Efatha Church Kahama

Efatha Church Kahama we bring the world to JESUS WE BRING THE WORLD TO JESUS

KARIBU KATIKA IBADA YA JUMAPILIKesho, tarehe 07/06/2026, Kanisa la Efatha Kahama linakukaribisha katika Ibada takatifu y...
06/06/2026

KARIBU KATIKA IBADA YA JUMAPILI

Kesho, tarehe 07/06/2026, Kanisa la Efatha Kahama linakukaribisha katika Ibada takatifu ya kumsibu Mungu na kumwabudu kwa roho na kweli. Njoo upokee nguvu ya Roho Mtakatifu itakayobadilisha maisha yako na kukuwezesha kufikia hatima yako.

Usipange kukosa ibada hii ya kipekee. Njoo ukiwa na matarajio makubwa, kwa maana Mungu yuko tayari kukutana na wale wanaomtafuta kwa moyo wote.

MUDA: Saa 2:00 asubuhi

Karibu sana, Mungu akubariki!

NAIBARIKI JUMAMOSI YANGU. Nafurahi katika BWANA; BWANA ni Nuru yangu, BWANA ni Wokovu wangu, BWANA ni Ngome ya Uzima wan...
06/06/2026

NAIBARIKI JUMAMOSI YANGU.

Nafurahi katika BWANA; BWANA ni Nuru yangu, BWANA ni Wokovu wangu, BWANA ni Ngome ya Uzima wangu. Nafurahi katika BWANA.

Jumamosi yangu Imebarikiwa na BWANA.

NENO LA SIKU©Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira – Kanisa la EfathaTAREHE: 04/06/2026SOMO: YESU NDIYE MLANGOYohana 10...
04/06/2026

NENO LA SIKU

©Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira – Kanisa la Efatha

TAREHE: 04/06/2026

SOMO: YESU NDIYE MLANGO

Yohana 10:9 “Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.”

Unaponena kwa lugha mpya ndipo unakuwa unaingia na unapomaliza kuchukua kile unachochukua katika Roho ndipo unatoka. Kutoka ni kwenda kuishi na kutenda katika ulimwengu ukiwa umebeba kile ulichopokea mbele zake.
Popote ulipo, iwe ni nyumbani, kazini au kwenye biashara yako, Nguvu hiyo hukuwezesha kutawala, kushinda vikwazo na kumfukuza ibilisi katika eneo lako la mamlaka.

Huwezi kumiliki pasipo hiyo Nguvu. K**a unataka kumiliki biashara kubwa na biashara hiyo ina ushindani mwingi hakikisha una hii Nguvu ya Mungu kwa sababu wengine watatumia nguvu za giza, hivyo lazima watakutoa nje.

Unapohitaji jambo fulani hakikisha una hiyo mamlaka na tangaza kile unachofahamu ili uweze kumfukuza ibilisi.

Je! una nguvu ya kupambana na hao wanaomiliki upande wa pili? Hakikisha una Mungu anayemiliki dunia na vyote ili uweze kuingia na kutoka.

NAIBARIKI ALHAMISI YANGU. Mimi Nimebarikiwa, katika BWANA sitapungukiwa na kitu. YESU ni BWANA.
04/06/2026

NAIBARIKI ALHAMISI YANGU.

Mimi Nimebarikiwa, katika BWANA sitapungukiwa na kitu.

YESU ni BWANA.

SOMO: TUNZA UJANA WAKO.Ni jambo la faida kwa mtu kujifunza nidhamu, uwajibikaji na kumtegemea Mungu tangu akiwa kijana. ...
03/06/2026

SOMO: TUNZA UJANA WAKO.

Ni jambo la faida kwa mtu kujifunza nidhamu, uwajibikaji na kumtegemea Mungu tangu akiwa kijana. Hii humjenga mtu kuwa na tabia imara na kumwandaa kwa majukumu makubwa ya maisha.

Maombolezo 3:27 "Ni vema mwanadamu aichukue nira wakati wa ujana wake."

NIRA ni kifaa kilichowekwa shingoni mwa ng'ombe ili waweze kufanya kazi au kuvuta gari. Kwa lugha ya mfano, nira inaweza kumaanisha: Nidhamu, Majukumu, Mafunzo ya maisha, Utii kwa Mungu na
Kuvumilia changamoto zinazojenga tabia.

MAMBO YA KUZINGATIA.

1. Ujana ni wakati wa kujifunza nidhamu
Mtu anayejifunza kujidhibiti akiwa kijana huwa na msingi mzuri wa maisha ya baadaye. Nidhamu katika masomo, kazi, maadili na ibada humjenga mtu kuwa imara.

2. Changamoto za ujana zinaweza kujenga tabia
Majaribu na majukumu tunayokutana nayo katika ujana yanaweza kutufundisha uvumilivu, hekima na utegemezi kwa Mungu.

3. Kujifunza kumtii Mungu mapema ni baraka
Mtu anayemjua Mungu na kufuata njia zake tangu ujana hupata mwongozo unaoweza kumlinda dhidi ya makosa mengi ya maisha.

4. Maandalizi ya maisha ya baadaye K**a vile mkulima humzoeza ng'ombe kubeba nira akiwa bado mdogo, vivyo hivyo mwanadamu huandaliwa kwa majukumu makubwa kwa kujifunza uwajibikaji akiwa kijana.
Matumizi katika maisha ya leo.

Kwa kijana, lazima azingatie Kusoma kwa bidii, Kuheshimu wazazi na viongozi, Kujifunza kazi na uwajibikaji, Kukuza tabia njema na Kumtumikia Mungu kwa uaminifu.

©Mtumishi Deusdedith Kusekwa

NAIBARIKI JUMATANO YANGU. Ni Siku ya kuchukua Urithi wangu. Mimi ni Mmiliki na nitamiliki pamoja na Wamiliki. YESU ni Mz...
03/06/2026

NAIBARIKI JUMATANO YANGU.

Ni Siku ya kuchukua Urithi wangu. Mimi ni Mmiliki na nitamiliki pamoja na Wamiliki.

YESU ni Mzuri.

Mungu wa Neema na Rehema; aliyetupa nguvu ya kuingia mwezi huu wa 6 aufanye uwe mwezi wa HABARI njema kwetu kwa jina la ...
02/06/2026

Mungu wa Neema na Rehema; aliyetupa nguvu ya kuingia mwezi huu wa 6 aufanye uwe mwezi wa HABARI njema kwetu kwa jina la Yesu...!

Yule malaika wa habari njema aliyemtokea bikira Mariam mwezi wa 6, akutokee na kukuletea habari njema kwenye kila eneo la maisha yako kwa jina la Yesu...!

●Luka 1:26-27,"Mwezi wa sita,malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya,jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu,jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; jina lake bikira huyo ni Mariamu."

NAIBARIKI JUMANNE YANGU. Ee NGUVU zangu, nitakuimbia kwa furaha, Mimi na Familia yangu tumebarikiwa. YESU asante.
02/06/2026

NAIBARIKI JUMANNE YANGU.

Ee NGUVU zangu, nitakuimbia kwa furaha, Mimi na Familia yangu tumebarikiwa.

YESU asante.

01/06/2026
NAIBARIKI JUMATATU YANGU. Mimi ni wa Kileleni na sio wa bondeni; kwenye Biashara zangu ni wa Kileleni, kwenye Kazi zangu...
01/06/2026

NAIBARIKI JUMATATU YANGU.

Mimi ni wa Kileleni na sio wa bondeni; kwenye Biashara zangu ni wa Kileleni, kwenye Kazi zangu ni wa Kileleni, kwenye Kilimo changu ni wa Kileleni, kwenye Ufugaji wangu ni wa Kileleni, kwenye Elimu yangu ni wa Kileleni, popote nilipo Mimi ni wa Kileleni.

Asante YESU.

Jumatatu yangu Imebarikiwa na BWANA.

Address

Kahama
717903744

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Kahama posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church Kahama:

Share