09/07/2024
DALILI ZA MTU ALIYE NA LAANA
Na mch. Rehema Maro
Laana ni hali au nguvu fulani inayomsukuma mtu na kumpelekea kushindwa katika mambo au maeneo mbalimbali licha ya kuweka juhudi au jitihada nyingi.
Kutegemeana na aina ya laana iliyopo kwenye ukoo unaotokea
Kwa mfano laana ya magongwa, laana ya umaskini, laana ya kukataliwa, laana za uzinzi, upagani, ushirikina, n. K
Watu wengi hawajui chanzo cha hayo matatizo
Maombolezo 5:7
[7]Baba zetu walitenda dhambi hata hawako;
Na sisi tumeyachukua maovu yao.
DALILI ZA MTU MWENYE LAANA
1. Kotofanikiwa kwenye kila kitu na kila uendako Kumb 28;1-14,16
2.Kila upatacho huisha na kupotea bila kutosheleza. Na akiba ya vitu haikai
Hagai 1;6
3.Uzao wako haufanikiwi yaani mifugo, mashamba, watoto wako na kila kitu
Kumb 28;18
4. Kutojiamini kwenye kila unachofanya Mithali 28:1
5. Magonjwa yasiyoisha kwa mtu Kumb 28;22
6. Kila alichokitegemea kiwe msaada kwake hakimsaidii. Laana huondoa tumaini la maisha na unachokitegemea
Kumb 28;23, 28;51
7.Kuwa mtu wa kushindwa na kuonewa, unapigwa na adui zako Kumb 28;25
8.kukataliwa hata baada ya kufa Kumb 28;26
9.Kukosa mwelekeo wa maisha siku zote Kumb 28;28-29
10. Kila upatapo kitu unanyang'anywa Kumb 28:31-33
11. Kuwa mtumwa kwa kila umuonaye mbele yako Kumb 28;36,48
12.Kudharaulika na watu wote Kumb 28:27
13.Kutopiga hatua yoyote kimaisha. Hali hii inamfuata mtu bila hata yeye kujua Kumb 28; 43-44
14. Familia kupungukiwa na mema
15. Mateso yanayo jirudiarudia Kumb28;67
16. Tabia fulani fulani zisizofaa mfano ulevi, uzinzi,ukahaba,nk
17.Kupoteza uwezo fulani ambao ulikuwa nao Kumb 28;37
18.Vifo vya mapema ndani ya familia au ukoo
19.Vifo vya ghafla visivyoeleweka vizuri kumb 28:67
20.Magonjwa ya akili na kuchanganyikiwa
21.Vifo vya kujinyonga au kunywa sumu
22. Kutokuolewa au kuoa
23.kutokusona au kukosa elimu
24.kupata au kunusurika ajali za mara kwa mara
25.Umaskini mkubwa (kutokuwa na chochote)
26.Kesi za mara kwa mara, kusingiziwa na hali ya madeni yasiyoisha Kumb 28;44
27. Hali ya watu kupotea na kutokujulikana waliko kwenye ukoo
28. Mimba kuharibika mara kwa mara
29.Kufa kwa watoto baada ya kuzaliwa
30. Mtu kutoona kutoka kwenye mkwamo wa maisha anaopitia
31. Akienda kwa wataalamu wa afya wanamwambia hawaoni chochote, wakati huo yeye anapata shida.