Ideca J. Ehembwe

Ideca J. Ehembwe Preaching and Teaching the word
Mentorship and Coaching

NGUVU YA KUANZAAyubu 8:7Mara nyingi sana watu wamekuwa na maono lakini shida ni pale walipoanza kuyapima maono yao na wa...
23/03/2024

NGUVU YA KUANZA
Ayubu 8:7

Mara nyingi sana watu wamekuwa na maono lakini shida ni pale walipoanza kuyapima maono yao na waliotuwangulia. Changamoto hii imewafanya watu kushindwa kusimamia maono yao kwa kuamini watakapoanza itakuwa k**a kichekesho.

Ayubu 8:7
"Tena ujapokuwa huo MWANZO wako ulikuwa ni MDOGO, Lakini MWISHO wako UTAONGEZEKA sana".
Hii inatufundisha mambo yafuatayo:

1. Ni lazima kuheshimu na kukubali kuwa Kuna MWANZO mdogo kwa Kila kitu. Hakuna namna mtu ataanza na kitu kikubwa, ukubwa wa maono aliyonayo mtu haudhiriki MWANZO bali baadaye. Kuukataa Mwanzo kwa kusema nitachekwa ni kuyasaliti maono yako.

2.Maongezeko yamefungwa katika muda, haiwezekani kuanza tu na kufikia lengo kuu kwasababu utumilifu wa wazo la mtu umefungwa katika muda. Kumbe unachotakiwa ni kuanza hata k**a katika udogo unaochekesha kwasababu baada ya MUDA maono yatakuwa na sasa unachokitaka kitaonekana.

3. Kuna uhakika wa kufanikiwa kutokea katika udogo, hapa natamani watu wapachukulie kwa uzito kwasababu wengi wamekata tamaa walipoona kuwa mwanzo wao haufanani na maono yao. Ahadi ya Mungu ni kuwa mwisho wa kitu kidogo ni maongezeko.

Andiko hili ni kwaajili ya wazee,vijana na watu wazima wenye ndoto na maono lakini wanaogopa kuanza kwasababu wanahisi wanaweza kuanza katika udhalili na uduni mkubwa.

Una maono ya duka Anza hata na genge kwasababu kutokea katika genge duka linaweza kuzaliwa, una maono ya kanisa kubwa Anza hata chini ya maturubali.

Hatuanzi kwasababu tumefanikiwa miundo mbinu ya kuanza lakini kwasababu tunao uhakika wa kufanikiwa kutokea pale tulipoanzia.

Pastor Ideca Jnr
Naioth International Church

17/02/2024

Ndugu zangu.
Awali ya yote namshukuru Mungu kwasababu hivi karibu tutakuwa tumemaliza ujenzi wa nyumba ya Mungu.

Nikukaribishe kuungana nami katika ujenzi huu kwa kuchangia chochote katika vilivyoorodheshwa ili tuweze kuanza ibada zetu.
Mbao 25@5,000
Nondo 6@18,000
Mabati 4@20,000
Misumari 3@4000

Tuma Mchango kwa;
0764208373
Jehoshafati Ideca Ehembwe

Karibuni sana.

Pastor Ideca Jnr
NIC - Tanzania

31/01/2024

Shalom mtu wa Mungu.
Tunaendelea na ujenzi wa kanisa letu, bado hatujamaliza.
Tunahitaji mabanzi zaidi, misumari, mabati ya kuezekea na siment kwaajili ya ndani.

Sadaka yako inaweza kutusaidia kukamilisha kazi hii ili tuweze kuanza ibada zetu mapema mwezi huu wa Februari.

MPESA
0764208373 (Jehoshafati Ideca Ehembwe)

Bank: EXIM BANK
0231006384 (Jehoshafati Ideca Ehembwe)

Karibu kuchangia chochote.
Mungu akubariki.

KOMAA ULINDE ULICHONACHO WANAKITAMANI HICHO (UFUNUO 3:11)Picha hii imenitafakarisha lakini imenitia moyo sana na kunipa ...
25/11/2023

KOMAA ULINDE ULICHONACHO WANAKITAMANI HICHO (UFUNUO 3:11)

Picha hii imenitafakarisha lakini imenitia moyo sana na kunipa fundisho kubwa sana.

Kijana amepata lisamaki lake lakini nyuma yake kuna Vipaka vingi vinamkimbiza ambavyo vinataka kumnyang'anya samaki wake na kuna watu ambao hawakimbii naye lakini wanapiga shangwe kuonesha kuwa anaweza kushinda.

Vipaka vinavyomkimbiza ni vingi kuliko idadi ya watu wanaompongeza kwa shangwe, kitu cha ajabu ni;

DOGO KAAMUA KUMLINDA SAMAKI WAKE NA KUFOCUS MBELE KULIKO KUWATAZAMA WAPIGA SHANGWE NA PAKA.

Jifunze kwenye maisha kutambua umebeba nini, Jifunze kuelewa ulichonacho kuna watu wanakitaka pia. Pambana kulinda ulicho nacho kuliko kutazama shangwe za watu au paka.

Wapiga shangwe wangeweza kuwazuia paka lakini wanapiga kelele tu, dogo akisema ageuke kuwacheki wapiga shangwe paka wanamk**ata.

KILA MTU ALINDE NA KUPAMBANIA CHAKE.
Young Pastor Ideca Jnr.
@ Son of Light 💡

HEKIMA ZA MDOGO ANGU TIMOTHY ONESMOChochote unachokitafuta hapa Duniani tayari kipo mikononi mwa watu wengine ziwe Fedha...
05/11/2023

HEKIMA ZA MDOGO ANGU TIMOTHY ONESMO

Chochote unachokitafuta hapa Duniani tayari kipo mikononi mwa watu wengine ziwe Fedha, Kazi nzuri, Elimu n.k.

Hivyo vyote vipo mikononi mwa watu na namna pekee ya kuvipata ni kujua jinsi ya kuishi na watu vizuri, Unyenyekevu, Subira, Utii na kupunguza kujifanya mjuaji kutakufanya upate Kila unachokitaka mapema sana.

Zile tabia za maneno k**a Mimi sipangiwi na mtu, Mara Kila mtu na maisha yake zitakufanya uchelewe kufika kwenye malengo na ndoto zako

Badilika mfanikio Yako Mungu ameshayakabidhi mikononi mwa watu Fulani, Nenda kayachukue kwa utii, unyenyekevu, upendo na shukrani 🙏

UNANITAMBUAJE?Kuna vile mtu anajijua na kuna vile mtu anajulikana, maisha ni zaidi ya vile unajijua kwasababu Unaishi kw...
01/11/2023

UNANITAMBUAJE?
Kuna vile mtu anajijua na kuna vile mtu anajulikana, maisha ni zaidi ya vile unajijua kwasababu Unaishi kwaajili ya wengine.

Call me Young Pastor, A son of Light (1Thes 5:5)
Mchungaji Kijana, Mwana wa Nuru.

NB:
Kesho Alhamisi kuanzia saa sita mchana nitazungumza live ujumbe maalumu kwaajili ya watu wote wenye maono.

K**a una maono au ndoto zako ambazo umeanza au unakaribia kuanza kutendea kazi, usikose kesho kwenye ukurasa huu

26/09/2023

Kiwango cha kufanikiwa kwa maisha ya mtu kinategemeana sana kiwango cha taarifa sahihi kuhusu mambo alichonacho mtu husika.
Jifunze kujua sana kuhusu ufanyacho ili kuwa katika nafasi nzuri ya kufanikiwa

Address

P. O Box 157
Kigoma
47103

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ideca J. Ehembwe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Ideca J. Ehembwe:

Share