SAA YA WASHINDI YA JCC

SAA YA WASHINDI YA JCC Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from SAA YA WASHINDI YA JCC, Religious organisation, Kibaha.

Katika group hili utajifunza lakini pia unaweza kuuliza maswali,na pia tunaweza kuwa na mjadala wa baadhi ya mambo ya kiroho.Karibu umwalike na mwingine kujiunga kwenye group hili.Tafadhali lugha isiyo na maadili usiitumie,Amina.

Wafilipi 2:12[12]Basi, wapendwa wangu, k**a vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi san...
04/03/2026

Wafilipi 2:12
[12]Basi, wapendwa wangu, k**a vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.

Wherefore, my beloved, as ye have always obeyed, not as in my presence only, but now much more in my absence, work out your own salvation with fear and trembling.

MJUE SANA MUNGU ILI UWE NA AMANI.   AYUBU 22:21Matokeo ya Wakristo wengi wa kanisa la leo,kukosa mwelekeo wa  kiimani,in...
12/05/2025

MJUE SANA MUNGU ILI UWE NA AMANI.

AYUBU 22:21
Matokeo ya Wakristo wengi wa kanisa la leo,kukosa mwelekeo wa kiimani,inatokana na kutokumjua Mungu wanayemwabudu.Wengi wao walikimbilia kwenye nyumba za ibada ili wakutane na wachungaji wa kuwalisha maarifa ya kumjua Mungu lakini kwa bahati mbaya wakakutana na vipofu wenzao na kujikuta wametumbukizwa shimoni.(Luka 6:39-40).
Kwahiyo k**a kila mtu anapaswa kuhitimu kulingana na mwalimu wake,uwe na uhakika kwamba ukiangukia kwa mwalimu kipofu utabakia kuwa kipofu na hii ndio hali ya wakristo wengi wa leo.Maandiko nayo hayafichi kuhusu ukweli huu k**a ilivyoandikwa kwenye kitabu cha nabii Isaya,(Isaya 56:10-11).
Mtume Paulo alishangaa sana alipofika Athens huko Ugiriki kuwaona watu wakiwa bize kwenye ibada huku wanaye mwabudu wakiwa hawamjui,na hakusita kuwaarifu ya kuwa yuko tayari kuwahuburia habari za Mungu yule ambao wao wanamwabudu bila kumjua,(Matendo 17:22).
Yesu naye alipokutana na mwanamke mMsamaria katika kisima cha Yakobo,aligundua kuwa mwanamke huyo na jamii yake wamekuwa wakimwabudu Mungu bila kumjua kwa muda mrefu sana na Yesu alikuwa tayari kumpa tumaini yule mama la kumjua Mungu wa wokovu wao,k**a ilivyoandikwa kwenye injili ya ,(Yohana 4:21-25).
Kwahiyo kumwabudu Mungu bila kumjua ni sawa na mlemavu anayetegemea fimbo kwa ajili ya kutembea,siku fimbo hiyo ikiondolewa kwako huweze tena kutembea na utajikuta uko palepale.Kwahiyo ndio maana Ayubu anasema,"Mjue sana Mungu ili uwe na amani;Ndivyo mema yatakavyo kujia"
*Ayubu 22:21*
Katika ulimwengu huu k**a humjui Mungu wako na unatembea kwa kumjua
-Mungu wa mchungaji wako pekee, au
-Mungu wa rafiki yako pekee au
-Mungu wa baba yako na mama yako tu,
Nataka nikwambie huwezi kuwa na amani ya kweli,kwasababu siku mchungaji wako akikuacha au familia yako ikikuacha ndo utahisi Mungu amekuacha na kubaki peke yako.Ndo maana tuna watu wengi leo ambao wamekataa njia ya kweli kwasababu ya wazazi wao,haya yote ni matokeo ya kutokumjua Mungu wa kweli.
Kwa leo wacha tuishie hapa kwenye somo hili zuri alilotupa Kristo,tutaendelea wakati ujao,Amina.

07/05/2025
SIRI ILIYOFICHWA NDANI YA PASAKA.UTANGULIZIBwana Yesu asifiwe uliyepewa neema na Kristo Yesu.Mungu amenipa neema kubwa k...
06/04/2025

SIRI ILIYOFICHWA NDANI YA PASAKA.
UTANGULIZI
Bwana Yesu asifiwe uliyepewa neema na Kristo Yesu.Mungu amenipa neema kubwa kukuletea habari njema za ufalme wa Mungu katika dunia hii ya sasa inayopoteza kwa kasi masikio ya kuisikia kweli ya Mungu,Amina.

Watu wengi katika ulimwengu huu wamekuwa wakiisikia na kuisherehekea Pasaka k**a sherehe zingine tu za kawaida,lakini hawajawahi kuijua siri iliyoko ndani yake.Mtu yeyote awe kiongozi wa dini au mfuasi wa kawaida wa Yesu,ukimuuliza kuhusu pasaka anachoweza kukueleza ni kuhusu pasaka ya Israel kutoka utumwani Misri au kufa na kufufuka kwa Yesu,basi

Leo,Yesu amenipa neema mimi k**a mtumwa wake nikufunulie SIRI ILIYOFICHWA NDANI YA PASAKA ambayo bila shaka hujawahi kukutana nayo,Amina.

1:PASAKA NI NINI ?
Pasaka ni NGUVU ya UKOMBOZI ya kuyatoa majeshi ya Mungu utumwani kwa njia ya mzaliwa wa kwanza.

Jina PASAKA linatokana na Neno la kiingereza "PASS OVER" likiwa na maana "PITA JUU YA", na limezaliwa kutoka kwenye tukio la Mungu kupita juu ya nyumba za Waisraeli bila kuwaangamiza wakati alipokuwa akipita kati ya Misri.
*Kutoka 12:10-13*
Lile neno linalo someka ni ,"Ni pasaka ya Bwana" katika mstari 11 kwa lugha ya kiingereza linasomeka, "It is the Lord's pass over",yaani, "usiku wa Mungu kupita ".
Sikukuu hii pia chini ya torati ya Musa ilikuwa inaitwa siku kuu ya mikate isiyotiwa chachu.
*Kutoka 12:14-17, Luka 22:1-2*
Sasa,zipo pasaka za aina mbili na dunia imeshindwa kuzibainisha na kuwajulisha wanadamu wa kizazi hiki katika ibada ya nne ya Agano Jipya kwamba ni Pasaka ipi iliyo ya kweli.Pasaka hizi mbili ni:
-Pasaka ya ibada ya tatu,chini ya torati ya kuhani mkuu wa kanisa la tatu,yaani Musa.
*Matendo 7:35-39*
Huyu Musa ndiye aliyekuwa kiongozi mkuu wa ukombozi wa kanisa la jangwani lenye ibada ya tatu.
~Pasaka nyingine ni Pasaka ya kanisa la nne chini ya kuhani Mkuu Yesu na mjumbe mpya wa Agano jipya lenye ibada ya nne.
*Ebrania 8:1-3 *
Pasaka hii iko chini ya Agano la Neema na kweli sio torati tena.*Yohana 1:17*
Hizi ni Pasaka mbili tofauti na zimebeba utukufu tofauti pia.Kwahiyo,k**a bado unaadhimisha pasaka ya Israeli kutolewa Misri uwe na uhakika huijui pasaka na hujawahi kuwa na Pasaka maishani mwako.
TOFAUTI YA PASAKA YA IBADA YA TATU NA ILE YA IBADA YA NNE YA AGANO JIPYA.

Pasaka hizi mbili zina tofauti kubwa na maagano tofauti kabisa,na hapa ndipo siri ilipo kuhusu pasaka.Tuanze kuangalia sasa:
I:Pasaka ya ibada ya tatu.
~Hii ilikuwa ni Pasaka ya kuyatoa majeshi ya Mungu kutoka kwenye utumwa wa Misri kwa njia ya mzaliwa wa kwanza.
* Kutoka 12: 41 - 42 *
~ Kwenye Pasaka hii mzaliwa wa kwanza alikuwa ni wazaliwa wa kwanza wote wa Misri wa binadamu na wa wanyama.
*Kutoka 12 :12 , Zaburi 136:10-11*
~Pasaka hii ya ibada ya tatu haikushughulika na utumwa wa dhambi zaidi ya utumwa wa Misri.Kwahiyo Israeli walitoka kwenye utumwa wa Misri ila mauti ya milele iliyotokea Edeni ya Adamu wa kwanza ilibaki palepale.
*Ebrania 9:1-10,Yohana 6 :49-50*

~ Pasaka hii ya ibada ya tatu ilikuwa ni kwa ajili ya Wayahudi au taifa la Israeli peke yao,haikuwa husu watu wa mataifa kwakuwa walikuwa bado hawana Agano na Mungu Mwenyezi.
*Kutoka 4: 22-23*
Hii ndiyo pasaka ya kanisa la tatu jangwani lenye ibada ya tatu chini ya kuhani mkuu Musa kupitia agano la torati.

Nataka leo tuishie hapa ili upate muda mzuri wa kutafakari haya machache.Namuomba Mungu azitume baraka tele juu yako popote ulipo kwa kutenga muda wako wa kufuatilia somo hili lenye siri kubwa.Ikiwa tupo pamoja ningefurahi maoni yako au maswali ili kunipa nguvu ya kusonga mbele na somo hili.Amani ya Kristo Yesu iwe nawe na kukufunika kwa Jina la Yesu unapojiandaa na Pasaka mwezi huu,Amina

Yoshua 1:7-87 Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu...
25/03/2025

Yoshua 1:7-8
7 Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kuume, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako.

8 Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.

Ni imani yangu kuwa umesoma kwa umakini mkubwa Neno hili,na Mungu wa mbinguni akupatie haja yako sawa sawa na ulivyo amini ,kwa Jina la Yesu.

NGUVU YA DHIKI INAVYOWEZA KUIUA IMANI YAKO.SEHEMU YA 2Amani iwe nawe uliyebarikiwa na Kristo Yesu.Namshukuru Mungu kwa a...
13/03/2025

NGUVU YA DHIKI INAVYOWEZA KUIUA IMANI YAKO.

SEHEMU YA 2
Amani iwe nawe uliyebarikiwa na Kristo Yesu.Namshukuru Mungu kwa ajili yako uliye "like" au ku "comment" katika sehemu ya kwanza ya somo hili.Hiyo ni ishara kwamba umesoma ujumbe huu wa Neno la Mungu,Mungu akubariki sana kwa kuendelea kuwa nami kwenye kazi hii,Amina.

Leo tunaendelea na ujumbe huu ambao naamini kuna kitu utajifunza na kupona ikiwa utaendelea kuufuatilia.

MIFANO YA WATU AMBAO IMANI ZAO ZILIUAWA NA DHIKI NDANI YAO.

Wapo watumishi wa viwango vya juu vya kiungu lakini dhiki ilifanikiwa kutikisa imani zao kabisa kiasi ambacho huwezi kuamini.Kwa mfano:

1:Yohana Mbatizaji.
~Wasomaji wa Neno wanakumbuka kwamba Yohana ndiye aliye paza sauti na kuudhihirishia ulimwengu huko Yordani kwamba yule aliyeingia majini na kumbatiza ni Masihi wa BWANA na kwamba hawezi kumbatiza kwakuwa yeye anahitaji kubatizwa na Yesu sio yeye kumbatiza Yesu.(Mathayo 3:13-17).

Lakini Yohana huyu huyu baada ya kupata dhiki ya kuk**atwa na Herode mfalme na kuwekwa gerezani,kuna jambo la ajabu sana na la kushangaza tunalisikia toka kwake.Neno Mungu linaeleza kuwa,wakati akiwa gerezani,aliletewa habari na wanafunzi wake kuhusu mahubiri ya Yesu na miujiza iliyokuwa inafanyika.
Yohana anatuma wanafunzi wake eti wakamuulize Yesu kwamba yeye ndiye Masihi kweli au wamngoje mwingine?
(Mathayo 11:1-11).
Tunajiuliza je,ile imani imetowekaje tena ya kutokumwamini mtu aliye mthibitisha mwenyewe kwamba ndiye Masihi? Dhiki imesababisha Yohana imani yake iingie mashakani,kivipi?
Yohana alitegemea kwamba ,kuk**atwa kwake na kuwekwa gerezani,Yesu atakuja kumwokoa na kumtoa gerezani,lakini cha ajabu licha ya Yesu kujua Yohana yuko gerezani ,yeye aliendelea kuhubiri injili wala hakwenda kumtoa gerezani.Sasa ,Yesu hakwenda kwasababu isingewezekana kuzuia kikombe anachopata kukinywea Yohana ili mapenzi ya Mungu yatimizwe.
Hapa ndipo wana wa Mungu wengi wamefia kiimani.Hawatangulii kulitafuta kusudi la Mungu kwenye mitihani wanayokutana nayo bali macho yao yanakimbilia kutafuta watu ambao wameshindwa kuwa nao kwenye mitihani hiyo ili wawasaidie.Nataka nikwambie,k**a kikombe unachokutana nacho kimeruhusiwa na Mungu,usitegemee kuipata faraja na tumaini kwa wanadamu kwakuwa mioyo yao itatiwa usingizi na uzito wa kukusaidia.Ndo maana tumetangulia kuona huko mwanzo kwamba ,Yesu bustanini aliwashirikisha wanafunzi wake waombe pamoja naye lakini mara tatu zote aliporudi kuwatazama k**a wanaomba,cha ajabu anakuta wamechapa usingizi.Yawezekana naongea na mtu hata sasa ambaye ameamua kuacha imani kwakuwa watu wamemwacha peke yake bila kujali anachopitia,k**a unataka kupona,usiwatazame hao watu mtazame Mungu na umwone Mungu.

Kumbuka mtihani ulioruhusiwa na Mungu,Mungu hawezi kuruhusu msaada wa mwanadamu kujiinua katikati yake,utazimwa tu ili kusudi la Mungu litimie.Kwahiyo unaweza kuwalaumu wanadamu kumbe wala hata hawajui walitendalo kwakuwa mkono wa Mungu umeingilia hilo.

Wote tunajua namna Mungu alivyo mruhusu shetani kumtesa Ayubu wakati Mungu akitaka ajitukuze kupitia Ayubu.Kila kitu kilitengwa mbali na Ayubu ,tangu mali zake,uzao wake ,marafiki zake na hata ndoa yake.Imani ya kumwamini Mungu kwa mke wa Ayubu ilipotea na kufa na akataka kuishawishi imani ya mume wake nayo ife,anamwambia hivi bado unamwamini tu huyu Mungu wako na kushik**ana naye,mkufuru ufe,(Ayubu 2:6-10).

Hapakuwa na wakumtia moyo Ayubu isipokuwa rafiki zake walizidi kumlaumu kwamba ametenda dhambi ndo maana yamempata hayo yote,(Ayubu 4:1-8).

Kwenye jambo k**a hili ukilazimisha msaada wa wanadamu utapata maneno yatakayo kuvunja moyo peke yake.Kwenye wakati na kikombe k**a hiki mtazame Mungu tu na kuililia huruma yake.Ndivyo alivyofanya Ayubu ,aliacha kubishana na watu akabakia analia na Mungu tu na mwisho akashinda.

Kwahiyo baada ya kikombe cha mateso kupita,wote na vyote vilivyo tengwa naye vilirudi.Rafiki zake walirudi kuomba msamaha na Ayubu aliagizwa awasamehe.Unajua kwanini ?.Ni kwasababu jambo hilo liliruhusiwa na mkono wa Mungu.Kwahiyo kuwa makini sana na jambo lililoruhusiwa na mkono wa Mungu kwenye kushughulika nalo,tofauti na hapo linaweza kuizika imani yako bila kujali wewe ni nani.

Nataka leo tuishie hapa ili nikuache utafakari mfano huu wa kwanza tu kwenye somo hili kabla ya kukuletea mifano mingine.Mungu akubariki kwa kuwa nami na ujumbe huu uumbe jambo jipya litakalo fufua kila imani iliyokufa au kudhoofika.
Nawasalimuni wote wapendwa wangu katika imani,na kristo Yesu aliye Bwana na Mwokozi wetu awe nanyi daima,Amina.

NGUVU YA DHIKI INAVYOWEZA   KUIUA IMANI YAKO.        SEHEMU YA KWANZA: UTANGULIZIBwana Yesu asifiwe uliye barikiwa na Bw...
13/03/2025

NGUVU YA DHIKI INAVYOWEZA KUIUA IMANI YAKO.

SEHEMU YA KWANZA: UTANGULIZI
Bwana Yesu asifiwe uliye barikiwa na Bwana.Ni neema kuu ya Mungu Mwenyezi inanileta kwako leo nikiwa nimebebeshwa ujumbe huu kwa ajili yako,na ni jukumu lako sasa kufuatilia hatua kwa hatua,Amina.

Ndugu mpendwa,watu wengi sana wokovu wao umefia wakati wa mitihani migumu ya maisha walipokutana nayo,licha ya kuanza vizuri tu awali.
Kipimo sahihi cha ukomavu wa kiroho kwa mtu ni wakati yuko katikati ya dhiki huku marafiki na ndugu wakiwa wamemwacha na kumtenga au kumkimbia na kubaki peke yake.Huu ndo wakati sahihi kujua kiwango cha imani alichonacho mtu na sio maneno mtu anayo yaongea wakati ana amani na mambo yakiwa yamemnyookea.

Wakati Yesu akiwa katika bustani ya Getsemane na dhiki kuu ikiwa imemsonga,aliona ni vema kuwashirikisha rafiki zake ambao ni wanafunzi wake ili waombe pamoja naye kwa dhiki anayoiona mbele yake.(Marko 14:32-51).
Lakini kila alipokuwa akirudi kuwatazama anakuta wameshalala zao usingizi.Kibinadamu ilikuwa rahisi kwa Yesu kuanza kulalamika na kuona hawa watu hawajali shida yake ,hawana upendo, nakadhalika.Lakini Yesu pamoja na hayo yote hakuvunjika moyo bali aliendelea kuomba mpaka aliposikia amani ndani yake ,na alipokuja mara ya tatu na kuwaambia laleni sasa.Najua hata sasa kuna watu wengi wamekata tamaa na kuacha imani au ibada kwakuwa tu hitaji lao halikubebwa kwa uzito na waumini au wanamaombi wenzao ,kisha wakajiona hawathaminiwi tena hawapendwi.Huu ndo kwao ulikuwa wakati wa kudhihirisha viwango vya imani yao,na k**a hukufanikiwa kuvuka na kusonga mbele,maana yake imani uliyokuwa nayo imeshindwa na kuuawa na dhiki uliyokuwa nayo.
Kwahiyo wakati wa dhiki tegemea kuwa:
~Kuna watu wakati unahisi unahitaji ushiriki wao kwenye dhiki hiyo ,wao ndo kwanza watakuwa bize na mambo yao tu.
~Kuna watu pia ambao walikuwa karibu sana nawe wakati wa raha watakukimbia na kujitenga nawe.
~Lakini wapo pia watakao kuwa wana kufuatilia kwa mbali ili kujua mwisho wako utakuwaje.

Ndugu mpendwa,wacha kwa leo tufikie nukta hii,na bila shaka umebarikiwa.Basi usikose kufuatilia sehemu ya pili.Ubarikiwe sana na Kristo Yesu,wa salaamu,Amina.

John 15:19(Yohana 15:19)If ye were of the world, the world would love his own: but because ye are not of the world, but ...
28/11/2024

John 15:19(Yohana 15:19)
If ye were of the world, the world would love his own: but because ye are not of the world, but I have chosen you out of the world, therefore the world hateth you.
K**a mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.

Ni kweli,wanadamu wengi wamejisahau na kuishi maisha ya udhalimu na ya kuchukiza mbele za Mungu.Ni jambo la kawaida kuona zinaa ,ulevi,mauaji,usaliti na mambo k**a hayo kukutana nayo kila kukicha.Wafanyaji wa mambo hayo ni watu wanajinasibisha kuwa wana dini nzuri tu kana kwamba wanamcha Mungu lakini kumbe ndani yao ni mbwa mwitu wakali

Dini na maneno ya kudanganywa udanganywayo na watumishi wachumia tumbo yataishia hapa hapa tu duniani au ulimwenguni.Unapaswa kutambua kuwa sisi sio wa ulimwengu huu,hivyo kuna siku utaondoka na kuyaacha yote yanayo kufanya usaliti wenzako au kuwauwa.Unapofanya maamuzi yako leo yawe ni maamuzi ya kukupa maisha mema ya leo na ya kesho.Badilika leo na umgeukie Muumba wako kwani ulimwengu huu unapita na mambo yake yote,Amina

Mchana Bwana ataagiza fadhili zake, na usiku wimbo wake utakuwa nami, Naam, maombi kwa Mungu aliye uhai wangu.~Zaburi 42...
22/11/2024

Mchana Bwana ataagiza fadhili zake, na usiku wimbo wake utakuwa nami, Naam, maombi kwa Mungu aliye uhai wangu.

~Zaburi 42:8

Usilie inuka futa machozi na usonge mbele,karibu utavuka,kwa Jina la Yesu,Amen.
22/11/2024

Usilie inuka futa machozi na usonge mbele,karibu utavuka,kwa Jina la Yesu,Amen.

Address

Kibaha

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SAA YA WASHINDI YA JCC posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share