Mafundisho ya Neno la Mungu, Maombi Na Maombezi

Mafundisho ya Neno la Mungu, Maombi Na Maombezi Waamuzi 15:18-19

18/11/2022

NGUVU YA SADAKA INAYOTOLEWA KWA MAELEKEZO YA MUNGU

Bwana Yesu Kristo Asifiwe sana.

Leo imempendeza Mungu tena tujifunze kwa habari ya sadaka ama matoleo yanayolewa kwa maelekezo ya Mungu.

Utaratibu wa kupokea ni kutoa kwanza, yaani wewe uwe wa kwanza kutoa. Unapotoa kwa mwanadamu mwenzako ama Mungu, unatengeneza nafasi ya wewe kupokea.

Luka 6:38
38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.

Kumbuka hakuna mwanadamu ambaye aliwahi kutoa sadaka kubwa akamzidi Mungu, Mungu ndo Mwanzilishi wa kutoa na ndio Mtoaji Mkubwa( Jehovah-Jireh). Mungu alitoa kipi? Alimtoa Mwana wake wa Pekee kwa Upendo kabisa( Yohana 3:16). So, tambua unapotoa unaonyesha upendo kwa Mungu kwani Mungu ni Pendo.

Sasa yamkini kuna jambo ama mambo kadha wa kadha unatamani ama umekuwa ukimwomba Mungu akumilikishe( akurithishe), na hujajua kwa nini mpaka leo bado hujayapokea/hujayamiliki/hujayarithi na kuwa yako.

Mwanzo 15::

7 Kisha akamwambia, Mimi ni Bwana, niliyekuleta kutoka Uru wa Wakaldayo nikupe nchi hii ili uirithi.

8 Akasema, Ee Bwana MUNGU, nipateje kujua ya kwamba nitairithi

9 Akamwambia, Unipatie ndama wa miaka mitatu, na mbuzi mke wa miaka mitatu, na kondoo mume wa miaka mitatu, na hua, na mwana njiwa.

10 Akampatia hao wote, akawapasua vipande viwili, akaweka kila kipande kuelekea mwenzake, ila ndege hakuwapasua.

11 Hata tai walipotua juu ya mizoga Abramu akawafukuza

Mungu alimtaka Ibrahim atoe SADAKA YA AGANO ili kuirithi hiyo nchi aliyoambiwa. Kuna mambo Mungu hawezi kuyafanya kwako ikiwa hujaugusa moyo wake. Sulemani alipogusa Moyo wa Mungu, Mungu alimwendea usiku katika ndoto na akamwambia aombe chochote atakacho na atampa. Ili Ibrahim airithi nchi, alitakiwa kutoa sadaka.

Sasa, utajuaje kuwa Mungu anataka utoe sadaka juu ya jambo fulani ndipo upokee muujiza wako ama utajuaje Mungu anataka utoe SADAKA YA AGANO? Njia rahisi na nyepesi Mungu anayoitumiaga ni MSUKUMO WA MOYO TOKA NDANI. Biblia inasema AMANI ya Mungu iamue mioyoni mwenu. K**a ni Mungu anakusemesha juu ya jambo tokea moyoni, utajihisi kuwa na amani.

Wako watu wengi Mungu aliwasemesha kwa habari ya kusapoti ujenzi wa huduma/makanisa na hawakufanya hivyo; wako watu wengi Mungu aliwasemesha kwa habari ya kusimama na kuombea watumishi wa Mungu na hawataki kufanya hivyo; na kadhalika na kadhalika. So, kwa kutokufanya hivyo, wamejikuta mipango yao, maisha yao, malengo yao hayatimii wala kufanikiwa. Kwa nini? Kwa sababu walikataa KUTII SAUTI YA MUNGU.

Sasa kuna wengine huwa wanasikia sauti ya Mungu na kuelewa kile ambacho Mungu anawataka wafanye, ila shetani anainuka, anawak**ata moyo na hatimaye wanashindwa kutimiza kile Mungu alichowasemesha. Tunaona katika mstari wa 11, tai wanatoa kwenye hiyo sadaka Abram aliyomwandalia Mungu kabla ya kupokelewa/kukubaliwa na Mungu na hivyo, Ibrahim anawafukuza hawo tai na anabaki kuilinda sadaka yake mpaka Mungu aipokee. Je, unajua kuwa nguvu ya giza huwa zinaibuka na kutaka kuzuia usimtolee Mungu wako SADAKA aliyokusemesha ili usije ukapokea baraka zako, muujiza wako, urithi wako?? Je, huwa unang'ang'ana kuhakikisha kuwa nguvu za giza hazikuzuii kumtolea Mungu wako na unatoa sadaka kamili aliyokuagiza Mungu??

Kila baraka ya Mungu ina kanuni yake. So, tujifunze kuwa watii na kusikiliza sauti ya Mungu ili tupate kufanikiwa kiroho na kimwili pia.

Mungu anapenda tuwe wasikivu na watii. Mungu anayo mengi ya kututendea ila kuwa wakati sisi wenyewe tunam-limit( tunamwekea mpaka) japo Yeye anatamani kufanya zaidi na kwa ukubwa.

Mungu awabariki na kuwalinda In Jesus Mighty Name

By Elisha!!

JE, KATIKA AHADI YA BWANA UNAYOITAZAMIA, UMEWEKA NA BIDII PIA?Bwana Yesu Asifiwe Sana! Nawasalimu kupitia Jina kubwa la ...
17/11/2022

JE, KATIKA AHADI YA BWANA UNAYOITAZAMIA, UMEWEKA NA BIDII PIA?

Bwana Yesu Asifiwe Sana! Nawasalimu kupitia Jina kubwa la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo Aliye Hai.

Leo imempendeza tena Mungu ku-share ujumbe huu pamoja nanyi.

*Kumbukumbu la Torati 2::*

1 Ndipo tukageuka, tukashika safari yetu kwenda jangwani kwa njia ya Bahari ya Shamu, k**a alivyoniambia Bwana; tukawa kuizunguka milima ya Seiri siku nyingi.

2 Bwana akanena, akaniambia,

3 Mlivyouzunguka mlima huu vyatosha; geukeni upande wa kaskazini.

Nataka tujikite zaidi kwenye mstari wa tatu. Mungu wetu ni Mungu anayesema kila siku na watu wake, japo sisi watu wake hatuelewi na wakati mwingine tunaelewa anachosema ila hatuzingatii.

Biblia imejaa ahadi nyingi sana za Mungu ila kuna wakati tunaona k**a hizo ahadi si zetu, zinawahusu watu fulani ama zimepitwa na wakati. Tunasahau kuwa Mungu ni Yule yule jana, leo na hata milele.

Ni kweli kwamba wana wa Israel walikuwa wameuzunguka mlima huo huo muda mrefu sana kwa kujua ama kutokujua, but ilipotimia wakati wa Bwana, aliwatoa kwenye huo mzunguko( mahangaiko).

Mara nyingi Mungu huwa hasemi exact time( muda) ambawo jambo fulani, linapaswa kutokea, but huwa anatoa taarifa tu. Unaonaje k**a Mungu angewaambia wana wa Israel kuwa mnakwenda kukaa jangwani na kuzunguka mlima kwa miaka 40, je wangekubali kutoka Misri? La, haswa wasingekubali! Mungu alipomwonyesha Yusufu kwa habari ya yeye kuinuliwa na kuwa mkuu, hakumwambia muda ambawo jambo hilo lingetokea, bali alimpa tu taarifa.

Ndivyo ilivyo hata leo, Mungu anaweza kukuonyesha jambo na kukupa matokeo ya mwisho tu na asikuonyeshe changamoto( magumu, process) ambazo utapitia ili ufikie huko. Mfano, k**a ni mtumishi, Mungu anaweza akakuonyesha ukiwa unaponya watu ama kuhubiri, but ikakuchukua miaka hata 30 ili kufikia hatua hiyo na ukawa umepitia changamoto ngumu sana sana.

Sasa, biblia inasema pasipo Imani haiwezekani kumpendeza Mungu. Na tena inasema Imani pasipo matendo, imekufa! Je, hii inamaanisha nini?

Yakobo 5::

16b Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.

17 Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita

Imani==Ahadi ya Mungu ama Neno la Mungu kuhusu jambo fulani na Matendo==Bidii, Jitihada mtu anayoitumia ili hiyo ahadi ama hilo Neno analoliamini limitie na kudhihirika.

Wakristo wa leo tunaamini ahadi za Mungu ama Neno la Mungu, ila hatuna bidii( hatuna matendo) yanayoambatana na hicho tunachokiamini na ndo maana hatuoni udhihirisho wa hiyo imani!

Imani kwa lugha nyingine ni uwezekano wa jambo kuwa hivi ama vile, na imani huwa inaambatana na nguvu fulani ndani yake; lakini matendo( bidii) ni kuumba hicho kisichoonekana.

Nabii nyingi za siku hizi zinaonekana kutotimia na hivyo watumishi wazitoazo hizo nabii wameonekana kuwa waongo. Kwa nini? Tunarudi pale pale, Imani ( Neno la unabii, uwezekano wa jambo kuwa) pasipo matendo( bidii, jitihada, kuumba) imekufa.

So, kwa kifupi tunapoamini jambo, ni lazima tuliweke kwenye matendo na kuweka na bidii, ndipo litimie( liumbike).

Mfano:: Chukulia kwa u mgonjwa na umesumbuliwa kwa muda mrefu na hiyo hali huipendi na imekuchosha; Na utambua kuwa kuna mstari( ahadi ya Mungu, Neno la Mungu) linasema:-

Isaya 53:5
Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

Kwa kutumia hii Ahadi ya Mungu unaweza ukadai uponyaji. Sasa je, utadai vipi? Ni lazima uweke matendo( bidii), uchukue hatua, uwe na shauku ya kupona na ndipo utauona wokovu wa Bwana maishani mwako. Kumbuka yule mwanamke aliyekuwa anatokwa na damu kwa miaka kumi na miwili, alijisemea moyoni mwake, nikigusa tu pindo la vazi lake nitapona( Neno la Imani) na akajitahidi kwenda aliko Yesu, akagusa( bidii, jitihada, matendo) na ndipo akapona. Pia mkumbuke yule kipofu Bartimayo, alipaza sauti yake kwa nguvu aliposikia Yesu anapita kwa kusema Nirehemu Mwana wa Daudi na ndipo Yesu akamwita na kumwuliza shida yake. Sasa je, Yesu hakujua shida yake hata amwulize? Alijua na ndo maana alitaka kujua ikiwa huyu kipofu alijua nini anataka. So, imani ni pamoja na matendo. Imani na matendo hufanyakazi pamoja.

Kuwa na imani na huna matendo, ni sawa na kupanda mbegu bila kumwagilia, bila kupalilia, bila kuweka mbolea na bado ukategemea kuvuna.

Kumbuka:: Mungu anapokuonyesha kitu/jambo huwa hamaanishi litatokea kesho ama ni lazima litokee hivi karibuni ama hakutakuwa na changamoto ama haliwezi kwenda kinyume na likashindikana kabisa, HAPANA, inategemea na wewe unasimamaje na una bidii gani.

Mfano 1::
Wakati wana wa Israel wako Misri, Mungu aliwaahidi na kuwaambia kwamba mnakwenda Kanaani kwenye nchi njema itiririkayo maziwa na asali, hakuwaambia habari za kukaa jangwani miaka 40, hakuwaambia kuwa watakufa jangwani k**a wakisitasita, na hakuwaambia kuwa wataingia wawili tu kati ya wale waliotoka Misri yaani Yoshua na Kaleb. Je, Mungu alisema uwongo? La, hasha! Je, wote hawakutoka Misri na Neno la Ahadi? Kufika ama kutokufika kwao, kulitegemea na wao wenyewe wanaambatanaje na Mungu!

Hesabu 32:11-12

11 Hakika yangu hapana mtu mmoja katika wale watu waliotoka Misri, tangu huyo aliyepata umri wa miaka ishirini, na zaidi, atakayeiona hiyo nchi niliyomwapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo; kwa sababu hawakuniandama kwa moyo wote;

12 ila Kalebu mwana wa Yefune, Mkenizi, na Yoshua mwana wa Nuni; kwa kuwa wao wamemwandama Bwana kwa moyo wote.

Mfano 2::
Mungu mwenyewe aliwaambia Israel kwa kinywa cha Nabii Yeremia kuwa watakaa miaka 70, lakini walitoka kwa kuchelewa. Je, unabii ulikuwa wa uwongo? Kwa nini muda ulipitiliza? Ni kwa sababu ya kutokukaa kwenye mkao mzuri na Mungu; So tambua kuwa ahadi za Mungu zinaweza kutimia ila kwa kuchelewa ikiwa hutokaa vyema na Mungu yaani kukosa bidii( jitihada)!

Daniel 9:2
katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.

Mfano 3::

13 Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa miaka mia nne.

14 Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi.

15 Lakini wewe utakwenda kwa baba zako kwa amani, utazikwa katika uzee mwema.

16 Na kizazi cha nne kitarudi hapa, maana haujatimia uovu wa Waamori bado

Hapa tunaona Mungu anamwambia Abramu kuwa wana wa Israel wangekaa Misri miaka 400.

Kutoka 12::

40 Basi wana wa Israeli kukaa kwao, maana, muda waliokaa ndani ya Misri, ulikuwa ni miaka mia nne na thelathini.

41 Ilikuwa mwisho wa miaka hiyo mia nne na thelathini, ilikuwa siku ile ile, ya kwamba majeshi yote ya Bwana yalitoka nchi ya Misri.

42 Ni usiku wa kuangaliwa sana mbele za Bwana kwa sababu ya kuwatoa katika nchi ya Misri; huu ndio usiku wa Bwana, ambao wapasa kuangaliwa sana na wana wa Israeli wote katika vizazi vyao.

Hapa tunaona wanatoka mwaka wa 430, badala ya 400. Kwa nini miaka 30 izidi? Kosa si kwa Mungu, bali ni kwa watu wenyewe, wahusika wenyewe. Ni kweli walikuwa na Neno la ahadi kuhusu kutoka mwaka wa 400, but je waliweka bidii( jitihada) ya kutosha?

Biblia inatukumbusha kuwa tusiwe wasikilizaji tu wa Neno, bali tuwe watendaji pia. So, unapokuwa na imani( neno la ahadi) juu ya jambo fulani, weka matendo( bidii, jitihada) pia.

Mungu awabariki.

By Elisha!

NAFASI YA MUNGU KATIKA MOYO WA MWANADAMUNawasalimu katika Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Nawakaribisheni nyo...
16/11/2022

NAFASI YA MUNGU KATIKA MOYO WA MWANADAMU

Nawasalimu katika Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Nawakaribisheni nyote tujifunze na tusikilize Neno la Mungu;;

Mwanadamu aidha anajua ama hajui, aliumbwa kuabudu. Mwanadamu hawezi kukamilika yeye mwenyewe bila Mungu ndani yake. Katika moyo wa kila mwanadamu, Mungu aliumba na kuacha NAFASI wazi kwa ajili Yake. Why, Mungu aliacha hiyo nafasi? Well, ni ili Yeye akae na kuishi ndani ya mwanadamu. So, ili mwanadamu akamilike, anahitaji Mungu akae na kuishi ndani yake.

Cha kushangaza na kustaajabisha ni kuwa, Mungu alipomuumba mwanadamu, hakumwambia amuabudu, bali alijua siku atapata UFAHAMU tu na ataanza kumuabudu. Mungu alitamani mwanadamu kwa *HIARI YAKE( WILL)* aamue/achague yeye mwenyewe aidha kumuabudu Mungu ama kutokumuabudu.

Wakati Mungu akimsubiri mwanadamu siku apate ufahamu na achague nini na kipi aabudu, Mungu alimwekea mpaka tu kwa kumpa agizo kuwa asile matunda ya mti mmojawapo katika bustani ya Edeni. Why, Mungu alimwekea mpaka, ilikuwa ni kumuepusha na UHARIBIFU NA MAUTI( Kumbuka KUTAMANI ilikuwa ni Uharibifu na Kujikuta wakiwa watupu ni MAUTI).

*Kumbuka::* Licha ya Mungu kuwakataza wasile na kuwaambia siku watakayokula, hakika watakufa; bado walikula tu na ikawa k**a Bwana alivyokuwa amesema. Lakini mbona waliendelea kuwa HAI, licha ya kufukuzwa bustanini? Je, walikufaje? Well, walitengana na Mungu, kukawa na mpaka kati yao na Mungu. *Ooooh, kumbe kufa ilimaanisha kutengana, kuwa na uadui na Mungu; Na mauti ya mwili ni matokeo tu.*

*Swali lingine la kujiuliza ni kwa nini Mungu aliwazuia kwenda kwenye njia ya mti wa Uzima?*

*Mwanzo 3::*
Baada ya kumfukuzia mbali Adamu, Mungu akaweka makerubi mashariki ya Bustani ya Edeni, pamoja na upanga wa moto ukimulika huku na huko kulinda njia ya kuuendea mti wa uzima.

Kumbuka Mti wa Uzima ni Yesu Kristo. Na Yesu alisema Mimi ndimi Njia, Kweli na Uzima na pia biblia inasema pasipo utakatifu hakuna anayemwona Mungu, So Akina Adamu hawakutakiwa kumkaribia Mungu aliye Mtakatifu wakiwa katika hali ya dhambi!

Siku zote kwa kuwa mwanadamu aliumbwa aabudu, anapokosa cha kuabudu, hakika atajifanyia mungu wake hata k**a ni kuchonga kinyago ama kufinyanga chochote kwani moyo wake utakuwa katika hali ya kiu k**a asipoabudu.

*Kutoka 32::*

1 Watu walipoona kuwa Mose amekawia sana kushuka kutoka mlimani, walimkusanyikia Aroni na kumwambia, “Njoo, tutengenezee miungu itakayotutangulia. Kwa maana huyu jamaa yetu Mose aliyetupandisha kutoka Misri, hatujui jambo lililompata.”

2 Aroni akawajibu, “Vueni vipuli vya dhahabu ambavyo wake zenu, wana wenu na binti zenu wamevaa, mkaniletee.”

3 Kwa hiyo watu wote wakavua vipuli vyao, wakavileta kwa Aroni.

4 Akavichukua vile vitu walivyomkabidhi, akavifanyiza kwa kusubu sanamu yenye umbo la ndama, akaichonga kwa kutumia chombo. Kisha wakasema, “Hii ndiyo miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”

5 Aroni alipoona hili, akajenga madhabahu mbele ya yule ndama na kutangaza, “Kesho kutakuwa na sikukuu kwa Bwana.”

6 Kwa hiyo siku iliyofuata watu wakaamka asubuhi na mapema na kutoa sadaka za kuteketeza na sadaka za amani. Baadaye watu wakaketi kula na kunywa, nao wakasimama, wakajizamisha
katika sherehe.

Hawa ni wana wa Israel ambawo tunaona baada ya kukaa muda mrefu bila kuabudu, walipatwa na KIU YA KUABUDU. But kwa bahati mbaya sana hawakuwa na Mungu wao binafsi ndani ya mioyo yao bali walitegemea Mungu wa Musa, so kuondoka kwa Musa na kwenda kukaa huko mlimani kwa muda mrefu ilikuwa kana kwamba Mungu katoka kati yao. Na hivyo basi, walijikuta wakipatwa na KIU; na katika KIU yao hiyo, hakuwepo wa kuizimisha maana hawakuwa na Experience(Encounter) na Mungu wa Musa.

*Yohana 4::*
13 Yesu akamjibu, “Kila mtu anayekunywa maji ya kisima hiki ataona kiu tena.

14 Lakini yeyote anywaye maji nitakayompa hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele.”

15 Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, tafadhali nipe maji hayo ili nisipate kiu tena na wala nisije tena hapa kuteka maji!”

Ni sawa sawa na wewe unajikuta tu una uhitaji/shauku na kitu/jambo fulani uncontrollably( bila kujikontro), matokeo yake unaweza kujikuta ukifanya kila linalowezekana ili tu kujiridhisha( to satisfy) nafsi yako na uwe na amani. Hiki ndicho kilichokuwa kimewatokea wenzetu.

But kwa bahati mbaya Uhitaji( KIU) hiyo haikuwapelekea kwenye Njia sahihi bali upotevuni! Ni kweli kwamba kuabudu huwa kunampa mtu *amani* moyoni mwake, but amani ya kweli hupatikana tu pale mtu anapomuabudu Mungu wa kweli, amani nyingine mbali ya Yesu, ni feki( ni ya muda tu, it is not genuine). Kuabudu miungu mingine ama vitu kunaweza kumpa mtu amani but si ya kudumu( si halisi, haina uzima ndani yake)!

*Yohana 14:27*

Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo k**a ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.

*Je, amani ya Mungu wa kweli imo ndani yako na pamoja nawe?*

K**a tulivyoona hapo mwanzo, kwa sababu ya uwepo wa nafasi wazi ya Mungu ndani ya moyo wa mtu, ikiwa huyo mtu hatomwabudu Mungu halisi, atajikuta tu kwa kutaka ama kutokutaka; kwa kujua ama kutokujua akiabudu mungu mwingine, miungu ya kigeni ama vitu vingine vya kidunia zaidi. Why? Ni kwa sababu, tuliumbwa tuabudu.

Je, kwenye hiyo nafasi ya kuabudu umeweka nini, umemweka nani? Je umemweka Mungu Halisi ama kitu ama pesa? Ni rahisi sana mtu kupata uzito ama kutokujisikia msukumo ndani yake wa kwenda ibadani na badala yake muda huo akautumia kuangalia movie na akapata amani kabisa. But, hii ni amani ya kweli, na je, yatoka kwa Mungu; ndio Kristo Yesu alitupa na kutuachia??

*Mungu wetu ni Mungu mwenye wivu, hawezi kushare moyo( nafasi) na mungu mwingine, sanamu, kitu na kadhalika. Mungu anataka apate nafasi nzima ndani yetu. Je, uko tayari kumpa Mungu Halisi nafasi moyoni mwako na atawale Yeye tu na si kinginecho??*

Hakuna mwenye mwili yeyote anayeweza kumwabudu Mungu Halisi katika roho na kweli pasipo kusaidiwa na kuongozwa na Roho Mtakatifu kwani tunamjua Yesu kupitia Roho Mtakatifu na tumemjua Baba kupitia Yesu.

*So, take your time( chukua muda wako) na utafakari, mwulize Roho Mtakatifu hivi nani yuko na kontro ya moyo wangu, je ni Mungu wa kweli, ama ni vitu viharibikavyo vya duniani??*

*Yohana 3:30*
Basi hii furaha yangu imetimia. Yeye[Yesu] hana budi kuzidi, bali mimi kupungua.

*Amen, Mungu awabariki na kuwaongezea mipaka kwa Jina la Yesu Aliye Hai*

*By Elisha*

Address

Kibaha

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mafundisho ya Neno la Mungu, Maombi Na Maombezi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Mafundisho ya Neno la Mungu, Maombi Na Maombezi:

Share

Category