa safari ya mateso yake.

Kwa mujibu wa Roman Missal, siku hii inaitwa rasmi Dominika ya Matawi ya Mateso ya Bwana (Palm Sunday of the Passion of the Lord). Ndani ya Misa yake kuna muundo wa kipekee unaounganisha mambo mawili: kwanza, ibada ya kubariki matawi na maandamano ya waamini; pili, usomaji wa simulizi la mateso ya Kristo (Passion). Muundo huu unaonyesha kwa uwazi teolojia ya siku hiyo, furaha ya mapokezi ya Kristo haiwezi kutenganishwa na ukweli wa msalaba wake (rej. Roman Missal, Palm Sunday).

Kihistoria, ushuhuda wa kale unaonyesha kuwa maadhimisho ya Dominika ya Matawi yalianza mapema sana katika Kanisa, hasa Yerusalemu. Mhujaji maarufu aitwaye Egeria katika karne ya 4 anaeleza jinsi Wakristo walivyofanya maandamano wakibeba matawi wakikumbuka kuingia kwa Yesu (rej. Itinerarium Egeriae, c. 381–384). Kutoka hapo, desturi hii ilisambaa hadi katika Kanisa la Magharibi na hatimaye kuwa sehemu rasmi ya liturujia ya Kanisa lote. Hivyo, si tu kumbukumbu ya tukio la Biblia, bali pia ni mapokeo hai ya ibada yanayoendelezwa kizazi hadi kizazi.

Kiteolojia, siku hii inaeleweka ndani ya fumbo la Pasaka. Kwa mujibu wa Sacrosanctum Concilium, Kanisa linaadhimisha kazi ya wokovu wa Kristo hasa katika fumbo lake la Pasaka, yaani mateso, kifo, na ufufuko (rej. SC, n. 5–6). Dominika ya Matawi ndiyo lango la kuingia katika fumbo hili. Ndiyo maana Injili ya mateso husomwa siku hiyo: ili kuonyesha kuwa yule anayeshangiliwa leo k**a Mfalme ndiye atakayesulubiwa kwa ajili ya wokovu wa wanadamu.

Aidha, Paschalis Sollemnitatis inaeleza wazi kuwa Dominika ya Matawi inaunganisha ushindi na mateso ya Kristo katika tendo moja la ibada (rej. PS, n. 28–30). Waamini wanapobeba matawi, wanaungana na umati wa Yerusalemu; lakini wanaposikiliza mateso, wanaalikwa kuingia katika ukweli wa sadaka ya Kristo. Hii ndiyo nguvu ya liturujia: kuifanya historia ya wokovu kuwa tukio hai katika maisha ya waamini.

Kwa hiyo, Dominika ya Matawi si sherehe ya furaha tu bali ni fumbo lenye pande mbili, ushindi na mateso. Ni mwanzo wa Wiki Takatifu, safari ya kiroho inayoanza kwa matawi ya ushindi na kuelekea msalaba, na hatimaye kufikia utukufu wa ufufuko. Kupitia maadhimisho haya, Kanisa linafundisha kuwa njia ya kweli ya ushindi wa Kikristo inapitia katika sadaka na upendo wa msalaba, k**a alivyoonesha Yesu Kristo mwenyewe.
©️Vox Magazine

Address

Kondoa Dodoma
Kondoa

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kondoa Catholic Diocese posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Kondoa Catholic Diocese:

Share