13/03/2025
NGUVU YA DHIKI INAVYOWEZA KUIUA IMANI YAKO.
SEHEMU YA 2
Amani iwe nawe uliyebarikiwa na Kristo Yesu.Namshukuru Mungu kwa ajili yako uliye "like" au ku "comment" katika sehemu ya kwanza ya somo hili.Hiyo ni ishara kwamba umesoma ujumbe huu wa Neno la Mungu,Mungu akubariki sana kwa kuendelea kuwa nami kwenye kazi hii,Amina.
Leo tunaendelea na ujumbe huu ambao naamini kuna kitu utajifunza na kupona ikiwa utaendelea kuufuatilia.
MIFANO YA WATU AMBAO IMANI ZAO ZILIUAWA NA DHIKI NDANI YAO.
Wapo watumishi wa viwango vya juu vya kiungu lakini dhiki ilifanikiwa kutikisa imani zao kabisa kiasi ambacho huwezi kuamini.Kwa mfano:
1:Yohana Mbatizaji.
~Wasomaji wa Neno wanakumbuka kwamba Yohana ndiye aliye paza sauti na kuudhihirishia ulimwengu huko Yordani kwamba yule aliyeingia majini na kumbatiza ni Masihi wa BWANA na kwamba hawezi kumbatiza kwakuwa yeye anahitaji kubatizwa na Yesu sio yeye kumbatiza Yesu.(Mathayo 3:13-17).
Lakini Yohana huyu huyu baada ya kupata dhiki ya kuk**atwa na Herode mfalme na kuwekwa gerezani,kuna jambo la ajabu sana na la kushangaza tunalisikia toka kwake.Neno Mungu linaeleza kuwa,wakati akiwa gerezani,aliletewa habari na wanafunzi wake kuhusu mahubiri ya Yesu na miujiza iliyokuwa inafanyika.
Yohana anatuma wanafunzi wake eti wakamuulize Yesu kwamba yeye ndiye Masihi kweli au wamngoje mwingine?
(Mathayo 11:1-11).
Tunajiuliza je,ile imani imetowekaje tena ya kutokumwamini mtu aliye mthibitisha mwenyewe kwamba ndiye Masihi? Dhiki imesababisha Yohana imani yake iingie mashakani,kivipi?
Yohana alitegemea kwamba ,kuk**atwa kwake na kuwekwa gerezani,Yesu atakuja kumwokoa na kumtoa gerezani,lakini cha ajabu licha ya Yesu kujua Yohana yuko gerezani ,yeye aliendelea kuhubiri injili wala hakwenda kumtoa gerezani.Sasa ,Yesu hakwenda kwasababu isingewezekana kuzuia kikombe anachopata kukinywea Yohana ili mapenzi ya Mungu yatimizwe.
Hapa ndipo wana wa Mungu wengi wamefia kiimani.Hawatangulii kulitafuta kusudi la Mungu kwenye mitihani wanayokutana nayo bali macho yao yanakimbilia kutafuta watu ambao wameshindwa kuwa nao kwenye mitihani hiyo ili wawasaidie.Nataka nikwambie,k**a kikombe unachokutana nacho kimeruhusiwa na Mungu,usitegemee kuipata faraja na tumaini kwa wanadamu kwakuwa mioyo yao itatiwa usingizi na uzito wa kukusaidia.Ndo maana tumetangulia kuona huko mwanzo kwamba ,Yesu bustanini aliwashirikisha wanafunzi wake waombe pamoja naye lakini mara tatu zote aliporudi kuwatazama k**a wanaomba,cha ajabu anakuta wamechapa usingizi.Yawezekana naongea na mtu hata sasa ambaye ameamua kuacha imani kwakuwa watu wamemwacha peke yake bila kujali anachopitia,k**a unataka kupona,usiwatazame hao watu mtazame Mungu na umwone Mungu.
Kumbuka mtihani ulioruhusiwa na Mungu,Mungu hawezi kuruhusu msaada wa mwanadamu kujiinua katikati yake,utazimwa tu ili kusudi la Mungu litimie.Kwahiyo unaweza kuwalaumu wanadamu kumbe wala hata hawajui walitendalo kwakuwa mkono wa Mungu umeingilia hilo.
Wote tunajua namna Mungu alivyo mruhusu shetani kumtesa Ayubu wakati Mungu akitaka ajitukuze kupitia Ayubu.Kila kitu kilitengwa mbali na Ayubu ,tangu mali zake,uzao wake ,marafiki zake na hata ndoa yake.Imani ya kumwamini Mungu kwa mke wa Ayubu ilipotea na kufa na akataka kuishawishi imani ya mume wake nayo ife,anamwambia hivi bado unamwamini tu huyu Mungu wako na kushik**ana naye,mkufuru ufe,(Ayubu 2:6-10).
Hapakuwa na wakumtia moyo Ayubu isipokuwa rafiki zake walizidi kumlaumu kwamba ametenda dhambi ndo maana yamempata hayo yote,(Ayubu 4:1-8).
Kwenye jambo k**a hili ukilazimisha msaada wa wanadamu utapata maneno yatakayo kuvunja moyo peke yake.Kwenye wakati na kikombe k**a hiki mtazame Mungu tu na kuililia huruma yake.Ndivyo alivyofanya Ayubu ,aliacha kubishana na watu akabakia analia na Mungu tu na mwisho akashinda.
Kwahiyo baada ya kikombe cha mateso kupita,wote na vyote vilivyo tengwa naye vilirudi.Rafiki zake walirudi kuomba msamaha na Ayubu aliagizwa awasamehe.Unajua kwanini ?.Ni kwasababu jambo hilo liliruhusiwa na mkono wa Mungu.Kwahiyo kuwa makini sana na jambo lililoruhusiwa na mkono wa Mungu kwenye kushughulika nalo,tofauti na hapo linaweza kuizika imani yako bila kujali wewe ni nani.
Nataka leo tuishie hapa ili nikuache utafakari mfano huu wa kwanza tu kwenye somo hili kabla ya kukuletea mifano mingine.Mungu akubariki kwa kuwa nami na ujumbe huu uumbe jambo jipya litakalo fufua kila imani iliyokufa au kudhoofika.
Nawasalimuni wote wapendwa wangu katika imani,na kristo Yesu aliye Bwana na Mwokozi wetu awe nanyi daima,Amina.