23/03/2024
NGUVU YA KUANZA
Ayubu 8:7
Mara nyingi sana watu wamekuwa na maono lakini shida ni pale walipoanza kuyapima maono yao na waliotuwangulia. Changamoto hii imewafanya watu kushindwa kusimamia maono yao kwa kuamini watakapoanza itakuwa k**a kichekesho.
Ayubu 8:7
"Tena ujapokuwa huo MWANZO wako ulikuwa ni MDOGO, Lakini MWISHO wako UTAONGEZEKA sana".
Hii inatufundisha mambo yafuatayo:
1. Ni lazima kuheshimu na kukubali kuwa Kuna MWANZO mdogo kwa Kila kitu. Hakuna namna mtu ataanza na kitu kikubwa, ukubwa wa maono aliyonayo mtu haudhiriki MWANZO bali baadaye. Kuukataa Mwanzo kwa kusema nitachekwa ni kuyasaliti maono yako.
2.Maongezeko yamefungwa katika muda, haiwezekani kuanza tu na kufikia lengo kuu kwasababu utumilifu wa wazo la mtu umefungwa katika muda. Kumbe unachotakiwa ni kuanza hata k**a katika udogo unaochekesha kwasababu baada ya MUDA maono yatakuwa na sasa unachokitaka kitaonekana.
3. Kuna uhakika wa kufanikiwa kutokea katika udogo, hapa natamani watu wapachukulie kwa uzito kwasababu wengi wamekata tamaa walipoona kuwa mwanzo wao haufanani na maono yao. Ahadi ya Mungu ni kuwa mwisho wa kitu kidogo ni maongezeko.
Andiko hili ni kwaajili ya wazee,vijana na watu wazima wenye ndoto na maono lakini wanaogopa kuanza kwasababu wanahisi wanaweza kuanza katika udhalili na uduni mkubwa.
Una maono ya duka Anza hata na genge kwasababu kutokea katika genge duka linaweza kuzaliwa, una maono ya kanisa kubwa Anza hata chini ya maturubali.
Hatuanzi kwasababu tumefanikiwa miundo mbinu ya kuanza lakini kwasababu tunao uhakika wa kufanikiwa kutokea pale tulipoanzia.
Pastor Ideca Jnr
Naioth International Church