Efatha Church Iringa

Efatha Ministry: Healing & Deliverance by the Blood of JESUS CHRIST.

SIKU YA NANE YA KUFUNGA NA KUOMBASOMO: MAMBO YA ROHONI HUTAMBULIKANA KWA JINSI YA ROHONI NA KWA IMANIMCH HERENA MWAKISIN...
08/05/2026

SIKU YA NANE YA KUFUNGA NA KUOMBA

SOMO: MAMBO YA ROHONI HUTAMBULIKANA KWA JINSI YA ROHONI NA KWA IMANI
MCH HERENA MWAKISININI

Waebrania 11:1-3 “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana. Maana kwa hiyo wazee wetu walishuhudiwa. Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo Dhahiri”.

Mungu ni wa kuaminiwa, tunapomwamini ni kwa sababu tumezisikia habari zake. Tumezisikia habari zake kuwa yeye ndiye muumbaji wetu na kwa njia hiyo tumeamini kwa kusikia.
Mwezi wa tano ni mwezi tunaomwendea Mungu kwa imani juu ya mambo tunayoyatarajia.

Neno la Kristo ndilo linalotufanya tumwamini Mungu na kwa kuamini kunasababisha jambo kutokea. Pasipo kuamini hakuna matokeo ya jambo lolote kutokea, lakini unapoomba kwa kuamini ndipo unasababisha jambo kutokea.

Kuamini kunapoambatana na matokeo kunasababisha wale wanaokuzunguka kuvutwa na kile ulichonacho, kuwafanya waone kuna umuhimu wa kuambatana nawe

Marko 11:22-26 “Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu. Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng'oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu. Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu. Lakini k**a ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu”.

Ili uweze kuona matunda ya kile unachokiamini na matokeo ya kile unachokitafuta lazima ujifunze kuachilia na kusamehe, ndipo Mungu atayasikia maombi yako na kusababisha matunda ya imani yako yakujilie.
K**a una kitu chochote ndani ya mwezi huu lazima ukiachilie ili Mungu aweze kusababisha matendo makuu yatokee kwako na ndipo utayaona matokeo ya kuamini kwako.

MAOMBI
Omba Mungu katika mfungo huu, Mungu akafufue vipawa ndani yetu na kila aliyelala akaamke.
Omba nguvu ya Roho Mtakatifu ije ikujaze kwa upya pale ulipopungua.
Omba Mungu akuachilie hekima na kutambua sauti yake
Kutoka 35:10-11 “Na kila mtu kati yenu aliye na moyo wa hekima na aje, na kuyafanya hayo yote ambayo Bwana ameyaagiza”.
Omba Mungu akufanye kwa upya na akufinyange vile apendavyo ili ufae kwa kazi yake.
Omba Mungu akatupe nguvu ya kushinda majaribu.
Yakobo 1:12 Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.
Ng’oa kila mbegu mbaya inayotokana na kuzaliwa, elimu na mazingira.
Vunja laana yoyote iliyoingia kwako na kwa kanisa na ondoa mzigo mzito kwenye maisha yako.
- Ondoa mzigo wa maradhi, magonjwa.
- Ondoa kudharauliwa
- Ondoa kunyanyaswa
- Ondo kukandamizwa
- Ondoa kukataliwa.
Nenda ukakatae kila roho za visasi na malipizi juu yako

08/05/2026

“K**a mume wako yupo hai, muoneshe hakukosea kukupata wewe”

© Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira

NAIBARIKI IJUMAA YANGU. Katika Mambo yote Tunashinda, na zaidi ya Kushinda kwa YEYE anayetupenda; MIMI NI MSHINDI. Halel...
08/05/2026

NAIBARIKI IJUMAA YANGU.

Katika Mambo yote Tunashinda, na zaidi ya Kushinda kwa YEYE anayetupenda; MIMI NI MSHINDI.

Haleluya, YESU ni Mzuri.

SIKU YA NANE YA KUFUNGA NA KUOMBAYale yanayoonekana magumu leo, Mungu anayageuza kuwa ushuhuda kesho. Hakuna machozi wal...
08/05/2026

SIKU YA NANE YA KUFUNGA NA KUOMBA

Yale yanayoonekana magumu leo, Mungu anayageuza kuwa ushuhuda kesho. Hakuna machozi wala maombi yako yatakayopotea mbele zake. Endelea kuwa mtu wa imani, maana Mungu bado anatenda na atakufikisha mahali pa ushindi.

Warumi 8:28 “_Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema._”

*SIKU YA SABA YA KUFUNGA NA KUOMBA*Mungu ametupa nafasi nyingine ya kumtafuta kwa moyo wa kweli na kuijua haki yake, ili...
07/05/2026

*SIKU YA SABA YA KUFUNGA NA KUOMBA*

Mungu ametupa nafasi nyingine ya kumtafuta kwa moyo wa kweli na kuijua haki yake, ili maisha yetu yaangaze k**a nuru ya ulimwengu.

Katika siku hii ya leo:
Pale penye giza, Mungu alete nuru.
Pale penye udhaifu, alete nguvu.
Pale penye ugonjwa, alete uponyaji.
Na pale penye maonevu, alete wokovu na amani.

Mungu akufanye kuwa vile alivyokuandalia kwa ajili ya utukufu wake.

Mathayo 5:14 “_Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima._”

NAIBARIKI ALHAMISI YANGU. Mimi nimebarikiwa na BWANA; Kwangu hakutakuwa na kulala njaa au kubangaiza Chakula bali nitaku...
07/05/2026

NAIBARIKI ALHAMISI YANGU.

Mimi nimebarikiwa na BWANA; Kwangu hakutakuwa na kulala njaa au kubangaiza Chakula bali nitakula Vinono, na nitatenda Mambo Makuu kwa Msaada wa BWANA.

Haleluya, YESU ni Mzuri, Furahini katika BWANA.

Alhamisi yangu Imebarikiwa na BWANA.

*SIKU YA SITA YA KUFUNGA NA KUOMBA*Katika safari hii ya kufunga na kuomba, kuna mambo lazima uyaache ili uweze kusonga m...
06/05/2026

*SIKU YA SITA YA KUFUNGA NA KUOMBA*

Katika safari hii ya kufunga na kuomba, kuna mambo lazima uyaache ili uweze kusonga mbele. Acha mizigo isiyo ya lazima, acha dhambi zinazokurudisha nyuma na chagua kukimbia kwa saburi.

Ushindi si kwa wenye kubeba mizigo, bali kwa wale wanaoachilia na kusonga mbele.

Waebrania 12:1 (SUV) “_Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa namna hii la mashahidi, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ituzingayo kwa upesi; tukipige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyo mbele yetu._”

05/05/2026

Kufunga ni kuadabisha mwili na mambo yote ili kuamsha nguvu ya Mungu ndani yako

Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira

Leo Jitamkie haya“Kwa msaada wa Mungu nitatenda mambo makuu.Tembea kwa amani, ukiamini kuwa Mungu tayari anatenda kwa aj...
05/05/2026

Leo Jitamkie haya

“Kwa msaada wa Mungu nitatenda mambo makuu.

Tembea kwa amani, ukiamini kuwa Mungu tayari anatenda kwa ajili yako

……………………………………………….

Today declare this:

“Through God, I will do great things.”
Walk in peace, believing that God is already working on your behalf.

SIKU YA TANO YA KUFUNGA NA KUOMBAKufunga si ishara ya udhaifu bali ni njia ya kujiunganisha na Mungu kwa undani zaidi. E...
05/05/2026

SIKU YA TANO YA KUFUNGA NA KUOMBA

Kufunga si ishara ya udhaifu bali ni njia ya kujiunganisha na Mungu kwa undani zaidi. Endelea kusonga mbele, mwana wa Mungu.

Kila sadaka unayotoa ina athari katika ulimwengu wa roho. Usivunjike moyo, hata k**a huoni, Mungu anaendelea kutenda kazi. Tamka kwa imani na utembee katika nguvu.

NAIBARIKI JUMANNE YANGU. Ni Siku ya Familia; Upendo wa BWANA umetuzunguka, Furaha ya BWANA ni Nguvu yetu. Asante YESU.Ju...
05/05/2026

NAIBARIKI JUMANNE YANGU.

Ni Siku ya Familia; Upendo wa BWANA umetuzunguka, Furaha ya BWANA ni Nguvu yetu.

Asante YESU.

Jumanne yangu Imebarikiwa.

Address

Wilolesi
Iringa
P.0.B0X2003

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Iringa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church Iringa:

Share