16/11/2023
MAKUNDI MAWILI YA WATU DUNIANI
2. Walioumbwa kutumika chini ya watu, chini ya maono ya wengine (Part 02)
Sehemu ya kwanza nilikuonesha kutumika chini ya, au chini ya maono ya mwingine si kizuizi cha wewe kuonekana, kutambulika, kazi yako kuonekana na kuwa mkuu!
Sasa tuendelee...
HAWA WALIOUMBWA KUTUMIKA CHINI YA;
• Sio wazuri wa kuanza vitu vyao wenyewe au kuanzisha vitu
• Ni watu ambao ni watulivu mno, watu wa mipango, wasiokurupuka k**a wale walioumbwa kuanza vitu, na kwa sababu ya utulivu huu na kutokurupuka, hawawezi kuchukua hatua za hatari (taking risk), na hivyo si rahisi kwao kuanza vitu
• Ni watu ambao ili wachukue hatua, lazima kwanza wajiridhishe uhakika na usalama tofauti na wale ambao wameumbwa kuanzisha vitu, huwa wanaanza na wanachoweza na walipo, mengine watajua hukohuko mbele
• Ni wasimamizi wazuri, wakikuta kitu kipo tayari, kwa uangalizi na usimamizi wao, lazima kikue, kiwe bora kuliko mwanzo
Mfano: Yusufu (Mwanzo 39:1-5)
• Uwezo wao hupata maana wakikuta tayari kitu kipo na wao waje kukiboresha, kukirekebisha, kukipa sura au mwonekano mzuri zaidi
• Watu hawa wana neema ya ubora, mpangilio kuliko waanzilishi, wasipoutumia huu uwezo kujenga, wanaishia kuwa wakosoaji, wapinzani wa wabeba maono
CHANGAMOTO ZAO
•Kwa kuwa ni watulivu, watu wa ubora, watu wa mipangilio, watu huanza kuwasifia kwamba wao ni bora kuliko waanzilishi, baba zao wa kiroho, waasisi walio juu yao, WASIPOKUWA NA HEKIMA KUJUA HICHO NDICHO WALICHOKUJA KULETA KWENYE TAASISI, WATAJUKUTA WANATAKA KUPINDUA TAASISI AU KUTAKA KUANZA VYA KWAO BADALA YA KUTUMIA UWEZO WAO HUO KUBORESHA KILE KILICHOPO WANACHOTUMIKA CHINI YAKE!
• Watu hawa hukutana na sifa za watu na kuwaonesha WANAWAZIDI AU NI BORA KIUTENDAJI, KIVIPAWA KULIKO WALIOJENGA TAASISI AMBAO NDIO SABABU YAO KUONESHA UWEZO NA WALICHOBEBA!
• Watu hawa hurogwa na sifa wanazopewa na kuamua wakaanze vyao, WAKIKUTANA NA MASHETANI YANAYOPAMBANA NA WAANZILISHI, NA VITA WAKUTANA NAZO WAANZILISHI, HUPOTEANA NA KILE TULICHOKUWA TUKIKIONA KWAO HUYEYUKA!
NINI WAFANYE WATU HAWA;
• Furahia kutumika chini ya, fanya kazi chini ya, k**a yako, bila kujali unalipwa mema, unatambuliwa, unaheshimiwa au la! Dunia haiwezi kukaa kimya kwa mtu anayejitoa, wa ubora na upekee, lazima utaonekana tu!
• Epuka jaribu la kutaka kuanza kitu chako, hautaweza hekaheka, ligi na mapambano ambayo wameumbwa kuanza vitu, baki kwenye kuboresha na kuvipa maana vilivyozalishwa na waanzilishi!
• Sikia furaha kuwa sababu ya maongezeko, utaratibu, mipangilio kwenye taasisi kwa sababu ya hekima zako, usitake kufanya zaidi ya hayo, utakwama!
• Mkubali na kumheshimu mwanzilishi, maana NDIYE ALIYETENGENEZA TAASISI, HUDUMA, KAMPUNI, MFUMO AU JUKWAA AMBALO WEWE UNATUMIKA NALO NA KUONESHA UWEZO WAKO, AMBAPO ASINGEFANYA HIVYO HUENDA TUSINGEKIONA ULICHOBEBA...
• Uwe mrekebishaji mtiifu, mboreshaji chini ya mamlaka, afanyaye mambo bora na mazuri lakini kwa ruhusa ya mwanzilishi na baraka zake, HAPO UTAUSHANGAZA ULIMWENGU NA HAUTAKWEPA UKUU!
Askofu Dickson Cornel Kabigumila
ABC GLOBAL DUNIANI
16.11.2023