10/12/2025
Mtu yeyote anayeenda mbali na maisha yake au hatima yake, yuko makini sana na nini afanye na nini asifanye.
Moja ya sababu kubwa na ya msingi kwanini Yusuph alimkimbia mke wa Potifa alijua lile ni kosa lenye uwezo wa kumkosanisha na Mungu na kutia dosari mchakato wa kufikia Hatima yake.
K**a unatambua unataka kwenda mbali Ogopa sana kundi la watu wasio jali makosa na hatua zao za kila siku. Adui wa hatima ni mwerevu na anatunza kumbukumbu.. hakuna kosa dogo lisilo na madhara k**a halijarekebishwa kwa kufuata utaratibu. Mchakato wa hatima hauchakachuliwi.
Epuka kufanya makosa yasiyo ya lazima, Ishi maisha yenye utaratibu, lipa gharama inayotakiwa ya kurekenisha kila unapokosea… Usichakachue mchakato wa safari yako… EPUKA SANA WATU WASIO JALI NA WASIO NA UTARATIBU. EPUKA SANA MTU ASIYETAMBUA MAMLAKA YOYOTE NA ANANAYEFANYA KILA KITU NAMNA ANAVYOTAKA. Watu wa namna hyo hawana mchnago wowote kwenye hatima yako.
Mungu akusaidie hekima ya kupita njia ya hatima na akuepushe na makosa yaliyotegwa na Shetani kukuangamiza.
Math 6:13
Usitutie majaribuni, bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu [kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amen