Nyumbayamungu

Nyumbayamungu kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote.

OLDUPAI (OLDUVAI) GORGE NDO PALIKUA SODOMA NA GOMORA?Ushahidi wa kuwa Olduvai Gorge au Oldupai ndo Sodoma na Gomora iliy...
26/02/2026

OLDUPAI (OLDUVAI) GORGE NDO PALIKUA SODOMA NA GOMORA?

Ushahidi wa kuwa Olduvai Gorge au Oldupai ndo Sodoma na Gomora iliyoteketezwa na moto enzi hizo. na nyayo za miguu ya Laitoli ni ushahidi wa Lutu na Familia yake walipokua wakiondoka baada ya miamba kuyeyushwa na Moto.

kwanini ndiyo Sodoma na Gomora?
tuanze na Maandiko

✍🏾BIBLIA INASEMAJE ?

BIBLIA INASEMA NI MJI ULIOKUWA BONDENI NA OLDUVAI NI BONDENI

Mwanzo 19:28 SUV
📖naye akatazama upande wa Sodoma na Gomora na nchi yote ya hilo Bonde, akaona, na tazama, moshi wa nchi ukapanda, k**a moshi wa tanuru.

*******************************
✍🏾Biblia inasema ni Mji unaofanana na Mji uliopo Misri unaoitwa Soari na ukicheki kweli Bonde la Olduvai ndo Bonde pekee lililopo Duniani linalofanana na Soari

Soari kuna Mitende na pia ugunduzi wa mabaki unaonesha pia Olduvai pana mabaki ya Mitende.

✍🏾IMEANDIKWA
Mwa 13:10 SUV
📖Lutu akainua macho yake, akaliona Bonde lote la Yordani, ya kwamba lote pia lina maji, kabla BWANA hajaharibu Sodoma na Gomora, lilikuwa k**a bustani ya BWANA, k**a nchi ya Misri hapo unapokwenda Soari.
*******************************
👉🏽unaambiwa Kabla ya Sodoma na Gomora kuharibiwa palikua k**a Bustani ya Bwana na palikua na maji , mabaki ya mitende ni ushahidi kuwa palikua na maji maana mitende huota penye maji tu. na Ngorongoro na wanyama ni sehemu iliyobaki pekee Duniani ambapo ndo panafanana na Bustani ya Bwana k**a inavyoelezewa kwenye maandiko Matakatifu kuwa kwenye Bustani ya Bwana wanyama wanaishi na Binadamu.

✍🏾🏛IMEANDIKWA Sodoma na Gomora ulikua ni Mji
Mwanzo 19:4 SUV
📖Hata kabla hawajalala, watu wa mji, wenyeji wa Sodoma, wakaizunguka nyumba, vijana kwa wazee, watu wote waliotoka pande zote.

🤯Ugunduzi wa Kisayansi na wa mambo ya kale unasema Olduvai ilikua ni Mji mkubwa sana na mabaki yapo yanathinitisha hilo hadi leo tena mengine yaliunguzwa na ule Moto

✍🏾Imeandikwa
Mwa 19:24 SUV
📖Ndipo BWANA akanyesha juu ya Sodoma na juu ya Gomora kiberiti na moto toka mbinguni kwa BWANA.
*******************************
🤯Ugunduzi Wa Kisayansi unasemaje ?
Kuhusu 🔥MOTO?

🦶🏼ukienda Oldupai Gorge utakuta kuwa kweli kuna miamba ina moshi na iliunguzwa kwa moto .Wanasayansi na wataalam wa mambo ya kale wanasema paliungua kiasili (Naturally) na k**a ni naturally inamaanisha hakuna mtu aliyeuwasha Moto huo yani Mungu ndo alipaunguza. Fikiria vizuri hapo.

✍🏾Biblia inasema Mke wa Lutu aligeuka Jiwe la Chumvi na ugunduzi unaonesha kuwa Olduvai pana asili ya Chumvi hadi leo.

💀Kingine kikubwa ni Fuvu la mtu wa kale lililogunduliwa hapo Limeungua hii inaonesha wazi kuwa Ni miongoni mwa watu waliounguzwa na Moto wakati ule.

MBALI NA HILO TUNAJUA SODOMA NA GOMORA VIPO KARIBU NA KAANANI NA KAANAN WAPO WANA ISRAEL NA SIFA YA WANAISRAEL NI KUTAHIRIWA

wakazi wanaozunguka Olduvai (Kaanan) ambao ni wamasai /Watanzania Tumetahiriwa k**a Vile Mwenyezi Mungu alivyoagiza

✍🏾Imeandikwa

AGANO LA WANAISRAEL KUTAHIRIWA.

Mpaka sasa Watanzania na waafrika wengine Waisrael tunatahiriwa na ni moja ya ushahidi wa wana Israel .
Mababu zetu wamekua wakitahiriwa tokea enzi za Ibrahim kwa maana babu yetu Ibrahim aliweka agano hilo na Mwenyezi Mungu.

✍🏾Imeandikwa

Mwa 17:10‭-‬11 SUV
📖Hili ndilo agano langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, Kila mwanamume wa kwenu atatahiriwa. Mtatahiriwa nyama ya magovi yenu, na jambo hilo litakuwa ishara ya agano kati ya mimi na ninyi.

TUPO NCHI AMBAYO WANYAMA WANAISHI NA BINADAMU JE? BIBLIA INASEMAJE KUHUSU WANYAMA KUUSHI NA WATU? NA NINI KINATOKEA SASA?

✍🏾IMEANDIKWA

Isaya 11:1-10 SUV
📖Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda. Na roho ya BWANA atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha BWANA; na furaha yake itakuwa katika kumcha BWANA; wala hatahukumu kwa kuyafuata ayaonayo kwa macho yake, wala hataonya kwa kuyafuata ayasikiayo kwa masikio yake; bali kwa haki atawahukumu maskini, naye atawaonya wanyenyekevu wa dunia kwa adili; naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, na kwa pumzi ya midomo yake atawaua wabaya. Na haki itakuwa mshipi wa viuno vyake, na uaminifu mshipi wa kujifungia. Mbwa-mwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwana-simba na kinono watakuwa pamoja, na mtoto mdogo atawaongoza. Ng’ombe na dubu watalisha pamoja; watoto wao watalala pamoja; na simba atakula majani k**a ng’ombe. Na mtoto anyonyaye atacheza penye tundu la nyoka, na mtoto aliyeachishwa atatia mkono wake katika pango la fira. Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; maana dunia itajawa na kumjua BWANA, k**a vile maji yanavyoifunika bahari. Na itakuwa katika siku hiyo, shina la Yese lisimamalo kuwa ishara kwa kabila za watu, yeye ndiye ambaye mataifa watamtafuta; na mahali pake pa kupumzikia patakuwa na utukufu.

*********************************
🤔Je unafikiri huyo chipukizi K*toka Nyumba ya Yese ni Yesu ?

HITIMISHO
🙌🏽Sijawahi Kufika Olduvai Gorge ila haya ni mambo ambayo kuna Sauti ipo ndani yangu hunionesha na kunisemesha . Nitaendelea kuwaandikia kwa kadri nitakavyojaaliwa.

ILI USIPITWE,
follow
Mrkilimanjaro Nyumbayamungu

Amani ya Mwenyezi Mungu ikae nanyi Nyote

by Mwal: Imanueli Minja

POMBE NI KWA AJILI YA MASKINI WENYE SHIDA NA WANAOKARIBIA KUDATA.MITHALI 31:4‭-‬7 SUV📖"Ee Lemueli, 👉🏾kunywa mvinyo hakuw...
08/05/2022

POMBE NI KWA AJILI YA MASKINI WENYE SHIDA NA WANAOKARIBIA KUDATA.

MITHALI 31:4‭-‬7 SUV

📖"Ee Lemueli,
👉🏾kunywa mvinyo hakuwafai wafalme, hakuwafai wafalme; Wala haifai wakuu waseme, Ki wapi kileo?
5. Wasije wakanywa na kuisahau sheria, Na kuipotosha hukumu ya mtu aliye taabuni.
👉🏾6. Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea; Kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini. Anywe akausahau umaskini wake; Asiikumbuke tena taabu yake."
********************

💡K**a unataka kuwa Tajiri Usinywe Pombe.

Wimbo Mpya ;SOLUTION 👇🏽👇🏽
https://audiomack.com/mrkilimanjaro/song/14289469

Mwal :Emanuel Minja
Mrkilimanjaro
Nyumbayamungu
+255656714001

KAANANI NI WAPI?Tunajua kuwa Mto Nile unashusha Maji K*tokea Ziwa Victoria. Hii Inamaanisha kuwa Ziwa Victoria liko Mlim...
26/04/2022

KAANANI NI WAPI?

Tunajua kuwa Mto Nile unashusha Maji K*tokea Ziwa Victoria. Hii Inamaanisha kuwa Ziwa Victoria liko Mlimani halafu Nchi ya Misri ipo Bondeni.

Tukisoma Biblia Tunaona kuwa kuna kipindi Abramu na Lutu walienda Kaanani. walipanda K*toka Misri Kuelekea Kusini

MWANZO 13:1 SRUV
📖Abramu akapanda kutoka Misri, yeye, na mkewe, na kila alichokuwa nacho, na Lutu pamoja naye, mpaka kusini.
*****************

🤗Tukisoma hapo Tunaona kuwa Abrahamu alipanda kuelekea Kusini na ukitazama kwenye Ramani hapo Kupanda kuelekea Kusini ukiwa unatokea Misri ni sawa na Kusema Kupanda kutoka Misri Kuelekea Tanzania, Kenya, Uganda, Ethiopia, Rwanda, Burundi ,Congo, Zambia ,Sudan, Zimbabwe nk. Maana Nchi hizi zipo kusini kwa Misri halafu ukitokea Misri kwenda hapo unakua k**a unapanda kuelekea maji yanapotokea. Kiuhalisia kutokea pale Misri kwenda ile Israel ya Asia pale ni Kuelekea Kaskazini Mashariki na pengine ni kushuka sio Kupanda.

inavyoonesha Kaanani ni kupanda Juu (Mlimani) ya Misri kupanda kuelekea mlimani halafu anasema Kusini mwa Misri .🙌🏽

By Mwal: Emanuel Minja
Mrkilimanjaro
Nyumbayamungu
Simu: 0656714001

ISAYA 11 (Sura Nzima)Ufalme wa amani1  Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi ...
24/04/2022

ISAYA 11 (Sura Nzima)

Ufalme wa amani

1 Basi litatoka chipukizi katika shina la Yese, na tawi litakalotoka katika mizizi yake litazaa matunda.
2 Na Roho ya BWANA itakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha BWANA;
3 na furaha yake itakuwa katika kumcha BWANA; wala hatahukumu kwa kuyafuata ayaonayo kwa macho yake, wala hataonya kwa kuyafuata ayasikiayo kwa masikio yake;
4 bali kwa haki atawahukumu maskini, naye atawaonya wanyenyekevu wa dunia kwa adili; naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, na kwa pumzi ya midomo yake atawaua wabaya.
5 Na haki itakuwa mshipi wa viuno vyake, na uaminifu mshipi wa kujifungia.
6Mbwamwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwanasimba na ng'ombe wanono watakuwa pamoja, na mtoto mdogo atawaongoza.
7. Ng'ombe na dubu watalisha pamoja; watoto wao watalala pamoja; na simba atakula majani k**a ng'ombe.
8. Na mtoto anyonyaye atacheza penye tundu la nyoka, na mtoto aliyeachishwa kunyonya atatia mkono wake katika pango la fira.
9. Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; maana dunia itajawa na kumjua BWANA, k**a vile maji yanavyoifunika bahari.

Kurudi kwa mabaki wa Israeli na Yuda

10. Na itakuwa katika siku hiyo, shina la Yese lisimamalo kuwa ishara kwa makabila ya watu, yeye ndiye ambaye mataifa watamtafuta; na mahali pake pa kupumzikia patakuwa na utukufu.

11. Na itakuwa katika siku hiyo, Bwana atapeleka mkono wake mara ya pili, ili ajipatie watu wake watakaosalia, kutoka Ashuru, na kutoka Misri, na kutoka Pathrosi, na kutoka Kushi, na kutoka Elamu, na kutoka Shinari, na kutoka Hamathi, na kutoka visiwa vya bahari.
12. Naye atawatwekea mataifa bendera, atawakutanisha watu wa Israeli waliotupwa, atawakusanya watu wa Yuda waliotawanyika, kutoka ncha nne za dunia.
13. Na wivu wa Efraimu utaondoka, na wale wanaomwudhi Yuda watakatiliwa mbali; Efraimu hatamhusudu Yuda, wala Yuda hatamwudhi Efraimu.
14. Nao watashuka, watalirukia bega la Wafilisti upande wa magharibi; nao pamoja watawateka wana wa mashariki; watanyosha mkono juu ya Edomu na Moabu; na wana wa Amoni watawatii.
15. Na BWANA atauangamiza kabisa ulimi wa bahari ya Misri; na kwa upepo wake uteketezao atatikisa mkono wake juu ya Mto, naye ataupiga, uwe vijito saba, na kuwavusha watu waliovaa viatu bila kulowa.
16. Itakuwako njia kuu kwa mabaki ya watu wake watakaobaki, watokao Ashuru, k**a vile ilivyokuwako kwa Israeli, katika siku ile waliyotoka katika nchi ya Misri.

YESU HANA DINI YESU NI KWA AJILI YA WATU WOTE ULIMWENGUNIEbr 2:3 SUV📖sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu ...
19/04/2022

YESU HANA DINI YESU NI KWA AJILI YA WATU WOTE ULIMWENGUNI

Ebr 2:3 SUV
📖sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia

🤗Kinachonifanya Nimwamini Yesu na Nisimwache Kisha ni Nimpende sana ni Kwa Sababu Yeye alitoka Mbinguni Moja kwa Moja kutuletea Habari Njema za Uzima wa Milele, alikuja kutuambia Mbinguni Panatusubiri.
Hakutoka Marekani wala, wala Afrika Kusini wala Ulaya bali alitoka Mbinguni🥰

YESU ALIKUJA KWA AJILI YA WAHUNI WALIOPOTEA .

Alikua akikaa Muda Wote na Wale wanaoonekana wameshindikana mfano wanawake Wanaojiuza, Wezi, na Wahuni wengine, hadi Makuhani wakamkataa wakisema Angekua Katoka Mbinguni asingekaa na wahuni .lakini Yesu aliwajibu 👇🏿

Luka 19:10 SUV
📖"Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea".

💡Ukweli ni Kwamba ukimkubali Yesu jambo baya likitaka kukujia Yeye analizuia na Yesu yupo kwa ajili Yeye Aumie Sisi Tufurahi yani Yesu hajawahi Kuwa Snitch(Mnafiki)

😜Tofauti ya Wahubiri walio wengi Wale Wahuni wanaotoka Hapa hapa Duniani wanaotuhubiria Pesa na kila saa kutujaza hofu kwa kutuhubiria Habari za Motoni na Wapo Wahubiri wengine Hata Malaika hajawahi kuwatokea bado wanajiita ni MANABII .

🙌🏿Injili ni Habari za Uzima wa Milele sio habari za Moto wa Milele 😪

Wafilipi 4:4 SUV
📖Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.

FURAHINI .
Amani na Upendo
Mwal: Emanuel Minja
Mrkilimanjaro

Simu: 0656714001
kutoka: Nyumba ya Mungu

🤯AMKENIII 🇹🇿UNABII WA ISAYA UNATIMIA KWA TAIFA TAKATIFU LA MUNGU, TANZANIA YANI KAANANI.😱Tunamsahau Mungu Tanzania Tupig...
16/04/2022

🤯AMKENIII

🇹🇿UNABII WA ISAYA UNATIMIA KWA TAIFA TAKATIFU LA MUNGU, TANZANIA YANI KAANANI.

😱Tunamsahau Mungu Tanzania Tupige Goti Tumwombe Mungu atuepushe neno Hili linasema, Tuache kulala na Kulewa . Unabii wa Isaya Umetimia

💡sisi watanzania Tunakunywa Pombe mgeni akija tunasema na kesho ni k**a leo kila siku ni sikukuu

TUNASAHAU TANZANIA NI NCHI TAKATIFU YA KANANI

😱Sasa Neno linasema hayawani njooni mje mle WENYEJI HAWAJIELEWI KAZI YETU KULEWA NA KULALA 😭

AMKENIIIII 👇🏿

Enyi hayawani wote wa nyikani, njoni, Mle, enyi hayawani wote wa mwituni. Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi. Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote. Husema, Njoni, nitaleta divai, Na tunywe sana kileo; Na kesho itakuwa k**a leo, Sikukuu kupita kiasi.

Someni Wenyewe Unabii Wa Isaya

Isaya 56:3‭, ‬7‭-‬12 SUV

Wala mgeni, aambatanaye na BWANA, asiseme hivi, Hakika yake BWANA atanitenga na watu wake; wala towashi asiseme, Mimi ni mti mkavu. Nitawaleta hao nao hata mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu; kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote. Bwana MUNGU, akusanyaye waliofukuzwa katika Israeli asema, Pamoja na hayo nitamkusanyia na wengine, zaidi ya hao walio wake waliokusanywa. Enyi hayawani wote wa nyikani, njoni, Mle, enyi hayawani wote wa mwituni. Walinzi wake ni vipofu, wote pia hawana maarifa; wote ni mbwa walio bubu, hawawezi kulia; huota ndoto, hulala, hupenda usingizi. Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote. Husema, Njoni, nitaleta divai, Na tunywe sana kileo; Na kesho itakuwa k**a leo, Sikukuu kupita kiasi.
Mwal :Emanuel Minja

Mobile : +255656714002

🌕🥚💕 PASAKA (SIKU YA 14 YA MWEZI ABIB)  NI KWA AJILI YA WABANTU SISI NDIO WANA WA ISRAEL NA KISWAHILI NDO KIEBRANIATorati...
16/04/2022

🌕🥚💕 PASAKA (SIKU YA 14 YA MWEZI ABIB) NI KWA AJILI YA WABANTU SISI NDIO WANA WA ISRAEL NA KISWAHILI NDO KIEBRANIA

Torati 16:1 SUV
📖Utunze mwezi wa Abibu, ukamfanyie pasaka BWANA, Mungu wako, kwa kuwa ilikuwa ni mwezi wa Abibu alipokutoa Misri usiku BWANA; Mungu wako.

PASAKA NI LINI? 👇🏿
💡Leo Jumamosi (16/04/2022) ndo Pasaka

Walawi 23:5 SUV
📖Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi wakati wa jioni, ni pasaka ya BWANA.

K*toka 12:42 SUV
📖Ni usiku wa kuangaliwa sana mbele za BWANA kwa sababu ya kuwatoa katika nchi ya Misri; huu ndio usiku wa BWANA, ambao wapasa kuangaliwa sana na wana wa Israeli wote katika vizazi vyao.

*********************

WAISRAEL NI AKINA NANI

👉🏾Sisi Wabantu Hatupaswi kusherehekea Pasaka k**a siku ya Kufufuka kwake Yesu bali tunapaswa Kusherehekea Pasaka k**a siku ya uhuru wetu. kwa maana Hata Yesu alisherehekea sikukuu ya Pasaka akikumbuka taifa la Israel kutoka Misri .

Wabantu ni Watu wenye Nguvu sana na wanaoweza kufanya kazi ngumu na kwenye jua ndo maana Mtumwa ambaye aliuzwa kwa bei kubwa ni Mbantu mfano mzuri ni Wanyakyusa na Wakongo watu wakubwa ambao wana nguvu na vipaji vikubwa ambao wapo Marekani hadi sasa wakionesha vipaji kwenye Mziki Mfano RickRoss, kwenye Basketball Mfano Jordan, Kwenye Ndondi mfano Mike Tyson hao wote ni Wabantu

KWA NINI WABANTU NDO WANA ISRAEL
👉🏾Baada ya kutekwa Utumwani Kwa muda Mrefu Mungu akaamua K*tuokoa kutoka Misri Kuja Kaanan Ambapo ndo hapa Tanzania yote, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Kongo ambayo zamani ndo ilikua ikiitwa Congo Empire ambayo ni miongoni wa maeneo yaliyogawanywa kwenye Mkutano wa Berlin na Chancellor Bismark.

MFALME SOLOMONI ALIKUA NI MTU MWEUSI

Wimbo ulio Bora 1:5‭-‬6 SUV
📖Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri, Enyi binti za Yerusalemu, Mfano wa hema za Kedari, K**a mapazia yake Sulemani. Msinichunguze kwa kuwa ni mweusi-mweusi, Kwa sababu jua limeniunguza. Wana wa mamangu walinikasirikia, Waliniweka niwe mlinzi wa mashamba ya mizabibu; Bali shamba langu mwenyewe sikulilinda.
***************************

KAANAN NI WAPI?
👉🏾Duniani Nchi Ambayo dhahabu ipo juu kwenye Ardhi ni Kongo ambapo ukichimba na jembe shambani unapata Dhahabu

Baada ya Afrika na Dola ya kongo kugawanywa ili kupunguza umoja wa wabantu na kuvunja Taifa Moja la Afrika ndipo Utawala wa Kifalme ukakosa nguvu baada ya kupigwa vita na wavamizi kwa maana wavamizi walitaka kuweka Serikali zao ili waweze kuchukua Dhahabu, mali na watu wenye Nguvu waliopo Eneo Hili wakawauza maana wana nguvu sana wanaweza kufanya kazi kwenye hali ngumu na ndo sifa ya Waisrael wana nguvu sana. Mfano Samson.
kwa maana Eneo hili sasa la Ukanda wa Afrika Mashariki imeandikwa ni Kaanan Ni nchi ya Asali na Maziwa.

Siku zote Dhahabu safi huchimbwa Kongo na Tanzania na kupelekwa Ulaya sio kutoka ulaya na Asia kuja Afrika (Hii inaonesha wazi kuwa Nchi ya Dhahabu ,Asali na Maziwa ni Ukanda huu Wa Dola ya Kongo ambayo kwa sasa Mungu amelirudisha Taifa lake La Kongo k**a Umoja wa Afrika Mashariki.

TAIFA LA ISRAEL NI NANI?
(Ni uzao wa Yakobo)
ukisoma Biblia utaona kuwa Taifa la Israel Mwanzo lilikuwa Kule Asia ambako ndo kwenye Yerusalem, Yusufu alipouzwa na ndugu zake Misri na ikatokea njaa kubwa ndipo asilimia Kubwa ya Waisrael ikaenda Misri kwa Maana walikua watumwa baada ya kumuuza Yusuph ile dhambi ya kumuuza ndugu yao utumwani ikawarudia wao ndo wakaenda kua watumwa Misri huku wakiwa chini ya ndugu yao Yusufu.

Baada ya kumtumikia Farao kwa Muda Mrefu Mungu akatimiza ahadi Aliyompa Ibrahim kuwa ataupa uzao wake Nchi nzuri hivyo Mungu akawaagiza Musa na Haruni kuwaondoa wana Israel Misri Kupanda kuelekea Kusini wakiwa na Ngombe na mifugo yao mingine na ukitazama ng'ombe ni wale wenye Mabaka mabaka ambao Yakobo alipewa na mjomba wake Labani baada ya Kuntumikia ili aweze Kumwoa Raheli na Lea. ambapo hadi leo ng'ombe hao wanaendelea kutumika kuolea kwenye makanila mengi ikiwemo Wasukuma na Wamasai

ZIWA VICTORIA LIPO MLIMANI
Ukitazama kwenye Ramani Kusini kwa Misri ni huku na ukitazama kutoka Misri kuja Tanzania ni kupanda kwa maana Maji ya Mto Nile yanashuka kutoka Ziwa Victoria kwenda Misri hivyo basi Ziwa Victoria lipo Mlimani Ndo maana Maji yanashuka kuelekea Misri

KAANAN NI NCHI YENYE DHAHABU SAFI AMBAYO NDO ILE NCHI YA EDEN AMBAYO ADAM ALIFUKUZWA

EDEN NI WAPI?👇🏿
Mwanzo 2:8‭-‬15 SUV
📖BWANA Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya. BWANA Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Ukatoka mto katika Edeni wa kuitilia bustani maji, na kutokea hapo ukagawanyika kuwa vichwa vinne. Jina la wa kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Havila, ambako kuna dhahabu; na dhahabu ya nchi ile ni njema; huko kuna bedola, na vito shoham. Na jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi. Na jina la mto wa tatu ni Hidekeli; ndio unaopita mbele ya Ashuru. Na mto wa nne ni Frati. BWANA Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.

Tukisoma hapo Tunaona kuwa
1. Eden kuna Miti ya Kila Aina na ukicheki hadi sasa Sehemu kwenye miti ya Kila Aina ni Tanzania tena Tanzania ndo unapatikana mti Mrefu kuliko yote Duniani na Miti hutoka Afrika kwenda sehem zingine Duniani huo ni Ushahidi wa Kwanza kuwa Eden ni Afrika hasa hapa Tanzania

2. Kuna mito Mikuu minne inayonyeshea Eden ambapo ukitazama Afrika tuna mito mikuu minne ambayo ni Nile, Zambezi ,Niger na Kongo

3. ukisoma hapo Juu utaona kuna mto Pishoni (MTO KONGO) unaopita kwenye Nchi yenye dhahabu safi Havila (KONGO DRC)

4. Mto wa Pili Gihoni (Nile) Unazunguka Nchi Yote ya Kush (Ethiopia)

PASAKA NI LINI?
Walawi 23:5 SUV
📖Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi wakati wa jioni, ni pasaka ya BWANA.

MWEZI WA KWANZA ABIB NI LINI?
K*t 9:31-32 SUV
📖Kitani na shayiri zilipigwa; maana shayiri zilikuwa na masuke na kitani zilikuwa katika kutoa maua.
32. Lakini ngano na kusemethu hazikupigwa; maana, zilikuwa hazijakua bado.

👉🏾Ni mwezi Ambao Shayiri zimekomaa zinapigwa pigwa yani zinavunwa lakini Mpunga haujakomaa bado yani mwezi wa nne huu ndo mwezi ambao Shayiri inavunwa hivyo huu ni mwezi wa Kwanza Kibiblia

SIKU YA 14 UTAIJUAJE?
Ni siku ya 14 baada ya Mwezi Kuandama ambapo ukitazama kwa sasa hivi Leo Tarehe 16(Gregorian Kalenda) ndiyo siku ya 14 ya Mwezi huu (Kalenda ya Mungu)

Hivyo wakati Waislam wanauita mwezi Huu Ramadhani Mwezi Mtukufu kwetu sisi Wana Israel Halisi tunauita ABIB na ni Mwezi Mtukufu Pia kwetu k**a tunavyoagizwa kuwa ni Mtukufu hivyo tuutumie Kumkumbuka Muumba wetu aliyetutoa Misri.

PASAKA ITAKUMBUKWA KWA KUFANYA NINI?

K*toka 13:3‭-‬10 SUV
📖Musa akawaambia hao watu, Kumbukeni siku hii, mliyotoka nchi ya Misri, kutoka nyumba ya utumwa; kwa kuwa BWANA aliwatoa mahali hapa kwa nguvu za mkono wake; na usiliwe mkate uliochachwa. Ninyi mwatoka leo katika mwezi wa Abibu. Itakuwa hapo BWANA atakapowaleta mpaka nchi ya Wakanaani, na Wahiti, na Waamori, na Wahivi, na Wayebusi, nchi hiyo aliyowaapia baba zako kwamba atakupa wewe, ni nchi imiminikayo maziwa na asali, ndipo mtakapoushika utumishi huu katika mwezi huu. Mtakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba, nayo siku ya saba itakuwa ni sikukuu ya BWANA. Mikate isiyochachwa italiwa katika hizo siku saba; mkate uliotiwa chachu usionekane kwako, wala chachu isionekane kwako, ndani ya mipaka yako yote. Nawe utamwambia mwanao siku hiyo, ukisema, Ni kwa sababu ya hayo BWANA aliyonifanyia hapo nilipotoka Misri. Nayo itakuwa ishara kwako katika mkono wako, na kwa ukumbusho kati ya macho yako, ili kwamba sheria ya BWANA ipate kuwa kinywani mwako; kwani BWANA alikutoa utoke Misri kwa mkono wenye uwezo. Kwa hiyo utaitunza amri hii kwa wakati wake mwaka baada ya mwaka.

💡Leo Jioni Mwezi utakua na siku 14 Utakua na umbo k**a la yai ndo maana unaona picha nyingi zinazowekwa kwenye salam za pasaka panawekwa mayai ya pink
mayai yale ni umbo la Full moon kipindi hiki cha pasaka

utakua full moon wenye utofauti na full moon zingine

1. umbo k**a la Yai na utakua na Rangi ya pekee tofauti na Full Moon zingine

2. Mwezi utakua na Rangi k**a ya mchanganyiko wa Pink na Rangi ya Machungwa ambapo hutokea mara Moja tu Kwa Mwaka tena siku Moja tu ya Pasaka.

Nitakua nikikuletea Makala haya kwa kadri nitakavyojaaliwa
by Mwal: Emanuel Minja
Mrkilimanjaro
Nyumbayamungu
+255656714001

🙌🏿NAWATAKIA PASAKA NJEMA

🤔HADI MAKUHANI WAKUU  WALIHUSIKA KWENYE MBINU ZA KUMUUA YESU HAPA WALITAKA KUMUUA TENA LAZARO ILI USHAHIDI YA KUWA YESU ...
15/04/2022

🤔HADI MAKUHANI WAKUU WALIHUSIKA KWENYE MBINU ZA KUMUUA YESU HAPA WALITAKA KUMUUA TENA LAZARO ILI USHAHIDI YA KUWA YESU ANAWEZA KUFUFUA UPOTEE NA WALIONA WAUMINI WANAHAMIA KWA YESU.

Yohana 12:9-11

"9. Umati mkubwa wa Wayahudi waliposikia kwamba Yesu ali kuwa Bethania, walikuja ili pia wamwone Lazaro ambaye alimfufua.
👉🏾10. Kwa hiyo makuhani wakuu wakafanya mpango wa kumuua Lazaro pia,
11. kwa kuwa baada ya kufufuliwa kwake Wayahudi wengi waliamua kuwakataa viongozi wao na kumwamini Yesu.:
IJUMAA NJEMA

📖Warumi 13:1 SRUV👉🏾Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo ume...
07/04/2022

📖Warumi 13:1 SRUV

👉🏾Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu.


.. 💖 .

WARAKA WANGU KWA MAKANISA YOTE YANAYOWATOA WATU KUNDINIAmani ya Mungu Mwenyezi iwe nanyi Nyote.Baada ya kuona ni utarati...
06/04/2022

WARAKA WANGU KWA MAKANISA YOTE YANAYOWATOA WATU KUNDINI
Amani ya Mungu Mwenyezi iwe nanyi Nyote.
Baada ya kuona ni utaratibu wa Muda mrefu ya kuwatenga watu wanaokosea kwenye Makanisa ,kwa kuwatoa kundini, nimeona niwaandikie na mtafakari k**a kweli ni sahihi kuwatenga wanaoonekana wameyakosea makanisa.

Je mnamhubiri Yesu?
2. Je mtu akikosea kwanini mnamtoa Kundini badala ya kumweka karibu zaidi ili aokolewe?
3. mnapomtenga mtu Nyie Hamna dhambi? je Maaskofu na Makuhani wa makanisa pale wanapofanya dhambi sirini, wao hujitoa kundini?

4. Je Kanisa ni kwa ajili ya watu wasio na dhambi au kwa ajili ya watu wote? tena zaidi sio kwa ajili ya waliopotea?

5. Yesu Yesu alisemaje?
NUKUU
Lk 5:32 SUV
👉🏾Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi, wapate kutubu.
****
Mnaweza kusema ,
NUKUU
Mt 18:18 SUV
👉🏾Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.
*****
kwa Neno hilo hapo Juu Tafakarini k**a kumfunga mtu asiuone uzima wa Milele ni Sahihi

6. Je mnakumbuka Habari ya Mwana Mpotevu?

NUKUU
Lk 15:22‭-‬23 SUV
👉🏾Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni; mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi;
*****

MAKANISA TAFAKARINI SANA NENO HILI KWA MAANA UNAPOMTENGA MTU KUPATA NENO LA MUNGU MAANA YAKE UNAMNYIMA CHAKULA CHA ROHO.

7. Watu wote waliopo Makanisani kila mmoja ni msafi?

NUKUU
Yn 8:7 SUV
👉🏾Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe.
*****
Makanisa Yote yanayotenga Watu tutafakari kwa pamoja k**a kweli yafaa kuwatenga watu juu ya Habari za Neno la Mungu hasa kipindi hiki cha Nyakati za Mwisho zinazojionesha kwa macho ya Nyama.

👉🏾Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nasi sote.
Mwl: Emanuel Minja
+255656714001

Address

Kilimanjaro

Telephone

+255656714001

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nyumbayamungu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share