03/06/2026
SOMO: TUNZA UJANA WAKO.
Ni jambo la faida kwa mtu kujifunza nidhamu, uwajibikaji na kumtegemea Mungu tangu akiwa kijana. Hii humjenga mtu kuwa na tabia imara na kumwandaa kwa majukumu makubwa ya maisha.
Maombolezo 3:27 "Ni vema mwanadamu aichukue nira wakati wa ujana wake."
NIRA ni kifaa kilichowekwa shingoni mwa ng'ombe ili waweze kufanya kazi au kuvuta gari. Kwa lugha ya mfano, nira inaweza kumaanisha: Nidhamu, Majukumu, Mafunzo ya maisha, Utii kwa Mungu na
Kuvumilia changamoto zinazojenga tabia.
MAMBO YA KUZINGATIA.
1. Ujana ni wakati wa kujifunza nidhamu
Mtu anayejifunza kujidhibiti akiwa kijana huwa na msingi mzuri wa maisha ya baadaye. Nidhamu katika masomo, kazi, maadili na ibada humjenga mtu kuwa imara.
2. Changamoto za ujana zinaweza kujenga tabia
Majaribu na majukumu tunayokutana nayo katika ujana yanaweza kutufundisha uvumilivu, hekima na utegemezi kwa Mungu.
3. Kujifunza kumtii Mungu mapema ni baraka
Mtu anayemjua Mungu na kufuata njia zake tangu ujana hupata mwongozo unaoweza kumlinda dhidi ya makosa mengi ya maisha.
4. Maandalizi ya maisha ya baadaye K**a vile mkulima humzoeza ng'ombe kubeba nira akiwa bado mdogo, vivyo hivyo mwanadamu huandaliwa kwa majukumu makubwa kwa kujifunza uwajibikaji akiwa kijana.
Matumizi katika maisha ya leo.
Kwa kijana, lazima azingatie Kusoma kwa bidii, Kuheshimu wazazi na viongozi, Kujifunza kazi na uwajibikaji, Kukuza tabia njema na Kumtumikia Mungu kwa uaminifu.
©Mtumishi Deusdedith Kusekwa