Global Christian Church -GCC

Global Christian Church -GCC Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Global Christian Church -GCC, Pentecostal Church, GCC, Kahama.

https://youtube.com/live/OJAg2AS-uv4Karibu uabudu nasi leo Jumapili tarehe 4/1/2026Pastor Jofrey Daudi
04/01/2026

https://youtube.com/live/OJAg2AS-uv4

Karibu uabudu nasi leo Jumapili tarehe 4/1/2026

Pastor Jofrey Daudi

KUTEMBEA KWA KUTAMBUA MAJIRA YAKO II Jumapili tarehe 4/1/2026 Pastor Jofrey

https://youtube.com/live/4cJ7j3o-FhwKaribu ibada ya mkesha unaweza bonyeza hapo juu kuungana nasi katika ibada ya leo ta...
31/12/2025

https://youtube.com/live/4cJ7j3o-Fhw

Karibu ibada ya mkesha unaweza bonyeza hapo juu kuungana nasi katika ibada ya leo tarehe 31/12/2025 kuamkia tarehe 1/1/2025

Pastor Jofrey Daudi

GLOBAL CHRISTIAN CHURCH - GCC KAHAMA Pastor Jofrey Daudi Dibson.MKESHA WA MWAKA MPYA Tuna kila sababu ya kumrudishia Mungu wetu sifa na utukufu kwa namna al...

https://youtube.com/live/bzJgxAJ7me8Karibu ushiriki pamoja nasi katika ibada ya leo Tarehe 28/12/2025Pastor Jofrefy Daud...
28/12/2025

https://youtube.com/live/bzJgxAJ7me8

Karibu ushiriki pamoja nasi katika ibada ya leo Tarehe 28/12/2025

Pastor Jofrefy Daudi
GCC - KAHAMA

GLOBAL CHRISTIAN CHURCH - GCC KAHAMA Pastor Jofrey Daudi Dibson.JINSI YA KUTOKA KWENYE MAJIRA MAGUMU Kuna majira unapitia ni magumu hata kuelezea lakini bado...

Bwana Yesu asifiweTunakushukuru sana kwa sadaka yako ya kumpongeza Mchungaji na familia yake juu ya huduma inayoendelea ...
21/12/2025

Bwana Yesu asifiwe

Tunakushukuru sana kwa sadaka yako ya kumpongeza Mchungaji na familia yake juu ya huduma inayoendelea hapa GCC
Ulipotoa ukazidishiwe zaidi.

Mch. Jofrey Daudi - GCC

https://youtube.com/live/5y1kOQD2ukMKaribu tushiriki ibada pamoja tupo live muda huu waweza bonyeza kitufe hapo juu.Past...
21/12/2025

https://youtube.com/live/5y1kOQD2ukM

Karibu tushiriki ibada pamoja tupo live muda huu waweza bonyeza kitufe hapo juu.

Pastor Jofrey Daudi

Pastor Jofrey Daudi Dibson II Global Christian Church GCC- KAHAMA NJIA YA KUWATIA WATUMISHI WA MUNGU MOYOPata muda wa kushiriki ibada hii kwa kusikiliza ...

FAIDA ZA KUSIKILIZA NA KUFUATA MAELEKEZO YA MUNGU1.      Mungu ataamuru Baraka yake ikujilie au ikufuate.Kumb 28: 1, 2Mb...
20/12/2025

FAIDA ZA KUSIKILIZA NA KUFUATA MAELEKEZO YA MUNGU

1. Mungu ataamuru Baraka yake ikujilie au ikufuate.

Kumb 28: 1, 2

Mbaraka wa Mungu ni Zaidi ya mafanikio ya mwanadamu. Unaweza ukafanikiwa kwenye biashara yako kwa mfano lakini usiwe na mbaraka wa Bwana juu ya hiyo biashara.

Kwa nini?

Kwa sababu biashara inaweza ikakupa faida nyingi lakini isikusaidie kukutoa kimaisha. Na ndio maana watu wengi wanafanya kazi za kuajiriw lakini maisha yao ni magumu sana kana kwamba hawana kazi lakini wana kazi. Unaweza ukajiuliza hivi hizo pesa na mishahara yao wanapeleka wapi? Lakini ukweli ni kwamba kazi zao au biashara zao hazina mbaraka wa Mungu ambao ungewafanikisha kimaisha.

Kwenye mbaraka wa Mungu kun ulinzi wa Mungu, Amani ya Mungu, utoshelevu wa Kimungu, uzidisho wa Kimungu na kibali cha Mungu.



2. Unapata uhakika wa ushindi

Waamuzi 7: 1-2, - 7, - 9 –

Gidioni aliandaa jeshi kubwa sana kwa ajili ya kupigana na Wamidiani lakini Mungu alimwambia apunguze jeshi hilo hadi kufikia wat5u 300, na kuna maelekezo alimpa ya nini cha kufanya.

-Mungu akikuahidi kuwa atakupigania ni kweli kwamba atakupigania. Unachotakiwa ni kusikiliza sauti ya Mungu inayokupa maelekezo au mbinu utakayotumia kumshinda adui.

Unaweza ukawa unajua mbinu nyingi sana za kumshinda adui lakini Mungu anataka umsikilize yeye kwa sababu Mungu yeye ni Bwana wa vita, anajua ni mbinu ipi uitumie saa hiyo unapigana kwenye vita yako au kwenye hali yako.

NB: Ni muhimu sana kusikiliza maelekezo ya Mungu anayokupa hata k**a ndani mwako unajua kuwa unafahamu namna ya kutoka kwenye shida uliyo nayo.

Haiingii akilini jeshi la watu 300 kupambana na jeshi lenye watu k**a mchanga wa ufukweni halafu wategemee kushinda. Ni lazima Mungu mwenyewe ahusike. Njia za Mungu si sawa na njia za mwanadamu, na mawazo ya Mungu si sawa na mawazo ya mwanadamu.

Kwa nini Mungu anataka umsikilize kwanza? Ni kwa sababu anafanya mambo yake yote kwa utukufu wake- yaani anafanya hayo ili ajitwalie utukufu. Kwa hiyo ukifanya chochote ili ujitukuze mwenyewe, utainua vita na Mungu mwenyewe ambayo hakuna anayeweza kukusaidia. (Mungu hampi yeyote utukufu wake).

Pia unaweza ukasoma habari za kuanguka kwa ukuta wa mji wa Yeriko katika Yoshua 6: 1 – 16





3. Unapata kufahamu chanzo au asili ya tatizo unaloliombea.

2 Samweli 21: 1 – 2 – 14

Hapa tunaona habari ya Mfalme Daudi katika kipindi chake kulitukia njaa ambayo ilidumu kwa muda wa miaka mitatu, na Biblia inasema ilikuwa mwaka kwa mwaka. Ndipo Daudi akautafuta uso Bwana na Bwana akamjibu.

Biblia haijaweka wazi mfalme Daudi aliomba maombi ya namna gani lakini tunaona kile alichomjibu Bwana. Bwana alimjibu “ni kwa sababu ya Sauli alivyowaua Wagibeoni”.

- Lile neno “ni kwa sababu ya” linaonyesha kuwa Daudi aliomba kujua chanzo cha ile njaa. Ni sawa na kwamba aliomba “kwa nini njaa imekuja juu ya nchi yake”.

- Jibu la Munngu kwa Daudi halikuondoa njaa iliyokuwa juu ya nchi bali lilimpa kujua chanzo cha njaa ile au sababu ya kuwepo kwa njaa ile.

- Kulikuwa hakuna namna yoyote ile ya ile njaa kuondoka isipokuwa kushughulikia chanzo chake.

Wakati mwingine unaweza ukawa unaombea jambo Fulani lakini Mungu akakusemesha kitu tofauti na jambo unaloliombea. Halafu unashangaa.

- Kumbe Mungu anakuonyesha chanzo cha tatizo lako na halitaondoka mpaka umeshughulika na chanzo hicho.

- Tusikimbilie tu kukemea tukidhani kila tatizo tunalopitia limesababishwa na Shetani kumbe mengine ni adhabu kutokana na kosa lililofanyika huko nyuma.

Kipindi kile cha Daudi hakukuwa na damu ya Yesu ndio maana iliwabidi walipize kisasi ili kuondoa chanzo cha tatizo la njaa ile lakini sisi tunayo damu ya Yesu inayonena mema kuliko damu za watu, wanyama na hata ndege.

Hebu fikiria Daudi kaka mwaka wa kwanza anaona njaa haiondoki, mwaka wa pili bado tu, unafika mwaka wa tatu ndio anaamua kuutafuta uso wa Bwana.

- Maana yake ameacha kuomba kwamba Mungu aiondoe njaa bali anaomba kujua chanzo cha njaa ni nini.

- Usifikiri Biblia inaposema mwaka kwa mwaka kwamba Daudi alikuwa haombi, alikuwa anaomba. Lakini alipoona hakuna mabadiliko yoyote ilibidi abadilishe prayer point.

- Mwaka wa kwanza Daudi anaomba lakini hatuoni Mungu akijibu chochote na mwaka wa pili vivyo hivyo, lakini mwaka wa tatu Mungu anajibu.

NB: Hebu kaa utafakari ni kitu gani ambacho Mungu amekuwa akikuonyesha au akikusemesha lakini huelewi wala hujui?

- Kwa sababu wengi wamekwama mahali na hawajasogea mbele kwa muda mrefu wakidhani kuwa Mungu hajawajibu maombi yao kumbe ni wao hawajamsikiliza Mungu kwa makini ili kupata maelekezo ya kufanyia kazi.

Ukishindwa kusikiliza sauti ya Mungu inayosema nawe ndani yako utashindwa kuvuka mahali pa kubwa sana katika viwango vya kumjua Mungu kwenye maisha yako.

https://youtube.com/live/OTZ-A4FaA14NGUVU YA MAONO  Pastor Jofrey Global Christian church Tupo live bonyeza link hapo ju...
14/12/2025

https://youtube.com/live/OTZ-A4FaA14

NGUVU YA MAONO Pastor Jofrey Global Christian church
Tupo live bonyeza link hapo juu kuungana nasi katika ibada ya leo Jumapili

Karibu ibada tarehe 14/12/2025

Pastor Jofrey Daudi Dibson II Global Christian Church GCC- KAHAMA Nguvu ya MAONO. Pata muda wa kushiriki ibada hii kwa kusikiliza ujumbe huu. Waweza toa ...

Address

GCC
Kahama
255

Telephone

+255746225395

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Global Christian Church -GCC posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Global Christian Church -GCC:

Share