Ukwata Darpwani

Ukwata Darpwani This is a religious organization which involves Christian students in Secondary Schools and colleges within TSCF found in Dar-es-salaam and Pwani regions.

*ALINIFUATA ATUBU,JAMBO AMBALO AMEKAA NALO NA LINAMHUKUMU SANA*Aliingia kwenye mahusiano na mume wa mtu mwenye mke na wa...
23/10/2024

*ALINIFUATA ATUBU,JAMBO AMBALO AMEKAA NALO NA LINAMHUKUMU SANA*

Aliingia kwenye mahusiano na mume wa mtu mwenye mke na watoto watatu.

Na huyo dada hakuwa tayari kuendelea kuwa mchepuko ila aliiwinda sana nafsi ya kuwa mke halali wa ndoa bila kujali afya ya ndoa ya mwanamke mwenziwe.

Na alizidi kumsumbua jamaa ili amhalalishe,jamaa shida ikawa kwamba ana ndoa tena halali kabisa na watoto..kwa hiyo ilikuwa ni ngumu otherwise waendelee kuwa na mahusiano ya siri. Mahusiano yakaendelea na walipendana mno! Kuna wakati ulifika hadi mwanaume akaanza kutamani wangeishi k**a mume na mke lakini atamwachaje wa ndani?

Mwanamke alikuwa ni mwenye akili nyingi sana. Alichofanya ni kuforce ndoa..ilibidi amshawishi amwache afanye mchezo ambao utatoa uhalali wa yeye kuachana na mke wake. Jamaa akatoa idhini.....

Dada akampanga mtu na kumlipa pesa iwapo k**a angefanikisha jambo lao...iko hivi;

Akamtuma ajenge ukaribu na mwanamke wa huyo brother awe anaenda ofisini kwake k**a kumuungisha vitu kwenye biashara yake.
(Huyo mwanamke alikuwa na duka na anauza vitu online)

Huyo jamaa akaipata namba ya huyo mwanamke akaanza kuagiza vitu,analetewa,siku zingine anafuata mwenyewe,wakawa wanachati,kwa kifupi wakazoeana,huku mwanamke asijue huyo mtu katumwa kuharibu ndoa yake....siku zingine akinunua kitu cha elfu 30 anaongeza 30 nyengine...wakati mwingine anamtumia hadi Elfu 50 k**a hela ya soda. K2a kifupi wakazoeana.

Basi kuna siku akamtongoza na kumwambia anampenda....haikuwa rahisi kwa mwanamke lakini kuna siku alinasa,akiangalia wameshazoeana na jamaa anamjali sana. Akamkubalia wakapanga waonane lodge fulani hapa hapa Dar es Salaam.

Siku waliyopanga kukutana,yule jamaa akamwambia aliyemtuma kwamba tayari kakubaliwa na wanaonana mahali fulani...akamtumia screenshorts zote

Na yule dada akaziforward kwa mwanamme wake.

Wakajipanga Mumewe aende akafanye fumanizi hiyo lodge,huku wakimpanga yule jamaa kule chumbani asibane mlango na wakiwa watupu ndio awaruhisu. Na kweli mume akapewa ishara aingie....huyo mchepuko akiwa ni k**a mwandishi akichukua matukio yote.

Jamaa akafanikiwa kumfuma mkewe akiwa wazi japo hawakuanza kitendo chochote...cha kwanza ni kuchukua nguo zote za mkewe na kushika mkononi na kumpiga picha...kisha akampigapiga mkewe na kumwambia nipe kwa hiari yako pete niliyokuvisha na kwamba amevunja agano la ndoa. Na akamwambia arudi nyumbani moja kwa moja akamtisha aondoke aende kwao nyumbani na kila kitu chake,halafu aandike talaka ama sivyo atazirusha picha zote mtandaoni na kuwaonyesha wazazi wake.

Mama akaandika talaka kwa hofu huku akimwomba mumewe misamaha akakataliwa na akaondoka jumla na kurudi kwao. Duka akaliacha nyumba akaiacha akaondoka na mtoto mdogo...wengine walikuwa shule za boarding.

Baada ya huo mchezo jamaa akaoa haraka wakaanza kuishi kwenye nyumba ile ile,mapenzi motomoto, wakakaa k**a miaka miwili na kitu fulani...mume akaanza kuungua ugonjwa usiojulikana,akawa anadhoofu tu...hangaika wee,tibu hiki na kile wapi.

Akaja kuporomoka kiuchumi kiasi cha kuuza nyumba na mali nyingi sana...akaendelea kudhoofu na akafa mwaka huu mwezi wa pili. Nasikitika kuwa hakupata neema ya kutubu.

Mwanamke aliachwa nyumba ya kupanga madeni yakawa mengi,na aliachwa na mtoto mmoja,akaanza kuugua pia. Nilikutana nae akiwa hospitali amekatwa ziwa la kulia kwasababu ya kansa. Yupo kwenye matibabu kichwani hana unyewele hata mmoja ndipo akakumbuka juu ya uovu walipmfanyia yule mama. Nikatafutwa nimwombee na kumkutanisha na yule mama na hajui kwa kumpata....Maana hana mawasiliano nae wala kufahamu aliko ni wapi.

Nikiwa namwombea niliambiwa kitu kigumu sana na cha kukatisha tamaa,nikaambiwa usiombe....mimi sikuacha kuonba rehema za Mungu juu yake nikimkumbusha rehema zake kwa mtumishi wake Daudi na wazawa wake.

Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna. Apandaye katika tamaa za kidunia, atavuna humo uharibifu;Wagalatia 6:7-8

Mimi nadhani inawezekana ukajenga mahusiano na mtu bila kumharibia mwingine...Hawa waitwao wakristu hawa,ni wabaya sana wanapotaka kufosi mahusiano yasiyokuwa yao...wanawake wa kiislamu akifuatwa na mume wa mtu akamtaka amwoe,yeye ndio anamshauri huyo mume akaongee kwanza na mke wake ikiwa ataridhia ili kutunza amani.

Ila hawa wa kwetu wapo tayari hata kuomba mke afe ili yeye ajimilikishe.

Inawezekana ukajenga familia yako bora bila kutoa machozi wengine...Mungu anaitwa mhukumu wa haki,mambo yanayofanywa na wanadamu mipango yao yote ya sirini anafuatilia ili ahukumu kwa haki.

By Kuhani Atson Mwansepe

25/10/2020

Bwana Yesu asifiwe.

Mliomaliza kidato cha sita msikose hii semina. HAKUNA KIINGILIO.
20/05/2018

Mliomaliza kidato cha sita msikose hii semina. HAKUNA KIINGILIO.

21/12/2016

Maandalizi ya Kongamano la Pasaka mwaka 2017 yameanza, Fomu zimekwishatolewa wilayani na matawini.Hakikisha unapata fomu ya kongamano.
Mungu awabariki.

16/09/2016

Wapendwa naomba kuwafahamisha kuwa Tar 24-25/9, yaani week ijayo kutakuwa na jointmass itakayofanyika Morogoro kanisa kuu la Anglican na kila mshiriki atatakiwa kuchangia sh 20,000 ikiwa ni gharama ya nauli na chakula. Nawaomba sana tuwahamasishe WanaUKWATA wetu kuhudhuria Jointmass hiyo. Tutaondoka Jmosi asbh sana na kurudi Jpili asbh baada ya ibada ya kwanza

Karibu Kamati Kuu UKWATA DARPWANI 2016/2017. Mungu awasimamie.
01/04/2016

Karibu Kamati Kuu UKWATA DARPWANI 2016/2017. Mungu awasimamie.

Hongera Kamati Kuu UKWATA DARPWANI mwaka 2015/2016 kwa kazi nzuri, Hakika Mungu awabariki.
01/04/2016

Hongera Kamati Kuu UKWATA DARPWANI mwaka 2015/2016 kwa kazi nzuri, Hakika Mungu awabariki.

http://ukwatadarpwani.or.tz/
28/03/2016

http://ukwatadarpwani.or.tz/

Ushirika wa Kikristo wa wanafunzi Tanzania (UKWATA) ni mojawapo ya idara zilizo chini ya Jumuiya ya Kikristo Tanzania au Christian Council of Tanzania (CCT). Ukwata DarPwani ni mojawapo ya Mikoa ya Ukwata kitaifa, ambao unajumuisha mikoa miwili ya Dar es salaam na mkoa wa Pwani.

17/03/2016

Shalom mpendwa.. Kambi ya maombi ya kuombea Easter conference itakuwa kuanzia tar 23 NIA NJEMA High School [Bagamoyo], tutakutana na kuondoka tar 23/03/2016 Jumatano. KKKT Mbezi beach saa 8 mchana. Endapo k**a utakuwa hujalipiwa na Wilaya au tawi fika na shilingi elfu tano (5000) kwaajili ya nauli na chakula kwa siku hiyo. Waratibu wote na wanamaombi mnatakiwa kufika. barikiwa. (By Mratibu maombi) DAR~PWANI)

15/03/2016

Shalom! Ndugu kiongozi wa UKWATA, Napenda kukumbusha/ kukutaarifu kuhudhuria kikao cha halmashauri cha mwisho cha maandalizi ya Easter conference. Kikao kitafanyika siku ya jmosi tar 19/03 kuanzia saa 3 asbh scripture union, karibu na hospitali ya Muhimbili. Tafadhali fika na michango yote ya Easter uliokusanya pamoja na asilimia 25 k**a unadaiwa. Natumaini utazingatia muda na Mungu akubariki. KATIBU UKWATA MKOA

13/03/2016

Fahari ya Vijana ni Nguvu zao.(Mithali 20:29a)
Tarehe 24/03/2016, tukutane Nianjema High School - Bagamoyo.

07/02/2016

Bwana Yesu asifiwe wapendwa.

YAH: MAMBO YA KUZINGATIA KWENYE KONGAMANO LA PASAKA 2016:

1.Neno Kuu; MITHALI 20:29a "Fahari ya Vijana ni Nguvu zao....".

2.Kitabu cha Mashindano ya Biblia; ESTA sura zote.

3.Wimbo Mkuu; TENZI NAMBA 81 "Chini ya Msalaba".

4.Eneo la Mkutano; Kongamano la Pasaka la DARPWANI litafanyika NIA NJEMA SECONDARY SCHOOL, iliyopo Bagamoyo.

5.Tarehe ya Kongamano; Kuanzia Alhamisi ya tarehe 24 mpaka Jumatatu ya Pasaka tarehe 28 Machi 2016. (24-28/03/2016).

6.Deadline; Mwisho wa kurudisha michango na fomu umesogezwa mbele mpaka Jumamosi ya tarehe 27/02/2016.(Tafadhali zingatia muda uliopangwa ili kuwezesha maandalizi ya Kongamano).

NB;
UKWATA Mkoa wa DARPWANI unaendelea kuhimiza matawi,wilaya, vikundi au miunganiko(Clusters) kujiandaa vyema katika kushiriki mashindano ya Biblia, Uimbaji, Ngonjera na Mashairi.

Mwisho;
UKWATA Mkoa unawatakia maandalizi mema ya Kongamano.
Fahari ya Vijana ni Nguvu zao (Mithali 20:29a.)
Mungu awabariki.

Address

Kinondoni

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ukwata Darpwani posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Ukwata Darpwani:

Share