14/12/2020
IBADA YA JUMAPILI TAREHE 13/12/2020 – KANISA LA EFATHA MWENGE
MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA.
SILAHA AMBAYO IBILISI ATATUMIA KUKUMALIZA.
1. UPWEKE NA KUACHWA
Ibilisi atatumia Upweke na kuachwa, ili kukuchinja. Ukiwa peke yako inamaana kuwa uko mwenyewe, na ukiwa umeachwa maana yake umetelekezwa yaani umetengwa.
• Upweke au kutengwa siyo kuzuri, ukiwa katika hiyo hali chochote chaweza kukutokea kwa wepesi na ni rahisi kwa ibilisi kukukandamiza . Mtu akiwa katika hali hii ni rahisi kushambuliwa na magonjwa na maradhi mbali mbali
• Kitu cha hatari katika dunia hii siyo kukosa pesa bali ni upweke, unaweza ukawa na kila kitu lakini ukiwa na upweke vitu vyote vitaishia kuchukuliwa
Upweke unaweza kufanya kitu gani?
Mwanzo 4:13-14 “Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki. Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua.” Upweke ni ishara ya laana au adhabu, ni vyema kumuadhibu mtu kwa viboko kuliko kumuacha awe pekeyake. Upweke unaitesa akili na moyo, upweke ni aina ya jela.
Unapokuwa mpweke mambo haya yatakujia moja kwa moja:-
1. “Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi” Unakuwa mbali na urithi wako, hauwezi kurithi chochote, hii inamaana kuwa chochote utendacho hautapata kitu, watu wengi wako huku duniani lakini ni wa pweke, utajuaje? Hawamiliki chochote. Wakati wengine wanachanua wao ni vurugu na wanapambana ili maisha yapate kwenda mbele
2. “Nitasitirika mbali na uso wako,” Wenye upweke mara zote huwa wanajificha mbali hawataki kuonekana maana yake wapo mbali na uwepo wa Mungu, unajuaje? Haijalishi wanaomba kiasi gani hakuna majibu kwao
3. “Nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani;” hana kitu maalum cha kufanya, anaweza akawa na biashara hii leo kesho ana biashara nyingine. Wapweke hawana kikao maalum, leo amepanga nyumba hii kesho anahama anapanga mahali pengine
4. “Hata itakuwa kila anionaye ataniua” Upweke unamuweka mtu katika hatari ya kuuawa, anaweza kuua au kuuawawa.
K**a wewe ni mpweke ni rahisi kwako kuua au kuuwawa, Kaini aliua kwa nini? Kwa sababu Mungu hakuitakabari dhabihu yake kwa hiyo akaghadhibika hivyo akaua
K**a unaye Mungu ndani yako kwanza kabisa tutaona pendo ndani yako, k**a unaye Mungu maana yake unayo kweli ndani yako, kwa hiyo unasema kile ulichonacho ndani ya moyo wako yaani unasema iliyo kweli.
Utajuaje kuwa huyu mtu ni mpweke? Utaona hana msamaha, anataliki kwa sababu ni mpweke.