Eglise Méthodiste Libre au Congo

Eglise Méthodiste Libre au Congo Evangélisation jusqu'à l'enlèvement de l'Eglise par Jésus Christ.

PENTECÔTE 2026
21/05/2026

PENTECÔTE 2026

02/05/2026

S E R V I C E D E C O M M U N I C A T I O N/26è CMLC

BUREAU DE LA REPRÉSENTATION LÉGALE

CALENDRIER YA MABARAZA ZA MWAKA ACTUALISÉ 2026

1. TANZANIA
- Mahali pa Mkutano: Kigoma
- Muda: 03-05/07/2026

2. KATANGA
- Mahali pa Mkutano : Kalemie
- Muda: 10-12/07/2026

3. KIVU-EST
- Mahali pa Mkutano : Uvira
- Muda: 17-19/07/2026

4. SUD-EST
- Mahali pa Mkutano : Mshimbakye
- Muda: 21-23/07/2026

5. LULENGE
- Mahali pa Mkutano : Fizi-Centre
- Muda: 24-26/07/2026

6. MOYENS-PLATEAUX
- Mahali pa Mkutano : Mshimbakye
- Muda: 28-30/07/2026

7. ABOKE
- Mahali pa Mkutano : Nundu
- Muda: 31/07 AU 02/08/2026

8. HAUTS PLATEAUX-NORD
- Mahali pa Mkutano : Nundu
- Muda: 06-09/08/2026

9. MITUMBA
- Mahali pa Mkutano : Uvira
- Muda: 11-13/08/2026

10. NORD-KIVU
- Mahali pa Mkutano : Goma
- Muda: 21-23/08/2026

11. KIVU-OUEST
- Mahali pa Mkutano : Kamituga/Mwenga
- Muda: 28-30/08/2026

12. HAUTS-PLATEAUX SUD
- Mahali pa Mkutano : -
- Muda: 04-06/09/2026

13. KINSHASA
- Mahali pa Mkutano : Kinshasa
- Muda: 18-20/09/2026

Imefanyika pa Bukavu, tarehe 30/04/2026

Wakili Halali Achukuae Nafasi

Rév. KIMBITI NDABASHWA

Anaye tangaza:
©️ Communicateur wa Ofisi ya Shirika

Clément ABABELE ✍🏽

18/04/2026

S E R V I C E D E C O M M U N I C A T I O N/26è CMLC

Yahusu : Kuahirisha vikao vya Baraza la mwaka 2026

No 009/ASBL/ECC/26è CMLC/BRL/RLS/2026

Kwa Mheshimiwa Surintendant wa Baraza la Mwaka Free Methodist Church - DRC na Tanzania (Wote)

Mheshimiwa Surintendant wa Baraza,

Tumechukua fursa hii kukuandikia barua hii yenye mada ambayo imetajwa hapo juu.

Tunakukumbusha kwamba mpango wa tarehe za Mabaraza ya mwaka 2026 ulikuwa wa kutekelezwa katika kipindi cha tarehe 1 Mei hadi 31 Julai 2026.

Kutokana na hali ya usalama mdogo katika baadhi ya maeneo ya mabaraza yetu, tuliamua kuahirisha ratiba hiyo. Tunatumaini kwamba tutatekeleza kazi za vikao vya mabaraza kuanzia Julai 2026 ikiwa usalama bora utaripotiwa katika maeneo hayo yote.

Kunazo sababu za kimsingi ambazo zimesababisha kusimamisha kwa mda mpangilio huu. Mabaraza yetu yote kumi na matatu yako viungo vya mwili mmoja. K**a kiungo kimoja kinatatizwa, basi viungo vyote vinatatizwa pia na mwili wote, yaani kanisa nzima.

Basi, hiyo ndiyo sababu kuu iliyopelekea kuchukua uamzi wa kusubiria hali bora ya kiusalama tangu sasa hadi mwezi wa Julai.

Pamoja na hayo, tudumu katika kuomba Mungu ili alete amani nchini DRCongo na ili vikao vya mabaraza vianze kutekelezwa Julai ijayo.

Salamu zetu katika jina tukufu la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu.

Kwa niaba ya FMC-DRC na Tanzania

Wakili Halali Achukuaye Nafasi

Rév. KIMBITI NDABASHWA

©️ Anaye tangaza:
Communicateur wa Ofisi ya Shirika/Clément ABABELE ✍🏽

05/03/2026

Enjoy the videos and music that you love, upload original content and share it all with friends, family and the world on YouTube.

27/02/2026

CALENDRIER YA MABARAZA YA MWAKA 2026

1. Kivu-Est :
Mahali: Uvira
Muda: 1-3/5/2026

2. Aboke
Mahali : Nundu
Muda: 4-6/5/2026

3. Sud-Est
Mahali: Mshimbakye
Muda: 8-10/5/2026

4. Hauts plateaux Nord
Mahali: -
Muda: 12-14/05/2026

5. Mitumba
Mahali: Uvira
Muda: 18-20/5/2026

6. Nord-Kivu
Mahali: Goma
Muda: 29-31/5/2026

7. Kinshasa
Mahali: Kinshasa
Muda: 4-7/6/2026

8. Kivu-Ouest
Mahali: Kamituga/Mwenga
Muda: 19-21/6/2026

9. Moyens-plateaux
Mahali: -
Muda: 3-5/7/2026

10. Lulenge
Mahali: Kilembwe
Muda: 10-12/7/2026

11. Hauts plateaux Sud
Mahali: -
Muda: 17-19/7/2026

12. Katanga
Mahali: Kalemie
Muda: 24-26/7/2026

13. Tanzania
Mahali: Kigoma
Muda: 29-31/7/2026

Mgr Dr Venance LUBUNGA W'EHUSHA

Anaye tangaza:
©️ Communicateur wa Ofisi ya Shirika

Clément ABABELE ✍🏽

S E R V I C E  D E  C O M U N I C A T I O N/26èCMLC.MAELEKEZO KUHUSU KUTEKELEZA MFUMO MPYA WA 52 ENVELOPPES.------------...
26/02/2026

S E R V I C E D E C O M U N I C A T I O N/26èCMLC.

MAELEKEZO KUHUSU KUTEKELEZA MFUMO MPYA WA 52 ENVELOPPES.
------------------------
Baada ya kutuma barua yetu ya tarehe 12 Februari 2026 iliyokuwa na shabaa ya kutekeleza azimio ya Halmashauri ya Baraza Kuu 2025 kuhusu mfumo mpya wa sadaka ya 52 enveloppes, tumepokea maulizo na maoni mengi kutoka kwenye Maparokia ambazo zinahunda Mabaraza yetu ya mwaka.

Kulingana na hayo yote, tunawatolea maelekezo yafuatayo kwa kuboresha mfumo huo mpya wa Shirika letu :
1. Mfumo wa 52 enveloppes umekomboa moja kwa moja mfumo wa Hiari ambao ulikuwa ukitumika miaka iliyopita;
2. Sadaka ya 52 enveloppes itakuwa inatolewa na kila mwanamemba wa Parokia anayebatizwa na asiyebatizwa bado. Naye anajiamulia kwa uhuru kiwango (engagement) atakachotoa kila siku ya Mungu kulingana na pato au uweza wake. Mkristo akizuilika siku ya Mungu moja au zaidi bila kuja kanisani, anawajibika kutimiza engagement yake aliyopatana na Mungu wake kwa kutoa. Yaani asikose kutoa hata siku ya Mungu moja;
3. Sadaka ya 52 enveloppes itatolewa kipesa. Mwanamemba akikosa pesa, ana uhuru wa kutoa mifugo, mazao ya shamba, au kitu Cho chote alicho nacho. K**ati ya 52 enveloppes ya Parokia itakadirisha beyi ya kitu kilichotolewa na kuamua kwamba kiwango chake kinafunika matoleo ya siku ya Mungu ngapi ;
4. Ikiwa mwanamemba ana ahidi kutoa kila siku ya Mungu au kila mwezi kitu fulani, matoleo yake yatakubaliwa vile ilivyo pasipo kugawanywa kwa kufunika siku za Mungu zingine au miezi mingine;
5. Kila Parokia itaunda K**ati (Comité) ya watu wasio chini ya 3 na wasiozidi 7, wanaume na wanawake, wakiwemo watu wawili wa K**ati ya Fedha ya Parokia. Kazi ya K**ati hiyo ni :
▫️ Kuhamasisha (sensibiliser) wanamemba ,
▫️ Kutengeneza orodha ya wanamemba ambao wanatoa sadaka hiyo kila siku ya Mungu ,
▫️ Kuhesabu pesa zilizotolewa ndani ya enveloppes na kuandika ndani ya buku lao kiwango kilichotolewa siku ile, wakishirikiana na K**ati ya Fedha ya Parokia,
▫️ Kutoa mashauri kwa wapastori kuhusu kuboresha zaidi mfumo huu,
▫️ Kupanga mishahara (barème salarial) ya wachungaji wakisaidiana na K**ati ya Fedha ya Parokia ,
▫️ Kila mwisho wa mwezi kutayarisha na kusahini PV ya pesa jinsi zilivyoingia, jinsi zilivyogawanywa na kutoa ripoti kwa wapastori.
6. Sadaka ya 52 enveloppes sio pesa za kufanya nazo garama nyingine za kibinafsi au za kanisa, bali ni pesa za kulipa mishahara ya wachungaji wetu ili wafikie kufanya kazi zao vizuri k**a walivyoitwa na Mungu na jinsi wanavyoelekezwa na KITABU CHA MAONGOZI cha Shirika letu;
7. Wachungaji wa Parokia wasingejiruhusu kuamuru lo lote kuhusu mfuko huo kwa K**ati ya 52 enveloppes kinyume na utaratibu wa mfumo wenyewe;
8. Kwenye Ofisi ya Shirika kuna K**ati(Comité) ya 52 enveloppes yenye kufuatilia kindani K**ati za Maparokia ili kuhakikisha kwamba K**ati hizo zinafanya kazi zao vizuri na zinatekeleza vema mfumo huu. Lakini pia ina kazi ya kujua shida au changamoto wanazokumbana nazo na kutoa mwelekeo;
9. Pakiwepo swali juu ya utekelezaji bora wa mfumo huu, ni vema K**ati ya Parokia na wote wahusikao wawasiliane na K**ati ya Ofisi ya Shirika kwa ajili ya kupata maelezo zaidi;
10. Kwa ajili ya kulinda utaratibu mwema, ni K**ati ya Ofisi ya Shirika pekee ndiyo ina jukumu ya kuwasiliana na Askofu kwa maswali yo yote kuhusu mfumo huu;
11. Sadaka ya 52 enveloppes sio pesa za kutuma kwa Jimbo au Baraza la mwaka, apana. Ifikapo kila mwisho wa mwezi K**ati ya kila Parokia ihusikayo na 52 enveloppes itajumuhisha pesa zote ambazo zilizotolewa kwa mwezi mzima na kuzigawa sehemu 4 sawa sawa;
12. Sehemu moja ya nne ( 1/4) itatumwa moja kwa moja kwa Ofisi ya Shirika kupitia namba za wachunga hazina wa Shirika zifuatazo 0975238710 na 0975035524 pasipo kupitia Jimbo wala Baraza. Na sehemu tatu ya nne (3/4) itabaki kwa Parokia kwa ajili ya kulipa mishahara ya wachungaji pasipo kutuma asilimia kwa Jimbo wala Baraza ;
13. Mara tu wanapotuma sehemu ya Shirika (1/4), Parokia itafanya capture d'écran ya pesa walizotuma kwa K**ati ya Shirika ili ifuatilie. Pamoja na hayo Parokia itaripotia kwa Jimbo pesa zilizotumwa kwa Shirika ;
14. Ripoti ya 52 enveloppes itasomwa na K**ati za Fedha ya vikao vya Parokia, Jimbo na Mabaraza ya mwaka;
15. Sadaka ya 52 enveloppes haiji kwa kuvunja sadaka ya KAWAIDA, CHAKUMI wala SHUKRANI. Sadaka hizo zinabaki vile vile na zinagawanywa kwa asilimia zile zile munazotuma kwa Baraza na Jimbo. Kinachoombwa ni kufanya matumizi bora ya sadaka hizo ili kupunguza uwingi wa michango kanisani ;
16. Wachungaji walio kwa ngazi ya Parokia na ambao hawakutumwa na Baraza la mwaka, watatunzwa kwa njia ya mapato mengine ya kawaida ya Parokia;
17. Wa délégués Laïcs wa Mabaraza ya mwaka, na Wakuu viongozi wa LAÏCAT Shirika wahusike sana kwa kufanya uhamasishaji (sensibilisation) na ufuatiliaji(suivi) wa kazi za K**ati za 52 enveloppes kwenye Maparokia yetu na kutoa Ripoti kwa K**ati ya enveloppes ya Shirika.

Imefanyika pa Bukavu, tarehe, 25 Februari 2026.

Katibu Mtendaji wa ECC/26è CMLC

Joseph AFUMBA SAMBO ALIMASI.

Imetangazwa na:
©️ Communicateur wa Ofisi ya Shirika

Clément ABABELE✍🏽

21/02/2026
S E R V I C E  D E  C O M M U N I C A T I O N/26èCMLC Shabaha : Kutekeleza azimio ya Halmashauri ya Baraza Kuu 2025 kuhu...
12/02/2026

S E R V I C E D E C O M M U N I C A T I O N/26èCMLC

Shabaha : Kutekeleza azimio ya Halmashauri ya Baraza Kuu 2025 kuhusu mfumo mpya wa sadaka ya bahasha 52 ( 52 enveloppes).

Kwa Révérend Surintendant Mkuu wa Baraza la Mwaka/26èCMLC (wote)
BP 2110 BUKAVU
---------------------------
Révérend Surintendant,

Pokea salamu zetu za mapendo na amani katika jina la Yesu Kristo.

Twaja mbele yenu kwa ajili ya kuwakumbusha kuhusu kutekeleza mfumo mpya wa sadaka ya HIARI(Mfumo wa 52 enveloppes) kulingana na azimio ya Kikao cha Halmashauri ya Baraza Baraza Kuu kilichofanyika tarehe 27-28 Novemba 2025, kwa njia ya mtandao wa zoom na whatsapp. Mfumo huo mpya, umeazimiwa uanze kutekelezwa tangu Januari 2026 katika eneo lote la Shirika.

Kwa ajili ya hayo tumependa ujue na kutekeleza mambo yafuatayo:
1. Mfumo wa 52 enveloppes unamaanisha juma 52 za mwaka;
2. Kila mkristo atajiamulia kwa uhuru kiwango atakachotoa kila siku ya Mungu kulingana na uweza wake;
3. Anayengojelewa kutoa sadaka ya 52 enveloppes ni kila mkristo anayebatizwa na asiyebatizwa bado;
4. Sadaka hiyo itawekwa ndani ya bahasha(enveloppe)yenye jina la mkristo kwa ajili ya kulinda siri. Bahasha hizo zitawekwa ndani ya kitunga siku ya Mungu, na K**ati husika itaenda kuhesabu. Baadaye itarudisha bahasha kwa wakristo;
5. Mfumo huo mpya umeazimiwa kwa ajili ya kusahidia wachungaji viongozi wa Maparokia Ili watumike kazi zao kwa bidii na wapate haki yao vilivyo;
6. Ifahamike kwamba bahasha(enveloppe)moja ya mwisho wa mwezi itatumwa moja kwa moja kwa Ofisi ya Shirika, kwa namba za mchunga hazina( Caissier)wa Shirika 0975238710 na Comptable wa Shirika 0975035524 pasipo kupitia Jimbo wala Baraza;
7. Kila Parokia inaombwa kuunda K**ati(Comité) ya watu wachache wasio chini ya tatu au zaidi ya saba wakiwemo watu wawili wa Chumba cha Fedha ya Parokia. Kazi ya K**ati ni:
- Kuhamasisha wakristo,
- Kutoa orodha ya wakristo ambao wanatoa sadaka hiyo kila juma,
- Kuripotia kwa wapastori wa Parokia kila mwisho wa mwezi.
8. Mfumo huo mpya sio wa kuja kuvunja sadaka zingine kanisani. Lakini mfumo huo ukitembea vizuri popote utawezesha kukomboa michango mingine inayoombwa na Maidara ya Shirika, vile vile kulipa mishahara ya wakuu wa Mabaraza ya mwaka;
9. Kwa ajili ya kuwezesha Maparokia yote yatumike sawasawa, Ofisi Kuu ya Shirika itaandaa mafundisho na kutoa mwelekeo kwa njia ya mtandao itakayohusisha au itakayolenga wanamemba wote wa K**ati ya 52 enveloppes ya kila Parokia ;
10. Pakiwepo na tatizo au swali lo lote moja kulingana na mfumo huo, ni vema kuuliza moja kwa moja Ofisi ya Shirika kwa namba hizi: 0844990327 , 0991742954 , 0998523250 .
11. Tuendelee kuomba Mungu ili amani irejee katika maeneo yote ya Shirika ;
12. Barua hii itakapo kufikia wewe Mkuu wa Baraza, ufanye haraka ili ifikie Maparokia. Kwani ni wao watakaotekeleza mfumo huo.
Habari nzuri tuliyo nayo ni kwamba Baraza la mwaka la Kinshasa limehanzisha mfumo huo tangu Januari 2026 na kutuma ripoti zao toka Maparokia zao k**a ilivyo azimiwa na Halmashauri ya Baraza Kuu 2025. Ripoti hizo zinaleta matumaini na wapastori wao wanashuhudia hivyo na tunawashukuru kwa hilo.

Tunakutakia kazi njema Révérend Surintendant, na Mungu atubaraki sote.

Bukavu, tarehe 12 Februari 2026

Katibu Mtendaji wa ECC/26èCMLC

Joseph AFUMBA SAMBO ALIMASI

©️ Anaye tangaza:
Communicateur wa Ofisi ya Shirika

------------------------------
Clément ABABELE ✍🏽

25/05/2025

Zoom is the leader in modern enterprise cloud communications.

Address

Kigoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Eglise Méthodiste Libre au Congo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share