Brazio With Word Of God

Brazio With Word Of God Karibu sana katika page hii inayotangaza ufalme wa Mungu kupitia watumishi wake

20/09/2021

Chakula chochote chaweza kuliwa lakini chakula kingine ni kizuri kuliko kingine. K**a ulimi upimavyo aina za mionjo ya vyakula ndivyo na mwenye akili agunduavyo maneno ya uongo.Mwenye akili potovu husababisha huzuni lakini mwenye uzoefu wa maisha atamlipa inavyofaa.

19/09/2021

Wapendwa katika bwana tumsifu yesu kristu
Mtu akitoa sadaka kitu kilichopatikana kwa udanganyifu dhabihu hiyo yake ina dosari.zawadi za wasiotii sheria hazikubaliki
Mungu mkuu hakubali sadaka za wasiomcha wala wingi wa sadaka hauwezi kuleta upatanisho. Mtu anayetoa sadaka kitu alichomnyanganya maskini ni sawa na mtu anayemuua mtoto mbele ya baba yake.
Chakula cha maskini ni uhai wake.Yeyote anayempora maskini chakula ni muuaji.
Wako katika kristu

17/09/2021

Wamchao bwana wataishi, maana tumaini lao liko kwake yeye anayewaokoa.
Amchaye bwana hatakuwa na woga. Hawezi kuogopa kwani bwana ndiye tumaini lake.Heri mtu ambaye anamcha bwana.Maana anatazamia yeye amtegemeze. Bwana huwaangalia kwa wema wale wampendao,yeye ni ngao imara na tegemeo lao thabiti.Yeye ni kinga yao mbali na upepo mkali. Ni kivuli chao wakati wa jua kali.Yeye huwalinda wasijikwae huwasaidia wasianguke.Bwana huijaza mioyo furaha na huyatia macho mwanga.yeye huwapa afya,uhai na baraka.

16/09/2021

Mtu uishipo usimwachie mtoto,mke,ndugu au rafiki akutawale. Usimpe mtu mwingine mali yako usije ukabadili nia ya kuomba urudishiwe.
Ungali bado unapumua,usikubali Mtu mwingine achukue nafasi yako.Maana ni afadhali watoto wako wakutegemee kuliko wewe kuwategemea wao. Fanya kila kitu ufanyacho kabisa,usiitie dosari heshima yako.
Mwisho wa maisha yako,wakati wa saa yako ya mwisho,gawa mali yako.

15/09/2021
14/09/2021

Usishindane na mtu mwenye uwezo,la sivyo utajikuta makuchani mwake.Usigombane na mtu yeyote tajiri la sivyo utajiri wake utakushinda mahak**ani maana dhahabu imewaangamiza wengi na kuipotosha mioyo ya wafalme. Usibishane na mtu anayepayukapayuka.Usiongeze kuni katika moto wake.
Usitaniane na mtu asiye na adabu la sivyo atawafedhehesha wazee wako

13/09/2021

Wapendwa katika Bwana kila mtu anatambua kuwa Mungu ni upendo. K**a Abrahamu alivyomtoa Isack kwa Mungu naye alitupa mwanae wa pekee. Mungu anajua tunahitaji upendo wake Kristu. Labda dunia ingetaka michezo Mungu angetupa Messi,k**a angeona wanahitaji Siasa labda angemtuma Samia na k**a Dunia ingetaka ngumi angemtuma Tyson lakini yeye anajua tunataka huruma yake hivo kumtuma mwanae wa pekee ili amwaminiye apate uzima wa Milele

10/09/2021

Mtoto mwenye hekima ni furaha ya baba yake lakini mwana mpumbavu ni huzuni ya mama yake.
Kwa nini umtese mama yako kwa upumbavu. Najua maneno haya hayana makandokando kabisa.mfurahishe mama yako aliyekuzaa kwa kuongea kwa busara mpe furaha baba yako kwa kuwa nayo hekima nawe utapendwa na Mungu na watu pia

10/09/2021

Ndugu katika Bwana,
Mtafuteni bwana maadamu anapatikana,mwiteni maadam yu karibu.
Mtu mbaya aache njia zake na mtu asiye haki aache mawazo yake,na amrudie bwana naye atamrehemu.

Address

Kariakoo

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Brazio With Word Of God posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Brazio With Word Of God:

Share