Living Word For All Nations Int’l Ministry

Living Word For All Nations Int’l Ministry Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Living Word For All Nations Int’l Ministry, Religious organisation, Kibaha.

Huduma Kwaajili Ya Kulitangaza Neno La Mungu Ulimwenguni Kote Wapate Kumfahamu Yesu Na Kumpokea

Matendo ya Mitume 20:20 ya kuwa sikujiepusha katika kuwatangazia neno lo lote liwezalo kuwafaa bali naliwafundisha waziwazi, na nyumba kwa nyumba,

*SOMO: K**A YEYE ALIVYO ~ 6/11/2024*📖📖*1 Yohane‬ ‭4‬:‭17‬ ‭BHND‬‬**…………..kwani maisha yetu hapa duniani ni k**a yale ya ...
06/11/2024

*SOMO: K**A YEYE ALIVYO ~ 6/11/2024*

📖📖*1 Yohane‬ ‭4‬:‭17‬ ‭BHND‬‬*
*…………..kwani maisha yetu hapa duniani ni k**a yale ya Kristo*
‭‭
TAFAKARI 👇

Inaweza Kukustaajabisha Unaposikia Maisha Yetu Ni Sawa Na Maisha Ya Bwana Yesu Alipokuwa Dunia. Unaweza Jiuliza Ni Kwa Namna Gani Hili Linawezekana Au Linatendeka? Lakini Hii Isikupe Mashaka, Huo Ndio Uhalisia, Aina Ya Maisha Aliokuwa Nayo Bwana Yesu, Yenye Sifa Ya Utawala Mkamilifu Na Uzoefu Wa Ushindi Dhidi Ya Kila Hali, Ndio Aina Ya Maisha Tuliopewa Na Tunayopaswa Kuishi K**a Watoto Wa Mungu; Bwana Yesu Alitamka Maneno Haya Wakati Wa Sala Yake Kwa Mungu Kwaajili Ya Watu Wote, Alisema; {*Yohana 17:22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja k**a sisi tulivyo umoja*} Tunayo Aina Moja Na Maisha Na Kristo, Asili Kamili Sawa Nae Ipo Ndani Yetu, Maisha Yetu Yanasifa Ya Ushindi, Ukuu, Ubora, Mafanikio, Utoshelevu, K**a Yeye Kristo Yesu, Alivyo!

MAOMBI 🙏

Asante Baba Kwaajili Ya Maisha Ya Bwana Yesu Kristo, Asante Kwa Kunipatia Asili Moja Nae. Naishi Katika Ubora Na Uweza Mkuu Sana Sawa Nae. Nikipokea Matokeo Yenye Uzoefu Sawa Kristo, Ambayo Ni Matokeo Ya Ushindi Na Ustawi Siku Zote, Katika Jina La Bwana Yesu, Amen!

Please Follow
Twitter :
Insta : &
Whatsapp : https://chat.whatsapp.com/Fd5pMyi0P9J7WvDnQ3hXCZ
Facebook : Word For All Nations Int’l Ministry

MINISTER HERY INOCENT
0620141375

*SOMO; MJONGEZI KINYWANI MWAKO – 31/10/2024* 📖📖*Zaburi 141;3**Ee Bwana, uweke mlinzi kinywani pangu, Mngojezi mlangoni p...
31/10/2024

*SOMO; MJONGEZI KINYWANI MWAKO – 31/10/2024*

📖📖*Zaburi 141;3*
*Ee Bwana, uweke mlinzi kinywani pangu, Mngojezi mlangoni pa midomo yangu*

TAFAKARI

Daudi katika kutaka na kutamani kuendelea kutembea katika mpango mkamilifu wa Mungu anafahamu shida / changamoto au zuio linaloweza kukwamisha safari yake ya kimahusiano na Mungu. Anabaini wazi kwa yeye kuwa mtu mwenye maneno mengi na muongeaji pasipo kujizuia anaweza kujikuta katika kumkosea Mungu na kuharibu mahusiano yake nae. Unapaswa kufahamu kuwa, hata katika agano jipya maandiko yanazungumza kitu kuhusu matamko yetu pale linapozungumza Zaidi kuhusu ulimi, inasema *Yakobo 3;6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfululizo wa maumbile, nao huwashwa moto jehanam* Weka zuio wa maneno ya kutamka, muombe Mungu kila siku akuongoze kwa Roho wake mtakatifu katika kuzungumza maneno sahihi, ili kwamba ujiepushe na kumkosea na kuharibu hatima yako kwa maneno yako mwenyewe. Ulimi ni moto.
Daudi akamuomba Mungu amuweke mlinzi kinywani mwake, mjongezi yaani asiwe mtu wa maneno mengi kwa kinywa chake. Huo ni wakati ambao uwepo wa Roho wa MUngu ulikuwa haujadhihirika k**a hivi sasa, hivyo kwa nafasi tuliopo sasa tunaweza kunufaika nae. Tukawa salama kwa msaada wake huku tukiendelea kujaza neno lake moyoni mwetu ili tuwe na matamko sahihi. Haleluya!

MAOMBI
Asante baba mpendwa kwa wingi wa neema na baraka zako katika masiha yangu, asante kwa Roho wako mtakatifu, ambaye ananiongoza katika matamko sahihi na mjongeo wa kinywa changu. Natamka baraka na mafanikio katika Maisha yangu, na ninanufaika kwa matamko sahihi. Amen!

Please Follow
Twitter :
Insta : &
Whatsapp : https://chat.whatsapp.com/Fd5pMyi0P9J7WvDnQ3hXCZ
Facebook : Word For All Nations Int’l Ministry

MINISTER HERY INOCENT
0620141375

*SOMO: ONESHA SHAUKU YAKO NA UHITAJI ~ 30/10/2024*📖📖*Habakuki‬ ‭2‬:‭1‬ ‭BHND‬‬**Mimi nitasimama mahali pa kuchungulia, n...
30/10/2024

*SOMO: ONESHA SHAUKU YAKO NA UHITAJI ~ 30/10/2024*

📖📖*Habakuki‬ ‭2‬:‭1‬ ‭BHND‬‬*
*Mimi nitasimama mahali pa kuchungulia, na kukaa juu mnarani; nitakaa macho nione ataniambia nini, atajibu nini kuhusu lalamiko langu*
‭‭
TAFAKARI 👇

Kitabu Cha Mika 7:7 Inasema;- *Lakini mimi, nitamtazamia BWANA; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia*
Mungu Wetu Ni Muaminifu Katika Njia Zote Na Mkamilifu Milele Yote. Tumuombapo Anasikia Na Anatujibu Mara Tu Tumuombapo, Lakini Katika Kupokea Majawabu Husika Tunatofautiana, Umejaribu Kulitazama Na Kulitafakari Hili? Jibu Ni Hili Hapa {* 1 Yohana 5:14 Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia*} Baadhi Ya Majawabu Hukawia Kwasababu Ya Muitikio Wa Muhusika Baada Na Kabla Ya Kupeleka Hoja Zake Kwa Mungu, Hii Inatokana Na Kile Kinachoitwa Shauku Na Mtazamo Juu Ya Mungu Na Kile Ulichokiomba. Je Unayo Mashaka Na Mungu? Unafikiri Uzito Wa Changamoto Yako Na Mazingira? Hupaswi Kuwa Na Mtazamo Huo, Kuwa Katika Hali Sawa Na Huo Mtazamo Wa Mstari Wa Ufunguzi, Unapokuwa Katika Kumuomba Mungu Na Baada Ya Kufanya Hivyo, Kuwa Katika Shauku Ya Kupokea Na Kuamini Kuwa Hakika Mungu Amekujibu. Mara Zote Tarajia Majibu Kana Kwamba Msafiri Aliyekituo Cha Basi Anasubiri Gari, Mara Zote Mtu Huyu Ataishi Kwa Imani Na Shauku Kubwa Kuwa Usafiri Utafika Mara Tu, Nae Ataelekea Katika Safari Yake. Haleluya! Kuwa Na Shauku Ya Kupokea Majibu, Haleluya!

MAOMBI 🙏

Imani Yangu Imeimarika Maradufu, Ninayo Shauku Ya Kiungu Inielekezayo Katika Kupokea Matokeo Chanya Na Ya Faida Siku Zote. Naishi Maisha Ya Matokeo Na Manufaiko Makuuu Katika Jina La Bwana Yesu Kristo, Amen!

Please Follow
Twitter :
Insta : &
Whatsapp : https://chat.whatsapp.com/Fd5pMyi0P9J7WvDnQ3hXCZ
Facebook : Word For All Nations Int’l Ministry

MINISTER HERY INOCENT
0620141375

*SOMO; SI MIMI TENA, BALI KRISTO ~ 24/10/2024*📖📖*Wagalatia 2:20 BHND**na sasa naishi, lakini si mimi tena, bali Kristo a...
24/10/2024

*SOMO; SI MIMI TENA, BALI KRISTO ~ 24/10/2024*

📖📖*Wagalatia 2:20 BHND*
*na sasa naishi, lakini si mimi tena, bali Kristo anaishi ndani yangu. Maisha haya ninayoishi sasa naishi kwa imani, imani katika Mwana wa Mungu aliyenipenda hata akayatoa maisha yake kwa ajili yangu*

TAFAKARI 👇

Maisha Mapya Ndani Ya Ufalme Tunaishi Kwa Kumuwakilisha Kristo Katika Utendaji Wa Kila Siku. Kutenda Kwetu Na Kufanya Lolote Katika Mwili Ni Sisi Lakini Kristo Alieahidi Kuwa Nasi Mpaka Mwisho Wa Dahari, Anawakilishwa Na Roho Wake Ndani Yetu, Yeye Ndiye Mtendaji Mkuu Na Muongozaji Wa Maisha Ya Wana Wa Mungu. Inawezekana Usione Msisimuko Au Hisia Fulani Kuwa Ndiye Kristo Akuongozaye Na Anaishi Ndani Yako Lakini Hio Haiondoi Uhalisia Huu Kuwa Ndiye Yeye Anaeishi Ndani Yetu, Kwakuwa Hatuishi Kwa Hisia, Wala Mihemko. Kinachotupa Uhakika Wa Haya Yote Ni Imani Tulionayo Kwa Kristo Yesu. Tunaishi Kwa Imani Ya Yote Yaliyosemwa Na Huo Ndio Uhalisia. Hivyo Basi Sasa Tunajuwa Tunasifa Ya Kuishi Sawa Saww Na Kristo, Maisha Yenye Sifa Sawa, Ikiwemo, Uzima, Uungu, Mafanikio, Ustawi, Matokeo Chanyw Siku Zote Nw Ushirika Kamili Wa Baba. Kristo Ndani Yetu Ni Uhai Na Uzima, Pia Ni Tumaini La Utukufu.

MAOMBI 🙏

Asante Baba Mpendwa Kwa Kuwa Upo Ndani Yangu, Kuishi Kwangu Na Kutenda Ni Wewe Katika Utendaji, Naishi Katika Baraka, Mafanikio, Ongezeko, Usalama Na Ustawi, Kwakuwa Kristo Ndani Yangu Ni Tumaini La Utukufu.

Please Follow
Twitter :
Insta : &
Whatsapp : https://chat.whatsapp.com/Fd5pMyi0P9J7WvDnQ3hXCZ
Facebook : Word For All Nations Int’l Ministry

MINISTER HERY INOCENT
0620141375

*SOMO; KWA KUUNGANA NAE YAMEFANYIKA ~ 20/10/2024*📖📖*Waefeso‬ ‭1‬:‭3‬-‭4‬ ‭BHND‬‬**Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Y...
20/10/2024

*SOMO; KWA KUUNGANA NAE YAMEFANYIKA ~ 20/10/2024*

📖📖*Waefeso‬ ‭1‬:‭3‬-‭4‬ ‭BHND‬‬*
*Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Maana, katika kuungana na Kristo ametubariki kwa kutujalia zawadi zote za kiroho mbinguni. Kabla ya kuumbwa ulimwengu, Mungu alituteua tuwe wake katika kuungana na Kristo ili tuwe watakatifu na bila hitilafu mbele yake. Kwa sababu ya upendo wake*
‭‭
TAFAKARI 👇

Yapo Mambo Yalifanyika Mara Tu Tulipokubali Kuungana Na Kristo Kupitia Ukiri Wa Wokovu. Mabadiliko Makubwa Ya Mafanikio Na Faida Kwetu Yalichukuwa Nafasi. Unapaswa Kuwa Unafahamu Kuwa Mabadiliko Haya Yalifanyika Mara Tu Ulipomkiri Bwana Yesu Kuwa Ndiye Bwana Na Mwokozi Wa Maisha Yako, Katika Roho Uliamishwa Mara Tu Na Kuwa Na Aina Mpya Ya Maisha Yaliyo Na Asili Moja Ya Kristo Sambamba Na Kuitwa Katika Ushirika Wa Kiungu. Faida Zilizopatikana Ni Pamoja Na Kupewa Baraka Zoote Za Rohoni K**a Zawadi, Hakuna Baraka Iliofichwa Au Kuwekwa Mbali Ama Utakayopewa Kwa Wakati Ujao Bali Mara Tu Ulipokiri Ulipewa Baraka Hizo. Jambo Jingine Zuri Lililochukuwa Nafasi Ni Ungano Takatifu Sambamba Nae, Tunayo Mahusiano Mazuri Maradufu Na Mungu Hivi Sasa, Nae Ametupa Nafasi Ya Kuwa Watakatifu Wake. Hatujitahidi Kuwa Watakatifu Bali Tumekwisha Kuwa! Haleluya!

MAOMBI 🙏

Asante Baba Mpendwa Kwa Baraka Kamilifu Ulizonipatia, Hakika Naishi Katiia Hizo Na Kuishi Maisha Ya Manufaa Yasiyo Na Mashaka Ya Aina Yoyote. Naishi Katika Ongezeko Na Ustawi Na Maisha Yangu Yanamtukuza Mungu Siku Zote, Katika Jina La Bwana Wetu Yesu Kristo, Amen!

Please Follow
Twitter :
Insta : &
Whatsapp : https://chat.whatsapp.com/Fd5pMyi0P9J7WvDnQ3hXCZ
Facebook : Word For All Nations Int’l Ministry

MINISTER HERY INOCENT
0620141375

*SOMO; SITAOGOPA MABAYA, YU! PAMOJA NAWE ~ 19/10/2024*📖📖*Zaburi 23:4**Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, ...
19/10/2024

*SOMO; SITAOGOPA MABAYA, YU! PAMOJA NAWE ~ 19/10/2024*

📖📖*Zaburi 23:4*
*Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji*

TAFAKARI 👇

Daudi Katika Mstari Wa Ufunguzi Anatujenga Kwa Habari Ya Uhakika Wa Usalama Tulionao Watoto Wa Ufalme, Tuliochagua Kumtumainia Mungu. Tunapotazama Aina Ya Maisha Na Namna Alivyoishi Maisha Ya Ushindi Mstari Wa Ufunguzi Unasadifu Ukweli Wa Kilichoandikwa. Tunao Uhakika Usiokuwa Na Mashaka Juu Ya Usalama Wetu. Hakuna Kinachoweza Kuwa Kinyume Chetu Na Kikashinda. Tupo Salama, Tunachopaswa Kufanya Ni Kumuamini Yeye Awezaye Kutuokoa Na Ambaye Amebeba Jukumu La Sisi Kuwa Hai Na Salama. Hali Zako Na Mazingira Visikutishe Au Kukukatisha Tamaa, Tamka Kwamba Unatoka Nje Ya Kila Upinzani, Changamoto, Taabu, Shida Na Mazingira Kwa Jina La Bwana Yesu, Kiri Kuwa Wewe Ni Jasiri Na Huogopeshwi Na Ubaya Wowote Wa Giza! Tangaza Jina La Bwana Yesu

MAOMBI

Hakuna Changamoto Inayopata Nafasi Katika Mazingira Yangu. Siogopeshwi Na Ubaya Wowote, Hali Wala Ujanja Wowote Wa Giza. Ninatawala Na Kufanikiwa Sana Katika Kila Hali. Mimi Ni Mshindi Siku Zote, Katika Jina La Bwana Yesu Kristo, Amen

Please Follow
Twitter :
Insta : &
Whatsapp : https://chat.whatsapp.com/Fd5pMyi0P9J7WvDnQ3hXCZ
Facebook : Word For All Nations Int’l Ministry

MINISTER HERY INOCENT
0620141375

16/10/2024
*SOMO: ATAWEZESHA ONGEZEKO ~ 15/10/2024*📖📖*Isaya‬ ‭60‬:‭22‬ ‭NEN‬‬**Aliye mdogo kwenu atakuwa elfu, mdogo kuliko wote at...
15/10/2024

*SOMO: ATAWEZESHA ONGEZEKO ~ 15/10/2024*

📖📖*Isaya‬ ‭60‬:‭22‬ ‭NEN‬‬*
*Aliye mdogo kwenu atakuwa elfu, mdogo kuliko wote atakuwa taifa lenye nguvu. Mimi ndimi Bwana; katika wakati wake nitayatimiza haya upesi*

TAFAKARI 👇
‭‭
Mungu Ni Mungu Mwenye Uwezo Wote Na Ukamilifu Usioweza Kufikiriwa Wala Kupimwa. Anayosema Na Kuahidi Anaouwezo Wote Wa Kutimiza Na Hakika Atatimiza. Katika Kujenga Ufahamu Mstari Wa Ufunguzi Unaonesha Mtazamo Gani Mungu Anao Kwa Watu Wake! Inaonesha Wazi Anatazamia Zaidi Kufanya Imara Taifa Lake Na Watu Wake. Kwenye Macho Ya Mungu Hakuna Mtoto Wake Aliyedhaifu Wala Mdogo Kwani Yeye Ndiye Awezeshaye Mchakato Wa Ongezeko Na Ukuuu. Usijitazame Katikw Udogo Na Uchache, Usitazame Hali Yako Ya Sasa, Ya Kibiashara, Uchumi, Afya NK. Ishi Kwa Mtazamo Wa Ukuu Sambamba Na Kuishi Kwa Imani Kuwa Kwa Wakati Wa Mungu Utainuka Na Kustawi Sana. Kumbuka Nini Maandiko Yanasema {*Waebrania 10:38 Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye*}

MAOMBI 🙏

Mimi Ni Taifa Kubwa, Naongezeka Na Kustawi Sana Kusikoweza Kuzuiliwa. Hatua Zangu Ni Hatua Za Ushindi Na Kwenda Mbele. Nimebarikiwa Sana Na Mungu, Natembea Katika Ukamilifu Wote Wa Baraka, Ushindi Na Matokeo Chanya, Katika Jina La Bwana Yesu, Amen!

Please Follow
Twitter :
Insta : &
Whatsapp : https://chat.whatsapp.com/Fd5pMyi0P9J7WvDnQ3hXCZ
Facebook : Word For All Nations Int’l Ministry

MINISTER HERY INOCENT
0620141375

*SOMO: ONGEZEKA KWA FAIDA ~ 11/10/2024*📖📖*Luka‬ ‭8‬:‭18‬ ‭NEN‬‬**Kwa hiyo, kuweni waangalifu mnavyosikia. Kwa maana yeyo...
11/10/2024

*SOMO: ONGEZEKA KWA FAIDA ~ 11/10/2024*

📖📖*Luka‬ ‭8‬:‭18‬ ‭NEN‬‬*
*Kwa hiyo, kuweni waangalifu mnavyosikia. Kwa maana yeyote aliye na kitu atapewa zaidi. Lakini yule asiye na kitu, hata kile anachodhani anacho atanyangʼanywa*

TAFAKARI 👇

Ni Muhimu Sana Kufahamu Siri Za Ustawi Na Kuongezeka Kwaajili Ya Faida Zetu Siku Zote. Ulimwengu Hutawaliwa Na Watu Wanaomiliki Kitu, Nguvu Zinafasiriwa Na Kile Mtu Alichonacho, Utajiri Na Uwezo Unafasiriwa Pia Kwa Namna Hiyo. Na Yeyote Aliyenacho Ataendelea Kuwa Nacho Maana Waliodhaifu Hawatotawala. Mstari Wa Ufunguzi Unafungua Fursa Ya Ufahamu Juu Ya Kuongezeka Na Kustawi, Unasema, “Kuweni Waangalifu Mnavyosikia” Hapo Imefungua Siri Kubwa Kuwa Kiwango Cha Maarifa Unachoingiza Ndicho Kitakacholeta Tija Katika Ustawi Wako. Kiwango Cha Taarifa Sahihi Ndicho Kitakachokuongoza Katika Kweli Yote. Kwetu Tunaoishi Ndani Ya Kristo Tunafahamu Kuwa, Tunachopaswa Kusikia Na Kuingiza Zaidi Kwenye Roho Yetu Ni Maarifa Ya Neno La Mungu. Kuwa Na Maarifa Ya Neno Huleta Mwanga Na Nuru Ya Mungu Inayofungua Uwezekano Wa Kumiliki Kwa Hiyo Nuru Ya Neno Hata Kutupa Fursa Ya Kudhidi Kukuwa Na Kuongezeka Katika Kila Jambo Jema! Haleluya!

MAOMBI 🙏

Ninayo Maarifa Sahihi Ya Neno La Mungu, Ninastawi Na Kuongezeka Siku Zote Katika Kweli Yote. Hatua Zangu Ni Za Kwenda Mbele Na Juu Siku Zote, Nikiongezeka Na Kubarikiwa Katika Kila Jambo, Katika Jina La Bwana Yesu, Amen!

Please Follow
Twitter :
Insta : &
Whatsapp : https://chat.whatsapp.com/Fd5pMyi0P9J7WvDnQ3hXCZ
Facebook : Word For All Nations Int’l Ministry

MINISTER HERY INOCENT
0620141375

*SOMO: ANGAZA PANDE ZOTE~ 10/10/2024*📖📖*Mathayo‬ ‭5‬:‭16‬ ‭BHND‬‬**Vivyo hivyo, ni lazima mwanga wenu uangaze mbele ya w...
10/10/2024

*SOMO: ANGAZA PANDE ZOTE~ 10/10/2024*

📖📖*Mathayo‬ ‭5‬:‭16‬ ‭BHND‬‬*
*Vivyo hivyo, ni lazima mwanga wenu uangaze mbele ya watu, ili wayaone matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni*

TAFAKARI 👇

Wana Wa Mungu Wamebeba Dhamana Kamili Ya Uwakilishi Wa Baba Na Ufalme Wake Wote Kwa Ujumla. Kila Alieitikia Mualiko Wa Wokovu Basi Ameyakubali Maisha Mapya Ya Nuru Ya Mungu, Iwezayo Kuathiri Mazingira Na Kuleta Badiliko Chanya Wakati Wote. Mstari Wa Ufunguzi Unatupa Maelekezo Kuwa Aina Hii Ya Nuru Na Muangaza Tulio Nao Ulete Tija Kwa Watu Wanaotuzunguka, Kimatendo Hata Atukuzwe Mungu Kwaajili Yetu. Hii Sio Tu Kwa Matendo Mema Ya Ukarimu Bali Matendo Kamili Ya Kuuwakilisha Uhalisia Wa Mungu, Yaani Watu Wakuonapo Wewe Wapate Taswira Kamili Ya Mungu. Wahitajipo Faraja, Nuru Yako Ikaangaze Katika Faraja, Wahitajipo Uponyaji, Nuru Ikaangaze Na Kuwaponya, Kile Ambacho Wangekihitaji Kwa Mungu Wakipate Kwako, Maana Ukamilifu Wa Mungu Na Ubora Wake Wote, Umewekwa Kwako,Haleluya!

MAOMBI 🙏

Nuru Iliondani Yangu Inaangaza Sana, Natembea Kwa Mjongeo Wa Kuleta Na Kusababisha Matokeo Chanya Siku Zote, Ubora Wa Mungu Mkamilifu Upo Ndani Yangu, Nasimama Katika Nafasi Ya Kuleta Mabadiliko Kwa Watu Wote Na Naangaza Sana Katika Kila Eneo, Jina La Bwana Yesu, Limebarikiwa! Haleluya!

Please Follow
Twitter :
Insta : &
Whatsapp : https://chat.whatsapp.com/Fd5pMyi0P9J7WvDnQ3hXCZ
Facebook : Word For All Nations Int’l Ministry

MINISTER HERY INOCENT
0620141375

*SOMO: YOTE KWA JINA LA BWANA YESU KRISTO ~ 9/10/2024*📖📖*Wakolosai‬ ‭3‬:‭17‬ ‭NEN‬‬**Lolote mfanyalo, ikiwa ni kwa neno ...
09/10/2024

*SOMO: YOTE KWA JINA LA BWANA YESU KRISTO ~ 9/10/2024*

📖📖*Wakolosai‬ ‭3‬:‭17‬ ‭NEN‬‬*
*Lolote mfanyalo, ikiwa ni kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba katika yeye*

TAFAKARI 👇

Maisha Mapya Ndani Ya Bwana Yesu Kristo, Yanaelezea Na Kuhusu Uhusikaji Wa Moja Kwa Moja Wa Mtembeo Na Mjongeo Wa Bwana Yesu Katika Maisha Ya Mtu. Hii Inahusiana Na Kristo Mwenyewe Katika Uongozi Wa Moja Kwa Moja Yaani Sio Mtu Tena Katika Utendaji Bali Kristo. Katika Kitabu Cha Wakolosai 3:10, Inasema; “*mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba*” Hii Inaweka Msisitizo Kwetu Na Kutupatia Maana Ya Kwamba, Lipo Badiliko Kubwa Lilitokea Mara Baada Ya Kuupokea Wokovu, Maisha Yetu Yalibadilishwa Na Kuwa Asilimia Mia Ni Yesu Kristo, Yeye Anaishi Ndani Yetu, Hivyo Katika Yeye Alivyo Ndivyo Tulivyo. Mstari Wa Ufunguzi Unatuelekeza Kuwa Tukiisha Kuuchukuwa Uelewa Huu Basi Tufahamu Tendo Lolote Linatendeka Ni Kwaajili Ya Kumuwakilisha Kristo, Hivyo Linafanyika Na Lifanyike Katika Jina La Bwana Yesu Kristo. Chukulia Mfano Wa Balozi Wa Marekani Awapo Nchi Nyingine, Mathalani Tanzania, Asilimia Mia Lolote Na Chochote Anachofanya, Basi Anafanya Kwa Jina La Marekani, Maana Anawakilisha Na Amekasimiwa Nguvu Na Nchi Ya Marekani Kuwakilisha Jina Na Nguvu Yake!

MAOMBI 👇

Natenda Yote Katika Kristo, Nikishukuru Kwa Kila Jambo Kwaajili Ya Utukufu Wake, Nafaidika Na Kunufaika Na Uwepo Wa Kristo Maishani Mwangu. Mimi Ni Balozi Kamili Wa Kristo Na Ufalme Wote, Si Mimi Tena Bali Kristo Katika Kila Jambo, Katika Jina La Bwana Yesu Kristo, Amen!

Please Follow
Twitter :
Insta : &
Whatsapp : https://chat.whatsapp.com/Fd5pMyi0P9J7WvDnQ3hXCZ
Facebook : Word For All Nations Int’l Ministry

MINISTER HERY INOCENT
0620141375

*SOMO; ITIKIA MUALIKO IPASAVYO ~ 1/10/2024*📖📖* Mathayo 22:9~14**Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaon...
01/10/2024

*SOMO; ITIKIA MUALIKO IPASAVYO ~ 1/10/2024*

📖📖* Mathayo 22:9~14*
*Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni. Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi. Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa. Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache*

TAFAKARI 👇

Bwana Yesu Katika Kuelezea Ufalme, Anatumia Mfano Huu Wa Mfalme Aliyeaandaa Harusi Ya Mwanawe Na Kutuma Watumwa Wake Kuwaaleta Walioalikwa Katika Karamu Ya Harusi Nao Hawakuwa Tayari Kuhudhuria Karamu Hio Bali Kila Mmoja Alienda Kwenye Shughuli Zake {*Mathayo 22:5 Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake*}
Wengine Walienda Mbali Zaidi Na Kuwaua Wale Watumwa. Huu Ni Mfano Halisi Wa Kinachoendelea, Harusi Ni Safari Ya Wokovu Hata Ile Siku Ya Mwisho Ya Dunia Hii, Ambapo Watumwa Walioagizwa Ni Wale Wahubiri Wa Habari Njema Za Wokovu Yaani Injili Ya Bwana Yesu Kristo. K**a Mfano Unavyoeleza Ndivyo Unavyomaanisha, Yani Kwamba Hivi Sasa Bwana Ameagiza Watumwa Wake Kila Pahala Kuwaeleza Wengine Habari Za Wokovu, Lakini Watu Na Ulimwengu Umekuwa Bize Na Shughuli Nyingine Za Dunia Zisizo Na Faida Kwao. Ujumbe Wa Ufunguzi Unalenga Kuamsha Watu Na Kuwataka Kuitikia Injili, Hio Ni Ishara Ya Kuitikia Mualiko, Ipo Siku Fursa Hii Haitakuwa Wazi, Na Hakuna Atakayeingia Kwa Bahati Mbaya Kwa Maana Bwana Anajuwa Waliowake! Haleluya!

MAOMBI 🙏

Asante Baba Kwa Fursa Ya Wokovu, Hakika Nipo Salama Kwa Kuitiii Sauti Yako. Nami Nasimama Sehemu Ya Mchakato Wa Kualika Na Kuwaambia Wengine Habari Hizi Za Ufalme, Hakika Maelfu Mengi Yanaitikia Wito Huu, Na Nakemea Kila Upofushwaji Wa Fikra Za Watu Unaoletwa Na Adui, Katika Jina La Bwana Yesu Kristo!

Please Follow
Twitter :
Insta : &
Whatsapp : https://chat.whatsapp.com/Fd5pMyi0P9J7WvDnQ3hXCZ
Facebook : Word For All Nations Int’l Ministry

MINISTER HERY INOCENT
0620141375

Address

Kibaha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Living Word For All Nations Int’l Ministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Living Word For All Nations Int’l Ministry:

Share