07/02/2020
TUNAMUHITAJI YESU WAKATI HUU
Ukikaa ukafikiri jinsi ambavyo dunia ilivyo kwa Sasa ya kupasa kutubu na kuiamini injili na kumkiri Yesu kwa kinywa chako kuwa Bwana na mwokozi ili upate iliyo kweli ndani yako maana yeye ndio lango la mbinguni hakuna mlango mwingine was kuingilia zaidi ya YESU ©Yohana 10:7, 9 Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo.9 Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.
©Mambo mengi Sana yanatokea kwasasa mathayo 24: 6 -8 Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado 7 Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali. 8 Hayo yote ndiyo mwanzo wa utungu.
©Utungu maana yake karibia kitu kinazaliwa K**a mama mjamzito anapotaka kujifungua lazima uchungu uanze huu ndio uchungu wenyewe siku yoyote ile Yesu atarudi kulichukua kanisa
© Tumeisha sikia juu ya tetesi za Vita Kati ya marekani na Iran Tena haya ni mataifa makubwa Sasa tishio limekuja la Corona vyombo vya habari vinasema takribani mataifa kumi tayari yameambukizwa virus vya Corona vilivyoanzia China wenzetu wapo kwenye kipindi kigumu mno mpk imefika hatua hawaruhusiwi kutoka nje na ugonjwa unasambaa kwa Kasi mno mpk Sasa takwimu zinasema watu 600 tayari wamepoteza maisha na watu laki moja tayari wameambukizwa hiyo ya mwezi mmoja tu. Na Uingereza na marekani tayari umefk ugonjwa,tuwe macho tusisinzie .
©mathayo 24: 29 Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika; dunia kwa sasa ipo katika dhiki kubwa ikitafuta suluhisho la kuendelea kuishi
©Manabii wa uongo palipo na manabii wa uongo Basi na manabii wa ukweli wapo lakini tuwe macho Sana na kupenda miujiza. mathayo 24:11 Na manabii wengi wa uongo watatokea, na kudanganya wengi.
Bali tumtafute Yesu anayetenda miujiza ©Yohana 16: 2-3 Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada. 3 Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi. Tujitahidi ndugu zangu kumtafuta Yesu was kweli na Mungu was kweli yeye mwenyewe anasema tumtafute madamu anapatikana ukishindwa kuishi katika kipindi Cha neema hiki je kipindi Cha kujiokoa mwenyewe utawezaje kilichojaa mateso makali
©Ufunuo 9:5 -6 Wakapewa amri kwamba wasiwaue, bali wateswe miezi mitano. Na maumivu yao yalikuwa k**a kuumwa na nge, aumapo mwanadamu.
6 Na siku zile wanadamu watatafuta mauti, wala hawataiona kamwe. Nao watatamani kufa, nayo mauti itawakimbia. Chukua hatua wokovu ni sasa.
Sala ya kumpokea bwana Yesu awe Bwana na mwokozi kwako Sema kwa imani ukimwamini utapokea wokovu
©Bwana Yesu ninatubu dhambi zangu zote nilizotenda kwa maneno, mawazo na vitendo ninazokumbuka na nisizo kumbuka naomba unisamehe futa jina langu kwenye kitabu Cha hukumu andika jina langu kwenye kitabu Cha uzima uwe kwangu Bwana na mwokozi wangu dhambi isinishinde kwa jina la Yesu. Imani ni kuwa na uhakika na Mambo yatarajiwayo imani yako iwe kwa Yesu.
✓✓7 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu.
Ufunuo wa Yohana 2:7✓✓✓✓✓✓